Prof. Mukandala hafai kuongoza tume ya katiba mpya

Prof. Mukandala hafai kuongoza tume ya katiba mpya

USA, UK, FRANCE, GERMANY nk ni mara ngapi wamebadirisha katiba zao tangu kuanzishwa kwake?
Kwani za kwao ni mbaya kama ya kwetu, hata walazimike kubadilisha?

Katiba za hayo mataifa zinapalilia demokrasia. Sisi katiba yetu inapalilia udikteta.
 
Tangu awali alipoteuliwa nilisema huyu siye, hiyo ilitokana na yeye kujitambulisha ni muumini wa CCM.

Hivi sasa tunashuhudia yeye akitoa maoni kuhusu kuwepo au kutokuwepo katiba mpya, yeye ni mkusanyaji maoni hivyo hatakiwi kuwa mtoa maoni na kama anataka atoe maoni basi inabidi aachie cheo cha uenyekiti aje upande wetu wa watoa maoni na si vinginevyo.

CCM ilimuweka Mukandala kwa lengo maalum la kuikwamisha katiba mpya ili hii mbovu iendelee kuwepo baada ya wao kuifanyia marekebisho wanayoyapenda, ni jukumu letu kusimama kidete na kumkataa huyu Mukandala.
Ndio maana uprofesa huu wa kipumbavu unatuletea mashaka mengi juu ya elimu yetu.Profesa anaongea utadhani mganga kienyeji na si msomi yaani hajui kama watanzania walisha ongea na wamesha ongea.Huyu binadamu hajui hayo eti ni msomi aliyewahi kuongoza USDM.Kama hawa ndio wanaitwa wasomi ni bora hata ambaye hakuingia Darasani anaweza akawa na mang'amuzi yenye akili na sio haya tunayoyaona.
 
Ndio maana uprofesa huu wa kipumbavu unatuletea mashaka mengi juu ya elimu yetu.Profesa anaongea utadhani mganga kienyeji na si msomi yaani hajui kama watanzania walisha ongea na wamesha ongea.Huyu binadamu hajui hayo eti ni msomi aliyewahi kuongoza USDM.Kama hawa ndio wanaitwa wasomi ni bora hata ambaye hakuingia Darasani anaweza akawa na mang'amuzi yenye akili na sio haya tunayoyaona.
Viongozi wa CCM wanatuona sisi mazoba ndiyo maana wanasema nyie pigeni kura sisi tutaunda serikali, na kale kamalawi nako kanasema CCM itaendelea kutawala zaidi ya miaka tisini ijayo!
 
Kwa sababu ameongea usilopenda kusikia?
Kuna wakati tusikilize na kuyafanyia kazi hata tusiyopenda kusikia.

Binafsi sihitaji katiba mpya maana naona mchakato ulioporwa na wanasiasa na kwa sasa la msingi ni watu kuuvaa uwajibikaji na kuacha ubinafsi.
Shida ya Africa sio Katiba bali ni utashi mbovu wa waAfrica, WAAFRICA BADO HAWAJASTARABIKA NA HATA UKIWALETEA KATIBA MPYA BADO TUTAONA HAIFAI TU.

TUSTAARABIKE KWANZA NA KUPENDANA WENYEWE KWA WENYEWE, HAYA YA KATIBA NI MAGUMU SANA KWETU.
Sawa mzungu
 
Kwa sababu ameongea usilopenda kusikia?
Kuna wakati tusikilize na kuyafanyia kazi hata tusiyopenda kusikia.

Binafsi sihitaji katiba mpya maana naona mchakato ulioporwa na wanasiasa na kwa sasa la msingi ni watu kuuvaa uwajibikaji na kuacha ubinafsi.
Shida ya Africa sio Katiba bali ni utashi mbovu wa waAfrica, WAAFRICA BADO HAWAJASTARABIKA NA HATA UKIWALETEA KATIBA MPYA BADO TUTAONA HAIFAI TU.

TUSTAARABIKE KWANZA NA KUPENDANA WENYEWE KWA WENYEWE, HAYA YA KATIBA NI MAGUMU SANA KWETU.
Wanataka katiba mpya iingize watu wa vyama mbalimbali au mamluki ili baadae matokeo yakitoka waseme hawakushirikishwa kwa hiyo wanajitoa. Mkitaka kujua katiba siyo suluhisho angalia uchaguzi wa Kenya.
Wanasiasa wa upinzani wanadhani katiba itakayowaingiza madarakani ndiyo itakuwa katiba bora. Mukandala akihoji wananchi wanasema hakuna haja hiyo kwa vile wananchi wengi wanasema kuna haja ya mabadiliko, upande wa pili wanasema wananchi wanataka katiba mpya.
 
