Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 78,790
- 128,275
Dawa ya deni kulipa, isiposhikwa hii ndege unaweza kusikia jengo la ubalozi linapigwa mnada.Habari
Nimeumizwa sana na taarifa toka kwa waziri kabudi.
Hii imenifanya niwaze mambo machache ambayo nahitaji tuyaongee hapa
Mimi ni mlipa kodi mwaminifu kwasababu nakaywa TAX katika mshahara wangu kwahiyo ndege hii inajasho langu.
Naomba kwanza niiombe serikali ikae ipitie mikata ba ya kununua vitu toka nje.
Nadhani ndege au chochote kianze kuhesabika kuwa mali yetu pale kitakapotua katika Ardhi ya Tanzania.
Kwanini iwe hivyo, hii itafanya wale wanaodai kama wanamambo yeyote yale washike ndege zitakapokuwa zinafanya service sio zikiwa katika manunuzi.
Pili. Serikali ikabidhi au iingie ubia na kampuni ya ATCL na ndege kwa kukodiwa na shirika hilo ili serikali ijinasue na kushikwa shikwa kwa vyombo hivi. Yaani ikiwa huyo mdai anaidai Tanzania kama serikali basi aishike serikali sio kampuni iliyokodishiwa kifaa.
Serikali ijiondoe kununua ndege kwenye nchi ambazo zinaroho ya korosho yaani wanakuuzia kitu bado wanaona wivu . Canada wameonesha upuuzi mkubwa sana .
Ndege imeagizwa bado inatengenezwa alafu mtu anakuja kushika kiwandani unamruhusu kwasababu tu inaalama za Twiga na ATCL?
Hivi nikipeleka gari langu garage mtu aweza lishika garage kama nadaiwa na mwenye garage akampa? Hii inaonekana hicho kiwanda wanamawasiliano na hao mabebelu.
Itoshe serikali kuchukua fedha zetu tukanunue kwingine waachiwe ndege yao.
Mwisho
Hata kama serikali awamu ya kwanza iliingia kwenye madeni hayo ambayo kwangu siyajui terms and conditions zake niwasihi kwa hekima kama watanzania tulivyo na uungwana . Hebu tujinyime tulipe deni hilo.
Hawa wazungu sio watu wa kuwachekea mimi nawachukia sana siwapendi kabisa .
Alafu wale wanaoshabikia hii mimi najikia vibaya sana sio jambo jema. Haya ni maendeleo yetu sisi sio ya mtu mwingine labda kama hutoagi kodi.
Kwa nini unataka kuishi kwa ujanjaujanja wakati dawa ya deni ni kulipa?