Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
ukiwekewa ushahidi wa vijana kulipwa ili wakapige mayowe kwenye ubalozi wa S.Africa utakuwa tayari kujiondoa jf ?Huu umbeya sasa, unajishushia hadhi yako kama kiongozi wa JF, yaani walipwe watu pesa waandamane?
Kumbe, hapa stori kwa macho ya TheCitizen
"The story behind ATCL plane seizure in South Africa"The story behind Air Tanzania plane seizure in South Africa
Fresh details have emerged on a decades-long legal tussle between the Tanzanian government and a retired white farmer that led a South African court to order the seizure of an Air Tanzania...www.thecitizen.co.tz
Kumbe aliahidiwa kufidiwa pesa yake tangu mwaka 2014 lakini hakupata chake.
Sijui kama ni kweli.
Ila kwa nini hawakumaliza deni?
Kama ni kweli - basi. Tusishangae.
Tanzania ni taifa la wapumbavu sijawahi kuona
Msamiati wa "hujuma za mabeberu" umepamba moto siku za karibuni kuvuta "hisia za kizalendo".Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi Kabudi amesema ndege ya Tanzania Bombardier Q400 iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni imekamatwa nchini Canada na kesi ipo Mahakamani
NDEGE NYINGINE YA TANZANIA YAKAMATWA CANADA
- Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi amesema ndege aina ya Bombardier Q400 imekamatwa
- Ndege hiyo iliyokuwa iwasili nchini hivi karibuni imekamatwa na kesi ipo Mahakamani
"Mhe. Rais ndege yetu aina ya Bombadier ambayo ilipaswa ifike Tanzania kutokea Canada imekamatwa na mtu yule yule ambaye aliikamata ndege yetu kule Afrika ya Kusini." - Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje.
======
Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amesema ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400 imakamatwa nchini Canada.
Amesema aliyesababisha Bombardier kukamatwa ni Hermanus Steyn, raia wa Afrika Kusini ambaye alifungua kesi ya madai Mahakama Kuu nchini Afrika Kusini akidai fidia ya dola 33 milioni.
Kesi hiyo ilisababisha Mahakama hiyo kuizuia ndege ya Tanzania aina ya Airbus A220-300 kuondoka nchini humo Agosti, 2019.
Steyn, anadai fidia baada ya mali zake kutaifishwa na Serikali ya Tanzania mwaka 1980. Hata hivyo, Septemba 3, 2019 mahakama hiyo iliamuru ndege hiyo iliyokuwa imezuiwa katika uwanja wa ndege wa Oliver Tambo kuachiwa baada ya Serikali kushinda kesi bila kutoa fedha yoyote.
Akizungumza leo Jumamosi Novemba 23, 2019 mjini Dodoma katika hafla ya kuapishwa kwa mabalozi, Profesa Kabudi amesema, “ndege imekamatwa na kesi ipo mahakamani. Aliyesababisha ni yuleyule (Steyn) aliyesababisha ndege yetu kuzuiwa Afrika Kusini.”
Profesa Kabudi amesema kuendelea kwa vitendo hivyo ni hujuma za mabeberu wasiofurahishwa na maendeleo nchini.
Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli aliyewaapisha mabalozi hao, Profesa Kabudi amesema, “tulikwenda mahakamani tukamshinda (Afrika Kusini) akakata rufaa na wiki iliyopita tukamshinda tena, huyohuyo sasa amekimbilia Canada amekamata ndege ya Bombardier Q400 ambayo ilikuwa ifike nchini.”
“Jambo linalosikitisha ndege zilizokuwa zinatoka Marekani aina ya Dreamliner mbili hazikukamatwa zimefika lakini kila ndege inapotakiwa kuondoka Canada tunashangaa hao matapeli wanajuaje na ndege zinakamatwa.”
Amesema Balozi wa Tanzania nchini Canada aliitwa nchini na kuelezwa jinsi nchi isivyofurahishwa na kukamatwa kwa ndege zake kila zinapokaribia kuja kuondoka nchini humo.
“Nimemwambia sio tu kwamba tunasikitika bali tunakasirishwa, na tunafikiri mheshimiwa rais kukushauri kama Canada inaendelea kuruhusu vitu kama hivyo sio wao peke yao wanaotengeneza ndege, hatukufanya makosa kununua ndege Canada, hata Brazil wanatengeneza ndege,” amesema Profesa Kabudi.
