Profesa Muhongo huna credibility ya kuwashauri watanzania kuachana na mradi wa JNHPP na usidanganye watu kuwa Hydro power zimepitwa na wakati


Muhongo ni msanii laghai
Mama akiingia mkenge Tu amekwisha
 
Yaani Profesa wa Geology na Geophysics hajui kwamba nishati ya gesi sio renewable siku moja itakwisha?

Naona labda watu wanamsingizia Muhongo hawezi kujitoa ufahamu mpaka kufikia kiwango cha kutoa hoja kama a layman!!
 
Mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu wa mazingira hauwezi kuiacha hiyo miradi ya maji salama. Tungewekeza kwenye wind na solar
Solar na wind? Unauelewa Kwenye masuala ya umeme kweli au?

Largest solar power station haijavuka 2500MW hapo hujagusa gharama zake

Mabadiliko gani ya Tabia ya nchi unayosemea?

Venus ilichukua miaka miilioni kadhaa kutoka kuwa kama Dunia na kuwa kama ilivyo leo...

Hata miaka 1000 ipite mto Rufiji utakuwa haujakauka...

Kinachoweza kufanya Mabadiliko ya tabia nchi yatokee ghafla labda dunia yetu igongwe astreoid, au zitokee volcano ambazo sisi hatujizui...
 

Amesema umeme wa maji pekee umepitwa na wakati kwasababu ya mabadiliko ya hali ya hewa
 
SSH ni dhaifu ndio maana kila mtu anajaribu kushawishi ujinga wake. Amefungalia mlango akitaka kuonyesha ana akili kumbe ameonyesha udhaifu wake.
What a shit!

Dyou think buying is all what leadership is?

You better behave and know that We respect Mama big time!
 
Hapana mimi ni mnyonge, bahati mbaya tu Rais wangu amedanja! Ila alichokuwa anasema Prof. Muhongo kurudisha gharama zilizotumika kwenye umeme wa maji huchukua muda mrefu kutokana na gharama kubwa ya miundombinu tofauti na umeme wa gesi!
Kwa hiyo tunanyeje?
 
Dunia nzima inaenda kwenye nuclear, gas na solar. Sisi bado tumegomea kwenye maji
Mzee!! Nuclear, gas na solar?

Hapa umeme wa uhakika ni Nuclear na Gas unajua cost yake, Unajua Gharama ya kujenga Nuclear reactor, Gharama ya Kuindesha...

Nuclear sio carbon emission source of electricity lakini waste zake, ndio zinawafanya watu waache kuzitumia
 
Rubish pro kwani kitu gani kinatofautisha umeme wa maji na gas zaidi ya gharama za uzalishaji, watu wanazungumzia kwamba eti maji hayaaminiki kwahiyo itafika wakati tutaambiwa maji hayafai kwa matumizi tutumie gas,hawajuhi kuwa nchi nyingi zinazozalisha umeme wa gas mala nyingi huwa hazina vyanzo vya umeme wa maji sasa mjinga mmoja anakurupuka heti umeme wa maji umepitwa na wakati,aende china kuna mabwawa yanayozalisha 50k meg ,blazil ,na nchi nyingi tu.
 
Uwe na kiasi. Muhongo hakuwa na heshima kwa watu zamani, lakini huwa haropoki. Ni kweli umeme wa bei rahisi ni wa maji. Lakini ukweli zaidi ni kuwa nchi ziendazo kisasa mchango wa umeme wa maji ni mdogo mno. Jiandae kuushangaa ukweli huu: Kati ya umeme wote wa Russia, umeme wa maji ni 20%; China 18%; EU haizidi 10 ( France 10, Germany 3); USA 6.6; UK 2. Tafuta ukweli huu hata kwa google
 
OK umeme wa kizamani anataka mradi uachwe pesa iliyotumika iachwe ife ili mwendazake aonekane hakufaa? siasa bw.
 
Muhongo sio mtaalamu wa nishati, yeye ni mtaalamu wa miamba.

Aache kabisa kuingilia fani za watu.
 
Badala ya kujibu hoja na kutoa ufafanuzi we unampamba mtu[emoji1][emoji1]
 
Hii umeiongea kwa Summary.

China sehemu kubwa ya umeme wake unatokana na Non Renewable sources hasa Makaa ya mawe...
Power plants kubwa ya coal ni Kama Megawatts 6000MW na hawa ndio wana largest power plants.

Kwenye Nuclear Japan ndio wana powerplants kubwa ila ni 7000MW ila dunia nzima inakumbuka ajali ya Fukushima

Kwenye Gas (ambayo sisi tunayo) ni Qatar hawa wanazalisha 8000MW

Solar India na China ndio wana zalisha umeme mwingi karibu 2500MW pekee

Wind wachina ndio wana power plants kubwa kama megawatts 7000

Kwenye Hydro China wana bwawa kubwa kabisa duniani 22,000 MW

Ukiangalia Wachina Waliwekeza Nguvu nyingi sana kwenye umeme wa maji alafu ndio wakaja huko kwingine...

Hebu jaribu kuangalia bwawa moja tu China linazalisha karibu mara tatu ya umeme wote unaotokana na gesi asilia wa Qatar...

Alafu mtu kama Professor anakuja kusema Umeme wa maji hauna Mashiko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…