USA, UK, FRANCE, GERMANY nk ni mara ngapi wamebadirisha katiba zao tangu kuanzishwa kwake?
Mfano UK unaweza kuona Waziri Mkuu anaingia madarakani baada ya aliyepo kujiuzulu bila uchaguzi na anakaa madarakani miaka mi4. Akishapitishwa tu ma malkia anaanza kazi. Halafu hao ndo wanatufundisha demokrasia!!
 
Kuna kitu kinaitwa "Civilization" sijui tuiteje kwa lugha yetu. Watu kuwa civilized inawezekana bila hizo piece of paper, ukileta pieces of paper na watu wenyewe hawajawa civilized watazichana tu na kuchambia.

Umeongelea maendeleo kuwa suala mtambuka linalohitaji factors nyingi, zipo main factors ambazo zikifuatwa kwa katiba hihii Taifa hili lazima lisonge mbele.

USA anamshutumu China kwa sheria za hovyo na Katiba mbovu lakini decipline ya chinese na ndoto zao za kutengeneza Taifa bora zimewafanya kupitia sheria na katiba hiyo hiyo kupiga hatua kimaendeleo.

Brother naomba kukwambia, TATIZO LA WAAFRICA NI UJINGA, UVIVU NA UPUMBAVU MWINGI AMBAO HAUWEZI KUACHWA KUPITIA HAYA MAKARATASI, EITHER WASTAARABIKE AU WATAWALIWE NA MIKONO YA CHUMA.
Sawa ni ujinga na upumbavu ila huo ujinga na upumbavu unaweza kunyooshwa na katiba nzuri.

Leo hii tukisema kila kiongozi atakaebainika ni fisadi atakula shaba straight away hakuna mtu ata mess up. Kiongozi yeyote akibainika kaomba rushwa au akishitakiwa kwa kuomba rushwa na ushahidi ukawepo anakula shaba rushwa itapungua by 90%. Kiongozi yeyote anayetumia madaraka kuminya haki za raia ku exercise uhuru wao kikatiba akishtakiwa na ushahidi anafutwa kazi mara moja. Kiongozi akitengeneza mikataba ya kifisadi na kuficha transparency basi hukumu yake iwe ni kutumbuliwa na asiajirike sehemu yeyote. Hakuna ku recycle watu wale wale kwenye system, habari ya mtu kufanya kazi kila awamu anahama mara mbunge, mara waziri, mara katibu mtu akishashika cheo cha umma mara moja akitoka akajiajiri.

Tunatakiwa tuwe na tume ya kulinda maslahi ya raia,haki zao na katiba. Hii iwe stand alone bila affiliation na chama na serikali kwa namna yeyote na ikibainika kuna mtu anazingua ni shaba tu. Kwa style hii tutakwenda vizuri.

Amini kwamba japo ujinga na upumbavu unasababishwa na kutokujitambua kwa raia sio raia wote ambao hawajitambui. Raia watawajibika kufanya kazi na kuchangia kodi ila system ya nchi ni lazima iongozwe na katiba na yeyote atakaevunja katiba ni shaba moja kwa moja. Huwezi ona huu ujinga ukiendelea.

Mfano mmoja ni uwepo wa Magufuli tu. Nchi ilikaa katika form baada ya yeye kuingia madarakani kwa maana kuna mambo aliyafanya yakawaogofya watu. Ajira ya serikali ilikuwa sio ya kuamini maana leo na kesho unakuwa haupo. Watu waliacha uzembe kabisa na kujitahidi kuwa serious na kazi. Ila tazama leo hayupo watu wame relax tu sababu katiba haina meno na wasimamizi ni butu.
 
Sawa ni ujinga na upumbavu ila huo ujinga na upumbavu unaweza kunyooshwa na katiba nzuri.

Leo hii tukisema kila kiongozi atakaebainika ni fisadi atakula shaba straight away hakuna mtu ata mess up. Kiongozi yeyote akibainika kaomba rushwa au akishitakiwa kwa kuomba rushwa na ushahidi ukawepo anakula shaba rushwa itapungua by 90%. Kiongozi yeyote anayetumia madaraka kuminya haki za raia ku exercise uhuru wao kikatiba akishtakiwa na ushahidi anafutwa kazi mara moja. Kiongozi akitengeneza mikataba ya kifisadi na kuficha transparency basi hukumu yake iwe ni kutumbuliwa na asiajirike sehemu yeyote. Hakuna ku recycle watu wale wale kwenye system, habari ya mtu kufanya kazi kila awamu anahama mara mbunge, mara waziri, mara katibu mtu akishashika cheo cha umma mara moja akitoka akajiajiri.

