Prof. Janabi apiga marufuku wagonjwa kusukumwa kwenye vitanda Muhimbili

Prof. Janabi apiga marufuku wagonjwa kusukumwa kwenye vitanda Muhimbili

Mimi sijaelewa kitu hapo....

Marehemu atafikaje kwenye gari bila kupitia kusukumwa kitandani kwanza?

Huyu anaandamwa na damu ya Chattle!

Kwa hiyo huo ndio promotion yake baada ya kazi nzito?
 
Dr janabi huwa ni mtu smart sana .......hana uswahili, hapendi shobo za kifarafara, ukimuomba nafasi ya kazi kama ipo anakupa na kama haipo ankuweza wazi......wapo marafiki zangu wengi walio pata kazi kupitia dr janabi
Kumbe kagawa kazi kwa marafiki zako, lazimq umsifie tuu.
 
Ufie wodini, mwili ubebwe na ambulance kwamba hizo gari zinaingia wodini? Najua mortuary ziko huko huko ndani ya majengo.

Hawa wasomi mbona wanatuchanganya?
Hospital ile ni kubwa umbal toka wodin had motuary n umbal wa kilometa moja au mbili au zaidi sasa ni kazi kubwa kwa muuguz mmoja kusukuma kitanda imagin labda cku iyo hilo wodi wana dead bodies zaid ya moja hiyo nenda rud huon kama ni kupoteza muda. Jaribu kulitafakari kwa upana hili jambo
 
Ameagiza miili ya marehemu kupelekwa chumba cha kuhifadhia maiti kwa gari la wagonjwa (Ambulance), badala ya utaratibu uliokuwepo wa kusukuma vitanda ili kutoa heshima kwa marehemu kwa njia hiyo.

Prof. Mohammed Janabi aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), pia amesema Wagonjwa waliotoka Kitengo cha Dharura watabebwa na gari la wagonjwa kupelekwa wodini.

Kwa mujibu wa Prof. Janabi, mabadiliko hayo yanalenga kuwapunguza kazi na mizunguko kwa Wagonjwa na Watendaji wa idara zinazopokea wagonjwa Hospitalini hapo pamoja na kuboresha huduma za Afya.

=======================

Miili ya marehemu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), sasa itapelekwa chumba cha kuhifadhia maiti kwa gari la wagonjwa Ambulance’, badala ya utaratibu wa kutumia vitanda.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Prof Mohammed Janabi, wakati alipokuwa anawaaga wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), alisema mabadiliko mengine ni wagonjwa wanaotolewa katika kitengo cha dharura watabebwa na Ambulance kupelekwa wodini.

“Ambalo tumeanza nalo leo ni kwamba bahati mbaya ikitokea mgonjwa amefariki mwili wa marehemu utachukuliwa na Ambulance kwenda kuhifadhiwa chumba cha kuhifadhi maiti.

“Wagonjwa waliotoka kitengo cha dharura watakuwa wanabebwa na gari la kubebea wagonjwa kupelekwa wodini.

“Kwa sababu ni hospitali kubwa, kwanza tutaanza kuboresha kwa wafanyakazi, itakuwa rahisi mwili kubebwa na Ambulance, kuliko kusukuma, kukiwa na vifo, mwili mmoja uko Kibasila, mwingine uko Sewahaji wanachoka wafanyakazi. Pia kutoa heshima kwa marehemu tunawahifadhi kwa njia hiyo,” amesisitiza Prof Janabi.

Amesema miongoni mwa vipaumbele vyake ni kuboresha huduma za afya na kuiendekeza Muhimbili kuwa hospitali ya Taifa.

Good job
 
Ufie wodini, mwili ubebwe na ambulance kwamba hizo gari zinaingia wodini? Najua mortuary ziko huko huko ndani ya majengo.

