Profesa Makame Mbarawa anatushinda kumng'oa?

Profesa Makame Mbarawa anatushinda kumng'oa?

Jeshi ni chama kinaitwa CCM ...hilo weka kichwani kuing'oa CCM madarakani ni mpaka ndani ya jeshi kufanyike uhasi fullstop zingine ni ngonjera. So kulitegemea jeshi kututetea sahau. Hapa namaanisha kila chombo cha ulinzi na usalama yaani vyote ni chama.
Kwahiyo ni chawa kumbe!
 
Madhara ya Sera za Mwendazake! Aliua Upinzani kwa Ukatili Mkubwa! Na yeye mwenyewe kafa!

Lakini ametuachia Bunge la ma-CCM lisilochaguliwa na Wananchi, ni Bunge lisilotetea Wananchi!

Kwa Bunge hili dhaifu ma-CCM yameamua kugawana Mbao! Bunge litajadiri na kupitisha Nchi kuuzwa!
Hii ndiyo point kuliko zote na Magufuri ataendelea kuhukumiwa mpaka mwisho wa ulimwengu kwa sababu zifuatazo:-
1.Ndiye mwasisi wa Rais anayekuwa Madarakani aonekane Mungu.
2.Ndiye mwasisi wa Rais anayekuwa madarakani miradi mikubwa kupendelea kwao.
3.Ndiye mwasisi wa ukabila,ukanda na ubaguzi Tanzania
4.Ndiye mwasisi wa kuwaengua wagombea viti vya uenyekiti,udiwani,ubunge ambao siyo wanaccm kwa sababu anazozijua yeye.
5.Ndiye mwasisi wa kupitisha wenyeviti wa Serikali za Mitaa na vijiji kwa lazima bila kuangalia athari itakayokuwepo baadaye,Rejea 2019.
6.Ndiye mwasisi wa kuiba kura kiwazi wazi na kuzima mitandao katika uchaguzi mkuu wa 2020
7.Ndiye mwasisi wa kutunga sheria za kuwawekea kinga Rais,Makamu wa rais,Spika,Naibu Spika,Waziri Mkuu na Jaji Mkuu
8.Ndiye mwasisi wa kuingiza wabunge wasiokua na chama chochote cha siasa kwa kutumia dola,bunge na mahakama bila utaratibu wa sheria yoyote nchini,rejea Covid 19 walivyoingizwa Bungeni na Ndungai.

Hivyo madhaifu yote haya tunayoyaona yametokana na Awamu ya tano ambayo Rais wa sasa alikuwa Makamu rais na Makamu Rais wa sasa alikuwa Waziri wa fedha aliyebariki utumiaji hovyo wa fedha za nchi na mwisho Waziri Mkuu ambaye ni mtendaji mkuu wa serikali bado ni yule yule.Kwa hiyo mambo yote machaifu yataendelezwa hata kama tutapiga kelele namna gani.Ni Mungu tu ndiye atakayeamua ugomvi la sivyo tukubali maumivu.
 
Sidhani kama wewe umewahi kufanya biashara yoyote inayotumia bandari zaidi ya kuja na negativity zile zile za kitanzania.

Ndugu zetu wanaoendesha bandari ile ni wezi watupu, kazi yao kuchora michoro ya wizi kila wanapoenda kazini asubuhi.
Twende mdogo mdogo..

Wezi washughulikiwe kama wezi. Na uwekezaji wowote uzingatie manufaa kwa nchi.

Sasa kama umekiri hao ni wezi, mbona unakubali wao kuwa sehemu ya negotiation team kupata muwekezaji mpya.! Ridiculous!
 
Binafsi nimeamini Prof. Mbarawa hafai kuwa mtumishi katika kiwango cha Uwaziri katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni waziri muoga, waziri picha tu. Ni Profesa aina ya le profeseri, yani yupo kama hayupo, na mambo mengi ya kuudhi na kuuza nchi hufanyika akiwa tuli kama kunyoa kichwa cha mwendawazimu.
Rais alishawahi kusema yeye ni mzanzibari maana yake si mtanzania, kwahiyo amedanganywa na Mbarawa wameamua kutuuza kwa waarabu upya
 
Habari Watanzania,

Binafsi nimeamini Prof. Mbarawa hafai kuwa mtumishi katika kiwango cha Uwaziri katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni waziri muoga, waziri picha tu. Ni Profesa aina ya le profeseri, yani yupo kama hayupo, na mambo mengi ya kuudhi na kuuza nchi hufanyika akiwa tuli kama kunyoa kichwa cha mwendawazimu.

