#COVID19 President Samia hires Tony Blair to help in the fight against COVID-19, and rebuild the country's reputation

#COVID19 President Samia hires Tony Blair to help in the fight against COVID-19, and rebuild the country's reputation

Na hizo nchi wafadhili wanakuwa hawajui kuwa kuna hizo firms na kuwa kazi yao ni kusema kinyume na uhalisia? Na hizo firm zinakuwa ni taasisi za nchi watuhumiwa kwamba wanaweka makubaliano ya mabadiliko?

Russia, China, Korea, n.k nao wanawalipa ngapi kusafishiwa image?

Kuna fundi mmoja wa viatu aliniambia, wasomi wa TZ ndio wajinga wakubwa, sikumuelewa ila kwa hiyo move, sitaki kuamini kuwa waliofanya na wanaotetea ujinga huo kuwa ni wajinga ila wanatumia MSOGA principle.

..hiyo link hapo chini ina maelezo ambayo yanatoa majibu ya maswali yanayotutatiza kuhusu pr / lobbying firms.



Cc TUJITEGEMEE, Chige, Ngungenge, Wacha1
 
Umeongea sahihi kabisa...

Lakini kwa nyongeza tu, Tony Blair Institute for Global Change is a non-profit organization, kwahiyo sidhani kama malipo yoyote tunayofanya!!

Nakumbuka back 2017 hii taasisi iliwekwa kitimoto kwa madai ya kupokea STG 9K from Saudi Arabia kama "malipo" ya kumsaidia Prince Mohammed bin Salman kufanya Saudi's Modernization Program. Hata hivyo, wenyewe wakasema hayo hayakuwa malipo bali donation, kwa sababu TBI huwa wanajiendesha kwa donations!

Sasa sioni ni namna gani wanaweza kuchukua malipo kutoka Tanzania kwa tafsiri yoyote ile, hata kwa kuita donation ikiwa pesa kutoka taifa kama Saudi Arabia tu ilionekana ni BIG ISSUE kwamba kwanini wapokee malipo wakati ni non-profit!
Unaelewaje neno Hire ?

Au walikosa kwenye Dictionary neno, kama Begged au asked ?
 
Former British Prime Minister Tony Blair has made two official visits to Tanzania since Samia Suluhu Hassan assumed the presidency in March this year after the sudden death of her predecessor, John Magufuli.

Government officials say that the Tony Blair Institute for Global Change has been hired by President Samia to handle two of her administration’s key projects: the fight against Covid-19 and rebuilding Tanzania’s international reputation.

In July, Blair paid his first courtesy call to Tanzania where he and President Samia discussed how to combat the Covid-19 pandemic.

Blair said his institute is responsible for facilitating the testing and distribution of vaccines, and may help Tanzania to access top vaccine producers.

Credits: The Africa Report

Tony Blair - Hired!l. Yaani kaajiriwa bongo.

Tony Blair - ni mwajiriwa wa PK pia ambako anasemekana kujiingizia malipo katika US $ maelfu elfu kibao.

Hapa kwetu analipwa je beberu huyu?

Kwa hili kumbe yule kiumbe m*yaji juu ya makaburi alikuwa na point ku withdraw adhima yake hiyo, japo alikuwapo kwenye kuzima mwenge 😁😁.
 
Asante Mkuu.
Nani main donors wa hii organisation?
Kwenye taarifa zao hawajataja Donors bali Partners.

Kwa maana nyingine, bila shaka kule wanakopeleka project, huwa wanapata interested partners. Kwa mfano, waliwahi kuwa (au bado wanayo) na project Burkina Faso ambako Belinda & Gates Foundation walitoa zaidi ya USD 3 Million.

Kama nilivyosema kwenye post nyingine, waliwahi kupokea controversial STG 9 Million kutoka Saudi Arabia.
 
Kwa maana nyingine, bila shaka kule wanakopeleka project, huwa wanapata interested partners. Kwa mfano, waliwahi kuwa (au bado wanayo) na project Burkina Faso ambako Belinda & Gates Foundation walitoa zaidi ya USD 3 Million.
Asante sana kwa ufafanuzi huu. Nina maswali mengi sana...ngoja nifuatilie comments za uzi huu naweza kupata majibu ya maswali yangu. Nitakayokosa, nitakutafuta tena kwenye uzi huu huu.
 
Wasomi wa kiTz bwana, eti ni donation, sio malipo. Huyu huyu alichukua hela za radar? Daaaah, sishangai kuwa hata Chenge na Obama wamesoma chuo kimoja, Chenge kasaini mikataba feki, Obama?
Kwani waliosema ni "donation" na sio malipo ni hao uliowaita "wasomi wa Tanzania"? We unaambiwa hizo pesa zilitolewa na Saudi Arabia, na walikohoji ni UK... sasa habari za wasomi wa Tanzania zinatoka wapi?

