Tetesi: Prof. Lipumba awafukuza kazi wakurugenzi wote wa CUF

Status
Not open for further replies.
uchaguzi wa meya kinindoni na ubungo cuf wasiwaachie tena chadema wagombee wenyewe
 
Boss ebu tuongee siasa vizuri hapa. Niambie hawa wafuasi wa lipumba ni wa wapi Wa haiba ipi za siasa za tanzania) na wakati anajiuzuru walijisiaje na hatima ya chama chao ni hipi kama lipumba anarudishiwa rungu.
 
Nilitaka kusema namna hii namimi ndio maana Watawala wanamchukia nakumuita kila aina ya Majina sababu jamaa hana BEI dhoruba iliyovuma nyakati za Zitto na Slaa ilikuwa inawapeleka kubaya lkn MBOWE amebakia kuwa alama ya Kiongozi maana yakuongoza upinzani
 


Hapa inabidi busara itumike...hakuna namna...Prof. Lipumba anajua anachofanya....wakiendelea kupambana na Profesa huyu CUF itasambaratika...hakuna jinsi, huyu Profesa ni mjanja na anatumia usomi wake katika kuendesha mapambano...duh, sijui mwisho wa 'ngoma' hii...
 
Boss ebu tuongee siasa vizuri hapa. Niambie hawa wafuasi wa lipumba ni wa wapi Wa haiba ipi za siasa za tanzania) na wakati anajiuzuru walijisiaje na hatima ya chama chao ni hipi kama lipumba anarudishiwa rungu.

Mimi si msemaji wao mkuu
sanasana nina speculate tu kama wengine kwa mujibu ninavyo ona
binafsi naamini asingekuwa na wafuasi asingepata wabunge
na wale wote waliomsindikiza hadi Buguruni kwenye ofisi za chama...

Kama wote wale 'kawanunua ' basi tatizo letu TZ ni kubwa saana
 
Wanyamwezi ni wasaliti sana fuatilia mkoa wa tabora kama kuna upinzani labda kidogo kaliua halafu angalia maendeleo wengi ni waendesha baiskeli njaaa kali kwa hiyo sitishangaa huyo jamaaa kutumiwa kama kondom

Heeeeee umeshahusisha ukabila?????!!!!!!wewe ni kabila gani, hata uanze kuponda Wanyamwezi wote kwa mambo haya...futa usemi au kauli yako...Tkukianza kuhusisha makabila na vyama vya siasa au na siasa kwa ujumla wake tutafika kweli????
 
Kama msajiri wa vyama vya siasa anampenda lipumba akae nae ofisini anywe nae chai lakini sio kumrudisha CUF huyu aliandika barua kwa hiyari yake kuachia nafasi aliyokuwa nayo; Jaji mutungi hakumbuki hili, hivi tukisema anakuja kumalizia kazi aliyotumwa na CCM tutakuwa tumekosea; wana CUF msikubali lipumba arudi alipotoka
 
Haaah professor, njaa ,uchwara ,uchu wa madaraka ,kibaraka wa ccm
Kweli kuna kazi nchi hii!!
Mkuu tena ana njaa kali sana. Nawahusia wana CUF wasikubali huyu msaliti na anakuja kuua chama katumwa na CCM
 
rasmi 25/09/2016 kwa 9:15 mu · Jibu

Hivi ccm wanafikiri kufanya hivi ndio kutapunguza kasi ya mabadiliko Zanzibar!
Huyu mzee ameshajulikana atalolifanya ni kuitaambua serikali ya Dk Shein, baada ya hapo kuna wasaliti ambao wataingizwa kutoka CUF kwenye hiyo serikali ya Dk Shein kuonyesha kwamba ina uhalali na CUF wanaitambua.
CCM wanatengeneza tatizo jengine tu hapo hamna mafanikio watayoyapata, Lipumba na hicho kikundi chake hatokubalika Zanzibar abadan.
Kwa wakati huu wamechelewa mbinu hii ya wagawe uwatawale haifanyi kazi katika akili za Wazanzibari walio wengi…


Elbattawi 25/09/2016 kwa 11:14 mu · Jibu

rasmi

Kila mtu anayechukia ukoloni wa CCM, anafahamu fika kwamba Lipumba ana ‘issue’ kibindoni tayari alizopangiwa na CCM, anakujanazo ndani ya CUF kwa kuzitekeleza.

(l) Kutaka kuzima au kubabaisha mataifa katika madai yaliyopo juu ya meza ya wazanzibari kuhusiana na matokeo ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2015.

(ll) Kama ulivyosema kwamba atataka kuitambua au niseme atajaribu kusema kwamba uchaguzi wa marudio wa Machi 20 ulistahili kisheria na kikatiba kufanywa, hivyo ulikuwa halali. Atasema, baada ya kutafakari vya kutosha CUF, imebadilisha uamuzi wake na sasa inaitambua serikali ya Dk Shein.

