Polisi wameshindwa kumkamata huyu tapeli anayewapiga Walimu kila siku?

Polisi wameshindwa kumkamata huyu tapeli anayewapiga Walimu kila siku?

yaani kati ya watu wanaotakiwa kuangaliwa kwa jicho la huruma hapa nchini ni waaalimu. wanatia huruma sana, wanafanya kazi mazingira magumu sana na hakuna tumaini la ukombozi wa maisha yao. ndio maana muda wote wamejaa hofu na mashaka ya kufukuzwa kazi. icho icho kidogo walichopata kama kibarua wanakilinda mno,na ni wachache sana wana ujasiri kuacha kazi wakajitegemee mtaani,ni kama wamelogwa na serikali, wanapenda kuajiriwa mno hata kama ni kwa kipato kidogo, as long as ana uhakika wa mshahara kila mwezi na anajua kuna mafao mwishoni ambayo hayafiki hata 200m.
Kweli. Walimu ni viumbe wa ajabu sana.
 
Taarifa zote za kiutumishi zinaanzia kwenye kituo chako cha kazi. Boss wako ama Mkuu wako wa kazi ama HR atakwambia kama kuna taarifa yoyote ya kiutumishi inakuhusu wewe ama watumishi husika kwenye kituo cha kazi A au B. Sasa inawezekana vipi wewe mtumishi unapigiwa tu simu na mtu humjui kiutumishi then unafata anachokueleza?! Sawa umemsikiliza, kwanini usiwasiliane na HR, Boss ama msimamizi wako wa kazi kuhakiki ulichoambiwa?! Kuna muda ndo maana Elimu zetu zinadharaulika sana aseeh, sasa mtumishi aliesoma adi Chuo Kikuu anakua hivi je layman wa kawaida tu ama mkulima alieko huko kijijini Mpitimbi si atatapeliwa nyumba ama hata yeye mwenyewe [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Unavyoongelea utapeli basi usihusishe TISS. TISS inajukumu moja kubwa sana kuliko chochote, kukusanya intelijensia kwa ajili na kulinda usalama wa taifa, na majukumu mengine mengi ya muhimu. Hawajamkamata huyo tapeli sababu hiyo kesi haiwahusu.

Utapeli ni petty crime maana yake sio jukumu la TISS, bali polisi. Sasa unachotakiwa kufanya ni uchukue hizo namba na ukashitaki polisi. TISS huwezi kuwaona popote na wala hawajulikani.

Usithubutu kabisa kufananisha uzito wa petty crime na kulinda usalama wa taifa au utakuwa unachafua vitu usivyovijua.
Jifunze tofauti ya vyombo vya usalama na kazi zake, sababu kamwe haziwezi kuingiliana hata iweje.
 
Heri ya mwaka mpya watu wangu wa nguvu. Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi. Naomba niseme kuwa huu ndio uzi wangu wa kwanza kwa mwaka huu wa 2024. Sikuwa nimepanga kuweka uzi hapa JF mapema hivi ila imenibidi nifanye hivyo baada ya kupokea ujumbe huu wa onyo kwa njia ya WhatsApp unaolenga kuwatapeli walimu.
1704095634241-png.2859091


Ujumbe huu umeambatana na audio ya tapeli maarufu wa mtandao ambaye amekuwa akiwasumbua sio tu walimu bali watanzania wengi, hasa watumishi wa umma. Sauti ya mtu huyu sio ngeni. Amekuwa akiwatapeli watanzania kwa muda mrefu sasa. Huenda hata wewe mwanaJF unayepitia uzi huu ulishawahi kukumbwa na dhoruba ya huyu bwana, ama akakutapeli au ukaponea chupuchupu. Sikiliza audio yake kwenye attachment hapo chini.

Kinachonisikitisha ni kuwa huyu jamaa amekuwa akiwatapeli watanzania kwa miaka mingi sasa bila kukamatwa na vyombo vya serikali. Hata TISS nao eti wameshindwa kumtia nguvuni pamoja na vifaa vyote vya kiintelejensia walivyo navyo. Ikiwa tapeli mdogo kama huyu amewashinda, je tuwaamini kulinda usalama wa nchi?

Tunaweza kusema labda polisi wa kawaida wanaodili na cybercrime hawana vifaa vya kumtafuta na kumpata. Hata TISS nao wameshindwa kweli kumtia mikononi huyu mshenzi na kumchukulia hatua za kisheria?

MAONI YANGU
Visa vingi vya utapeli wa rejareja mara nyingi vinalengwa kwa walimu. Hivi walimu wana uwezo mdogo wa kufikiri kiasi hiki hadi kila siku walengwe wao tu? Ikiwa sisi tunawategemea walimu kutufundishia watoto wetu halafu wao wanakuwa na akili ndogo ya kutapeliwa kirahisi tutarajie nini?

Ndio maana ubora wa elimu unazidi kushuka mwaka hadi mwaka kumbe ni kwa sababu elimu inatolewa na watu wenye upeo mdogo wa kufikiri. Mkuu Mpwayungu Village hawa walimu wenzako wanatuangusha sana. Nadhani baada ya kazi ya upolisi, kazi ambayo inasomba watu wasiokuwa na wito ni kazi ya ualimu. Tuna safari ndefu sana ya kufikia maendeleo ya kweli ikiwa think-tank yenyewe tunayotegemea ni ya aina hii ya walimu. Inasikitisha sana.
Ukiona polisi hawamkamati mhalifu anayejulikana basi fahamu polisi ni TRA wa
 
Hujanielewa vizuri mkuu. Nimesema huyo tapeli amekuwa akiwatapeli watu kwa muda mrefu bila kukamatwa. Huenda polisi wamemshindwa. Je, ikiwa polisi wameshindwa kwanini TISS wasiingilie kati? Wewe usalama wa nchi na raia unauchukulia kwa uzito gani? Unataka wananchi watapeliwe hadi lini ndipo hatua zichuliwe?