Najua tatizo lenu... ni kwa sababu tu hii habari mnaona ni kama inamsemanga JPM, and that's it! Poleni sana, manake ni nyie nyie mnaopinga hadi chanjo kwa sababu tu JPM alikuwa anakejeli chanjo!!
 
Kwani waliosema ni "donation" na sio malipo ni hao uliowaita "wasomi wa Tanzania"? We unaambiwa hizo pesa zilitolewa na Saudi Arabia, na walikohoji ni UK... sasa habari za wasomi wa Tanzania zinatoka wapi?

Najua tatizo lenu... ni kwa sababu tu hii habari mnaona ni kama inamsemanga JPM, and that's it! Poleni sana, manake ni nyie nyie mnaopinga hadi chanjo kwa sababu tu JPM alikuwa anakejeli chanjo!!
Unaamini wafuasi wa JPM wanaweza kufanya lolote kwa sasa? Hata alipokuwepo, wengi wa wafuasi wake ni wale waliokuwa wamejipanga barabarani na wale waliokuwa wakikimbiza jeneza na kutandika khanga barabarani, hawana wanachoweza kufanya zaidi ya kusubiri kudra za mtawala mwenye maono ya kuona nchi nzima ya TZ ikitoka kule ilipo na wala sio kwa hao wanaojiona wasomi kwa kukopi!

Kama uliwaona wakina January na Ridhi mtaani wakipigwa roba za mbao, basi jua nao ni wafuasi wa jiwe!

Ubaya ni kuwa, mnalazimisha nchi yenye milk teeth iwe sawa na nchi yenye zaidi ya miaka 300 ya uhuru na civilization, tena kwa kuruka hatua za ukuaji, tutoke kwenye utumwa, tuingie kwenye capitalism, tutaendelea kuwa watumwa wa kisasa wa ndani na nje ya mipaka milele amina, na MSOGA theor is making sure of that.

Samahani, Julius, Ben na John ndio maraisi waliokuwa na mwelekeo halisi, waliojua tutokapo na tupaswapo kuwa, kama ulihitaji kujua mimi ni wa muelekeo gani, basi ni huo na falsafa za hao wajuvi ni bora sana kuwahi kuwepo hapa Tanganyika kwa maoni yangu.
 
The assignment that this regime has bestowed upon Mr. Tony Blair to rebuild the Tanzania image abroad is mostly likely to be an exercise in futility.

Needless to say, President Samia Suluhu Hassan has inherited the brutal instruments of repression that her predecessor was using to torment his critics with impunity.

Worse enough President Samia Suluhu Hassan is effectively using the said instruments to perpetrate terror and violence on the limbless people of Tanzania.

Judging by President Samia's autocratic style of leadership, it won't be possible for Blair's magic to click especially to the vigilant western democracies whom had hoped that following her rise to power she would open a new chapter by abolishing the Magufuli's authoritarian policies but only to be disillusioned after realizing that the new President has chosen to perpetuate her predecessor's dictatorial rule.

Surely it won't be a bed of roses for the former British Prime Minister to teach an old dog 🐕 new tricks. President Samia will be compelled to change the way she rules so as to convince the development partners that she is not a recalcitrant girl. We shall wait to see.
 
Former British Prime Minister Tony Blair has made two official visits to Tanzania since Samia Suluhu Hassan assumed the presidency in March this year after the sudden death of her predecessor, John Magufuli.

Government officials say that the Tony Blair Institute for Global Change has been hired by President Samia to handle two of her administration’s key projects: the fight against Covid-19 and rebuilding Tanzania’s international reputation.

In July, Blair paid his first courtesy call to Tanzania where he and President Samia discussed how to combat the Covid-19 pandemic.

Blair said his institute is responsible for facilitating the testing and distribution of vaccines, and may help Tanzania to access top vaccine producers.

Credits: The Africa Report
Kwanini kazi hii lisipewe Jeshi ?
 
Hivi kweli Tanzania hatuna watu very professional and creative kufanya kazi hii!? Kweli!? Yaani hata wewe hapo , mkuu Chige na ubobezi wako kwenye masuala ya namna hii huwezi kusaidia kumuwezesha Mama atimize malengo yake kwa haraka na ufanisi kuwaletea maendeleo halisi Watanzania!? Kweli huwezi!? Aah ebu apia kama kweli huwezi!
Inategemea...

Tuchukulie muktadha wa habari yenyewe... "to help fight against COVID-19 and rebuild the country's reputation"

Tukisimama hapo, that's more than needing professionals but exposure matters!!

