Prof. Janabi: Chama cha Figo Tanzania kitawasilisha pendekezo la kuvuna Figo za Marehemu

Prof. Janabi: Chama cha Figo Tanzania kitawasilisha pendekezo la kuvuna Figo za Marehemu

View attachment 3069413

Chama cha Figo nchini kimejiandaa kupeleka mapendekezo Serikalini kuanzisha uchukuaji wa Figo kwa marehemu, ili kuongeza idadi ya wapandikiziwaji kwani wengi wanashindwa kumudu kutokana na uchache wa watoaji figo hizo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Mohamed Janabi, kwenye maadhimisho ya siku uchangiaji viungo Duniani leo Hospitalini hapo.

Source;
EATV

MY TAKE
Kwa namna yoyote hali hii ikipita inaweza kuleta mtafaruku kwenye kuvuna hizo FIGO kwa marehemu au watu kumaliziwa wakiwa wodini ili wawahishe FIGO kwa wahitaji.
Ukatili ,tusikubali huu ushauri wa kihuni
 
hili jambo lina ukakasi kidogo.
Unapochukua Figo ya marehemu alafu ukaitumia kupata hela alafu ndugu wa marehemu mkashindwa kuwapooza hyo sio sawa.mnakuwa mnawaibia.
Watapoozwa kama marehemu alisema hivo lakini kwa nijuavyo huwa ni Donation hivo ndugu hawatopata chochote. Na kwanini wapate wakati na wao kila mmoja ana figo mbili,

Hapa Tanzania kila ukoo una wato si chini ya laki moja. Sasa tuseme wazima ni elfu moja, figo elfu moja kila mmoja akiuza yake wanaanzisha kampuni kubwa sana
 
Kawaida mtu mwenyewe kabla hajafa anasema kuwa viungo vyake vitumike kuokoa maisha ya watu wengine. Na hilo linawekwa kisheria. Uhuni unaweza kufanyika lakini si rahisi.
Ni kweli ila kwa ridhaa yako unaacha usia
Kama itakubalika basi inaweza kuwa biashara haramu kubwa sana mpaka kwa majirani wakihitaji
Au kama itahitajika haraka na hakuna kwenye bank ya viungo basi watachomoa hata mtu alie hali na kummaliza
India wana mchezo huo sana, tuombe isije kutokea na kwetu
Itabidi tuwe tunawafuta wagonjwa mpaka ndani
 
hili jambo lina ukakasi kidogo.
Unapochukua Figo ya marehemu alafu ukaitumia kupata hela alafu ndugu wa marehemu mkashindwa kuwapooza hyo sio sawa.mnakuwa mnawaibia.
Haicbukuliwi kimagendo. Ni lazima marehemu kabla hajafa awe ameruhusu hilo jambo kwa kuandika. Kinyume na hapo ni wizi na kumdhulumu marehemu. Ndivyo wanavyofanya huko mbele
 
ila njaa ni mbaya sana.....kila mtu alipewa figo yake asa kwanini utamani ya marehemu alafu uiuze 😀😀😀🤓aya bhana
 
Sasa si mpaka ndugu wakubali
Mbona wanalazimisha ku donate
Kwani wao hapo wanapo toa huduma wanatoa bure

Ova
Kweli mkuu, hawana haki ya kuchukua bila maelekezo ya mwenye viungo au ndugu, vingonevyo ni wizi kama wizi mwingine tu hata kama mtu kafa
Wanachukuaje viungo kwa lazima kisa mtu kafa?
Kesho watauwa kisa Figo
 
This is what I expect toka kwa wabongo. Mnataka organ na huduma bure no wonder hospital zinafungwa kwa kuzidiwa gharama za uendeshaji. Janabi atapiga kelele bure tu.
Hao hawajawah kuumwa waache
 
View attachment 3069413

Chama cha Figo nchini kimejiandaa kupeleka mapendekezo Serikalini kuanzisha uchukuaji wa Figo kwa marehemu, ili kuongeza idadi ya wapandikiziwaji kwani wengi wanashindwa kumudu kutokana na uchache wa watoaji figo hizo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Mohamed Janabi, kwenye maadhimisho ya siku uchangiaji viungo Duniani leo Hospitalini hapo.

Source;
EATV

MY TAKE
Kwa namna yoyote hali hii ikipita inaweza kuleta mtafaruku kwenye kuvuna hizo FIGO kwa marehemu au watu kumaliziwa wakiwa wodini ili wawahishe FIGO kwa wahitaji.
Ni kweli Bongo hakuna uaminifu watu wataanza kupewa sumu wodini wafe ili wapige dili figo
 

Chama cha Figo nchini kimejiandaa kupeleka mapendekezo Serikalini kuanzisha uchukuaji wa Figo kwa marehemu, ili kuongeza idadi ya wapandikiziwaji kwani wengi wanashindwa kumudu kutokana na uchache wa watoaji figo hizo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Mohamed Janabi, kwenye maadhimisho ya siku uchangiaji viungo Duniani leo Hospitalini hapo.

Source: EATV

MY TAKE: Kwa namna yoyote hali hii ikipita inaweza kuleta mtafaruku kwenye kuvuna hizo FIGO kwa marehemu au watu kumaliziwa wakiwa wodini ili wawahishe FIGO kwa wahitaji.
da!!!
 
Kweli mkuu, hawana haki ya kuchukua bila maelekezo ya mwenye viungo au ndugu, vingonevyo ni wizi kama wizi mwingine tu hata kama mtu kafa
Wanachukuaje viungo kwa lazima kisa mtu kafa?
Kesho watauwa kisa Figo
Ah kabisa mambo ya kulazimisha kudonate wapi na wapi

Ova
 
Naanza kumpinga mwenyewe hapa hapa.

Wazo lake ni jema sana sema tumegumbwikwa na ufisadi na uroho mnoo

Imagine ni lini umeenda hospital ukaptiwa damu Bure?

Kila Leo watu wanajitoa damu Bure lakini ukienda unauziwa Tena Hela ndefu!!

Hii Nchi hapana Wacha nizikwe na viungo vyangu vyote tu hawana utu.
Organ donation ni jambo jema na Janabi ana wazo zuri ila kalileta kwenye jamii ya watu ambao bado wako stone age. He's up for an uphill battle.
 
Hapana sio kwa stone age.......

Sote tunafahamiana namna wabongo tulivyo obsessed na mambo ya pesa na mipango ya pesa.

Inaweza kuwa na malengo mazuri kuokoa maisha ya ndugu zetu wanaougua hayo maradhi lakini.

Ikaaribiwa na wachache watakaoweka mbele maslahi yao
Mkuu Wala usiende maili buku mbele jiulize tu kwanini damu tunauziwa na Ili Hali Kuna watu wanajitolea Bure kabisaa damu Yao?

Lini umeenda hospital ukakuta damu zipo za kutosha na wanatoa Bure?
 
Back
Top Bottom