Profesa Assad ni muongo, duniani 73% ya ndege zote za biashara hununuliwa kwa pesa taslimu

Profesa Assad ni muongo, duniani 73% ya ndege zote za biashara hununuliwa kwa pesa taslimu

Nimesikitika kuona msomi kama Assad aki-personalize tofauti zake na Hayati Magufuli kwa kusema mtu kichaa tu ndie ananunua ndege kwa cash, profesa akasema mikopo/lease ndio njia sahihi.

Binafsi sijui hizo takwimu amezipata wapi za kua vichaa tu ndio wananunua ndege kwa pesa tasilimu ama cash.

Utafiti unaojulikana Duniani kote uliofanywa na Chase & Associate unaonyesha kua ndege zote za biashara 73% hununuliwa kwa cash ama wanaita outright purchase. Je, wote hao 73% ni vichaa? Ama profesa ndie ana akili kuwazidi?

Profesa anataka kuaminisha umma kua njia pekee na ya lazima ya kununua ndege ni kwa mkopo, kwa cash unakua kichaa, hivi huyu jamaa ana akili kweli?

Profesa ameongea kama mtu ambae hakwenda shule, profesa analazimisha mtazamo wake ndio uwe mtazamo wa watu wote.

Nilikua namkubali profesa lakini hii la ku-personalize tofauti zake na Magufuli na kumshambulia marehemu kua ni kichaa tena kwa mtazamo wake binafsi imesababisha nimemuondoa akili profesa Assad.

Mtu gani huyu eti Prof. Amesubiri Mwendazake kaaga Dunia ndio amekua kifutu anajitutumia kubishana na kutukana Marehemu.
Hasira zake zinatokana na nini hasa amejaa sumu namna hii, kimsingi Watanzania waliiona nia njema ya Rais Magufuli na wakampa heshima katika Safari yake ya mwisho. Hilo litoshe kua pigo takatifu kwa wanafiki wote na wazandiki wa wanaotaka mtazamo wao ndio uwe maoni ya Watu wote.

Tunaendelea kua na imani na Mwendazake haijalishi watambagaza kiasi gani.

Asante John.
Pumzika kwa Amani.
 
Biashara za serikali ni Reli, barabara, bandari, viwanja vya ndege, maji, elimu na afya.Huko kwingine sijui kununua ndege, meli na mabasi ni kupuyanga,ujima na ushamba tu hakuna cha usalama wa nchi wala usalama wa chochote.

Sasa kama hujui fahamu kwamba ATCL yako imenunua mandege ya Trillion 1 Tshs ikiwa haina business plan yoyote. Na kama isingekuwa kununua kwa chash hizo ndege huenda hata wangelazimika kuokota business plan popote ile wazipate kwa mkopo.
Sidhani kama serikali inakatazwa kuwa na biashara zake. Unapaswa kujua uchumi wa nchi ukitegemea mashirika binafsi ni nini kinaweza kutokea na hata kuhatarisha usalama nchi.

Pili kuhusu SGR ilisemwa wazi ya hilo, yamkini hata kwenye ndege imesemwa lakini mimi sina taarifa hivo siwezi kujibia jambo nisilolifahamu kwa kutaka sifa au kutetea hoja yangu. Nitasema jambo ambalo nina ufahamu nalo tu.
 
Nasikia mmea ukipiga,ukafumba ule moshi kwa dakika 3 nzima unaweza ukapasua mapyumb
 
Mimi kwa ufahamu wangu kununua cash ni vizuri maaana unaepukana na kulipa interest. Makosa yaliyofanyika tu ni kununua ndege nyingi.
 
Wewe bado ni lofa Tu kwahiyo kama umefanya nae kazi Sisi inatuhusu?
Bado unaupumbavu Kichwani,
We unadhani wote humu ni wajinga kama wewe.

We umesoma hapo ila mimi ni mwl. wako nimekufundisha nikakupa na hiyo jeuri ya kuwatambia watu kuwa umesoma UDSM.
 
Kwa taarifa yako kwa wale wa UD wanajua yule jamaa ni mzee wa ma benz tangu ametoka US.Hicho ki IST kama kimekuuma pambana na hali yako.

Tatizo liko kwa yule anayejiita mtetezi wa wanyonge kumbe ni mpigaji konki per se.
Mtumia IST mchumia tumbo fidhuli na jinga la mwisho lenye husda
 
Huyo profesa aliamua tu apunguze nyongo. Tungenunua kwa mkopo ingekuwa ni sawa na IPTL nyingine. Kwenye huo mkopo kungezuka upigaji mwingi sana na kesi ambazo zingekuwa kichaka cha upigaji. Kosa la marehemu ni kupuuza vipaumbele vya taifa. Kununua ndege kibao huku shule haina madawati, hospitali haina madawa, wakulima hawajalipwa fedha zao ni kosa lisilosameheka. Na hiyo hasara imekujaje wakati ATCL haikuwa na mshindani fastjet?
 
Hakimu Mfawidhi ameongea kama mtu ambae hakwenda shule, analazimisha mtazamo wake ndio uwe mtazamo wa watu wote.

Nilikua namkubali Hakimu Mfawidhi lakini hii la ku-bwabwaja na kumshambulia profesa kua hana akili tena kwa mtazamo wake binafsi imesababisha nimemuondoa akili .
 
Ndugu hapa ATCL umepotosha kwa 100%. Hasara ya ATCL haina uhusiano wowote na mtaji uliowekezwa na serikali wakati wa kununua zile ndege. Hasara ile imetokana na gharama za uendeshaji wa kila siku vs mapato
Sasa umeongea hapa. Kwahiyo sasa unataka kuniambia gharama sa uendeshaji wa shirika zizaweza kushuka ili hiyo faida ipatikane? Kitu ni kile kile ila huelewi sijui usemacho. Kwa muda mfupi kiasi hiko unadhani sasa shirika linaweza kujiendesha kwa faida wakati halijafikia break even point tangu shirika lifufuliwe. Hasara sasa sio kitu cha kuepukika.

Labda unambie, hiyo hasara imetokana na wizi wa fedha labda kuna mtu anatuhumiwa kuchota hela za hilo shirika ndo tuseme kuna makosa aliyofanya Hayati kutununulia ndege? Kama ni suala na kiutendaji, wahusika si wapo. Kwa kusema tuanze kukimbilia kwenye kutaka kuuza ndege kama njia ya kufufua shirika. Huyo anachokifanya ni kutaka kuliua shirika warudi kwenye upigaji kama awali hamna jipya.
 
Story za Kwenye kahawa usizilete hapa siku nyingine...
angalia jinsi ulivyojivua boksa mchana kweupe,kama hujui kitu si Bora ukae kimya Tu kuna haja gani ya kudhalilisha utu wako
 
Kuna watu bhana wamejaa unafiki licha ya biblia,quran na mavazi yao yanayoakisi uchaji wa Mungu wao.

Baada ya kuona camera zinakumulika umeamua kutumia IST ili uonekane ni mtu mwadilifu sana kumbe ni nafiki kubwa lililojaa ujuaji wa kijinga tu na chonganishi!

"Wanaotumia IST wanawake" Ukaona utumie kauli ya mjinga mwenzako ili uonekane mwema kumbe nafiki.

Sasa kama ungekuws mwadilifu kwanini umepokea hela ili uchonganishe watu?

Kama hujaelewa halikuhusu...pita kushoto nenda zako!

Uzi tayari
Saivi mnalipwa na nan? Maana nasikia hata chamani kumbe hamjulikami watu kama nyie ndio mnasababishaga watu wawe mizimu ili wawasaidie shida zenu
 
Back
Top Bottom