Profesa Kabudi: Trilioni 360 za makinikia haikuwa kodi sahihi, Nilikosea kutumia neno “Jalala”

Profesa Kabudi: Trilioni 360 za makinikia haikuwa kodi sahihi, Nilikosea kutumia neno “Jalala”

Unajua huyo Mzee amekiuka kiapo chake Cha Baraza la Mawaziri, hakutakiwa kusema hayo Kwa kuwa yangekuwa nje ya kiapo chake.

Unajua Mzee Edo pamoja na kuambiwa mara kadhaa kusema kuhusu Richmond yake iliyomuondoa hakuthubutu kufungua kinywa chake kusema licha ya watu wengi kuhisi ameonewa.

Huyo Mzee wa Jalalani nahakika Angekwepo JPM asingesema hata mara moja
Mkuu tukio la Edo halikuhusisha marisasi. Hili tukio lina guilt nyingi mtu anakuwa anakereketwa kusema
 
Mkuu tukio la Edo halikuhusisha marisasi. Hili tukio lina guilt nyingi mtu anakuwa anakereketwa kusema
Kwani hata huyo Kabudi ameshikiwa Bastola kusema hayo? Nadhani anatafuta kuungwa mkono na Wananchi, na katika watu hawatarudi Bungeni 2025 ni pamoja na huyo Mzee wa Jalalani

Lakini ni ukweli katika watu JPM aliwaamini ni pamoja na huyo Mzee
 
Mnayasema hayo hadharani na mnategemea wawekezaji serious walete mitaji yao. Kama wale wawekezaji walioenda Kenya mnategemea kuna siku watakuja huku? Hapana, Huku watakuja wawekezaji matapeli wanaokuja bila mitaji na wanaipatia huku huku.

Nchi hii ina wasomi waliochanganyikiwa, badala ya kukalia viti kwa nafasi walizopewa ni bora kwa kuwasaidia wapelekwe hospitali ya watu wenye matatizo ya akili.
 
Kauli hii ya Profesa Kabudi inadhihirisha kuwa Lissu alikuwa sahihi Sana kwa sababu hata kama ni mbinu za kutaka mjadala, kwa wasomi kama maprofesa kutumia mbinu ya uongo "ulio dhahiri" kiasi hiki ulikuwa ni upungufu wa weledi.

Labda tuwasikie Wataalam wa daplomasia ya uchumi waje watufafanulie mbinu hii ya "Uongo mkubwa wa dhahiri" kama Lissu alivyokuwa "Profesorial Rubbish".

======


  • Asema zilikuwa mbinu za majadiliano, ataja tishio la Acacia
  • Afafanua suala hilo limekwisha, atamtafuta mwigulu amweleze
  • Atamba uamzi ule umeleta heshima, faida kubwa kwa nchi
  • Asema alikosea kutumia neno jalala, asisitiza kibiblia ni sahihi.

Nukuu za Prof. Palamagamba Kabudi kwenye gazeti la leo la Jamhuri, Oktoba 4, 2022
mbele ya meza ya mfalme watu hujikomba na kujishtukia,lakini akina yaheee tupo tu.
 
Kwani hata huyo Kabudi ameshikiwa Bastola kusema hayo? Nadhani anatafuta kuungwa mkono na Wananchi, na katika watu hawatarudi Bungeni 2025 ni pamoja na huyo Mzee wa Jalalani

Lakini ni ukweli katika watu JPM aliwaamini ni pamoja na huyo Mzee
JPM alibariki kodi zisizo na uhalisia na zisizolipika, huu ulikuwa udhaifu.
 
Kwenye madai ambayo hayakuwepo, ni fiction, hiyo pesa kwangu ni nyingi sana, bado naendelea kumpongeza Kabudi.
Pale tapeli anapompongeza tapeli mwenzie aka mwana fisiemu
 
Wenye akili walimwelewa na hadi sasa wanamwelewa kabudi. Wajinga ndio hawaelewi.
Kuna kitu 'mbinu za majadiliano' kwa wale lazima kitu kielezwe kwa kingereza ndio wakubali kuna fani..negotiation skills, strategy etc, etc. Nendeni mkamueleze huyo kichaa lissu aliyediriki hadi kumdharau mwalimu wake wa sheria chuo kikuu Prof Kabudi.
Profesa wa mchongo aka kabudo
 
Huu ni uthibitisho kwamba JPM alikuwa anaendesha nchi kwa ulaghai, utapeli, uzandiki, na propaganda. Alizungukwa na waongo na wanafiki, na yeye alipenda uongo na unafiki.