(lll) Pia, ana mkakati mzito aliyopangiwa na CCM, kufumfukuza Maalim Seif na viongozi wengine (kundi lake) ndani ya CUF (this is very serious issue), kwa sababu ya kutaka kuwachanganya kimawazo au kuwababaisha wazanzibari, wanachama na wafuwasi wa CUF, juu ya mwelekeo wa Zanzibar.

Itakumbukwa mkutano wa Kiembe Samaki wa CCM, Balozi Seif Ali Iddi (Nduli) alisema nini kuhusu CUF kuwa, mwaka huu ndiyo mwisho wake. Uchambuzi wa kitaalamu wa kauli ile ndiyo haya matokeo ya sasa.

Kuna mambo mengi ya ubaya dhidi ya wazanzibari waliyoikataa CCM, Lipumba anakuja nayo kapewa kuyatekeleza. Ndiyo sababu ‘speed’ au niseme kasi ya kumrejesha imekuwa kubwa.

CCM, wanahofu na hatua zinazochukuliwa na CUF chini ya Maalim Seif kuhusu Zanzibar na Tanzania, ambayo nayo inaathirika zaidi.
Ingawa kwa sasa tunaweza tukasema kwamba, kwa hatua iliyofikiwa kuhusu masuala ya Zanzibar, CCM wananafasi finyu na ndogo mno kunusurika na mkono wa dunia. Ndiyo maana wanajaripu kupapatua kwa njia za kijasusi, kupitia uhuni wa Lipumba na gengi lake.

Inafaa tujiulize, tena tujiulize sana tangu CUF kuasisiwa, sasa ni miaka 24 kwa hesabu, lini imetokea Mwenyekiti wake, kuanzia Mapalala kupelekwa ofisini kwa vikosi vya polisi, geti la ofisi kuvunjwa, walinzi kupigwa mabomu na uhalifu mwingine kama kweli kuna nia njema huko mbele.

Kwa Wazanzibari, haya si mageni labda kwa wenzetu upande wa bara ambao wao kwao yanaweza kuwa mageni, hawaifahamu CCM hulka yake kwa undani. Ingawa sasa kidogo kidogo wameanza kupata picha. Wazanzibari chini ya CUF, wamewazoea CCM wala hawawababaishi tena.

CCM, wanaamini kuwa dunia yote ni kama vile serikali yao ilivyo, viongozi kutembea kwa ving’ora na misururu ya gari za ulinzi kuelekea katika mikutano ya kinafiki ya hadhara na kurudi majumbani, wakisubiri siku inayofuta kwenda mashamba Unguja na Pemba, kudanganya watu. Dunia haiku hivyo tena sasa, imebadilika. Sindano ikianguka mto-pepo, dakika hiyo hiyo wanaisikia waliyoko Toronto.
Umoja wa ulaya (EU) imesema kuhusu uchaguzi wa Zanzibar, Jumuiya ya Madola (Commonwealth), Marekani na Uingereza na kadhalika wote wamesema na kutokuitambua Serikali ya Zanzibar, Lipumba anarejeshwa CUF kwa mabavu na ajenda ya kigaidi. Nani atamkubali kumpokea gaidi mkuu wa wazanzibari?.

Mwaka wa kwanza Julius Nyerere, kufanya ziara Pemba, ilikuwa mwaka 1965 hapa ilikuwa ni mwaka mmoja tangu kuunda Muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Mzee mmoja mwenye asili ya Tanganyika, Ibrahim Mkumba alitunga na kughani utenzi kwa ajili ya Nyerere.

“Kila ajaye kwa shari – Aijuwa yake siri – Ivunde yake dhamiri – Asiweze kusimama.”
Maneno hayo ya ushairi yalikuwamo ndani ya utenzi uliyokuwa na zaidi ya beti 110 uliyoghaniwa na Mzee Ibrahim Mkumba aliyekuwa akiishi Chanjamjawiri, pale kwenye njia inayoelekea Skuli ya Kidongo (sasa Skuli ya Chanjamjawiri).

Kwa fumbo la kishairi la Mzee Mkumba, hatunashaka kwamba, dhamira aliyonayo ndani ya nafsi yake Ibrahim Lipumba, itamsuta na hataweza kusimama. Mwenyezi Mungu Jala Jalal, hatasimama naye, hatampa nguvu za kuweza kuwafanyia ugaidi wanzanzibari. – amin.
Wazanzibari, mjini na mashamba, Pemba na Unguja ni waelewa wa mambo yote kuhusu nchi yao. Miaka zaidi ya 50 ya Muungano ‘uchwara’ wamekumbana na mengi na sasa wamechoka kuishi katika hali ngumu ya umasikini na ufukara, hawatatetereka tena na mbinu ovu za CCM. Wazanzibari wako makni sana.
 
CUF walitenda kosa kubwa sana kupuuzia barua ya Lipumba kujiuzulu.
Ni kosa la kitechnikali,hawakufungua macho kuona mbali.
Nawaonea huruma sana,kosa hili litawatafuna kweli kweli.
 
Reactions: nao
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…