Psychic Powers: Ni nguvu za kufanya miujiza. Wengi wanazo bila kujitambua. Je, wewe unazo?

Psychic Powers: Ni nguvu za kufanya miujiza. Wengi wanazo bila kujitambua. Je, wewe unazo?

Pasco hebu nifafanulie hapa, kulingana na mada yako; huku kwenye imani/dini yangu kuna wakati tunapambana na hizo nguvu ulizoziita za giza pamoja na wachawi kwa ujumla. Katika mapambano haya siku zote tunazishinda na kuwashinda wachawi kwa kutumia JINA LA YESU na Maandiko ya Biblia Takatifu. Je, kama kweli hizo nguvu hazimo katika jina hili na Biblia yetu, kwanini hao wachawi wasinishinde siku zote endapo nguvu zetu binafsi ndizo zinazopambana? Ufafanuzi pls!
 
Mh hapa sasa ndio penyewe nimekua nikifanya kitu nahisi kama kuna siku nilishakifanya lakin tatizo sikumbuki ni wapi na lini kwa mfano naweza kukutana na mtu popote pale iwe njiani au kwenye gari na tukianza kupiga piga stori nakuwa kama napata picha ya hayo tunayozungumzia yalishapita lakini kiuhalisia haijawahi kutokea, hapa nitakua katika kundi gani mkuu Pasco
Mkuu MC RAS PAROKO, hii inatwa De-javu, yaani unakutana na mtu unajiona uliisha wahi kumuona!, au unafika mahali papya kwa mara ya kwanza, unajiona kama uliishawahi kufika hapo!.

Sababu kuu ni mbili.
1. Huwa unatembea kwa astra travel, hivyo huyo mtu umekutana nae huko, au hapo mahali ulipatembelea hivyo kumbukumbu zimehifadhiwa kwenye sub-concious mind yako, unapomuona au kufika mahali hapo, phisical mind inalink na sub-concious na hivyo kukujulisha ulishamuona, au mahali hapo uliishafika!.
2.Remote viewing - Gathering of information at a distance. Hii ni kuwa kabla hujafika hapo, mind yako imetembelea hilo eneo au imemuona huyo mtu kabla, hivyo unapomuona, unajiona uliisha muona au hapo mahali uliishafika!.
3. Kwa waumini wa Hinduisim, Buddhiisn na Krisna, wanaamini kwenye life after life na life before life katika kitu wanachoita reincarnation, hivyo hoyo mtu ulikutana nae katika life before, na hapo mahali ulifika kwenye maisha yako ya before, hivi hayo maisha yako ya sasa ni "after life!".
Pasco.
 
Pasco hebu nifafanulie hapa, kulingana na mada yako; huku kwenye imani/dini yangu kuna wakati tunapambana na hizo nguvu ulizoziita za giza pamoja na wachawi kwa ujumla. Katika mapambano haya siku zote tunazishinda na kuwashinda wachawi kwa kutumia JINA LA YESU na Maandiko ya Biblia Takatifu. Je, kama kweli hizo nguvu hazimo katika jina hili na Biblia yetu, kwanini hao wachawi wasinishinde siku zote endapo nguvu zetu binafsi ndizo zinazopambana? Ufafanuzi pls!
Mkuu Amri kuu ni Upendo, kuna vitu havijaandikwa popote kuhusu source of power za Mungu au za Shetani!.

Hii n i tafsiri yangu binafsi.

