Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

Prof. Kitila Mkumbo: Ushauri wa Kishujaa umesababisha Tanzania ishtakiwe katika Mahakama za Kimataifa. Wasomi wetu waliwadanganya Viongozi

Amesoma kesi zilizopo huko kwenye mahakama za usulihishi na kuishia hapo tu. Angeelezea na sababu za hizo leseni kufutwa pia.

Huko Nachingwea mtu kapewa leseni kafanya utafiti kidogo tu, sijui hana hela eneo kalitekeleza miaka kisa ana mining licence; alitaka serikali imuachie tu eneo kwa utashi wake huyo mwekezaji uchwara.

Hizo leseni zote zilifutwa kwa sababu ya kutoendeleza hayo maeneo, serikali ikaunda kitengo cha kupambana na hizo kesi. Mwamba kafa mmevuruga wizara ya sheria hasa ofisi ya mwanasheria mkuu iliyopewa kazi ya kuangalia kesi zote sasa hivi mnataka kulaumu calculated moves za serikali iliyopita.

Kwanza ni wanasiasa wa Tanzania tu ndio wanatabia hizi nchi zilizoendelea uwezi kukuta wanasiasa wakakosoa maswala ya national Internet either serikali ipo sawa au imekosea; wanasiasa watakuwa upande wa serikali tu kwenye maslahi ya nchi.

Nchi ina waropakaji uwezi tofautisha msomi mwenye Phd na darasa la saba.
Hivi wewe unaelewa maana ya uwekezaji au unatoa hadithi za bulicheka kufanya utafiti wa madini kama lithium unajua ni million ngapi dollari unajitaji?? Mafuta tu shell walikuwa na boti inatumia dollari milioni 2 kwa siku imepaki hapo Dar kwa mwaka alafu leo unasema mwekezaji alitekeleza eneo huo ujinga ndio utakao wapa Tanzania hasara mpaka waamke. Kuwekeza maana yake ni kwamba unaweza kusubiri kitega uchumi chako kipate soko sasa kama hakuna soko unamnyanganya aliewekeza kwanza ummpe huyo aliekuja sasa wakati soko lipo ndio sababu Tanzania migogoro na wawekezaji haitoisha kama watu hawaelewi maana ya uwekezaji na haki za mtu kuwekeza. Huyo mpya mwambie awasiliane na aliewekeza kwanza na sio kumnyanganya aliewekeza kwanza na kumpa mpya kama mtwara Dangote na Azam shamba la miwa bagamoyo
 
Amesoma kesi zilizopo huko kwenye mahakama za usulihishi na kuishia hapo tu. Angeelezea na sababu za hizo leseni kufutwa pia.

Huko Nachingwea mtu kapewa leseni kafanya utafiti kidogo tu, sijui hana hela eneo kalitekeleza miaka kisa ana mining licence; alitaka serikali imuachie tu eneo kwa utashi wake huyo mwekezaji uchwara.

Hizo leseni zote zilifutwa kwa sababu ya kutoendeleza hayo maeneo, serikali ikaunda kitengo cha kupambana na hizo kesi. Mwamba kafa mmevuruga wizara ya sheria hasa ofisi ya mwanasheria mkuu iliyopewa kazi ya kuangalia kesi zote sasa hivi mnataka kulaumu calculated moves za serikali iliyopita.

Kwanza ni wanasiasa wa Tanzania tu ndio wanatabia hizi nchi zilizoendelea uwezi kukuta wanasiasa wakakosoa maswala ya national Internet either serikali ipo sawa au imekosea; wanasiasa watakuwa upande wa serikali tu kwenye maslahi ya nchi.

Nchi ina waropakaji uwezi tofautisha msomi mwenye Phd na darasa la saba.
Wewe acha kutetea ujinga kana kwamba wewe ndiye unayejua tu peke yako vipi kesi iliyosababisha ndege ya kwanza kukamatwa ilikuwaje ? Je ni utafiti?

Ama kuhusu wanasiasa kukosoa watangulizi ktk serikali mwasisi ni nani kama siyo huyo Magu unayetaka asikosolewe?

Muwe mnapima pande zote kabla ya kutoa hoja zenu.
 
Lisu unanpenda hee huyu ndo mwanasheria pekee anarikodi gan kwenye haya mambo au ndo Lesbia mwenzenu maana hamuachi kumtaja taja kila kona
Sijui hilo jina la 'zithromax' uliliokota wapi kwa akili kama unazoonyesha hapa!
Mwenye ufahamu wa mambo yanayohusu hilo jina hawezi kuwa na akili za kipuuzi namna hii.
 
