Pongezi kwa Yanga sc na wana Yanga wote kwa ushindi mnono huko Tunis. Yanga dumuni na Kocha Nabi atawafikisha mbali

Pongezi kwa Yanga sc na wana Yanga wote kwa ushindi mnono huko Tunis. Yanga dumuni na Kocha Nabi atawafikisha mbali

ToniXrated

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
1,134
Reaction score
2,993
Igweeee igweeee!!

Napenda kwanza kukiri kuwa mimi ni shabiki kindakindaki wa Simba Sc, timu ambayo ni mahasimu wakubwa wa klabu ya Yanga hapa nchini Tanzania.

Bila ya kupoteza muda, napenda niwamwagie salamu za pongezi timu ya Yanga SC, viongozi na mashabiki wake kwa ujumla kwa kufanikiwa kufuzu kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Pongezi nyingi zaidi nazielekeza kwa Kocha Nasrideen Nabi, kwa mara nyingine ameonesha kuwa ni kocha anayelielewa soka la Afrika. Jana amewaduwaza Watunisia wenzake pale Tunis. Mashabiki wa Club Africain hawakutegemea kuiona timu yao ikicheza kama 'underdog' ndani ya ardhi yao ya Tunisia.

Yanga walipiga mpira mkubwa sana, nimekoshwa sana na uchezaji wa Sure Boy pale kati na sijui kwanini huyu jamaa anawekwa benchi pale Yanga, hata hivyo hayo niwaachie wenyewe wana Yanga.

Nabi amefundisha jinsi ya kucheza na Waarabu ndani ya ardhi yao, alichokifanya ni kuuchukua mchezo walioucheza Club Africain hapa Dar wiki moja iliyopita na kwenda kuuhamishia kwa Yanga kule Tunisia. Zile zile mbinu za kupoteza muda walizokuwa wakizitumia Club Africain ndiyo amezitumia kwenda kuwaumiza nazo pale Tunisia.

Mara zote nimekuwa nikisema kuwa mimi ni muumini wa soka la kasi, wachezaji wanatakiwa wakimbie muda wote, wakiwa na mpira au wasipokuwa na mpira. Timu yangu ya Simba ina la kujifunza kutoka kwa Yanga na naamini kuwa kama Simba isipobadili aina ya soka la kobe (polepole) inalolicheza basi Yanga wana muda mrefu sana wa kutawala Ligi Kuu ya NBC hapa Tanzania.

Yanga siyo kwamba wana wachezaji wenye vipaji sana kuliko Simba. Yanga wana wachezaji wanaocheza soka la kisasa, soka la kasi kitendo kinachofanya mpira kuwa na 'actions' nyingi ndani ya dakika 90.

Simba tuna kawaida ya kucheza soka la taratibu sana, napenda kuliita soka la kizamani kutokana na aina ya wachezaji mafaza (wasiotaka kukimbia uwanjani) tuliokuwa nao, kitendo kinachowapa wapinzani wetu kujipanga katika kujilinda na kushambulia. Kwakweli hatupo 'aggressive' kama walivyo Yanga SC.

Narudisha tena pongezi kwa Kocha Nabi kwa kutumia akili kubwa ya kumuanzisha Aziz Ki benchi, nadhani hii iliwastua pia Club Africain, hawakutegemea kukutana nalo hili. Walikutana na kiungo flani pale kati aliyewapelekesha sana, naye si mwingine bali ni Sure Boy huku juu wakikutana na Feisal sehemu waliyotegemea wangemkuta Aziz Ki.

Nabi anajua kupanga mabadiliko yenye athari, alimuingiza Aziz Ki kipindi ambacho waarabu wamechanganyikiwa kwa kuona muda unakwenda, huku hawapati walichokuwa wakikitaka nacho ni ushindi. Aziz Ki akawafunga mdomo ndani ya ardhi ya Tunis.

Mwisho napeleka wito wangu kwa Yanga SC kuwa wasijiroge kusikiliza kelele za mashabiki kuwa wamfukuze kocha Nabi. Huyu Kocha dumuni naYe hata miaka mitano, hakika atakuja kuwafikisha mbali. Viongozi muungeni mkono kipindi cha usajili ili atoe mapendekezo yake awaletee wachezaji wa maana watakaoendana na falsafa zake.