Wewe unaona hii ni petty crime lakini ni crime kubwa kuliko unavyodhani. Unajua huyu tapeli ameishatakatisha pesa ngapi kutoka kwa raia so far? Utakatishaji wa pesa anaufanya huyu jamaa unahatarisha usalama wa taifa. Wewe hutaki TISS waingilie kati una agenda gani na huyu tapeli sugu? Jitafakari kwanza mkuu.
Unavyoongelea utapeli basi usihusishe TISS. TISS inajukumu moja kubwa sana kuliko chochote, kukusanya intelijensia kwa ajili na kulinda usalama wa taifa, na majukumu mengine mengi ya muhimu. Hawajamkamata huyo tapeli sababu hiyo kesi haiwahusu.

Utapeli ni petty crime maana yake sio jukumu la TISS, bali polisi. Sasa unachotakiwa kufanya ni uchukue hizo namba na ukashitaki polisi. TISS huwezi kuwaona popote na wala hawajulikani.

Usithubutu kabisa kufananisha uzito wa petty crime na kulinda usalama wa taifa au utakuwa unachafua vitu usivyovijua.
Jifunze tofauti ya vyombo vya usalama na kazi zake, sababu kamwe haziwezi kuingiliana hata iweje.
 
Unavyoongelea utapeli basi usihusishe TISS. TISS inajukumu moja kubwa sana kuliko chochote, kukusanya intelijensia kwa ajili na kulinda usalama wa taifa, na majukumu mengine mengi ya muhimu. Hawajamkamata huyo tapeli sababu hiyo kesi haiwahusu.

Utapeli ni petty crime maana yake sio jukumu la TISS, bali polisi. Sasa unachotakiwa kufanya ni uchukue hizo namba na ukashitaki polisi. TISS huwezi kuwaona popote na wala hawajulikani.

Usithubutu kabisa kufananisha uzito wa petty crime na kulinda usalama wa taifa au utakuwa unachafua vitu usivyovijua.
Jifunze tofauti ya vyombo vya usalama na kazi zake, sababu kamwe haziwezi kuingiliana hata iweje.
Naamini wewe ni TISS mkuu niamini kwamba ninachoamini kuhusu wewe ni sahihi.
 
Hujanielewa vizuri mkuu. Nimesema huyo tapeli amekuwa akiwatapeli watu kwa muda mrefu bila kukamatwa. Huenda polisi wamemshindwa. Je, ikiwa polisi wameshindwa kwanini TISS wasiingilie kati? Wewe usalama wa nchi na raia unauchukulia kwa uzito gani? Unataka wananchi watapeliwe hadi lini ndipo hatua zichuliwe?

Wewe unaona hii ni petty crime lakini ni crime kubwa kuliko unavyodhani. Unajua huyu tapeli ameishatakatisha pesa ngapi kutoka kwa raia so far? Utakatishaji wa pesa anaufanya huyu jamaa unahatarisha usalama wa taifa. Wewe hutaki TISS waingilie kati una agenda gani na huyu tapeli sugu? Jitafakari kwanza mkuu.
Unajuaje polisi wamemshindwa kama taarifa yenyewe umeileta leo humu saa 11:08? Umechukua hatua gani juu ya hizo namba? Una uhakika gani kwamba labda polisi hawana taarifa za huyo tapeli kama hata wewe umeshindwa kuchukua hatua yoyote ile ikiwemo kutoa taarifa kwa hao polisi? Una uhakika gani hao waliotapeliwa hawakuwa kama wewe?

Usalama wa raia ni wa ndani na usalama wa mmoja mmoja sababu huyo tapeli hawezi dhurumu watu hata 5000 kwa wakati mmoja acha raia million 60,000,000. Na ukilinganisha huyo tapeli ahatarishi maisha ya watu kwa kifo. Hivyo hiyo hatari yake haikizi hata vigezo vya jambazi wala hata mwizi mkabaji.
Na usalama wa taifa asilimia kubwa ni nje na ni mzito zaidi sababu unahusidha raia wengi kwa maelfu, malaki na mamilion au wote kwa pamoja nchi nzima na matokeo ni vifo vya kikatili visivyohesabika. Na pia unahusisha usalama wa serikali na Rais wake kitu ambaco ni muhimu zaidi kwa nchi kuitwa mchi.

Explain kivipi utapeli wa pesa unaweza hatarisha usalama wa taifa? Hivi unatambua ni kiasi gani mafisadi wanaiba pesa serikalini? Au unamaanisha kitu usichokijua sio hatari?

Sio sitaki TISS waingilie, bali kama nilivyosema; majukumu ya vyombo kamwe hayawezi kuingiliana, na kama ikitokea basi ina maana chombo kimoja lazima kiwe labeled incompetent means kitakuwa ni useless na hakuna umuhimu wa hiko chombo kuwepo.
 
Back
Top Bottom