Unawajua Watzn vizuri? Watzn walio wengi kwenye Uongozi Ukiwa unamshauri anaona wewe ni threat kwake Kwa hiyo hawezi fanyia kazi Ushauri wako..

Unadhani Jiwe aliposema ukinishauri ndio sifanyi aliongea uongo? Ndio hulka za Watzn hizo Kwa taarifa Yako
Hapana.

Natamani sana pangekuwepo na mada ihusuyo hili jambo la wasomi kushindwa kutimiza majukumu yao kwa nchi yao na tukaujadili kwa kina.
"Kutoa ushauri" kwa kiongozi husika hakuji kwa njia moja. Na siyo lazima iwe mtu kwa mtu..

Taratibu za uongozi wa nchi haufanyiki kiholela, ukifanywa na mtu mmoja kwa kujiamria tu anachotaka yeye. Kuna mikutano mingi tu inayofanyika huko ndani na nje ya shughuli za serikali ambako wasomi hawa wanaweza kuwasilisha mawazo yao na kuchukuliwa/kuingizwa katika taratibu za utendaji wa nchi.
Wasomi wetu wamewasilisha machapisho wapi, hata nje ya serikali yakihusu nyanja walizosomea zinazoihusu nchi yetu moja kwa moja?

Kwa hiyo, hoja yako ya "msomi kuogopa kuwasilisha ushauri kwa kuogopa kuonekana kuwa ni 'threat'" siyo sahihi.
 
Prof. Kitila Mkumbo anadai Tanzania imeshtakiwa na makampuni ya madini, na mashauri hayo yanapelekea serikali kuingia hasara.

Prof anadai Wasomi walitoa ushauri ili kuwafurahisha viongozi badala ya kuwaambia ukweli kuhusu madhara ya kuvunja mikataba ya kimataifa.


Jamani Tundu Lissu ajengewe tu mnara wa kumbu kumbu! Haya alionya hizi vimburu wanajifanya kuzungumza sasa!
 
Sijui hilo jina la 'zithromax' uliliokota wapi kwa akili kama unazoonyesha hapa!
Mwenye ufahamu wa mambo yanayohusu hilo jina hawezi kuwa na akili za kipuuzi namna hii.
Huyo ni Zinjanthropus bado hajawa binadamu
 
Hahahah mkuu sijui nicheke kwanza. Unaona Sasa, Kitila anapokosoa maamuzi ya serikali unasema sababu amekosa ulaji na mambo kama hayo. Kwanini Mpina naye akipiga kelele usione na yeye ni sababu ya kuwa nje ya serikali?

NB: Najua utasema sio mtazamo wako ila unaongelea unafiki wa Kitila kusema wenzie wakati naye amefanya kile kile. Lakini nachosema ni kwamba basi Kitila na Mpina wawe treated equally kwamba wote ni wanafiki au wote ni wapambanaji. Otherwise na wewe utaingia kwenye kundi la unafiki unalomweka kitila.

Kitila Mkumbo
Najua kwa nini huoni tofauti kati ya hao wawili.
Mimi naina tofauti kubwa sana kati yao, kama ya usiku na mchana.
 
Prof. Kitila Mkumbo anadai Tanzania imeshtakiwa na makampuni ya madini, na mashauri hayo yanapelekea serikali kuingia hasara.

Prof anadai Wasomi walitoa ushauri ili kuwafurahisha viongozi badala ya kuwaambia ukweli kuhusu madhara ya kuvunja mikataba ya kimataifa.

Duuhh mtamkumbuka sana Tundu Antipas Lissu, kile ni kichwa ambacho sijui kwann serikali inashindwa kumtumia
 
Najua kwa nini huoni tofauti kati ya hao wawili.
Mimi naina tofauti kubwa sana kati yao, kama ya usiku na mchana.
Unaweza nipa tofauti Moja?
Kikubwa nachoona Kitila alikua upinzani muda mrefu ila Mpina alikua CCM maisha yake yote so madudu yote anayajua kwa undani. Why alipokua waziri hakuchukua hatua, Leo Hana kitengo ndio alie lie? Bora kitila atajitetea alikua mgeni serikalini so asingeweza furukuta.
 
Mkuu ngoja nikueleweshe... Hayo madai ya toka mwaka 1974 yalikuwa yakilipwa kidogo kidogo kila mwaka,
Mwinyi alipunguza, Mkapa alipunguza, Kikwete alipunguza..

Sasa tukapata eti mzalendo no moja.. Akakataa.....
Kuna kesi imeisha juzi juzi, Serikali itatakiwa kulipa Billioni 290 ..kama sikosei.. Na kosa lilifanyika 2016 kwa Serikali kuchukua ardhi kwa nguvu maeneo ya Bagamoyo na kumpatia Bahresa kujenga kiwanda cha sukari..