Tunatakiwa tuwe na tume ya kulinda maslahi ya raia,haki zao na katiba. Hii iwe stand alone bila affiliation na chama na serikali kwa namna yeyote na ikibainika kuna mtu anazingua ni shaba tu. Kwa style hii tutakwenda vizuri.

Amini kwamba japo ujinga na upumbavu unasababishwa na kutokujitambua kwa raia sio raia wote ambao hawajitambui. Raia watawajibika kufanya kazi na kuchangia kodi ila system ya nchi ni lazima iongozwe na katiba na yeyote atakaevunja katiba ni shaba moja kwa moja. Huwezi ona huu ujinga ukiendelea.

Mfano mmoja ni uwepo wa Magufuli tu. Nchi ilikaa katika form baada ya yeye kuingia madarakani kwa maana kuna mambo aliyafanya yakawaogofya watu. Ajira ya serikali ilikuwa sio ya kuamini maana leo na kesho unakuwa haupo. Watu waliacha uzembe kabisa na kujitahidi kuwa serious na kazi. Ila tazama leo hayupo watu wame relax tu sababu katiba haina meno na wasimamizi ni butu.

nimekuelewa sana, wenzio wanataka katiba mpya yenye sheria laini laini na urahisi kwenye uchaguzi, UKIWAAMBIA TUANDIKE KWENYE KATIBA MZEMBE, MWIZI, FISADI WAFE watakuambia haki za binadamu.

Hata Katiba mpya tuliyonayo inatoa inasema wezi washitakiwe, wazembe wafukuzwe kazi nk. Shida inakuwa kwenye utekelezaji wa hizo sheria.
 
Tatizo letu ni kudhani katiba mpya inahusu Chadema na vyama vingine kuruhusiwa kufanya siasa bila kujua katiba ni zaidi ya siasa. Katiba ndiyo inayoshikilia maisha yote ya kila siku ya wananchi, leo unakuta kidudumtu kinasema eti yeye hahitaji katiba mpya! Huyu ni mpumbavu kwani yeye anajua katiba inahusu vyama vya siasa tu bila kujua inahusu hata ndoa yake na wanawe, pia inahusu hata biashara tuzifanyazo nchini na elimu na mambo yote tuyafanyayo kila siku.
Acha kukariri. Sasa hayo ya ndoa yake na wanae kwenye katiba ya Sasa hamna?
Au kwa uelewa wenu kikosi kazi kinapaswa kukusanya maoni yale tu yanayotaka katiba mpya? Au hujui kama zaidi ya 97% ya katiba mpya yamo kwenye katiba ya zamani pia?
 
nimekuelewa sana, wenzio wanataka katiba mpya yenye sheria laini laini na urahisi kwenye uchaguzi, UKIWAAMBIA TUANDIKE KWENYE KATIBA MZEMBE, MWIZI, FISADI WAFE watakuambia haki za binadamu.

Hata Katiba mpya tuliyonayo inatoa inasema wezi washitakiwe, wazembe wafukuzwe kazi nk. Shida inakuwa kwenye utekelezaji wa hizo sheria.
Hio sheria sio kali, nani anayepaswa kusimamia hao wezi washitakiwe? Kama msimamizi anatoka CCM na analipwa na CCM kutakuwa hamna maajabu.

Wasimamizi wanatakiwa walipwe na raia na wawe chini ya wananchi ili tukipeleka malalamiko mahakamani yawe na mashiko. Shauri lisiposhughulikiwa tunakiwasha with valid reason inayotambulika kikatiba.
Hata PCCCB ingekuwa chini ya raia rushwa ingekuwa kwenye zero rate. Sasa maafisa wa TAKUKURU wanakuwa funded na serikali ya CCM ili wawakamate watumishi wa serikali we uliona wapi hilo?
 
Hio sheria sio kali, nani anayepaswa kusimamia hao wezi washitakiwe? Kama msimamizi anatoka CCM na analipwa na CCM kutakuwa hamna maajabu.