Nimekuwa kisoka nadhani kutokana na umri kunitupa mkono kiasi ya kuwa sina ushabiki maandazi wa kukandia wapinzani wetu pindi wanapofanya vizuri. Huwa napenda kuuangalia mpira katika taswira tofauti na ya kishabiki.

Asanteni kwa kuwa nami.
 
Nakuunga mkono..hongera sana kwao,hii ni move nzuri kwa soka la bongo..imefika kipindi timu ikisikia imepangwa na team ya Tanzania iogope kama sisi tulivyokuwa na mentality ya kuwa tukikutana na team za kaskazini (waarabu) basi tunaenda kuchezea kipondo..hongera sana watani wa matopeni,mihogo oyeee!
 
Igweeee igweeee!!

Napenda kwanza kukiri kuwa mimi ni shabiki kindakindaki wa Simba Sc, timu ambayo ni mahasimu wakubwa wa klabu ya Yanga hapa nchini Tanzania.

Bila ya kupoteza muda, napenda niwamwagie salamu za pongezi timu ya Yanga SC, viongozi na mashabiki wake kwa ujumla kwa kufanikiwa kufuzu kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Pongezi nyingi zaidi nazielekeza kwa Kocha Nasrideen Nabi, kwa mara nyingine ameonesha kuwa ni kocha anayelielewa soka la Afrika. Jana amewaduwaza Watunisia wenzake pale Tunis. Mashabiki wa Club Africain hawakutegemea kuiona timu yao ikicheza kama 'underdog' ndani ya ardhi yao ya Tunisia.

Yanga walipiga mpira mkubwa sana, nimekoshwa sana na uchezaji wa Sure Boy pale kati na sijui kwanini huyu jamaa anawekwa benchi pale Yanga, hata hivyo hayo niwaachie wenyewe wana Yanga.

Nabi amefundisha jinsi ya kucheza na Waarabu ndani ya ardhi yao, alichokifanya ni kuuchukua mchezo walioucheza Club Africain hapa Dar wiki moja iliyopita na kwenda kuuhamishia kwa Yanga kule Tunisia. Zile zile mbinu za kupoteza muda walizokuwa wakizitumia Club Africain ndiyo amezitumia kwenda kuwaumiza nazo pale Tunisia.

Mara zote nimekuwa nikisema kuwa mimi ni muumini wa soka la kasi, wachezaji wanatakiwa wakimbie muda wote, wakiwa na mpira au wasipokuwa na mpira. Timu yangu ya Simba ina la kujifunza kutoka kwa Yanga na naamini kuwa kama Simba isipobadili aina ya soka la kobe (polepole) inalolicheza basi Yanga wana muda mrefu sana wa kutawala Ligi Kuu ya NBC hapa Tanzania.

Yanga siyo kwamba wana wachezaji wenye vipaji sana kuliko Simba. Yanga wana wachezaji wanaocheza soka la kisasa, soka la kasi kitendo kinachofanya mpira kuwa na 'actions' nyingi ndani ya dakika 90.

Simba tuna kawaida ya kucheza soka la taratibu sana, napenda kuliita soka la kizamani kutokana na aina ya wachezaji mafaza (wasiotaka kukimbia uwanjani) tuliokuwa nao, kitendo kinachowapa wapinzani wetu kujipanga katika kujilinda na kushambulia. Kwakweli hatupo 'aggressive' kama walivyo Yanga SC.

Narudisha tena pongezi kwa Kocha Nabi kwa kutumia akili kubwa ya kumuanzisha Aziz Ki benchi, nadhani hii iliwastua pia Club Africain, hawakutegemea kukutana nalo hili. Walikutana na kiungo flani pale kati aliyewapelekesha sana, naye si mwingine bali ni Sure Boy huku juu wakikutana na Feisal sehemu waliyotegemea wangemkuta Aziz Ki.

Nabi anajua kupanga mabadiliko yenye athari, alimuingiza Aziz Ki kipindi ambacho waarabu wamechanganyikiwa kwa kuona muda unakwenda, huku hawapati walichokuwa wakikitaka nacho ni ushindi. Aziz Ki akawafunga mdomo ndani ya ardhi ya Tunis.

Mwisho napeleka wito wangu kwa Yanga SC kuwa wasijiroge kusikiliza kelele za mashabiki kuwa wamfukuze kocha Nabi. Huyu Kocha dumuni naYe hata miaka mitano, hakika atakuja kuwafikisha mbali. Viongozi muungeni mkono kipindi cha usajili ili atoe mapendekezo yake awaletee wachezaji wa maana watakaoendana na falsafa zake.