  1. Wengi wanadhani kuwa Mungu ndio aliumba vitu vyote!, sii kweli, Mungu hakuumba vitu vyote!, bali ameumba dunia na vyote vilivyomo. Nje ya dunia, sio vyote!. Shetani yuko nje ya dunia!.
  2. Mwanzo wa Mungu, pia ndio huo huo mwanzo wa shetani!. Alikuwa ni 2nd in command akiwa 2nd with powers, mpaka leo mpaka kesho shetani ameondolewa tuu ile position ya 2nd in command but not his powers!.
  3. Mungu ni omnipotent na omnipresent, so does shetani!. Hivyo kwa vile Mungu ni power za mwanga (light) ukiwa nazo unaitwa "enlightened", na shetani pia ni power!, nguvu zake ni za giza "powers of darknes" kwa vile Mungu yupo ndani yetu, vivyo hivyo shetani yupo ndani yetu!. Ukitenda mema, ndio unatumia nguvu za Mungu, ukitenda maovu unatumia nguvu za shetani!.
  4. Mungu ana watumishi wake, mwanaye Yesu Kristo, Malaika na Roho Mtakatifu ambavyo vyote pia ni powers na ukitenda mema, huwakarinisha ndani yetu. Shetani pia anakundi lake la malaika wabaya, mapepo, majini, maruhani, liroho!.
  5. Ukimtumiakia Shetani, wenyeji wa mwili wako wanakuwa ni watumishi wa shetani, ndipo unaposikia fulani ana mashetani, majini, anatumia nguvu za giza!, wale watumishi wa Mungu, wanakukimbia!. Ukitumia nguvu za Mungu, watumishi wa shetani wanakumbia, na ndio hao mapepo wanaotolewa!. Kinachotolewa kwako ni watumishi tuu wa shetani au watumishi wa Mungu, sio Mungu mwenyewe wala sio shetani mwenyewe!.
Kwa maana hiyo vita vyote vya Mungu na shetani, vyote vinapigwana ndani yetu, Mungu is always there ila anayewakaribisha watu wake ni wewe kwa sababu Mungu yuko ndani yetu!. Na shetani pia yupo!, anayewakaribisha watu wake ni wewe mwenyewe!. Ukiwa imara katika Mungu, shetani hawezi kufanya kitu, hata wakuloge, hulogeki hata wakutupia majini, mapepom mashetani, hayawezi kukuingia!. Anayamkaribisha Shetani ni wewe, na anayemfukuza pia ni wewe regardless unatumia jina la nani!.
Pasco.
 
Imani yao hawa Monks inapingana au inashabihiana vp na imani ya kikristo na/au uislam?
Mkuu Sabayi, hawa monks wamevuka stage ya imani!, they are powers!. Kama hukujua unajua baada ya kukufuka Yesu iliishi wapi?. Alitembeaje?!. Alikulaje?, hayo ndio maisha ya hawa monks!, Yesu alitembea juu ya maji!, hawa jamaa wanatembea juu ya maji!. Yesu alikuwa akiibuka na kupotea, hawa jamaa wanatokea na kupotea!. Yesu alikuwa akitembea kwa kupaa!, hawa jamaa wanatembea kwa kupaa!. Ukristo ni wa juzi tuu! na Uislamu ni wa jana tuu, dini ya hawa jamaa ilikuwepo kitambo sana!.

Kwa hizi dini za zamani Hinduism, Buddhiism na Taoism, kuzilinganisha na Ukristu, ni kama mlima na kichuguu!.

Wewe ambaye umezaliwa kwenye kichuguu, umekulia kwenye kichuguu, na unaishi humo humo ndani ya kichuguu, nyie humo ndani ndio mmeambiwa hicho kichuguu chenu, ndio mlima mkubwa kabisa kuliko yote!. Kwa sababu unachikijya ndio hicho hicho kichuguu, hivyo kinakuwa ndio mlima mkubwa wako!.

Ili kuweza kulinganisha, inakubidi wewe sikumoja utoke humo ndani ya kichuguu itembee tembee huko nje, utakaouna mlima mkubwa, uuliza hilo dubwana ni nini?, utaambiwa huo ndio mlima mkubwa!, utashangaa na kuuliza huo utakuwa ndio mlima wakati umeelezwa mlima mkubwa ni ule wewnu wewe ulimotoka!. Ndipo utakapoambiwa mlima mkubwa ni huo unauona!, mule wewe ulimotoka sio kwenye mlima mkubwa, bali umetoka kwenye kichuguu tuu!. Ukilinganisha huo mlima na kile kichuguu sasa ndio utajua ulima ni upi na kichuguu ni kipi!.