Wasimamizi wanatakiwa walipwe na raia na wawe chini ya wananchi ili tukipeleka malalamiko mahakamani yawe na mashiko. Shauri lisiposhughulikiwa tunakiwasha with valid reason inayotambulika kikatiba.
Hata PCCCB ingekuwa chini ya raia rushwa ingekuwa kwenye zero rate. Sasa maafisa wa TAKUKURU wanakuwa funded na serikali ya CCM ili wawakamate watumishi wa serikali we uliona wapi hilo?

Unachofikiri hata mimi nafikiri lakini binafsi huwa naamini kinakuwa hakipo kwenye sheria wala Katiba bali ni uchizi tu wa kiongozi mmoja ambaye anapaswa kuongoza miaka kuanzia 20 na kuendelea.

Naamini: watu wanapaswa kustaarabika kwanza na ili ustaarabu uje lazima kwanza kuwe na series ya viongozi makatiri watakaochapa watu viboko na wajitambue.
Hakuna Taifa lililoendelea duniani bila ya watu wake kupitia taabu kwanza kujijenga.
Leo hii hata ukiweka Katiba yenye sheria ngumu kwa hawa wahuni bado wataizidi ngumu na hukumu zitatoka kwa wanyonge tu.

USA sheria zilikuja na kuanza kuheshimiwa baada ya watu kushikishana adabu kwanza mitaani ili kila mtu ajue wajibu wake na kuheshimu mwenzie.
Katiba bora inahitaji ulinzi bora ili ifanye kazi na huo ulinzi bora unatokwa raia, hao raia ili wailinde lazima wastaarabike kwanza.

Chief watu wanaongea theory sana wakiamini kitabu kinaweza kujilinda bila watu, yaani meli itembee yenyewe baharini bila Captain na team yake?
 
Unachofikiri hata mimi nafikiri lakini binafsi huwa naamini kinakuwa hakipo kwenye sheria wala Katiba bali ni uchizi tu wa kiongozi mmoja ambaye anapaswa kuongoza miaka kuanzia 20 na kuendelea.

Naamini: watu wanapaswa kustaarabika kwanza na ili ustaarabu uje lazima kwanza kuwe na series ya viongozi makatiri watakaochapa watu viboko na wajitambue.
Hakuna Taifa lililoendelea duniani bila ya watu wake kupitia taabu kwanza kujijenga.
Leo hii hata ukiweka Katiba yenye sheria ngumu kwa hawa wahuni bado wataizidi ngumu na hukumu zitatoka kwa wanyonge tu.

USA sheria zilikuja na kuanza kuheshimiwa baada ya watu kushikishana adabu kwanza mitaani ili kila mtu ajue wajibu wake na kuheshimu mwenzie.
Katiba bora inahitaji ulinzi bora ili ifanye kazi na huo ulinzi bora unatokwa raia, hao raia ili wailinde lazima wastaarabike kwanza.

Chief watu wanaongea theory sana wakiamini kitabu kinaweza kujilinda bila watu, yaani meli itembee yenyewe baharini bila Captain na team yake?
Tuonyeshe mchakato wa kupata hao madikteta unafanyikaje? Na uendelevu wa kupata hao madikteta wa maendeleo upo guaranteed na nani? NADHANI WEWE NDIYE UNAYEONGEA THEORY TENA ZA KITOTO. You are kstill in your make believe world?
 
Tuonyeshe mchakato wa kupata hao madikteta unafanyikaje? Na uendelevu wa kupata hao madikteta wa maendeleo upo guaranteed na nani? NADHANI WEWE NDIYE UNAYEONGEA THEORY TENA ZA KITOTO. You are kstill in your make believe world?

Tukiwa serious tutawapata tu, ila tukiendelea na huu mzaha mzaha wakutaka piece of papers iwaongoze na sio watu wenye maono makali tutasubiri sana.
mnapaswa kushikishana adabu na kuheshimiana kwanza na mkianza kuogopana ndio mnatengeneza huo utaratibu wa kuishi.

Unafikiri mataifa ambayo watu huandamana na kusacrifice roho zao kupambania nchi zao na viongozi wenye misimamo mikali ni wajinga.

Chief chukua huu mfano: Wewe unataka Katiba mpya na CCM wenye nchi hawaitaki kama walivyofanya mwanzo, MMEWAFANYA NINI? zaidi ya kulalamika kwenye keyboard mpaka wenyewe wameamua tena kufanya some process tena with manupulation, Lakini kesho tu mkiingia barabarani mkazichapa lazima wakae mezani na mtengeneze hiko kitabu. Huwezi kuwastaarabisha watu kwa kuungaunga vipande vya karatasi, watu hustaarabika kwa bakora na risasi kuwaonyesha uelekeo then ndio unawawekea utaratibu.
 