Nimekuwa kisoka nadhani kutokana na umri kunitupa mkono kiasi ya kuwa sina ushabiki maandazi wa kukandia wapinzani wetu pindi wanapofanya vizuri. Huwa napenda kuuangalia mpira katika taswira tofauti na ya kishabiki.

Asanteni kwa kuwa nami.
Kuanzia Leo,wewe ni rafiki yangu ambaye ni shabiki wa Simba.Sitakuita Tena majina mabaya tunayowaitaga wa shabiki Hoya Hoya wa Simba.
 
Kikubwa alichopatia nabi ni kwamba alienda na approach ya kucheza. Walipokuwa na mpira walicheza sio ile unaenda kupaki basi na kutegemea counter attacks.

Wale waarabu walionekana kabisa kuwa uaezekano wao wakupata goli ni through set piece na sio open play. Kitu mimoja ambacho kwangu mie ningesema waarabu walikosea ni kutofanya high pressing especially ukizingatia wao ndio walikuwa nyumbani. Many a time the outlet ball kwa diara ilikuwa towards kibwana au morison which by the way lazima tukubali distribution nzuri ya diara.
 
Igweeee igweeee!!

Napenda kwanza kukiri kuwa mimi ni shabiki kindakindaki wa Simba Sc, timu ambayo ni mahasimu wakubwa wa klabu ya Yanga hapa nchini Tanzania.

Bila ya kupoteza muda, napenda niwamwagie salamu za pongezi timu ya Yanga SC, viongozi na mashabiki wake kwa ujumla kwa kufanikiwa kufuzu kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Pongezi nyingi zaidi nazielekeza kwa Kocha Nasrideen Nabi, kwa mara nyingine ameonesha kuwa ni kocha anayelielewa soka la Afrika. Jana amewaduwaza Watunisia wenzake pale Tunis. Mashabiki wa Club Africain hawakutegemea kuiona timu yao ikicheza kama 'underdog' ndani ya ardhi yao ya Tunisia.

Yanga walipiga mpira mkubwa sana, nimekoshwa sana na uchezaji wa Sure Boy pale kati na sijui kwanini huyu jamaa anawekwa benchi pale Yanga, hata hivyo hayo niwaachie wenyewe wana Yanga.

Nabi amefundisha jinsi ya kucheza na Waarabu ndani ya ardhi yao, alichokifanya ni kuuchukua mchezo walioucheza Club Africain hapa Dar wiki moja iliyopita na kwenda kuuhamishia kwa Yanga kule Tunisia. Zile zile mbinu za kupoteza muda walizokuwa wakizitumia Club Africain ndiyo amezitumia kwenda kuwaumiza nazo pale Tunisia.

Mara zote nimekuwa nikisema kuwa mimi ni muumini wa soka la kasi, wachezaji wanatakiwa wakimbie muda wote, wakiwa na mpira au wasipokuwa na mpira. Timu yangu ya Simba ina la kujifunza kutoka kwa Yanga na naamini kuwa kama Simba isipobadili aina ya soka la kobe (polepole) inalolicheza basi Yanga wana muda mrefu sana wa kutawala Ligi Kuu ya NBC hapa Tanzania.

Yanga siyo kwamba wana wachezaji wenye vipaji sana kuliko Simba. Yanga wana wachezaji wanaocheza soka la kisasa, soka la kasi kitendo kinachofanya mpira kuwa na 'actions' nyingi ndani ya dakika 90.

Simba tuna kawaida ya kucheza soka la taratibu sana, napenda kuliita soka la kizamani kutokana na aina ya wachezaji mafaza (wasiotaka kukimbia uwanjani) tuliokuwa nao, kitendo kinachowapa wapinzani wetu kujipanga katika kujilinda na kushambulia. Kwakweli hatupo 'aggressive' kama walivyo Yanga SC.

Narudisha tena pongezi kwa Kocha Nabi kwa kutumia akili kubwa ya kumuanzisha Aziz Ki benchi, nadhani hii iliwastua pia Club Africain, hawakutegemea kukutana nalo hili. Walikutana na kiungo flani pale kati aliyewapelekesha sana, naye si mwingine bali ni Sure Boy huku juu wakikutana na Feisal sehemu waliyotegemea wangemkuta Aziz Ki.

