Profesa Assad ni muongo, duniani 73% ya ndege zote za biashara hununuliwa kwa pesa taslimu

Profesa Assad ni muongo, duniani 73% ya ndege zote za biashara hununuliwa kwa pesa taslimu


Soma hapo ujue Eithiopia Airline wanamiliki ndege ngapi walizonunua cash na order walizoweka kwa cash kuletewa ndege na ambazo wamekopa/lease.

Halafu mtu anakuja kuropoka eti kununua cash ni ukichaa.
Kweli wewe mataga.. Yaani unaleta link ya Wikipedia ndo kama ushahidi..? Hivi unajua hata wewe unaweza kuingia na uka-edit habari yeyote uliopo pale..?

Prof. Assad yuko sawa, ni mjinga pekee ambae anaweza kulipa cash dola milioni 200 kununua ndege moja ya biashara..
 
Kwa wewe mtu mmoja kumuondoa haimpunguzii credit zake.

Hamshambulii marehemu anashambulia utendaji wa marehemu na iwe angalizo kwa watu wajao na waliopo.

Kuwa kiongozi si kuwa ndio unajua kila kitu na wenzio ni magarasa tu.

Hebu pita vizuri, nami nilikua nakukubali ila kwa chuki yako hii kama ya kidini nadhani nimekudharau.
Achana naye huyu mwendaazimu hata hiyo link ya source yake aliyoiweka haifanyi kazi
 
Ukimsikiliza prof. Assad utaelewa kuwa alikuwa bitter, angeweza hata kusema, "anayenunua ndege cash ni m**nge" sema tu mazingira hayafai. He's bitter with Magufuli regime, unajua kuna wale wametoa constructive criticism kama Zitto, Ila prof yeye ameonyesha chuki ya wazi kabisa. Asamehewe tu!
Wenye akili mdogo Kama wewe Ndio wanafaa kusamehewa. Hakuna asiyejua zitto kubwa la wanafiki. mtu yeyote mzalendo wa kweli huwezi kucriticise wizi wa meko kwa tabasamu, Lazima uoneshe kukwerwa Kama kweli tunachukia mabilioni ya Watanzania kuibiwa huwezi kuchekacheka au kutabasamu. Assad ni mzalendo wa kweli.
 
Kitu ambacho ujamwelewa ni kuwa kwa inchi maskini kama Tanzania kununua ndege kwa Cash ndio ukichaa

Katika hiyo research yako uliyoweka link nitajie mataifa yenye hadhi kama Tanzania ambayo yamenunua ndege kwa cash?

Unalipa ndege cash na miundombinu huna wala maji safi huna, then how do you call it?
Kwani ukinunua kwa mkopo hakuna riba?
 
Ni dhahiri atakuwa alikuwa anafanya kazi kwa kutumwa na JPM akamshtukia! Hata kujitokeza sasa kaburi likiwa bado bichi ni dhahiri hafanyi haya kwa dhamiri yake bali kutumwa! Bora angekaa kimya tubaki na nadharia zetu kumuheshimu!
Wewe dada nawe mambo ya kaburi bichi ndo unamletea Nani jukwaa hili la GT wewe ni great sinker. Magufuli alikuwa mwizi . over.
 
Achana naye huyu mwendaazimu hata hiyo link ya source yake aliyoiweka haifanyi kazi
Mkuu James Martin
Hawa hawanipi shida, wajua tatizo sio chama tatizo huwa ni mtu/utendaji wa mtu,
Ndio sisi husimamia kutaka kuwepo taasisi imara na si mtu imara na kila mmoja awajibike kwa kiapo alichoapa kwacho na si kama sasa unaapa kwa kumuogopa mtu na kujihadaa mwenyewe ukidhani unamhadaa Muumba wako

Sasa hawa mimi nawadunga hizi antibiotics kabla ya kuangalia utaratibu wa kuwafungulia hizi dose za Covid 19
 
Hivi kwanini uhuru wa vyombo vya habari uliminywa na mtu kutaka serikali isemwe kwa mazuri tu bila kukosolewa!?
"You are not free to that extent" maneno ya nani akiashiria nini?

Kuweni na utu na aibu, haya uyasemayo ni kwakuwa palikuwa na uhuru wa kuhoji na kuwaweka wazi waTanzania ma wakati huo ukihitaji 'data' kwa wizara/sehemu yoyote unapata na kuiweka wazi kwa wazalendo wote na si wazalendo uchwara

Jishughulishe kufikiri kidogo basi kama, JK angeamua kuficha mambo kama kipindi hiki hivi si angeitwa Malaika au?
Kama kuna uhuru na uwazi mngetuambia Ukweli mauaji ya MKIRU, shambulio la Lissu kwa Nini ripoti haikusomwa baada ya kuandaliwa, Risisti na mikataba ya ujenzi wa uwanja wa Chato iko wapi?
Kwa hiyo Kuhoji machache ya hayo ni kutujibu kwa hiyo quotation yako kuwa "you are not free to that extent".kwa makusudi unapotosha kwa maslahi ya Nani? Halafu unajiita mzalendo wa kweli?
 