Sasa hivi naamini hata Marehemu JPM alikuwa sahihi kumtimulia mbali pasi hata na kueleza sababu za kumtimua.

Ufafanuzi wa TPA kuhusu kuuzwa bandari ya Dar es Salaam (usiniambia eti kukodisha). Ukishakuwa umepewa sehemu kwa miaka 99, hapo umeuziwa, ndio uhalisia. Yani two good generation gonna live with the same contract and ownership, hata Mangugo alikuwa anafikiria sawasawa.

Kwa msioijua bandari ya Dar es Salaam, nawamegea kidogo.

Hao DP World wamepewa gati namba 5 mpaka 8.

Hayo ndiyo magati ambayo tangu enzi za Kikwete na JPM yamekuwa yakiendelezwa sana. Tena kwa gharama kubwa za serikali. Ambacho hakikuwa kikifanyika ni uwekaji wa mitambo ya kisasa tu, ila upanuzi na ujenzi umetumia fedha nyingi sana za serikali.

Mfano gati namba 5, 6, 7, 8 huku ndio asilimia 90 ya mizigo yote ya bandari ya Dsm imekuwa ikishushwa miaka yote.

Ishu ya kusema eti hakuna mkataba, ni uongo, iweje tujue wamepewa eneo hilo. Hicho ni nini?

Kama hawa DP World ni wakombozi wetu hivyo, kwanini wasipewe gati namba 1 hadi 4?!

Waendelee hapo, tuone ukongwe wao.

Miaka 99, akili au matope?

Tupige kura hapa Prof. Makame Mbarawa atupishe kwanza.
Nafiiri Mzanzibar hawezi kuwa na uchungu na maliza za Tanganyika.Huu Muungano ni upuuzi
 
Mkuu

Nakuunga mkono asilimia zote, ukoo wa majini umekuja huku bara kumrejesha sultan kwa mgongo wa uwekezaji wa kinyonyaji. Npiga kura huyo waziri aondoke au seikali nzima iwajibike
Prof., Msomi na ueledi wote, na uzoefu wake, anashindwa kudadavua mambo kiufasaha! Halafu kwenye ma dili makubwa anakuwa kimya kabisa kama haimuhusu.
 
Upuuzi.
Wakati Kikwete anagawa gesi kwani wabunge wa upinzani hawakuwepo kututetea?

Wakati Kikwete anataka kugawa bagamoyo kwani hao wapinzani hawakuwepo bungeni? Kwa nini wasingetutetea wakati huo?

Ni ufinyu wa mawazo kumlaumu Magufuli (rip) kwa kosa linalofanywa na Samia. Let's be logical.

Uchaguzi wa 2015 uliweza kuifunza CCM. Magufuli akaja kupora nguvu za wananchi kuweka serikali madarakani. Matokeo yake ndio haya sasa.
 
Uchaguzi wa 2015 uliweza kuifunza CCM. Magufuli akaja kupora nguvu za wananchi kuweka serikali madarakani. Matokeo yake ndio haya sasa.
Haisaidii kumlaimu marehemu mjomba wako wew sasa piga kazi, wew si uko Hai? Piga mzigo
 
Anasimamia maslahi binafsi. Kwa nini Wazenjj wanaiingiza Bara kwenye mikataba bila hiyari. Kama mkataba ni mzuri kwa nini usihusishe na bandari za Zenji....!!?
Halafu umenikumbusha kitu muhimu, kule Zenji si kuna maji na uwanda wa bahari pia, kwa nini hima hima hawawapeleki huko hawa Dubai P
 
Habari Watanzania,

Binafsi nimeamini Prof. Mbarawa hafai kuwa mtumishi katika kiwango cha Uwaziri katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni waziri muoga, waziri picha tu. Ni Profesa aina ya le profeseri, yani yupo kama hayupo, na mambo mengi ya kuudhi na kuuza nchi hufanyika akiwa tuli kama kunyoa kichwa cha mwendawazimu.

Sasa hivi naamini hata Marehemu JPM alikuwa sahihi kumtimulia mbali pasi hata na kueleza sababu za kumtimua.

