Polisi watia fora maandamano CHADEMA: Polisi wanaanza kuelewa kuwa upinzani siyo uadui!

πŸ“πŸ”ŠπŸ†’πŸ‘ŒπŸ‘πŸ‘ŠπŸ€πŸ‘πŸ™πŸ₯‚
 
Polisi wanaanza kuelewa kuwa upinzani siyo uadui!
Imebidi nicheke nilipokusoma mkuu 'Retired'. Naheshimu sana michango yako humu.

Huu ndio "ustaarabu" anaouzungumzia mama, na kwa bahati mbaya hata Mwenyekiti Mbowe ukamzoa.

Ni picha nzuri sana hiyo uliyoweka hapo; na bila shaka Samia naye akiiona picha hiyo atakuwa ameridhika sana na kazi yake anayoifanya sasa.
Lakini, ni kama kuna mahali humu humu JF nilimwona hivi karibuni (mwaka huu) akiweka sahihi yake kwenye sheria mpya zinazohusiana na maswala ya uchaguzi. Bila shaka nawe uliiona picha hiyo.
Ninakuomba picha hizo uziweke vizuri, kwa sababu siyo siku nyingi nitakuomba uziweke humu humu zikiwa sambamba.

Hawa polisi inawachukua muda gani kupewa amri ya kuhakikisha CCM inashinda kila mahali wakati wa uchaguzi?
Naamini nimejieleza vya kutosha kwa kifupi, sababu za kicheko kilichoniijia wakati nikisoma habari yako hii.

Naomba nieleweke vyema, sijapinga hali hii mpya, kama CHADEMA nao wanaielewa vyema na kuitumia kwa manufaa ya chama chao ipasavyo.

"Mama anaupiga mwingi."
 
Zamani mbowe alivyokua anakunywa kuonyagi akivunjika mguu anasingizia kapigwa na wasiojulikana je sahivi atamsingizia nani
 
Maandamano huleta tija idadi inapokuwa kubwa. Mfano, kila mkoa watu waandamane kumkataa kiongozi kila siku kiongozi anatoka.

Mpira ni burudani. Binadamu yoyote huburudika na kuhuzunika. Hata wewe lazima una kakitu kako ambako unakahusudu kanakupa burudani ila ni ka kipumbavu kwenye masikio ya wengine.

Unaweza kuta huwa unatazama tamthilia za mapenzi ya kikorea yaliyotafsiriwa na inakuhuzunisha au kukufurahisha kabisa. Yaani watu wamekaa kwenye chumba wanaigiza kusalitiana wewe huku una huzuni.
 
Hapana mkuu. Yaani hapa nilipo ni mtu mzima naweza hata nikawa baba yako lakini sijawahi kuelewa haya mambo ,sijui lakini labda mie ni mjinga.
Ngoja mimi nikuchangie upande wa "mpira" tu, ingawaje nashawishika sana kuingia huko kwenye maandamano, ambayo wewe umeyapa fikra nyembamba sana.

Mchezo wa mpira wa miguu; kama ilivyo michezo mingine yote, wewe huoni ufundi wowote unaotumika huko? Mtu akienda shule na kusomea uinjinia na kuwa hodari sana katika eneo hilo; bado utaona kazi yake kama ni mchezomchezo tu wa uchoraji na manamba mengi yasiyoleta maana yoyote kwako?

Hapana, nashawishika kusema kuwa huoni ufundi unaotumika katika mchezo wa mpira na kuufanya kuwa kiburudisho kwa watu wengi wengine. Hiyo ni kazi inayofanywa na wachezaji mahiri, ambao hufunzwa kazi hiyo na makocha waliofuzu katika kazi hiyo.
Hapana, siyo kwamba huoni, bali umeifanya akili yako isifanye kazi barabara kukuonyesha umuhimu wa kazi hiyo ya kucheza mpira.

Kama watu wapo tayari kutoa pesa zao mifukoni, ujue hapo kuna kazi muhimu inafanyika.
 
Hapa mbowe yupo sehemu the dons pale, anakunywa Serengeti lite ya baridiii, jana kashaingiziwa mzigo na wabelgiji,
Mwanaume kuwa mbeya mbeya utaishia kuingezewa ukubwa wa kipenyo Cha hilo TUNDU nyambafu
 
Dah roho imeniuma sana, yaani wamewaachia waandamane???? Walitakiwa wawatengue viuno kwa kipigo cha mbwa koko wahuni kabisa hawa
 
Wewe una matatizo, RWANDA baada ya kutoka vitani ilishauriwa iwe na michezo mbalimbali ili kutibu majereha mbalimbali ya mauaji, ndipo ulisikia Kagame cup, nk. Maandamano ni burudani tosha siku moja ujiunge uone utamu wake, kuwa serious muda wote sio kupata hela maisha hayako hivyo.Ila wewe ulivyo yawezekana ukipata nafasi ya kuongoza hata michezo mashuleni utapiga marufuku, TFF utaifutilia mbali, sasa si uendawazimu huo??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…