Kama kuna uhuru na uwazi mngetuambia Ukweli mauaji ya MKIRU, shambulio la Lissu kwa Nini ripoti haikusomwa baada ya kuandaliwa, Risisti na mikataba ya ujenzi wa uwanja wa Chato iko wapi?
Kwa hiyo Kuhoji machache ya hayo ni kutujibu kwa hiyo quotation yako kuwa "you are not free to that extent".kwa makusudi unapotosha kwa maslahi ya Nani? Halafu unajiita mzalendo wa kweli?
Naomba niku ignore kama mwenzio, soma between the lines halafu ndio uje hapa ondoa mihemko na uokotolezi wa quotation/s ambazo hujatuliza kifikicho chako

Nakupita kushoto
 
Huyo Assad hafai kuwa mtumishi wa uma kama bado anafundisha UDSM serikali imuondoe, ni hafai hafai
Hufai wewe na ndio maana awamu ya 5 imekula matrilioni ya pesa.Kifupi humjui huyu Profesa.Soma habari zake katika post alieituma Mr Ole Mushi April 7,2019 simu no.0712702602,JF. ANAHESHIMIKA DUNIANI KOTE.Mh Rais Mstaafu Kikwete alituwekea watu mahiri sana.Awamu ya 5 ya ulaji wa matrilioni ya fedha ndio iliyomuondoa msomi huyu tena bila ya kufuata sheria na utaratibu kama alivyoainisha msomi mwingine Profesa Issa Shivji.Nadhani wewe uliyeandika ndio wale wanaojiita sijui Sukuma Gang.#KAZI IENDELEE.Salaam za Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania.
 
Ukimsikiliza prof. Assad utaelewa kuwa alikuwa bitter, angeweza hata kusema, "anayenunua ndege cash ni m**nge" sema tu mazingira hayafai. He's bitter with Magufuli regime, unajua kuna wale wametoa constructive criticism kama Zitto, Ila prof yeye ameonyesha chuki ya wazi kabisa. Asamehewe tu!
Uko sahihi kabisa, mzee alikuwa na nyongo kali sana tumboni na leo kaitema: Japo tukiwa wakweli hata marehemu naye alikuwa anawatemea wenzake nyongo kali na kuwadhalilisha hadharani mara nyingine kwa taarifa za majungu tu. Lakini nadhani tukubali kwamba haya ndiyo madhara ya kuminya uhuru wa kujieleza, baada ya uongozi kuondoka tunasikia makelele na manung'uniko mengi ambayo huenda tungeyasikia zamani tungeyaone leo ni kitu cha kawaida kisicho na msingi wowote ule.
 
Kwa maana hiyo...mikopo ambayo mtukufu mwendazake amechukua katika kipindi chake lazma kutakua na upigaji umefanyika eehh? Maana mkopo wowote lazma uendane
Mbezi Boy tunaongelea ATCL usichanganye mambo.
 
Kasema kununua Airline kwa kutumia Taslimu.

Kwasababu inapoingiza fedha deni linalipwa.

Taslimu ziingizwe kwenye Elimu Afya ya Jamii na Miundombinu ya kuunganisha Vijiji kwa Vijiji.
Kwa hiyo angenunua kwa mkopo halafu faida inayopatikana tunalipa Deni?
 
Huyu Prof. Assad ni msomi asiyekuwa na maarifa. Kishimba si msomi lakini ana maarifa. Katika dunia ya leo ni bora kuwa na maarifa kuliko kuwa msomi bila maarifa.
 
Nimesikitika kuona msomi kama Assad aki-personalize tofauti zake na Hayati Magufuli kwa kusema mtu kichaa tu ndie ananunua ndege kwa cash, profesa akasema mikopo/lease ndio njia sahihi.

Binafsi sijui hizo takwimu amezipata wapi za kua vichaa tu ndio wananunua ndege kwa pesa tasilimu ama cash.

Utafiti unaojulikana Duniani kote uliofanywa na Chase & Associate unaonyesha kua ndege zote za biashara 73% hununuliwa kwa cash ama wanaita outright purchase. Je, wote hao 73% ni vichaa? Ama profesa ndie ana akili kuwazidi?

Profesa anataka kuaminisha umma kua njia pekee na ya lazima ya kununua ndege ni kwa mkopo, kwa cash unakua kichaa, hivi huyu jamaa ana akili kweli?

Profesa ameongea kama mtu ambae hakwenda shule, profesa analazimisha mtazamo wake ndio uwe mtazamo wa watu wote.

Nilikua namkubali profesa lakini hii la ku-personalize tofauti zake na Magufuli na kumshambulia marehemu kua ni kichaa tena kwa mtazamo wake binafsi imesababisha nimemuondoa akili profesa Assad.

Hivi profesa yeye kwenye maisha ama kwenye public settings ameweza kufanikisha lipi?, Amewahi kua mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa NBC, enzi za utawala wake benki ilikua inaelekea kufa/kufilisika kabisa. Bila yeye kuondolewa bank isingekuwepo sasa hivi. Asijionyeshe kua no brainy saana, alipewa nafasi mbona hakutuonyesha huo u brainy wake?

Analalamikia kua hakupewa nyaraka za SGR, JNHP, ATCL, kwa nini hakujiuzuru kuonyesha credibility? Maana hapo ni sawa na kua alizuiwa kutekeleza majukumu yake ya msingi kwa maslahi mapana ya nchi, kwa nini hakujiuzuru?

Mkuu hapo uliposema ulikuwa unamkubali Assad naomba ufute hiyo kauli, maana uzi wako naona sehemu kubwa kama umemshambulia sana! Kitwanga hilo alishalisema zamani sana tangu mwendazake yupo na uzi upo humu watu wakasema ni kwavile katumbuliwa, wengine wakauliza eti hakuwa kalewa? Kwa uzi huu wako inaonyesha hujawahi kumkubali Asad hivyo hata kama alilosema lina ukweli lazima utapinga tu
 
Back
Top Bottom