To rebuild country's reputation kama habari inavyosema, inahitaji zaidi ya professionals bali people with exposure!! Mtu anayeweza hata kubisha hodi na kufunguliwa mlango Bretton Woods na kufikisha ujumbe kwamba "Tanzania is reborn"!

How many professionals do we have wenye hizo sifa?

Tunaposema kusaidia kupambana na COVID-19 wala sio jinsi ya kuwahamasisha watu jinsi ya kunawa mikono bali jinsi tunavyoweza kuna na access medical stuff for COVID-19! Professional TUJITEGEMEE anaweza kutoa ushauri mzuri kabisa wa jinsi ya kupambana na ugonjwa, lakini anaweza kuwa na limited access to donors wanaosaidia kupambana na COVID-19 duniani!!

Kwa mfano nimekupa mfano wa Belinda and Gates Foundation kutoa zaidi ya USD 3 Million kwa Tony Blair Institute kwa issue ya Burkina Fasso... je, ni Tanzanian Professionals wangapi wenye uwezo wa kupiga hodi na kufunguliwa kwa mikono miwili pale Belinda & Gates Foundation!
 
Sioni jipya kwa hili la Tony Blair na Samia ni Sawa tu na kampuni ya Net Group Solution ya south Africa na awamu ya tatu ya Benjamin Mkapa. Net Group Solution ililetwa kwa gharama kubwa kwa ajili ya kuboresha shirika la Tanesco lakini badala ya ndio mambo yakaenda hovyo zaidi. Ni ujinga kuajiri watu wa nje wawafanyie kazi ambazo hata nyie mkijipanga vizuri mnaweza kufanya tena vizuri zaidi kuliko hao watu wa nje. Hiki ni kiwango cha hali ya juu ya kutojiamini kwa viongozi wetu wa juu na kutafuta short cuts ambazo hazina mashiko na hazitupeleki popote. NAONA TU HII NI NJIA NYINGINE YA UPIGAJI WA KODI ZA WANANCHI AU MIKOPO NA MISAADA TOKA NJE.

Yaani ni kichefuchefu mkuu…Sijui tumelogwa na nani
 
... yule mtu aliiharibu sana nchi! Anatafutwa expert wa kurekebisha aliyofanya "shujaa" ushujaa wa wapi huo? Nakubaliana na Dr. Anthony Diallo kwa 100%.
Mama yuko vizuri hata sisi mabavicha 2025 tunaenda na mama
 
Unaamini wafuasi wa JPM wanaweza kufanya lolote kwa sasa?
Kwani si ndo mnaoongoza kutetea YOOOOTE aliyoyaacha JPM hata kama ni ya kijinga!!
Ubaya ni kuwa, mnalazimisha nchi yenye milk teeth iwe sawa na nchi yenye zaidi ya miaka 300 ya uhuru na civilization, tena kwa kuruka hatua za ukuaji, tutoke kwenye utumwa, tuingie kwenye capitalism, tutaendelea kuwa watumwa wa kisasa wa ndani na nje ya mipaka milele amina, na MSOGA theor is making sure of that.
Ndivyo mnavyodanganyana kwa sababu Mungu Mtu wenu aliwadanganya hawezi kuwa mtumwa wa mabeberu wakati from Day 1 anaingia madarakani, hadi siku zake za kuishi hapa duniani zinaisha, HAKUWAHI HATA MARA MOJA KUKATAA CHOCHOTE TOKA KWA MABEBERU!!

Nchi iliendelea kupokea misaada toka kwa mabeberu ikiwa hadi misaada ya kijinga kabisa kama vile kujengewa vyoo!!

Nchi iliendelea kunufaika na shughuli za NGO's za mabeberu! Kwahiyo kauli kama hizo, danganyaneni wenyewe, au tafuta watu wa kuwaambia lakini sio mimi!
Samahani, Julius, Ben na John ndio maraisi waliokuwa na mwelekeo halisi, waliojua tutokapo na tupaswapo kuwa, kama ulihitaji kujua mimi ni wa muelekeo gani, basi ni huo na falsafa za hao wajuvi ni bora sana kuwahi kuwepo hapa Tanganyika kwa maoni yangu.
Sina haja ya kuwajadili hao wengine, labda uniambie wewe what's so special alichofanya JPM?! Ametuwekea mwelekeo upi?

Mwelekeo wa kuua na kufunga watu waliokuwa wanampinga?

Mwelekeo ya kutuletea watu kama akina Sabaya ambao walitumika kunyanyasa wapinzani huku wakifanya ujambazi?!

Ametuwekea mwelekeo upi hasa?!