Hivi ndivyo ulivyo Ukristu na hizi dini!. Nimekaa kidogo India, nimezisoma kidogo, ndipo nikagundua kumbe Ukristu ni kichuguu tuu!. Pamoja na ukichuguu wa Ukristo, ninaendelea kushikamana nao, ila when it comes to powers, powers zote ziko ndani yetu!.
Pasco.
 
hapa sasa nimeunganisha dot nishapata jibu hakika kweli hii dunia ni ya ajabu sana..hasa juu ya usili wa haya mambo hili somo lilifaa kufundishwa mashuleni japo hata kwa mara moja kwa wiki tuu.

hakika kuna mistari kwenye bible inasema MNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA.

hii mada kuna society 1 ambayo imejipatia sana umaarufu hapa nchini kwa sasa na inaaminika ukiingia huko unakuwa tajili hakika naanza kuamini yawezekana mambo yenyewe ndio kama haya.
ukizingatia kuwa nembo yao ina picha ya JICHO hapo ndio kabisaaa nakosa jibu sahihi ngoja niendelee kuunganisha dot.
kwakuwa mm nitomaso next week end lazima nifike huko upanga kwenye sineme zao. ili nipate ushahidi mwenyewe
 
Huyu TB JOSHUA anaonekana kama ni noma sana, yeye anapasua mbuga toka Nigeria mpaka EA!!! Dah... saaaasa hebu nieleze kwa hawa wahubiri wa bongo ni nani noma zaidi? Gwajima, mzee wa upako, Mwingira, Rwakatare, Swai, Malasusa, Pengo na mtokambali? kama vp ni-PM tu man sidhani kama wengine wanataka kulijua hili....
 
Mimi ninazo 2:
  1. Astral projection: Nimewahi kuhama kutoka ndani ya mwili wangu kama mara 2 hivi, moja ni pale nilipokuwa natembea barabarani halafu nikajaribu kuhama kutoka kwenye mwili, nilipourejea nikaukuta umelala chini kwenye vumbi katikati ya barabara, sikufurahia tendo hilo zaidi ya kuogopa! Pili, ni pale nilipokuwa nimekaa kwenye kiti nikisikiliza mziki laini na kujaribu kuzama kwenye huo mziki na kuuacha mwili wangu ambao baadaye nilijikuta nimelala sakafuni!
  2. Hii ya pili bado sijaijua jina au haipo kwenye list hapo juu: Nina uwezo wa kuwaona watu walio uchi ambao wenzangu huwa hawawaoni kila ninapojaribu kuwaonesha, wamefikia mahali wanadhani mimi ni mchawi!

Nimeipenda mada hii, nadhani ni ukweli mtupu ingawa inaweza kuonekana kituko kwa wengine!
 
Mimi huogopa kwa kweli kuingia deep katika haya mambo kwa sababu huwa yanaogopesha sana. Wakati mwingine yanakuwa kama yanakinzana na Imani tulizolelewa nazo.
Big up kwako Pasco na wadau wengine wenye nia na hii elimu ya ufahamu. Mimi naitumia selectively kwa mambo machache.
Huwa nasoma vitabu vya mind & psychology na kugundua mambo mengi sana.
Mkuu Utali, usemayo ni kweli, mimi nilifikia stage ya kujiungana Illuminati waitwa Rosecrusins, hawa ndio the most powerful of all, wanaweza kuchange their body vibration at will na kuwa invicible!. Tatizo lao wanataka kwanza lazima ufanyiwe ukubali kula kiapo cha usiri, ndipo ufanyiwe initiations ndipo uwe member!. Hili la kiapo na initiations liliniogopesha!. Freemasons ni cha mtoto!.

Kiukweli lazima uwe very selective, unatafuta powers zipi kwa sababu za Mungu na za shetani ziko hapo hapo from within!.
Pasco.
 
Mkuu Utali, usemayo ni kweli, mimi nilifikia stage ya kujiungana Illuminati waitwa Rosecrusins, hawa ndio the most powerful of all, wanaweza kuchange their body vibration at will na kuwa invicible!. Tatizo lao wanataka kwanza lazima ufanyiwe ukubali kula kiapo cha usiri, ndipo ufanyiwe initiations ndipo uwe member!. Hili la kiapo na initiations liliniogopesha!. Freemasons ni cha mtoto!.