Ajabu mpaka Leo Kuna mijitu mijinga inaendelea kuimba ujinga wa awamu ya tano. Anajifanya kupambana na ufisadi huku pembeni ana Makonda, na Sabaya. Tenda za kujenga stiglers, sub contractors wote ni vikampuni vyake, pamoja na inner cycle yake. Wenye vikampuni hivyo ndio wanapiga mdomo sana kuhusu mradi, kwa sababu wamekaa pale wananyonya nchi. Akina polepole, ana kikampuni pale kina tenda, kinafiki anajifanya mzalendo kuupenda mradi, nyuma ya pazia ana kampuni inakula Hela zetu pale stiglers.

Stendi ya Magufuli Mbezi, kikampuni chake, kimevuta Hela, na stendi hakijaimaliza, inabidi Hela itafutwe kwingine, masoko mapya nchi nzima, stendi ya nyamhongolo, barabara za Kanda ya ziwa via mayanga construction, barabara ya kigoma inayojemgwa na nyanza road, kampuni ambayo ana hisa, imejengwa miaka zaidi ya 20 haiishi huku akiwa bize kufutia ukandarasi kampuni za wenzake.

Wafanyakazi anatimua timua huku wale wa Chato wakiajiriwa bila interview na kujazwa serikalini.

Uwanja wa ndege Chato, imejenga kampuni yake, hospitali ya Kanda Chato...endless list.

Hakuna utawala mchafu kama wa awamu ya JPM.

Miradi mingi ya ujenzi wa madaraja na barabara ni kampuni za JPM lakini alikuwa anawapachika wachina.

Oohh masikini na wanyonge, jitu limejaza matrilioni kwenye akaunti za Siri, mfugale anaulizwa hizi Hela vipi, badala ya kujibu, na yeye anakufa

Sasa hao jamaa wa mgodi wakaidai bilioni 700 ambayo waliilipa kupitia professorial rubbish
Aa kumbee nyie ndio mlio mpeleka mfugale paradise👆👆
 
Mkuu mimi binafsi katika kazi zangu nimepata access ya kuwajua sub-contractors wengi wa bwawa la umeme na reli ya mwendokasi na waliokua wameanza kujiweka sawa kwa ajili ya bomba la mafuta.

Nakuhakikishia katika kipindi ambacho watu wamepata hizo tenda kwa haki, bila rushwa na bila kumjua mtu ni kipindi cha JPM.

Mnapotosha kwa faida ya nani? Hebu taja hiyo kampuni ya Polepole iliyokua inahudumu kwenye bwawa la umeme, vinginevyo wewe ni qumer tuu.
😂😂😂😂😂😂😂😂
Sukuma gang umechafukwa
 
Ikulu ni nyumba ya udalali - Simkumbuki aliyetamka haya maneno.
Mfano dangote anawekeza lkn haweki hiza zake wazi Kwa DSM stock exchange, anahipatia hasara kubwa Kwa Taifa letu.
Kazi kubwa kwake kuja ikulu kuongea, pindi anapoingia raisi mpya Ikulu, what hell our president doing in the state House 🚮🚮🚮
 
JPM alibariki kodi zisizo na uhalisia na zisizolipika, huu ulikuwa udhaifu.
Mkuu zilipikwa kodi hasa.. Kwa neno UZALENDO

Unaumiza raia wako makusudi... Mtu anakwambia kabisa mimi mtaji wangu huu... Nauza kiasi hiki... Unasema ni mwongo...
Matokeo yake watu wameyumba kiuchumi kwa fujo za utawala ule..

Ukienda kwa DPP ofisini kwake asilimia 50 za kesi ni uhujumu uchumi sijui kakwepa kodi... Kumbe mtu kabambikwa kodi kakataa wakamtengenezea kesi akae ndani..
ili DPP afanye mazungumzo na huyo mtu akiwa gerezani kumlazimisha wachukue nusu ya salio lake kwenye account..

Ule uongozi ulipenda kesi za ajabu na nyingi za kutengeneza ili kuweza kuaminisha watu.. Eti tuna kiongozi Mzalendo...
Tuna Katiba inayompa Rais madaraka ya kufanya lolote bila kuhojiwa.. Ndio matokeo yake

Yaani Jiwe asinge pambanishwa na combination ya covid + ibilisi na kukutanishwa uso kwa uso na IZIRAELI ile March 2021 ..... Nchi ilikuwa inaenda shimoni
 
Mkuu kumbe ulikuwa hufahamu- ngoja nikwambie Mungu hajawahi kuumba msomo, wazir, wala nani- Mungu aliumba mwanadamu mwanaume kwa udongo na mwanamke kwa mifupa ya mwanume mengine yote ni mbwembwe tu
Kabisaa!!!
 
Kadhi Mkuu 1 said:
Kibongo bongo ni sawa, kama vile mtu anauza kitu elf 25 mwisho unanunua elfu 3.

Kwa kweli wasi wasi wangu ni mmoja tu hii habari ikiwafikia waliokuwa wakidaiwa hii kodi, je mtakuwa na ujeuri wa kusema, hapana, tuliwabambikia tu makusudi! Huu ujinga utatumaliza!
 
Back
Top Bottom