Nabi anajua kupanga mabadiliko yenye athari, alimuingiza Aziz Ki kipindi ambacho waarabu wamechanganyikiwa kwa kuona muda unakwenda, huku hawapati walichokuwa wakikitaka nacho ni ushindi. Aziz Ki akawafunga mdomo ndani ya ardhi ya Tunis.

Mwisho napeleka wito wangu kwa Yanga SC kuwa wasijiroge kusikiliza kelele za mashabiki kuwa wamfukuze kocha Nabi. Huyu Kocha dumuni naYe hata miaka mitano, hakika atakuja kuwafikisha mbali. Viongozi muungeni mkono kipindi cha usajili ili atoe mapendekezo yake awaletee wachezaji wa maana watakaoendana na falsafa zake.

Nimekuwa kisoka nadhani kutokana na umri kunitupa mkono kiasi ya kuwa sina ushabiki maandazi wa kukandia wapinzani wetu pindi wanapofanya vizuri. Huwa napenda kuuangalia mpira katika taswira tofauti na ya kishabiki.

Asanteni kwa kuwa nami.
Pamoja na yote lakini Nabi pia akubali kuwa yeye ndiye aliyechangia wana Yanga kutolewa klabu bingwa. Kwasababu ya makosa yake kiufundi. Kwanini?
Mosi ni kitendo chake cha kuwachezesha Aucho na Feisal kwenye eneo la kiungo. Hii pair ya kiungo ni ajabu inafanywa kwenye michezo mikubwa ya kimataifa lakini hauoni ikifanyika kwenye michezo ya ligi kuu. Laiti kama ingekuwa ndio wanaocheza kwenye ligi kuu tungesema kaona ni partnership nzuri kwenye safu ya kiungo lakini kocha kaamua kucheza kamari anaacha kuwachezesha viungo ambao wanajulikana ndio walioifanya Yanga waonekane imara msimu uliopita. Aucho & sure boy au sure boy & Bangala au Bangala & Aucho. Lakini yeye kaja na kituko cha kulazimisha Aucho na Feisal wakati unae Sure boy.

Pili ni kitendo cha kulazimisha Lazima Aziz K aanze nalo limekuwa ni tatizo, mechi tatu zote ni makosa ya kimfumo na uchaguzi wa wachezaji ndio iliyoifanya Yanga kutopata matokeo. Jana Nabi karekebisha baadhi ya makosa yake ndio maana Yanga imeweza kupata matokeo. Yanga wakipata mipira wanaonekana wanatafuta kitu. Walikuwa wanashambulia kwa kasi na accuracy ya pasi ilikuwa ni kubwa.

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
 
Kikubwa alichopatia nabi ni kwamba alienda na approach ya kucheza. Walipokuwa na mpira walicheza sio ile unaenda kupaki basi na kutegemea counter attacks.

Wale waarabu walionekana kabisa kuwa uaezekano wao wakupata goli ni through set piece na sio open play. Kitu mimoja ambacho kwangu mie ningesema waarabu walikosea ni kutofanya high pressing especially ukizingatia wao ndio walikuwa nyumbani. Many a time the outlet ball kwa diara ilikuwa towards kibwana au morison which by the way lazima tukubali distribution nzuri ya diara.
High pressing ilishindikana kwa sababu pale kati walipakatwa na Sure boy, Aucho. Na kusababisha Ball possession yao kuwa very low.

Ktk mazingira haya lazima utegemee counter attack tu. Hawakuwa na option nyingine ya kutafuta goli.
 
High pressing hawakufanya sio kwa sababu ya sureboy...haikuwa strategy yao. Maana opportunity ya kufany hiyo pressing zilikuwepo.
Sure boy jana kweli aliupiga mwingi.
 
Pamoja na yote lakini Nabi pia akubali kuwa yeye ndiye aliyechangia wana Yanga kutolewa klabu bingwa. Kwasababu ya makosa yake kiufundi. Kwanini?
Mosi ni kitendo chake cha kuwachezesha Aucho na Feisal kwenye eneo la kiungo. Hii pair ya kiungo ni ajabu inafanywa kwenye michezo mikubwa ya kimataifa lakini hauoni ikifanyika kwenye michezo ya ligi kuu. Laiti kama ingekuwa ndio wanaocheza kwenye ligi kuu tungesema kaona ni partnership nzuri kwenye safu ya kiungo lakini kocha kaamua kucheza kamari anaacha kuwachezesha viungo ambao wanajulikana ndio walioifanya Yanga waonekane imara msimu uliopita. Aucho & sure boy au sure boy & Bangala au Bangala & Aucho. Lakini yeye kaja na kituko cha kulazimisha Aucho na Feisal wakati unae Sure boy.

