Profesa Shivji: Mkataba wa Bandari unaegamia zaidi upande mmoja na hauna ukomo wa muda. Hauwezi kuvunjwa kwa sababu zozote zile

Wakishamaliza kugawana keki ya taifa, watakuja mpaka kwenye maboga na viazi vyetu.
 
Hata uki plead non est factim huutengui.
 
Spinning.


Huo mkataba wa bandari uko wapi?

Uwekeni hapa, kuna MOU ya TPA na DP World mbona hamuiweki ujionee?
 
Nipo hapa na mimi nasubiria majibu bloangu
 
Ni wajinga tu watakaomwamini Shivji na kumpuuza Mwanasheria Mbobezi kama Zembela na Jaji aliyehukumu kesi nyingi za migogoro ya mikataba Mheshimiwa Maulid Mwana wa Kitenge.
 
Shivji hajaona kifungu cha 5:4?


Wazi kabisa kinasema miezi 12 au ile miezi 12 mkataba uliiweka pale ya nini?


Nyinyi hata mki spin vipi, mkataba ni mwema sana kuliko mikataba yote tuliongia nchi hii.

Hicho kifungu unakielewaje, ili tujadiliane? Nanukuu kwa tafsiri isiyo rasmi:
5:4. Nchi Wanachama zinakubali kwamba Miradi ya Awamu ya 1 (kama ilivyofafanuliwa katika Kiambatisho 1) itakuwa ndiyo miradi ya kipaumbele katika kuiendeleza na kuitekeleza. Serikali ya Tanzania itahakikisha kwamba TPA haitaongeza mapendekezo mengine yoyote ya Miradi yoyote ya Awamu ya 1 kuanzia Tarehe ya Kusainiwa hadi tarehe ambayo majadiliano kati ya DPW na TPA kwa Miradi ya Awamu ya 1 yamesitishwa au baada ya kumalizika muda wa miezi 12 kutoka Tarehe ya kusainiwa kwa Mkataba huu, yoyote iliyo ya mapema.
 
Jeshi linalokubali kutumika kisiasa haliwezi kufanya lolote nje ya mitazamo ya watawala. Kinachofanyika ni kuhakikisha viongozi wa jeshi wanapata marupurupu yasiyoendana na kazi yao, kisha kwa ajili ya ubinafsi wanawatii viongozi wa kisiasa hata kwa mambo ya hatari.
 
Shivji Mkomunisti huyo, anapenda siasa za kimaskini.
Kwani kakataa uwekezaji au kaeleza mkataba ulivyo!¿
Tatizo mnapenda kusikia mnayoyataka......ukweli hauna tabia hizo, yaani hauna kona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…