Ile ardhi ilikuwa ya mwekezaji wa nje.. Jiwe akatuma wasaidizi wake wakafyeka kila kitu kwenye hiyo ardhi..Kisha wakampa hati mpya Bahkresa..

Hapo yote yanafanyika kwa Jiwe mwenyewe na washauri wanampamba bila kujua kwamba watu wakienda mahakamani itakuja kuleta hasara kwa Serikali
Kwanza inabidi uelewe tunajadili vitu gani. MADENI YA TAIFA (National debts) yatokanayo na mikopo sii madeni yanayojadiliwa hapa. Pili, ardhi alopewa Bakhresa ilikuwa haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 yani lilikuwa pori, ulitaka JPM afanye nini?

Kama raia wanachukuliwa ardhi zao wakishindwa kuziendeleza mnaona sawa lakini Mzungu ni kosa! Hivi nyie watu mkoje? Mmerogwa au!
 
Hizo leseni wengine walipata toka enzi za Mkapa na hakuna cha maana walichofanya.

Achilia mbali sheria na regulations mkataba pia una ‘performance clause’ umepewa eneo uchimbe madini; sio ulihodhi tu.

Uwezi kazi kwanini uachiwe umiliki tu, hizo kesi watashindwa sio kwa sababu serikali ilikosea, wameingia na kuvuruga strategy waliyoikuta na kufanya mambo kwa staili wanayoijua wao wenyewe.

Wapi umeambiwa leseni zilifutwa sababu ya performance? Umeambiwa walifuta leseni baada ya kubadili regulations mwaka 2018 so it doesn't have to do anything na performance indicators.

Kingine kama Kuna clause ya mkataba imekiukwa anaye determine ni settlement/arbitary sio mmoja wa parties. Yaani unaamka asbuhi unasema "umeniibia" unavunja mkataba? Hapana mnapeleka shauri la kuvunja mkataba na mnaeleza msingi kisheria ni upi ndio unavunja. Hata talaka husemi umemuacha mtu kichochoroni huwa mnaenda huko mahakamani.

Jamani mambo ya kitaaluma msiingize siasa.
 
Unaweza nipa tofauti Moja?
Kikubwa nachoona Kitila alikua upinzani muda mrefu ila Mpina alikua CCM maisha yake yote so madudu yote anayajua kwa undani. Why alipokua waziri hakuchukua hatua, Leo Hana kitengo ndio alie lie? Bora kitila atajitetea alikua mgeni serikalini so asingeweza furukuta.
Sikuwa na sababu ya kufanya hivyo, ingawa hilo liliniijia akilini nilipobandika hayo maneno; na bado sioni sababu muhimu ya kufany hivyo kwa sasa nikijua kwamba haya sasa yamekuwa kama malumbano na siyo mjadala tena.
 
Uwezi kazi kwanini uachiwe umiliki tu, hizo kesi watashindwa sio kwa sababu serikali ilikosea, wameingia na kuvuruga strategy waliyoikuta na kufanya mambo kwa staili wanayoijua wao wenyewe.
Imebadilika vipi wakati Kabudi Bado anaongoza timu za kufanya majadiliano ya mikataba kwenye eneo la madini. Ama unamaanisha Kabudi ni underperforming maana hata juzi mikataba imesainiwa na zile kampuni za Australia na Kabudi ndio alipewa credit.
 
Hapana.

Natamani sana pangekuwepo na mada ihusuyo hili jambo la wasomi kushindwa kutimiza majukumu yao kwa nchi yao na tukaujadili kwa kina.
"Kutoa ushauri" kwa kiongozi husika hakuji kwa njia moja. Na siyo lazima iwe mtu kwa mtu..

Taratibu za uongozi wa nchi haufanyiki kiholela, ukifanywa na mtu mmoja kwa kujiamria tu anachotaka yeye. Kuna mikutano mingi tu inayofanyika huko ndani na nje ya shughuli za serikali ambako wasomi hawa wanaweza kuwasilisha mawazo yao na kuchukuliwa/kuingizwa katika taratibu za utendaji wa nchi.
Wasomi wetu wamewasilisha machapisho wapi, hata nje ya serikali yakihusu nyanja walizosomea zinazoihusu nchi yetu moja kwa moja?

Kwa hiyo, hoja yako ya "msomi kuogopa kuwasilisha ushauri kwa kuogopa kuonekana kuwa ni 'threat'" siyo sahihi.
Wasomi waliookotwa jalalani au unazungumzia wasomi wapi??
 
