Projects za Mchungaji Kimaro akiwa KKKT Kijitonyama

Projects za Mchungaji Kimaro akiwa KKKT Kijitonyama

Kwenye ufiraji kunahusiana nini na Kanisa? ufiraji ni tabia ya mtu binafsi usichanganye mambo mawili kwa pamoja.

Nashukuru umelielewa hilo. Hayo ndio ungemwambia Kimaro kwamba uaminifu sio suala la dini ni la mtu binafsi. Kusema dini A ni waaminifu na dini B sio waaminifu ni ujinga wa kiwango kikubwa. Uaminifu is personal sio connected kwa religion.
 
Nasikitika sana na kuumia ndani ya nafsi yangu nikitafakari juu ya ufalme wa mbingu na mienendo ambayo sisi wanadamu tunaenenda🤔
Dhana ya kujiona na kujihesabia haki inaondoa sana utukufu wa Mungu
 
Kwenye hizi taasisi kuna namna huwa uongozi wa juu hawataki wa chini afanye makubwa yanahoonekana sana? Kisa cha likizo ya siku60 ni nn
Labda wamejaribu kuiga utaratibu wa RC tatizo wamefanya ionekane kama walikuwa na lengo la kum-seize angehamishwa bila kuambiwa habari za mapumziko isingekuwa issue kubwa sana,ukimuangalia huyu Kimaro ana kitu cha ziada ambacho siyo wengi wanacho so upo uwezekano amehamishwa kwenda pengine ili hayo mazuri aliyoyafanya hapo K/nyama akayafanye na huko na ni kitu chema sana ili kuendeleza uinjilishaji na siyo sahihi waumini kuwa wabinafsi kumng'ang'ania mtumishi maana kila mtu anapenda kupata mafundisho mazuri waache na wenzao wakayapate.

Sijui KKkT baada ya Mungu wachungaji huwa wanaapa kwa nani ila Catholic upo utaratibu wa kawaida wa Padre kuhamishwa na Askofu wakati wowote baada ya kuhudumu parokia fulani kwa miaka mitatu au zaidi,wapo wanaohamishwa ghafla kutoka sehemu A kwenda B kwa sababu wanakuwa na vitu vya ziada ambavyo ni vya ziada ktk utendaji wao na hizo sehemu huwa ni zile zilizokuwa chini sana kimaendeleo ili wakaziendeleze kwa ushawishi wao na mahubiri yao.
 
Acha kufundisha watu unafiki ww. Mnapenda mtu anaye sugur-coat uovu ili iweje.

Unafiki gani nimeongea?. Kukiri hadharani kuwa vijana wa kikiristo sio waaminifu ni kosa kubwa Sana kwa mchungaji. Kisa kaibiwa na washirika wake anawaingiza vijana wote wa kikiristo.

Mchungaji ni mlezi na mshauri. Alipoona Kuna shida ya uaminifu kwa vijana alitakiwa aandae semina kabambe hapo kanisani kwake kuhusu uamnifu na afundishe jinsi ya kuwa mkristo.

Tatizo lako na Kimaro mnauchukia Ukristo na kuhamia uslamu hamuwezi. Mmebakia kutukana na kufanya Ukristo hauna maana kisa makosa ya wajinga wachache ambao mmeshindwa kuwarekebisha.
 
Tujikumbushe, projects kadhaa ambazo Mchungaji Dkt. Kimaro amezifanya akiwa Mchungaji Kiongozi, KKKT Usharika wa Kijitonyama,
1. School of Healing (Morning & Evening Glory) -Youtube Channel (mwanzoni ikiwa Eliona Kimaro TV baadae KKKT Usharika wa Kijtonyama) inayowafikia watu wote Duniani.
2. TAMASHA LA MBINGU KUJAA SIFA (kila mwaka)
3. Jengo jipya la Sunday School (lililogharimu yapata takribani 200m TZS)
4. Ununuzi wa Kiwanja pembezoni mwa kanisa yapata 300m TZS
5. Kusomesha yatima yapata 100
6. World Pray Online (WPO), Call Centre ya maombi masaa 24, siku 7 za wiki.

NB: Ikumbukwe waliokuwa wanasali hizo Morning & Evening Glory wengi hawakuwa waumini wa KKKT bali wa madhehebu mengine na Waislam kuondoka kwake Dkt Kimaro tutarajie mabadiliko kiasi.

***Mchungaji Kiongozi (Mpya) Anna apewe ushirikiano kuendeleza alipoishia Dkt Kimaro.



Mungu ambariki sana Mtumishi wake kwa kutumia vizuri kipawa alichopewa.Nadhani muda wake hapo ulikuwa umeisha,kazi yake ilikuwa imeshakamilika.Sasa itakuwa ameitiwa sehemu nyingine. Pengine labda huko Maneromango,Mkuranga, au Zanzibar na kwingineko ambako kuna hitaji wabunifu kama yeye ili kulijenga na kuliinua kanisa la Bwana.

Tusisaha, kila mahali ulipo kama ikiwa unareport kwa mtu mwingine(yaani unaye bosi) na kabla yako kulikuwa na mtu mwingine.Ujue hapo unapita tuu.atakuja mwingine.Dr.Kimaro alilijua hili kwa sababu hakuanzia huduma hapo,kuna mahali alitoka.Huko atakaoenda atakuta pia kazi walizozifanya walio mtangulia,kama ambavyo Mch.Ana amekuta kazi za Mch.Dr.Kimaro na walio mtangulia.

Uzuri mmoja wa watumishi wa KKKT,wakifika mahali wanasimamiaga maendeleo ya hapo as if watakuwa hapo milele.Hawanaga ubinafsi ule wa nawezaje kufanya maendeleo hivi wakati sina uhakina na kama nitakaa muda gani hapa.

Kile wanachofanya baadhi ya waumini cha kuendelea kuongelea vibaya maamuzi yaliyoganywa na mamlaka iliyojuu yake,ni kuendelea kumfarakanisha Mch Dr.Kimaro na hiyo mamlaka .Ni kumvika roho ya ujeuri,kiburi na majivuno na kuua kabisa roho ya unyenyekevu,hekima utilivu,uvumilivu na utu wema.Yaani wanambebesha lawama kwamba hao wanaofanya hivyo amewatuma yeye(Ingawa mimi binafsi siamini hivyo).Hasa ukichukulia wote walionekana wanaandamana ni wachaga.

Yeye mwenyewe Mch.Dr.Kimaro alisema wazi ametii mamlaka yake atafanya hivyo kama alivyotakiwa kufanya.

Mzee Jakaya Kikwete(kama ,sijakosea) aliwahi kusema,kiongozi bora na mkomavu utamjua pale linapotokea jambo gumu la kumtikisa.Aliyebora atakuwa mtulivu sana (Very calm) .Ila kiongozi wa hovyo likitokea jambo gumu litamvuruga na atakurupuka vibaya
 
Kila usharika KKKT una baraza la wazee, sharika ngapi zimefanya hayo yote? Nenda Usharika wa Sinza, hiyo Youtube Chalinze ikiwa live viewers wakizidi sana 15 na bado wanapambana na Deni mpaka kesho, Mwenge hali kadhalika.
NB: Kimaro hata apelekwe GEZAULOLE ataonyesha maajabu, jiulize kabla ya Kimaro-Knyama hapo Kinyama mbona kulikua jiiiii
Mimi nikajua Kkkt wana uelewa kidogo, kumbe nako kuna ng'ombe wanaoenda Kanisani kwa sababu ya kumfuata mchungaji fulani kama ilivyo wale ng'ombe wa mwamposa na huko kwa wakina gwajima.
This kind of madness will never be found in a Roman Catholic church.
 
Nashukuru umelielewa hilo. Hayo ndio ungemwambia Kimaro kwamba uaminifu sio suala la dini ni la mtu binafsi. Kusema dini A ni waaminifu na dini B sio waaminifu ni ujinga wa kiwango kikubwa. Uaminifu is personal sio connected kwa religion.
Na mimi nashukuru pia kwa kunielewa.
 
Nashukuru umelielewa hilo. Hayo ndio ungemwambia Kimaro kwamba uaminifu sio suala la dini ni la mtu binafsi. Kusema dini A ni waaminifu na dini B sio waaminifu ni ujinga wa kiwango kikubwa. Uaminifu is personal sio connected kwa religion.
Hayo ndio ungemwambia Kimaro kwamba uaminifu sio suala la dini ni la mtu binafsi[emoji817][emoji818]
 
Hii ni kweli kabisa!

Yani hao Viongozi wanataka waumini wasipate badiliko la kimwenendo,

Wanataka waumini wabaki na Ukristo wa jina badala ya mwenendo na tabia?!

Wanajiita Wakristo lakini wachawi, ndugu na ndugu hawaongei miaka nenda , washirikina kama wasio amini

Sasa yanakuja mafundisho mnaleta mikingamo?!

Aibu yenu!

Siku 60 ?

Tunasubiri taarifa ya uchunguzi.

Hayo yote anaweza kuyafanya nje ya KKKT kwani shida ipo wapi?. Aige mfano wa Mch Mitimingi baada ya kuona anachofanya hakikubaliki na uongozi ndani ya TAG , aliamua kuanzisha ministry yake.
 
Hayo ndio ungemwambia Kimaro kwamba uaminifu sio suala la dini ni la mtu binafsi[emoji817][emoji818]
Mnatetea ujinga hadi mnajitoa ufahamu. Unatenganishaje uaminifu na dini wakati dini hiyo hiyo inatusihi tuwe waaminifu.
 
Back
Top Bottom