Pili ni kitendo cha kulazimisha Lazima Aziz K aanze nalo limekuwa ni tatizo, mechi tatu zote ni makosa ya kimfumo na uchaguzi wa wachezaji ndio iliyoifanya Yanga kutopata matokeo. Jana Nabi karekebisha baadhi ya makosa yake ndio maana Yanga imeweza kupata matokeo. Yanga wakipata mipira wanaonekana wanatafuta kitu. Walikuwa wanashambulia kwa kasi na accuracy ya pasi ilikuwa ni kubwa.

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
Uko sahihi kabisa. Hakuwa na sababu yenye mashiko ya kuwaacha mafundi kama Sure Boy nje, halafu anawaanzisha akina Tuisila Kisinda ambao mfumo wa timu uliwakataa tangu mwanzo.

Wakati mwingine apange kikosi kwa ajili ya ushindi! Kama alivyofanya jana. Badala ya kupanga kikosi ili kuwafurahisha watu fulani fulani.
 
Kikubwa alichopatia nabi ni kwamba alienda na approach ya kucheza. Walipokuwa na mpira walicheza sio ile unaenda kupaki basi na kutegemea counter attacks.

Wale waarabu walionekana kabisa kuwa uaezekano wao wakupata goli ni through set piece na sio open play. Kitu mimoja ambacho kwangu mie ningesema waarabu walikosea ni kutofanya high pressing especially ukizingatia wao ndio walikuwa nyumbani. Many a time the outlet ball kwa diara ilikuwa towards kibwana au morison which by the way lazima tukubali distribution nzuri ya diara.
Pamoja mchambuzi wa mbususu
 
Pamoja na yote lakini Nabi pia akubali kuwa yeye ndiye aliyechangia wana Yanga kutolewa klabu bingwa. Kwasababu ya makosa yake kiufundi. Kwanini?
Mosi ni kitendo chake cha kuwachezesha Aucho na Feisal kwenye eneo la kiungo. Hii pair ya kiungo ni ajabu inafanywa kwenye michezo mikubwa ya kimataifa lakini hauoni ikifanyika kwenye michezo ya ligi kuu. Laiti kama ingekuwa ndio wanaocheza kwenye ligi kuu tungesema kaona ni partnership nzuri kwenye safu ya kiungo lakini kocha kaamua kucheza kamari anaacha kuwachezesha viungo ambao wanajulikana ndio walioifanya Yanga waonekane imara msimu uliopita. Aucho & sure boy au sure boy & Bangala au Bangala & Aucho. Lakini yeye kaja na kituko cha kulazimisha Aucho na Feisal wakati unae Sure boy.

Pili ni kitendo cha kulazimisha Lazima Aziz K aanze nalo limekuwa ni tatizo, mechi tatu zote ni makosa ya kimfumo na uchaguzi wa wachezaji ndio iliyoifanya Yanga kutopata matokeo. Jana Nabi karekebisha baadhi ya makosa yake ndio maana Yanga imeweza kupata matokeo. Yanga wakipata mipira wanaonekana wanatafuta kitu. Walikuwa wanashambulia kwa kasi na accuracy ya pasi ilikuwa ni kubwa.

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
Sure boy game zote Tatu za kimataifa kabla ya marudiano na Africain alikuwa majeruhi ndomana alikuwa haonekani kwenye mechi
 
Nyie mnaodiss selection ya kikosi mkumbuke kocha hufanya selection kulingana na timu anayoenda kucheza nayo.
Huwezi enda na kikosi kilekile cha siku zote utachezea kipondo mpaka basi.
 
Nyie mnaodiss selection ya kikosi mkumbuke kocha hufanya selection kulingana na timu anayoenda kucheza nayo.
Huwezi enda na kikosi kilekile cha siku zote utachezea kipondo mpaka basi.
Hata kama ila kocha kuna makosa kayafanya. Kweli Kisinda jamani Kisinda wakupewa dakika zote za kicheza nawakati tokea apewe namba hajawahi kushawishi kiwango chake.

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom