Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mm binafisi siitaki tena ccm baada tu ya magufuli kufariki wameanza kumgeuka wamesahau kabisa kabla ya 2015 walikua wakipita mjini na manguo yao kijani walikua wana zomewa wengine wana diriki kusema rais ali shauriwa vibaya, inaoneka walikua wana jali matumbo yao tu wa tz tuamukeni.
Muhongo anaongea pumba tupu hata hajui kuwa gesi inapatikana katika nchi chache sana na siyo rahisi kuzifikia nchi nyingi kwa matumizi ya umeme bali mpaka iwekwe kwenye mitungi na kusafirishwa kwa matumizi ya nishati na siyo umeme wa matumizi ya nyumbani na viwandani.Akichangia katika mpango wa maendeleo wa Serikali bungeni amesema anashangaa watu wanavyohangaika na umeme wa maji na huku dunia ya sasa ni umeme wa gesi
Uchumi wa sasa duniani ni umeme wa gesi, umeme wa maji umepitwa na wakati.
Mbunge wa Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo amesema uchumi wa gesi pekee ndiyo utakaoifikisha Tanzania kwenye uchumi thabiti.
Profesa Muhongo ametoa kauli hiyo wakati akichangia kwenye mpango wa Serikali leo Aprili 9,2021 bungeni Jijini Dodoma
Waziri huyo wa zamani wa Wizara ya Nishati na Madini amesema Tanzania kuendelea kuwaza kuhusu madini yaliyopo ni kuchelewa huku akikosoa mawazo ya kutegemea uzalishaji wa umeme mkubwa kwa kutumia maji.
Amesema Tanzania inatakiwa ijikite katika matumizi ya umeme mchanganyiko badala ya kutegemea mabwawa ya Maji ambayo wakati wowote yanaweza kukauka.
"Kuwekeza katika umeme wa maji halafu unasema utaleta fedha, huko ni kujidanganya kwani umeme wa maji huchukua muda mrefu kuanza kutoa faida, huko wenzetu wamepita wanafanya mambo kisasa” amesema Profesa Muhongo.
Amesema dunia ya sasa imegeuka na madini mengi yanayotarajiwa Tanzania yapo lakini wengine wameelekeza kwenye dhahabu, Tanzanite na madini mengine ya zamani lakini wanaacha kuangalia madini mapya ambayo yataliingizia Taifa fedha nyingi.
NB: Baada ya Dkt. Magufuli kuondoka sasa kila mtu CCM rangi yake ya zamani imeanza kurudi
Hivi kweli mmeanza kupinga project ya Rufiji baada ya Dkt. Magufuli kudondoka
CCM acheni unafiki
Sasa badala ya kutunza catchments mnahangaika na dirty sources?Hali halisi ya mto Rufiji inaanzia mkoa wa Mbeya kupitia Iringa, Dodoma, Morogoro na Pwani. Mto Ruaha si ule wa miaka ya sitini, daraja la Mkapa lilijengwa kwa kiwango cha upana wa mto Rufiji miaka ya sitini ambapo sasa kiko chini ya nusu
Come Rain Come Sun Bwawa la Stigliers GeogEthiopia wako kwwnye conflict na Egypt kwa sababu ya grand Ethiopian Dam, na wenyewe wamekurupuka? Au hawana maono?
Hao wafanyabiashara watano uliowataja ndio tunawategemea waendeleze mradi wa SGR?
[emoji106][emoji106][emoji106]Hii ni miradi inaitwa WHITE ELEPHANTS. Unaweza ukaimaliza lakini isikupe Desired Return on Investment.
Kwa mfano SGR hata ikimalizika kwenda huko Rusumo sijui ambako tuna target mzigo wa Rwanda, bado haina faida kwa vile throughout ya Rwanda ni less than 800k metric tons per annum.