Hivi una habari hata ile mipago aliyoifanya ni vision ya waliomtangulia, huku vision yake yeye ikiwa ni ununuzi wa ndege ambayo ni mradi wa hovyo!! Maybe Mradi wa Bwawa la Nyerere lakini wenzake pia walitaka kuwekeza huko lakini walipoona kuna gas ya kutosha, wakaona haina haja!!

Ni mwelekeo upi hasa unaosema wewe?

SGR fine lakini nao ni mwelekeo ambao uliandaliwa na waliomtangulia na yeye akaja kufanikisha tu!! Tofauti pekee, waliomtangulia walitaka kuifanya unelectrified SGR with Chinese Company being ndie mjenzi mwenyewe, yeye akaamua iwe electrified na kumpa tenda Mturuki lakini maandalizi yalianza long ago kabla hajawa waziri!!

Sasa huo mwelekeo ambao ni very special ni upi hasa?!

Btw, hivi unafahamu kwamba rushwa kubwa kubwa zote zilizowahi kutikisa taifa hili zimetokea wakati wa Mkapa unayedai eti ndo miongoni mwa walioweka mwelekeo!! Si ndo Mkapa huyo huyo ndie aliuza karibu mashirika yote ya umma, hadi TANESCO kabla haijarudi serikalini?

Lakini pamoja na madudu hayo ya Mkapa katu usimlinganishe The Late Magufuli kwa sababu Mkapa was far more visionary than Magufuli!!
 
Unaamini wafuasi wa JPM wanaweza kufanya lolote kwa sasa? Hata alipokuwepo, wengi wa wafuasi wake ni wale waliokuwa wamejipanga barabarani na wale waliokuwa wakikimbiza jeneza na kutandika khanga barabarani, hawana wanachoweza kufanya zaidi ya kusubiri kudra za mtawala mwenye maono ya kuona nchi nzima ya TZ ikitoka kule ilipo na wala sio kwa hao wanaojiona wasomi kwa kukopi!

Kama uliwaona wakina January na Ridhi mtaani wakipigwa roba za mbao, basi jua nao ni wafuasi wa jiwe!

Ubaya ni kuwa, mnalazimisha nchi yenye milk teeth iwe sawa na nchi yenye zaidi ya miaka 300 ya uhuru na civilization, tena kwa kuruka hatua za ukuaji, tutoke kwenye utumwa, tuingie kwenye capitalism, tutaendelea kuwa watumwa wa kisasa wa ndani na nje ya mipaka milele amina, na MSOGA theor is making sure of that.

Samahani, Julius, Ben na John ndio maraisi waliokuwa na mwelekeo halisi, waliojua tutokapo na tupaswapo kuwa, kama ulihitaji kujua mimi ni wa muelekeo gani, basi ni huo na falsafa za hao wajuvi ni bora sana kuwahi kuwepo hapa Tanganyika kwa maoni yangu.

Mkuu

Huyo jamaa tangu nimjue mlengo wake nimetokea
kumwona mutu wa hovyo sana......

Huyo ni msoga pure, linakujaga na hoja zake za
kutetea upuuzi, Upuuzi yaani upuuzi.....

Quote zake huwa hata sihangaiki nazo, Hili Taifa ni
Taifa la Watanzania na siyo Taifa la familia zao na
marafiki zao mabeberu.

Atakupotezea muda kwa maandishi yake marefu
na quotation za kwenye Encarta.......

Shukrani!
 
Na hizo nchi wafadhili wanakuwa hawajui kuwa kuna hizo firms na kuwa kazi yao ni kusema kinyume na uhalisia? Na hizo firm zinakuwa ni taasisi za nchi watuhumiwa kwamba wanaweka makubaliano ya mabadiliko?

Russia, China, Korea, n.k nao wanawalipa ngapi kusafishiwa image?

Kuna fundi mmoja wa viatu aliniambia, wasomi wa TZ ndio wajinga wakubwa, sikumuelewa ila kwa hiyo move, sitaki kuamini kuwa waliofanya na wanaotetea ujinga huo kuwa ni wajinga ila wanatumia MSOGA principle.
Rais SSH hayupo katika hilo kundi, elimu yake ya kuunga unga. Ana inferiority complex.
 
Kwani waliosema ni "donation" na sio malipo ni hao uliowaita "wasomi wa Tanzania"? We unaambiwa hizo pesa zilitolewa na Saudi Arabia, na walikohoji ni UK... sasa habari za wasomi wa Tanzania zinatoka wapi?

Najua tatizo lenu... ni kwa sababu tu hii habari mnaona ni kama inamsemanga JPM, and that's it! Poleni sana, manake ni nyie nyie mnaopinga hadi chanjo kwa sababu tu JPM alikuwa anakejeli chanjo!!
Kwamba nchi nzima ilimuelewa sana JPM kwenye chanjo?
 
Back
Top Bottom