Tangu awali alipoteuliwa nilisema huyu siye, hiyo ilitokana na yeye kujitambulisha ni muumini wa CCM.

Hivi sasa tunashuhudia yeye akitoa maoni kuhusu kuwepo au kutokuwepo katiba mpya, yeye ni mkusanyaji maoni hivyo hatakiwi kuwa mtoa maoni na kama anataka atoe maoni basi inabidi aachie cheo cha uenyekiti aje upande wetu wa watoa maoni na si vinginevyo.

CCM ilimuweka Mukandala kwa lengo maalum la kuikwamisha katiba mpya ili hii mbovu iendelee kuwepo baada ya wao kuifanyia marekebisho wanayoyapenda, ni jukumu letu kusimama kidete na kumkataa huyu Mukandala.
Spidi hii ya kusuasua kuhusu KATIBA mpya, Kuna Kila dalili Uchaguzi mkuu KUYEYUKA.
 
Tangu awali alipoteuliwa nilisema huyu siye, hiyo ilitokana na yeye kujitambulisha ni muumini wa CCM.

Hivi sasa tunashuhudia yeye akitoa maoni kuhusu kuwepo au kutokuwepo katiba mpya, yeye ni mkusanyaji maoni hivyo hatakiwi kuwa mtoa maoni na kama anataka atoe maoni basi inabidi aachie cheo cha uenyekiti aje upande wetu wa watoa maoni na si vinginevyo.

CCM ilimuweka Mukandala kwa lengo maalum la kuikwamisha katiba mpya ili hii mbovu iendelee kuwepo baada ya wao kuifanyia marekebisho wanayoyapenda, ni jukumu letu kusimama kidete na kumkataa huyu Mukandala.

Nitajie vitu vitatu vikubwa vibovu kwenye hii katiba ya sasa ambavyo unaona kwenye katiba mpya itakuwa tiba

Taja vitu ambavyo vitamgusa mtanzania moja Kwa moja mpaka mtanzania wa vijijini
 
Umejitafakari kibnafsi bila kuangalia kesho ya kizazi chako. Yaani wewe unaamini watoto wako unaoendelea kuwasomesha wataendelea kuishi kama uaminivo? Lazima ukubali kuwa kuna Political evolution. Leo sio kesho!
RASIMU alosimamia Judge WARIOBA irudi mezani mjadala uanzie hapo.

Mzee wetu arudishwe kwenye Tume na AAPISHWE Ili amalizie KAZI aliyoianza.

Mukandala ATOSWE na arudi kufundisha.

Hatimaye tupate KATIBA mpya Kwa maslah mapana ya nchi yetu.

Ameeeen
 
USA, UK, FRANCE, GERMANY nk ni mara ngapi wamebadirisha katiba zao tangu kuanzishwa kwake?

Yani hapo unakaa vikindu unajilinganisha Maisha na watu wa masaki na mbezi beach

Jitolee mfano na watu wa level zako,

Sema mbona msumbiji rwanda uganda wamechange katiba zao.?
 
L
Acha kukariri. Sasa hayo ya ndoa yake na wanae kwenye katiba ya Sasa hamna?
Au kwa uelewa wenu kikosi kazi kinapaswa kukusanya maoni yale tu yanayotaka katiba mpya? Au hujui kama zaidi ya 97% ya katiba mpya yamo kwenye katiba ya zamani pia?
Mtu anapokuambia yeye hahitaji katiba, wewe unamuelewaje?
 
Wanataka katiba mpya iingize watu wa vyama mbalimbali au mamluki ili baadae matokeo yakitoka waseme hawakushirikishwa kwa hiyo wanajitoa. Mkitaka kujua katiba siyo suluhisho angalia uchaguzi wa Kenya.
Wanasiasa wa upinzani wanadhani katiba itakayowaingiza madarakani ndiyo itakuwa katiba bora. Mukandala akihoji wananchi wanasema hakuna haja hiyo kwa vile wananchi wengi wanasema kuna haja ya mabadiliko, upande wa pili wanasema wananchi wanataka katiba mpya.
Nakuona wewe ni mmoja wa wale wanaojua katiba ni kwa ajili ya urais na ubunge! Hili nalo ni tatizo.Urais na ubunge ni sehemu ndogo sana sana kwenye katiba, unahitaji uelimishwe uijue katiba ya nchi ni nini na inahusu mambo gani.
 
Back
Top Bottom