Mzigo wa ndani ni very insignificant kwa vile Magufuli hakuwa na vision. Anajenga reli huku anaua sekta binafsi. Amefirisi akina Yusuf Manji, amewatisha kina Mo Dewji kwa kuwateka, amesababisha vifo vya akina Mufuruki na Shamte kwa chuki zake, Je anategemea local traders gani wasafirishe mzigo kwenye SGR?
Hiyo Stiglers Gorge ni upotevu wa Matrilioni ya hela tu kwa kuwa mabadiliko ya tabia nchi ndiyo adui mkubwa wa hydro electricity. Kamwe hawezi kupata hizo megawatt 2100 kama alivyotamba kwenye maradio na matv.
Ameshia kuharibu baioanuai ya selous tu na kuteremsha hadhi ya pori tengefu
[emoji106][emoji106]Wewe ndiye hujui, tuliza akili yako ufundishwe. Athari za mazingira kwa binadamu zinazosabanishwa na umeme wa hydro ni kubwa kuliko hiyo bei rahisi ya kunulia unit moja TANESCO. Soma athari za Guri Dam la Venezuela ambalo ndiyo kubwa kuliko yote katika South America au Three Gorges Dam ya China
Mkuu usiongee Kama si mtu mkomavu kwenye siasa za Tanzania.Kama aliweza kuwabana wazungu wa kwenye madini mpaka Boss wa Barrick akaja, kilimshinda nini huko kwenye Gas? Kama kwenye gas tumepigwa na kina JK, mbona alikuwa hawaambii wananchi, bali alikuwa anatumia propaganda chafu kusema wapinzani wanatumika na mabeberu kutaka kuuza nchi, wakati hakuna mkataba wowote wapinzani wamewahi kuingia na wageni?
Kama yeye aliogopa kuwataja waliouaza raslimali za nchi, na kuishia kuwachafua wasiohusika, una uhakika gani na huu mradi wake wa maji, hasa ukizingatia kuwa Magufuli hakuwa rais muadilifu?
Unauhakika umefika 50%Unapokula kichwa mradi wa umeme kutoka bwawa la Nyerere ambao umefikia 50% itabidi watuambie umeme tutatoa wapi?.
Thubutu zake, nani anafanya biashara ya kuanika nguo kavu?
Mkuu usiongee Kama si mtu mkomavu kwenye siasa za Tanzania.
Unapozungumza kuhusu namna gani aliwabana watu wa madini na kuwasema wapinzani wanauza nchi hakuwa amekosea mana ni kweli mtu Kama Lissu alifikia hatua kusema tukigusa hiyo mikataba tutashitakiwa MIGA huko process yote ya mabadiliko ya mikataba ya madini ilipingwa vikali sana na wapinzani hata humu jukwaani ushahidi upo humu mfono Zitto Kabwe alitoa makala nyingi sana humu kupinga hii mikataba Lissu aliziita ripoti zile kuwa Rubbish nadhani unakumbuka lakini mpambano ule mwisho ukaja na majibu mikataba ikabadilishwa.
Kaburi la gas nalo lilikuwa na mambo yake mengi mno kumbuka vurugu za mtwara enzi za mkwere kutaka gas kuletwa bagamoyo. Unapotaka kumsema Magufuli kwenye hili itabidi pia uangalie matatizo hayo yalianzia wapi hili suala la gas lingekuwa jepesi asingeacha kuligusa ila mikataba yake imekuwa tofauti na hii mingine na huwezi kufukua makaburi yote lazima Kuna mengine yatakushinda tu huo ndio ukweli ( labda tumnange tu kisiasa lakini ukweli ni huo).
Leo tunamsikia Mama anasema hadharani Kuna mambo amejaribu kusolve yamemshinda why wakati yeye ndio rais?
Hapo ndio ujue kuwa Kuna vitu vingine ni vigumu kuviondoa hata Kama una nia njema mkuu.
Hili suala la Magufuli hakuwa rais muadilifu unalitengeneza hivo ili likupe nguvu kwenye hoja yako huku hata wewe mwenyewe ukijipinga hapo juu kuwa alipigania madini kwa nguvu zote why ikawe yeye si muadilifu?