Kiukweli lazima uwe very selective, unatafuta powers zipi kwa sababu za Mungu na za shetani ziko hapo hapo from within!.
Pasco.

Asee mkuu pasco una akili nyingi na wewe sii wa kawaida. Hivi hawa Illuminat na free manson wana tofauti gan?

Nliwahi kusoma kitabu cha Dan Brown "the lost symbol" kuna professor flan mule ndan anaitwa Langdon anaonesha kwamba freemanson is just a secret societ ambay fundamentaly wana gud intention na dunia na watu wake. Sema wanahis kuna knowledge ambazo haziwez kuwa revealed, ni kw ajili ya wachache wenye uadilifu na nia njema na dunia.
 
Billioness, monks wa Tibet ni habari nyingine!, wanaitwa shaven heads, wanavaa shuka ya orange huku wamenyoa vipara, saa zote wanatembea na tasbihi huku wakifanya mantra!.

Hawa monks kwanza wanatembea peku!, kwenye milima ya ncha kali bila hata scratch miguuni mwao!. Pili wanatembea kwa miguu hadi kilometa 600 kwa siku!, kinachofanyika ni kuonekana kama wanatembea, wakati i actual case wanapaa!, miguu haigusi chini, wanatembea hewani japo wanachapa miguu!. Kula yao pia ni issue!. Wanaweza kupiga 40 days bila chakula, bali ni maji tuu na vijani fulani, wanatumia powers fulani kusimamisha metabolisim na hata ku control heatbeat!.
Hawa monks ni miongoni mwa noble kweli kama aliowazungumza Yesu, hawabebi begi la safari, wala mfuko wa chakula, kila wafanyacho kitajiseti chenyewe mbele kwa mbele, Temple yao iko Kisutu opp. Kisutu Sec.
Pasco.

Au kaka ndio maana Steve Jobs yule founder Apple Inc. Kabla ya uzinduzi wa Apple comptures alienda India kwanza kujifunza Buddahism na inasemekana Jobs hakuwa anapenda kuvaa viatu kama Monks. Je kwa elimu uliyoipata wewe uko South hizi dots nazojaribu kuziunganisha hapa zinaweza kuwa ndio mafanikio ya Steve Jobs na Apple kwa ujumla.
Kitu kingine kama ombi binafsi ebu endelea kutupa experince ya uliyojifunza India..na sehemu zote ulizawai pita vitu vipi vya kustajabisha na kufurahisha ulivyowai viona.
Na nimeshawai ona CNN hawa Monks wa Tibet wakijichoma moto hadhalani kama njia ya kudai uhuru wao kutoka China..hii inakuaje?
Kitu kingine mi ni mpenzi wa busara za Dalali Lama huyu kiongozi wa Tibet vipi nae anauwezo ka hao Monks wengine au ye kajikita kwenye politics tu
 
Mimi ninazo 2:
  1. Astral projection: Nimewahi kuhama kutoka ndani ya mwili wangu kama mara 2 hivi, moja ni pale nilipokuwa natembea barabarani halafu nikajaribu kuhama kutoka kwenye mwili, nilipourejea nikaukuta umelala chini kwenye vumbi katikati ya barabara, sikufurahia tendo hilo zaidi ya kuogopa! Pili, ni pale nilipokuwa nimekaa kwenye kiti nikisikiliza mziki laini na kujaribu kuzama kwenye huo mziki na kuuacha mwili wangu ambao baadaye nilijikuta nimelala sakafuni!
  2. Hii ya pili bado sijaijua jina au haipo kwenye list hapo juu: Nina uwezo wa kuwaona watu walio uchi ambao wenzangu huwa hawawaoni kila ninapojaribu kuwaonesha, wamefikia mahali wanadhani mimi ni mchawi!

Nimeipenda mada hii, nadhani ni ukweli mtupu ingawa inaweza kuonekana kituko kwa wengine!
Mkuu Mpigania Uhuru, tangu nimeanzisha hii mada, wewe ndio wa kwanza mwenye higher powers, wengine tunazo tunazo ila ni za kawaida!. Hapo ulipo wewe tayari ni bilionea ila tuu, hujayatia mkononi mabilioni yako. Yi have some of top powers, hivyo mtafute Uri and off you go!, wewe sio mwenzetu!.