Hawa wasomi mbona wanatuchanganya?
Tulia kama hujui muhimbili ipoje unaweza ukaonekana una hoja na wajinga wenzako wakakuunga mkono

Ukifika muhimbili utaelewa Mkurugenzi alikuwa na maana gani ilipo mochwari ni mbali sana wafanyakazi na mwili kusukumwa mpaka huko ni kuchoka na kudhalilisha Mwili wa marehemu
 
My Professor hili mimi naona tumekimbilia kwenye jibu la kimhemko, Ambulance hazipo kubeba MAITI, hazikutengenezwa kwa ajili hiyo, Ambulance zinatakiwa zibebe wagonjwa, maiti za hospital, zipelekwe mortuary kwa vitanda, tatizo muhimbili hospital yetu miundo mbinu yake ni ovyo mno, maiti Zibebwe na gari maalum za kitengo cha police foresinc, hizi gari zimetengenezwa kwa ajili hiyo, nashangaa hadi leo police wanabeba maiti kwenye open defender huu ni unyama na ushenzi wa hali ya juu, we can buy 200 V8,lakini hatuwezi kununua hizi 2.4L special foresinc vehicles
 
Well done, big up brother
Safiii sanaaa
Ila muhimu zaidi matibabu na dawa zipatikane kwa wingi na kwa wepesi zaidi
Hasa kwa wazee na wagonjwa wote
 
Gari za kubeba MAITI ni hizi hapa
 

Attachments

  • Screenshot_20221004-140145_Google.jpg
    Screenshot_20221004-140145_Google.jpg
    104.9 KB · Views: 6
Professor nadhani angeanza na vya msingi hapo Muhimbili, kuna shida kubwa sana kwenye kupata huduma especially kama huna kitu na humjui mtu, unaweza kufa hapo wanakuangaia tu. Utaganda kwenye foleni hadi ukome, huku ukishuhudia wenzako wanakuja wanashikwa mikono na manesi wanaingizwa kwa daktari wanapata huduma na kuondoka. Yaani panatakiwa pawepo na utaratibu mzuri wa kueleweka wa kumsaidia mgonjwa na atumie uprofessor wake kutafuta muarobaini wa kupunguza hizo foleni hapo Muhimbili, watu watamuelewa ila siyo hizi siasa za kubeba maiti na ambulance kitu ambacho hakina uhalisia
 
Kwanza maiti huwa zinasukumwa kwa MACHELA MAALUMU AMBAZO ZIPO KAMA JENEZA toka wodin kwenda mortuary....kama watatumia magari itasaidia ila zile ambulance zipo busy sana aisee so ukizitumia kubebea maiti pia unaweza jikuta unashindwa kutimiza majukumu mengine unazunguka mule hospital kubeba miili maana wanaofariki wanakuwa location tofauti au waseme maiti ziwe zinaachwa mpaka USIKU ambulance ikapite kuzikusanya. So kama mtu kafariki leo na ndugu wana haraka na mwili wao kama waislamu inakuwa changamoto maana watalazimisha ambulance ikabebe maiti wakati ukute ina ratiba zingine. So ni wazo zuri ila ZISITUMIIKE AMBULANCE ILA HOSPITAL INUNUE KIGARI MAALUMU.
 
Kwa ma director wale
wa idara pale muhimbili waliojaa ukabila na umungu mtu huku hawajui chochote kuhusu tiba , sina hakika kama tutafika.Kuna wakuu wa idara na Directors wapo zaidi ya miaka 15.
 
Kwanza maiti huwa zinasukumwa kwa MACHELA MAALUMU AMBAZO ZIPO KAMA JENEZA toka wodin kwenda mortuary....kama watatumia magari itasaidia ila zile ambulance zipo busy sana aisee so ukizitumia kubebea maiti pia unaweza jikuta unashindwa kutimiza majukumu mengine unazunguka mule hospital kubeba miili maana wanaofariki wanakuwa location tofauti au waseme maiti ziwe zinaachwa mpaka USIKU ambulance ikapite kuzikusanya. So kama mtu kafariki leo na ndugu wana haraka na mwili wao kama waislamu inakuwa changamoto maana watalazimisha ambulance ikabebe maiti wakati ukute ina ratiba zingine. So ni wazo zuri ila ZISITUMIIKE AMBULANCE ILA HOSPITAL INUNUE KIGARI MAALUMU.
Ambulance zipi zipo bize mkuu?niko hapa muhimbili hizo gari zimepaki hapo emagence kuna nyingine hata kuwashwa tu haijawashwa siku mbili au tatu mpk janabi anasema hayo amejua inawetekana hajakurupuka.
 
Baada ya kuwaza kuwaboreshea huduma waliokuwa hai badala yake anawaboreshea huduma marehemu ambao wao yameshawaishia hapa duniani.........kweli maiti zinataka stara lakini waliokuwa hai ndio wanataka stara zaidi ili waendelee kubakia kuwa hai.....
 
Back
Top Bottom