Mradi wa bandari ya bagamoyo ambao aliukuta mezani hauja pitishwa na rais ameukataa huku akieleza ubaya wa mkataba huo ambao kama ungepitishwa kabla hajaingia nina hakika asinge weza kuubali haya yote yanaonyesha uadilifu wake Leo amekufu wenye tamaa wanataka kuurudisha wapige hela kisha unakuja kumuita Magufuli si muadilifu angekubali fungu akawaweka mezani wachina wakampa chochote asingekubali huo mradi? Kwanini useme Magufuli si muadilifu ?
Tukija kwenye huu mradi nina kila sababu ya kumuamini Magufuli zaidi ya hawa maprofesa ambao rangi zao tunazijua tangu mwanzo.
Figisu za kuzuia huu mradi zilianza zamani kwa kigezo cha kuharibu mazingira na wanaharakati wa humu humu ndani waliunga mkono huku wakijua kabisa hatuna umeme wa uhakika na mazingira yalivyo kwa nchi yetu ni bora huo umeme wa maji ni nafuu kuliko gas na vyanzo vingine kwa Tanzania yetu hii bado hatuna uwezo huo.
Leo wakiibuka watu Kama hawa kwangu inakuwa ngumu kuwamini labda naweza kusema kuwa watu hawa ni mawakala wa huo umeme mbadala wanao unadi na kunafungu wanapata huku wakitudanganya wananchi na vile wengi elimu ni ndogo basi ndio tatizo kabisa.
Hiyo gas ambayo tunamiliki 30% eti ndio itumike kuzalisha umeme wa kutosha taifa zima? Serious?
Hebu fuatilia bei za gas za majumbani tu humo uone hali jinsi ilivyo.
Mkuu mimi naishia hapa, wakiona huu mradi ni mbovu okay fine waufute kisha walete hiyo miradi ambayo haijapitwa na wakati kisha baada ya miaka 10 Mungu akitupa uzima turudi tena kujadili outcome yake.
Kama Huwezi kutofautisha l na r wewe ni mburula. Kwenye miradi unaandika miladi. Huna ubongo wa kushiriki mjadala huu. Nenda kaoge umsubiri mumeo
bi samia ana mwezi madarakani.
mmeshamshangilia kana kwamba hakuwahi kuwepo kabisa duniani.
Elimu ya Watanzania kwa kweli ni duni. Unajuwa kabisa wako kwenye mgogoro na Misri kuhusu Grand Renaissance Dam bado unaniuliza je wamekurupuka?
Jibu ni ndiyo wamekurupuka. Walipaswa kuangalia treaties za mwaka 1893 na nyingine ya 1910
Kwani ameongelea reli mkuu??? Hivo vinu vya stigler gorge life span yake ni miaka mingapi compared na pesa iliyowekezwa??? Uchumi wa dunia unahama kutoka hydro power plants inahamia kwenye gesi na nuclear sisi tunawekeza trillions of money kwa vitu ambavyo lifespan yake haitafika 30 yrs to come!! Hicho kinachofanyika sasa kilitakiwa kifanyike miaka 50 iliyopita.
Tunamshangilia kwa kujitenga na siasa za kidhalimu, lakini tathmini halisi ya awali ya utendaji wake, tutaitoa ndani ya siku 100.
Akili azitoe wapi wakati kachanganya audit ambazo sio sehemu ya majukumu yake.
Environmental audit ni kazi ya NEMC sio CAG. Kichele ni fisadi alietumwa kumchafua Magufuli he needs to be sucked.
Ngereja hata bungeni hayupo ataibukia wapi ?Dooh nimecheka saana haya watu wanafufuka mmoja mmoja wanaaanza upya kuchomoa makucha yao.
Hawana tena cha kuhofia mana enzi za shamba la bibi zinarudi kila mtu anaanzisha ubunifu mpya wa kupiga pesa.
Huyu ni Muhongo tayari bado namsubiri Ngereja naye atakuja na lipi.
