Polisi yasikitishwa na kifo cha kada wa CHADEMA, Ali Kibao. Latoa wito kwa mwenye taarifa za kweli na uhakika awasilishe kwa mujibu wa taratibu

Polisi yasikitishwa na kifo cha kada wa CHADEMA, Ali Kibao. Latoa wito kwa mwenye taarifa za kweli na uhakika awasilishe kwa mujibu wa taratibu

R.I.P muungwana Ally Kibao..

ni jambo la maana zaidi ikiwa kuna yeyote alie na taarifa sahihi za kuaminika juu ya tukio hili la kinyama dhidi ya utu wa mwanadamu, kuziwasilisha kwa vyombo vya kiuchunguzi ili hatimae hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya wahusika wa unyama huo, na haki stahiki itendeke kwa aliedhulumiwa, ikiwa kweli ipo huruma na uchungu wa dhati juu ya jambo hili baya na la aibu sana kwa Taifa..

kuficha ushahidi, kuficha ukweli au kusita kutoa ushirikiono wa taarifa sahihi za uhakika unazo zifahamu kuhusu uzandiki huu dhidi ya binadamu ni kudhulumu, ni kukandamiza haki na stahiki za almaruhum Ally Kibao, na hakika utaulizwa siki ya mwisho mbele za haki..

Once again R.I.P kamanda Ally Kibao 🤭
Umenena ukweli kabisa na sina cha kuongeza.
 
Wauaji wakubwa nyie. Hapo umefurah sana na starehe unafanya. CCM ni mashetani wakubwa.
 
Luckas ni kweli humu ndanj hatujuani lakini kuna wakati utu na ubinadamu ukujie haya mambo hayakuanza leo unaonekana kama umefanya dhihaka tunapotaniana kucheka na kukosoana ila kwa hili umenikwaza sana
Makada wanajiamini sana huku mtaani. Takribani kila kada anajisi ni wenye hati mmiliki na uhuru juu ya kila kitu - hata uhai wa wale wenye tofauti kimtizamo.
Hata Katibu Kata - CCM ana ubavu wa kuingilia msafara wa Mh. Raisi akidai kuwa ni mwenyekiti wetu; sisi ndio tunaongoza nchi.
Mwenendo wa Lucas n.k huku JF ndio hali halisi ya makada.
Kiburi cha uzima, mali na madaraka
 
Jana nimesoma Sana story ya Patrice Lumumba, hata sijui kwanini nilijukuta nairudia maana sio mara ya kwanza kuisoma, ila Jana nikajifariji kitu kimoja kwamba hawa watesi pamoja na kutesa, kudhalilisha mpaka kuua ila Vifo vyao vinakuwa vya shida zaidi, tofauti na wale waliowaua, mbaya zaidi wanawaachia familia zao aibu na kutazamwa kwa masimango, watoto/ndugu zao wanaishi maisha ya shida maana nao wanakuwa kwenye kundi la uhalifu japo pengine hawajui wala hawajashiriki.

Sisi Wakristo tunasoma kwenye biblia kwamba Mungu alimfinyanga binadamu kupitia udongo lakini kumtofautisha na viumbe wengine alitupulizia pumzi yake (Uhai) Leo mwanadamu unaamua kuitoa hiyo pumzi, sidhani kama Mungu huyu tunayemwabudu Kanisani/Msikitini atavumilia kwa muda mrefu......Rest in Power Mzee Medi.
 
Back
Top Bottom