Ili akamilishe hizo ' Sifa ' zako zote ulizompa hapo inambidi pia awe ' Mzalendo ' wa kweli kwa nchi yake ya Tanzania kwa kuitangaza vyema pia huko huko alipo na siyo ' kutegea ' tu mambo ' negative ' yanayotokea huku ' Bongo Land ' kisha anayatumia kwa ' maslahi ' yake ya Kiharakati na Kisiasa CHADEMA zaidi.
Yes ni ' Mwerevu ' na ni mfano mzuri wa ' Kuigwa ' hasa kwa Watu wanaopenda kufikiri outside the box ila ana mapungufu ya Kimsingi ya kutokuwa Mzalendo, Mvumilivu, hana Staha na amewekeza sana kwa kupenda kuwa emotional hata katika mambo ambayo hayahitaji nguvu au akili nyingi kuyakabili.
Mwisho mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni na kama kawaida yangu sijaumbwa kuwa ' Mnafiki ' na huwa ' nanyooshaga ' tu maelezo ni kwamba pamoja na hayo ' mapungufu ' yake ila Mange Kimambi amesaidia sana kuwafanya ' Watendaji ' wengi kuwa makini na 'Utendaji ' wao, amesaidia kuwafanya Watanzania wawe na uwezo wa Kuhoji, Kutathmini na Kuchambua mambo kwa mapana yake lakini pia amesaidia kutufanya Sisi wana Jamii tuishi kwa nidhamu na uangalifu mkubwa ili tusije kuharibu ' Heshima ' zetu katika Jamii.
Mtazamo wangu Kwake ni kwamba Mange Kimambi ana faida nyingi kuliko hasara na ni ' mtaji ' mzuri sana kwa Serikali au Jamii inayohitaji ' maendeleo ' hasa yanayoanzia katika ' Fikra ' na kwenda katika ' Utekelezaji ' na kama akitumika kama ngazi ya kuipeleka Tanzania katika ' mafanikio ' itapendeza mno kuliko kuonekana kama ' adui ' namba moja wa nchi / taifa / Serikali.
Yangu ni hayo tu Mkuu
Akhsante na tuko pamoja Mkuu.