TANZIA Professor James Shaba afariki dunia. Alifanyia postmortem mwili wa Hayati Sokoine

TANZIA Professor James Shaba afariki dunia. Alifanyia postmortem mwili wa Hayati Sokoine

Wa kwanza wa TANZANIA ni yupi?
Rashid Mfaume Kawawa alikuwa waziri mkuu wa mwisho wa Tanganyika January 1962 mpk 9 December 1962.

Kuanzia 10 December 1962 mpk February 1972 nafasi ya waziri mkuu ilifutwa.

Mwaka 1972 February nafasi ya waziri mkuu ilirejeshwa na Rashid Mfaume Kawawa akawa waziri mkuu wa kwanza wa Tanzania mpk mwaka 1977.

Kawawa alifuatiwa na Sokoine
 
Mkuu please. Acha kusema mbege ni pombe chafu. Dah!

Hata mzee Mengi mwenyewe kwenye sherehe zake aliiweka na alikunywa vilevile.

Huyo unayemjibu ni mkabila nashangaa hujamjuwa.

Ni mlokole ambaye ni mkabila.
Huyo pimbi siyo mlokole ni mlevi mbwa fulani alitumia ujana wake vibaya sasa ni mzee anaishi kwa kudoea pombe. Ana chuki sana na Wachaga anafikiri ndiyo itaondoa umasikini wake.
 
Kweli wahenga walisema, muda unaongea, na wenzetu walisema, Time Heals!
Ni mwaka 1984, ndiyo kwanza kijana mtanashati, msomi na nimepata kazi nzuri shika la umma.l
Ndo kwanza nimehamishiwa Dar toka mkoani, sasa niko makao makuu ya shirika langu.
Kwa sheria za kazi miaka hiyo nilikuwa -entirled" kupatiwa nyumba.
Kwa vile nilikuwa sijapatiwa nyumba, mwajiri wangu aliniweka hotel kubwa ya kisasa, New Africa Hotel,
Siku hiyo ilikuwa week end mimi niko Bandari Grill, na girlfriend wangu, ambaye atskuja kuwa mke wangu.

Pembeni yangu kama meza ya tatu ,nikamwona mzee mmoja yuko peke yake, akinywa Konyagi, kavu na huku yuko kimya.

Mara wakaingia vijana, kaka zangu, mmoja namfahamu ni Kapteni wa Air Tanzania, lakini yeye hanifahamu.
Nilimfahamu Kapteni George Mazula kwa vile nilikuwa na safari nyingi Mwanza na Musoma miaka hiyo na ndege aina ya Fokker Friendship 50.

Sasa wale vijana kaka zangu wakaingia wakaanza kumzonga yule mzee.
Wakaanza kumcheka wanamwambia "Profesa uko njwii, uko njwii....acha Konyagi Profesa Shaba"

Nikageuka kumtazama huyo mzee, na nikajiuliza, kumbe huyu ndiye Profesa Shaba?
Jina lilikuwa linajulikana sana, lakini mtu mwenyewe mfupi na mwembamba na ndevu za kutosha usoni.

Proffessor akameza fundo la Konyagi akawajibu wale vijana,
"Ninyi vijana, ninyi vijana" na huku akionyesha wazi kuwa kinyaji kimekolea.
"Ninyi vijana mtakuja tu mortuary, mtakuja tu. Nimemwona Sokoine nanyi mtakuja tu"

Wale vijana na Capt Mazula, walitoweka pale kama wamefukuzwa, wote wakaogopa na kutokomea haraka haraka.
Nami nilipigwa butwaa ,lakini nikamsalimia kwa adabu, "shikamoo Proffessor Shaba"

Tukaanza maongeze lakini kwa jinsi nilivyo mchulia kiheshima nikagundua kuwa amekulia Tukuyo na alikuwa anaifahamu familia yangu toka babu yangu.

RIP Proffessor James Shaba, Mungu akuweke mahali pema peponi.
Ali gwa kukaja??
 
Mara ya mwisho nilimwona pale soko la samaki la ferry.

Nakumbuka wakati akiwa Muhimbili, enzi za chama kushika hatamu. Kukatoka mwongozo kuwa mwenyekiti wa tawi wa chama awe na uwezo wa kumsimamisha mtaalam yeyote mahali pa kazi kama akienda kinyume na maadili ya chama. Wakati huo pale Muhimbili mwenyekiti wa tawi wa chama alikuwa Mama ambaye aliajiriwa pale hospitalini Muhimbili kama mfabya usafi.

Professor (RIP), akasema, mwenyekiti wa chama ni nani mbele ya profesa au dokta! Wakadai amekashfu chama, wakamsimamisha kwa muda. Mambo haya ya watu wenye uwezo mdogo kabisa kuwa juu ya wenye akili kubwa kwa Tamzania, hayakuanza leo!

Basi, Mungu wa huruma, tunamwomba amjalie pumziko jema la milele profesa Shaba.

Prof. SHABA NA PROF SARUNGI ndiyo miongoni mwa miamba ya kwanza kabisa katika tiba kwa bara la Afrika.
 
Back
Top Bottom