Hilo la astra projection, nimesoma procedure zote, nikaogopa maana kuna warning kali inatolewa kuwa ukiwa out of body, anything ikitokea kwenye ule mwili wako uliouacha, ukirudi, huwezi tena kuingia, huku nyuma utabaki tuu kushuhudia msiba!.

Hilo la pili, umejaaliwa power ya Sixth sense ya second sight - Perception outside the known human senses. Hao unaowaona ni wachawi na wanga, wao hawakuoni kama unawaona na wengine wote wasio na hiyo sixth sense huwa hawaoni!, ila akitokea mtu akapandisha mashetani, huwaona na kupiga makelele!.

Unachotakiwa
  1. Kwanza uifanyishe mazoezi ya kuicomand hiyo sense!. Kwa sasa inaibuka pale tuu wachawi wanaibuka!. Sasa fanya mazoezi kuiibua hata bila ya wachawi kwa kuanza na vitu vodogo home!. Mfano itazame saa au mobile phone, concentrate!. Then mpe mdogo wako akaifiche chumbani. Kisha ingia room, funga macho, kumbuka ile vision ya simu, fingua macho, itaopna simu ilipo!.
  2. Fanya mazoezi ya kuona vitu vingine visivyoonekane na sio mpaka wachawi!. Kwa sasa unawaona wakiwepo, then kwa mazoezi ile wakija tuu unawaona!, kisha sio tuu kuwaona wachawi bali hata wezi!, hata kama umelala usingizi, mwizi akiingia tuu kwako, unashtuka, uki will, unamuona beyond everthing!.
  3. Mazoezi haya yanaitwa Dowsing - Ability to locate objects, unachofanya ni kuichannel hiyo power ya sixth sense, sio tena kuona wachawi, bali kuona mali!. Ukifanikiwa kwenye ku locate vitu vodogo vidogo, anza na vikubwa. Take time, nenda Mererani, omba kuangalia row Tanzanite. Then angalia udongoni kulocate Tanzanite zilipo, kwa miadi ya just 10% ya thamani. Jamaa atachimba akiikuta then unafuatilia mawe makubwa makubwa!.
  4. Tafuta kitabu cha Fortune Secret cha Gellar ujifunze jinsi ya kuzichanneli hizo powers. Yeye sasa ni bilione mkubwa mwenye ma royalities kibao kutokana na kubashiri yalipo mafuta, hivyo wanachimba visima vya mafuta!. Tazama row gold, chukua ramani, saka gold, utaiona ilipo, nenda eneo husika, angalia ardhini ile gold utaiona!. Ikichimbwa, 10 percent ni yako, kwa sababu exploration costs billions!.
  5. Unaweza jikuta unazo powers nyingine kibao ila bado hujajijua!.
Pasco.
 
Asee mkuu pasco una akili nyingi na wewe sii wa kawaida. Hivi hawa Illuminat na free manson wana tofauti gan?

Nliwahi kusoma kitabu cha Dan Brown "the lost symbol" kuna professor flan mule ndan anaitwa Langdon anaonesha kwamba freemanson is just a secret societ ambay fundamentaly wana gud intention na dunia na watu wake. Sema wanahis kuna knowledge ambazo haziwez kuwa revealed, ni kw ajili ya wachache wenye uadilifu na nia njema na dunia.
Mkuu Sixga, sio kweli kuwa nina akili kihivyo, bali hivi vitu nimevisoma tuu!.
Ma master wa Illuminati ni rosecricians, fremasons ni kiji branch kidogo ila wote ndio wale wale, "secret society!". Tofauti ya Illuminati na Freemasons ni illuminadi mambo yao yote siri!, freemasons public service yao sio siri!. Ukiwasoma wanaonyesha kama kama wana god intentions, kama ni hivyo why hizo secrets meeting?!. Nawafahamu baadhi ya matajiri ni freemasons, ukiwaangalia unaona vicheko kwenye midomo yao but evil machoni mwao!, hata huyu "tajiri wetu", japo misaada mingi, but deep down he is evil!.
Pasco.
 
Back
Top Bottom