Shida ya Lipumba ni unafiki.Leo kaongea km Profesa halisi wa wa uchumi.Lakini wakimuwekea bahasha mezani tu anajitoa ufahamu wote mpaka mtu unajiuliza,Hivi huyu ndo Prof Lipumba au msukule wake?!!! Aache kubadilika badilika km kinyonga.
Mzigo ulitoka wewehoja ya Lipumba dhaifu saina
ukituhumiwa kwa kosa la kula njama za kuiba kuku wa Rashidi ina maana mlijipanga lakini kuku hakuibiwa. Kuku angeibiwa ungetuhumiwa kuiba kuku.
huwezi kuambiwa sasa rudisha kuku wa Rashidi wakati kuku tangia hapo anae Rashidi.
Mwendazake amepiga kozi 3 tuMama anajenga uchumi upi wakati mwendazake aishajenga uchumi? Au mwendazake aliishia kwenye linta?
Kwan amesha acha kuwafurahisha?Hapa ndyo tutamuelewa Kigogo2014 na Lissu,Samia hana jipya kwa kuwa na yeye ni product ya wizi wa kura za October, 2020
Utamkumbuka wewe na ukoo wako.Kaua uchumi na kufubaza demokrasia.Tuliwaambia JPM alikuwa mzalendo halisi na mtamkumbuka. Haya sasa mbona!??? Bi Mkubwa ajiuzulu tuu asingoje ilee 2025.
Unamiaka mingapi kwenye hilo jukwaa ? Maana unahitaji kupashwa habari zaidi.Lipumba aelewe zike ni tuhuma tu na serikali kwa zaidi ya miaka 5 imwshindwa kupata ushahidi na kusimamisha kesi dhidi ya huyo singa
Hapa hata wewe Missile of the Nation umechemka sana.Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa
Out of contextPamoja na maneno matamu ya Profesa Lipumba, naomba kumuuliza Prof. mbona hatukumuona akiyasema haya kumshauri Bwana Magufuli? PILI, naomba kujua wakati Prof. anakipokea chama chake kwa kuwapora wananchi na kujimilikisha, kilikuwa na hali gani? wabunge wangapi? na sasa chama hicho kipo wapi? Naomba Prof. anijuze kabla ya kutoka nje kuhangaika na kibanzi kilicho kakika macho ya wenzake, anatoaje maboriti yaliyo katika macho yake?