Amesema wameandaliwa wanasheria kwenda Canada kuipigania ndege hiyo.
Kushikiliwa kwa ndege hiyo kunarejesha kumbukumbu ya ndege nyingine ya Tanzania aina ya Bombardier Q400-8 iliyozuiwa nchini Canada mwaka 2017 kutokana na madai ya Sh87.3 bilioni zilizokuwa zikidaiwa na kampuni ya kikandarasi.
Mabalozi walioapishwa katika hafla hiyo ni Meja Jenerali Anselm Shigongo Bahati (Misri), Mohamed Abdallah Mtonga (Abu Dhabi), Jestas Abouk Nyamanga (Ubelgiji), Ali Jabir Mwadini (Saudi Arabia) na Dk Jilly Elibariki (Burundi).
Chanzo: Mwananchi
Tanzania maandamano yamekatazwaKuandamana wana haki. Wapeleke taarifa police, kisha police watautaarifu ubalozi kuhusu protesters na dhumuni Lao, halafu watafanya maandamano yao. Kwenda ubalozini bila kuwataarifu utachukuliwa ni uvamizi, na mtambue hawa si kama South Africa waliowaonea aibu. Vienna convention ya diplomatic relations itadeal na nyinyi labda mjitoe UN, vinginevyo mjiandae kushughulikiwa.
Maandamano ya kuleta watu kwa malori yaliyoratibiwa na bashite yanaruhusiwaTanzania maandamano yamekatazwa
Yes, kule kuminya nyongeza ya mishahara ya wafanyakazi ni kwaajili ya kununua ndege ambazo hazikupangiwa bajeti.Sijui kwa nini, yaani naona sawa tu haya madege kukamatwa! Ni kipaumbele cha mtu mmoja, bunge lenyewe pengine halipitishi hiyo baketi ya kununua madege! Mkulima asipangiwe cha kufanya......
Hawa wanyama pori hawatakuelewa mzalendo wetu. Moyoni mwao ni wafu.Kweli wabongo wafadhilaka wapundaka acheni chuki linapokuja suala la utaifa ni lazima tuache tofauti zetu tuwe kitu kimoja ndio maana wazungu ni rahisi sana kututawala sababu wanajua visokorokwinyo ni wengi hata maandiko matakatifu yanasema it’s better to have hundreds enemy’s than having one fool brother ndio maana wakoloni ilikuwa rahisi kututawala
Sasa huo ushahid umeuficha uvunguni ili mimi nijiondoe JF? Watanzania wengine mnafurahisha sana. Wacha majungu weka ushahidi.ukiwekewa ushahidi wa vijana kulipwa ili wakapige mayowe kwenye ubalozi wa S.Africa utakuwa tayari kujiondoa jf ?
Wapinzani wanararuliwa risasi na mapanga, wamejaa magerezani. Umoja na uzalendo huo utatoka wapi mkuu?.
Napenda kuona viongozi wa upinzani na wa chama tawala wakiraruana kwa hoja nzito kwa maendeleo ya watanzania tupingane, tukosoane tusemane kwa mambo yetu ya ndani na lengo likiwa moja tu kutaka Tanzania mpya ya maziwa na asali.
Very trueNapenda kuwaambia hawa mazulumati haki za watu hazipotei tawala upita lkn taifa halipiti udumu milele.Awamu zijazo zitakuja kulipa madeni yote yaliyosababishwa na awamu ya hasara.Watu wametunza vielelezo wote waliobomolewa nyumba zao,fukuzwa kazi,bambikwa uhujumu uchumi,taifishiwa mali zao,wariporwa hela na mali zao,nk hawa wanasubiri ipite awamu hii ya kibabe itaingia ya waungwana hapo ndipo serikali itakoburuzwa Sana mahakamani watu wakidai haki zao.Tunaliona awamu zijazo zitapata tabu sana kulipa madeni.Kama ambavo mkulima anapigania haki yake
Hivi balozi anakuwa anafahamu kila kitu au ni baada ya miti kuteleza sasa tunaomba kwa style hiyo, make sidhani kama ni serikali ya Canada ndiyo imeikamata, bali ni mahakama. sasa Hapo hawoni kwamba Muhimili huo utakua unaingilia mambo ya Mahakama au wanadhani ni kama kwetu?
Asante kwa kutukumbusha hata hao wadai kodi nao wamenyookaHizo Habari ndio mnazipenda badala ya kushughulika na Ada na kodi za January