Ufafanuzi wa TPA kuhusu kuuzwa bandari ya Dar es Salaam (usiniambia eti kukodisha). Ukishakuwa umepewa sehemu kwa miaka 99, hapo umeuziwa, ndio uhalisia. Yani two good generation gonna live with the same contract and ownership, hata Mangugo alikuwa anafikiria sawasawa.

Kwa msioijua bandari ya Dar es Salaam, nawamegea kidogo.

Hao DP World wamepewa gati namba 5 mpaka 8.

Hayo ndiyo magati ambayo tangu enzi za Kikwete na JPM yamekuwa yakiendelezwa sana. Tena kwa gharama kubwa za serikali. Ambacho hakikuwa kikifanyika ni uwekaji wa mitambo ya kisasa tu, ila upanuzi na ujenzi umetumia fedha nyingi sana za serikali.

Mfano gati namba 5, 6, 7, 8 huku ndio asilimia 90 ya mizigo yote ya bandari ya Dsm imekuwa ikishushwa miaka yote.

Ishu ya kusema eti hakuna mkataba, ni uongo, iweje tujue wamepewa eneo hilo. Hicho ni nini?

Kama hawa DP World ni wakombozi wetu hivyo, kwanini wasipewe gati namba 1 hadi 4?!

Waendelee hapo, tuone ukongwe wao.

Miaka 99, akili au matope?

Tupige kura hapa Prof. Makame Mbarawa atupishe kwanza.
Swali ambalo limeulizwa sana mkataba huu ni wa muda gani? Wapi palipoandikwa miaka 100? Au wapi palipoandikwa miezi 12 ambayo TPA wamesema? Jibu lipo kwenye kufungu cha 23(4) cha mkataba.

Kifungu hicho kinasema mkataba ukishasainiwa, pande mbili za mkataba (serikali ya TZ na serikali ya Dubai) hakuna upande utakaoruhusiwa kukosoa (denounce), kujitoa (withdraw), kuzuia (suspend) au kuvunja mkataba (terminate) kwa sababu yoyote ile.

Kifungu hicho kinasema hata ikitokea upande mmoja ukashindwa kutekeleza masharti ya mkataba, bado hairuhusiwi kuvunja, wala kujitoa kwenye mkataba huo. Maana yake ni kwamba, Mwarabu akisema atapanua bandari ya Dar iwe kubwa zaidi, halafu akashindwa kufanya hivyo, haturuhusiwi kuvunja mkataba. Sijui unaelewa?

Hawakuishia hapo, kifungu hichohicho kinaeleza kwamba hata tukiingia kwenye mgogoro wa kidiplomasia na Dubai, bado haturuhusiwi kuvunja mkataba (we can not terminate the agreement even in severance of diplomatic relation). Yani hata ikitokea sisi na UAE tumevunja uhusiano wa kibalozi, tukamfurusha balozi wao, bado wataendelea kuendesha bandari yetu. Hata ikitokea tukapigana vita, bado haivunji mkataba. Waaarabu wataendelea kuendesha bandari yetu, penda tusipende.

Kwa lugha rahisi huu mkataba ni wa MILELE. Kwahiyo wale waliokua wanauliza kifungu gani kinachoeleza muda wa mkataba? Ni kifungu cha 23(4). Kinasema mkataba huo ni wa MILELE na MILELE mpaka Kristo atakaporudi kulichukua Kanisa.

Hii ni zaidi ya ndoa ya Kikristo ambayo ukishaapa kanisani, hata kama ana matege, ni wako huyo mpaka kifo kiwatenganishe. Na huu mkataba kifungu cha 23(4) kinasema ukishasaini tu, ngoma ni MILELE. Hakuna namna ya kutoka. Bahati mbaya tumeshasaini tangu October 2022.

Halafu "mjinga" mmoja aliyekua ripota wa TBC huko Namtumbo leo kawa Msemaji wa serikali, amekaa kwenye V8 anatuona Watanzania wote wajinga. Anatuambia eti ni mkataba wa miezi 12. Shame.!

Mnataka kuharibu urithi wa vizazi vyetu sababu ya matumbo? Hivi Nyerere angechumia tumbo tungepata uhuru? Endeleeni kutetea matumbo yenu, sisi tunatetea watoto na wajukuu zenu. Lakini ipo siku mtajibu. Kama si hapa, basi hata mbinguni.
 

Attachments

  • Screenshot_20230607-202253_2.jpg
    Screenshot_20230607-202253_2.jpg
    21.5 KB · Views: 3
Back
Top Bottom