Na muda si mwingi tutasikia Accacia nayo imefufuliwa upya na kupewa mgodi huko geita kwasababu nchi inahitaji zaidi wawekezaji kuliko wao wanavyo tuhitaji.
Hoja za Dam55 zimekuzidi uwezoNimecheka kwa nguvu hiki ulichoandika hapa, sio kwamba una utetezi wa nguvu, bali umejaribu kuweka maelezo marefu ukidhani ndio utakuwa umeweza kutetea utakacho.
Tuanze na hilo la uadilifu, toka ameingia madarakani tumeona vikundi vya mauaji kwa jina la watu wasiojulikana, wengi wa wanaomkosoa wametekwa, kuuawawa, kushambuliwa na hata kuachwa na vilema vya maisha, huku serikali yake ikaicha kuchukua hatua stahiki. Chaguzi zote za nchi tumeona zikigubikwa na mauaji, wizi wa kura wa wazi, ushenzi, ukatili na uhayawani wa wazi, na haya yote yalikuwa ni maagizo yake. Aliondoa uhuru wa vyombo vya habari, ili aweze kufanya mambo kwa namna aitakayo yeye, bila hayo kuwekwa hadharani. Hakuna mtu muadilifu anafanya mambo haya, wala kukwepa uwazi. Toa utetezi usioacha shaka wa uadilifu wake kwenye maeneo haya.
Kwenye hilo la kwamba wapinzani wanataka kuuza nchi, nimetaka uniambie ni hatua gani kachukua kwenye waliouza nchi kwa vitendo kama hiyo Gas. Hakuna mzungu atasubiri auziwe nchi na mtu asiye madarakani, wakati walioko madarakani wanaweza kumuuzia kirahisi. Lisu alitoa maoni yake, kuwa hiyo mikataba ni michafu hivyo mazingira ya kushitakiwa yako wazi, mfano wa uchafu wa hiyo mikataba ni huo wa Gas. Hapa naona ulibebwa na propaganda, ndio maana unatumia kwenye utetezi wako, lakini huna content za maana zinazobeba utetezi wako zaidi ya propaganda mfu.
Hayo ya madini, ili nijue kweli una uhakika na ukisemacho kuhusu mikataba ya madini kubadilika, maana sio ww au mimi tumeona mikataba, huenda ww mwenzangu umeona mkataba. Sasa naomba unitolee ufafanuzi wa ule mkataba wa Barrick/Twiga wa sisi kupata 16% na faida ya 50/50, maana huwa sielewi Kabudi huwa anaongea nini. Zingatia mama juzi kasema huko kwenye mkataba wa Barrick kuna mambo hayako sawa. Ukitoa ufafanuzi wa hili nitajua unajua unachoongea, au ni wale wa kubebwa na porojo za kisiasa.
Hilo la gas sioni kama una uelewa nalo maana umetoa mfano wa bei ya gas ya majumbani. Kwa taarifa yako gas ya majumbani sio hii ya hapa kwetu, ni vyema ukae kimya kwenye hili maana utaaibika. Hilo la kwamba eti 30% ndio izalishe umeme wa nchi nzima, hapa pia umeonyesha uelewa finyu. Kwanza unajua tunahitaji % kiasi gani ili kuzalisha umeme wa kututosha? Huenda tunahitaji 10-20% tu kwa mahitaji yetu. Nakushauri kwenye hili la gas, hebu jipe muda wa kujua nini unaoongea, maana naona unabebwa na hisia zaidi, huku ukionyesha huna lolote ulijualo kwenye hili.
Hilo la mradi wa Bagamoyo, mimi nadhani ni rahisi, huo mkataba na hata wakati unazuiwa tulishauri mapungufu ya mkataba yaangaliwe, kisha yafanyiwe kazi halafu mradi uendelee. Lakini sio unazuia mkataba huo huku kukiwa na kificho cha mkataba husika, halafu unaenda kujenga uwanja wa ndege wa karibia 40b kijijini kwako, huku kukiwa hakuna uhitaji wowote wa hivyo.