Kwanza inabidi uelewe tunajadili vitu gani. MADENI YA TAIFA (National debts) yatokanayo na mikopo sii madeni yanayojadiliwa hapa. Pili, ardhi alopewa Bakhresa ilikuwa haijaendelezwa kwa zaidi ya miaka 30 yani lilikuwa pori, ulitaka JPM afanye nini?

Kama raia wanachukuliwa ardhi zao wakishindwa kuziendeleza mnaona sawa lakini Mzungu ni kosa! Hivi nyie watu mkoje? Mmerogwa au!
Mkuu kwa nchi ilivyokubwa.. JPM hakuona mapori huko mbele ya Bagamoyo.. Au Msata..?
Sasa kulikuwa na ulazima gani mpaka tunastakiwa na tunatakiwa kulipa..
 
Unaweza kuleta ushahidi ata wa picha kuonyesha hiyo migodi ikiwa imeendelezwa ata kidogo.
Sasa kesi wameshindaje kama Wana makosa? Au unadhani mahakama za nje unaweza shinda kesi bila facts on the table?

Hizo picha kama hakuna hao serikali ya Tanzania si wangeshinda kesi asubuhi tu!!

Hata ukimkuta mtu anakuibia Kuna procedure za kisheria. ukimpiga alafu ukampeleka kituoni tayari kesi inakugeukia hata kama ulikua na haki.

Tatizo lenu CCM ni kukurupuka Kila wakati badala ya kushirikisha akili. Nilishangaa sana mnabadili sheria nzito hivyo kwa hayo ya dharura? What was the rush? Kwani mkijipa wiki nzima mngepoteza Nini? Oneni Sasa mmekurupuka mnatuletea hasara.
 
Sasa kesi wameshindaje kama Wana makosa? Au unadhani mahakama za nje unaweza shinda kesi bila facts on the table?

Hizo picha kama hakuna hao serikali ya Tanzania si wangeshinda kesi asubuhi tu!!

Hata ukimkuta mtu anakuibia Kuna procedure za kisheria. ukimpiga alafu ukampeleka kituoni tayari kesi inakugeukia hata kama ulikua na haki.

Tatizo lenu CCM ni kukurupuka Kila wakati badala ya kushirikisha akili. Nilishangaa sana mnabadili sheria nzito hivyo kwa hayo ya dharura? What was the rush? Kwani mkijipa wiki nzima mngepoteza Nini? Oneni Sasa mmekurupuka mnatuletea hasara.
Wanashinda hizo kesi zama hizi tu huko nyuma hakukuwa na mambo ya hovyo; si ajabu ata awa contest hayo madai kama walivyowapa Symbion hela kirahisi tu.


Halafu sijui case gani una refer nyingine bado hazina maamuzi.
 
Wapi umeambiwa leseni zilifutwa sababu ya performance? Umeambiwa walifuta leseni baada ya kubadili regulations mwaka 2018 so it doesn't have to do anything na performance indicators.

Kingine kama Kuna clause ya mkataba imekiukwa anaye determine ni settlement/arbitary sio mmoja wa parties. Yaani unaamka asbuhi unasema "umeniibia" unavunja mkataba? Hapana mnapeleka shauri la kuvunja mkataba na mnaeleza msingi kisheria ni upi ndio unavunja. Hata talaka husemi umemuacha mtu kichochoroni huwa mnaenda huko mahakamani.

Jamani mambo ya kitaaluma msiingize siasa.
Leta huo ushahidi sheria mpya ndio zilivunja hiyo mikataba.

Sikatai serikalini kuna vimeo wengi hasa kwenye kuingia mikataba but give them some credit.

Hakuna mwekezaji wa nje anawekeza kwa muda mrefu nchi yoyote hasa kwenye developed nations bila ya kuweka ‘stabilisation clause’ wanajua government changes na mikataba yao huwa na corruption kwenye kuipata.

Hiyo clause inailinda kampuni dhidi ya sheria mpya baada ya wao kuingia kwenye mkataba, ndio sababu moja wapo iliyochelewesha majadiliano ya LNG awakutaka kuwekeza kwa sheria za Muhongo zilizopelekwa kwa hati ya dharura kwa sababu zilikuwa na mipaka ya kuvuna kutokana na recoverable reserve amount zilizopo kwenye kila kisima. Wao walitaka waendelee na sheria zilezile walizopatia vitalu.

Kwa hivyo huko serikalini wanajua sheria mpya sio applicable kwenye existing contracts, hizo aziwezi kuwa sababu za kuvunja hiyo mikataba; huyo Kitila anaropoka tu.
 
Back
Top Bottom