Psychoanalysis Trends za Viongozi Wetu, Humbleness ya Rais Samia ni Bonafide Genuine, ni asili yake, ni nature yake, ndivyo alivyo, Ila...

Psychoanalysis Trends za Viongozi Wetu, Humbleness ya Rais Samia ni Bonafide Genuine, ni asili yake, ni nature yake, ndivyo alivyo, Ila...

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Moja ya topic ngumu sana humu JF, ni topic za kitu kinachoitwa Trends Readings za psychoanalysis trends, kinacho tokana na ku Psychoanalyse Trends kisaikolojia kwa kutumia tabia za mtu za nyuma, tabia zake za sasa kuweza ku détermine tabia zake za huko tunakwenda na ni nini kitakachokuja kutokea baadae in near future in short term, médium term na long term.

Trends Reading ni Nini, na Zina Kazi Gani, na Zina Faida Gani?.
Kwa kifupi, trends ni mielekeo, hivyo trends readings ni kusoma mielekeo, faida ya kusoma mielekeo, au direction, na kuangalia kule mliko toka, hapo mlipo mlipo, ili kujua kule mnakokwenda. Ni kama somo la Historia, ni kujifunza mambo ya zamani, kule tulikotoka, kulinganisha ya sasa hapa tulipo, hivyo kuweza kujua kule tuendako. History is the study of the past in relation to the present, to determine the future. Hivyo faida kubwa kabisa ya trends reading is the determination of the future. The future haijiji tuu kama kudra ya Mwenyezi Mungu, inakuwa determined na matendo yako ya nyuma, matendo yako ya sasa, hivyo kuipanga kesho yako iweje.

Trends Reading Sio Utabiri, Sio Ubashishiri, Ni Usomaji wa Mienendo na Mielekeo, Matokeo ya Trends ni Uhakika Zaidi Kuliko Utabiri na Ubashiri.
Kuna watu wanachanganya ubashiri, utabiri na trends readings. Japo yote matatu, yanaweza kusema kitatokea nini in future, mtabiri yeye anatumia mizimu kuuliza na kuona kitatokea nini, hawa wanaitwa scorchers, kuna wasoma nyota wanaoweza kukuambia yajayo kwa kusoma nyota yako, hawa wanaitwa astrongers, kama Sheikh Yahaya Hussen. Kuna wabashiri, hawa ni watu wa kubahatisha tuu kama bahati nasibu, Simba na Yanga zikicheza, kuna matokeo matatu tuu, au kushinda, kushindwa na sare. Wabashiri wanabahatisha lolote likitokea, wanakula bingo kwenye betting. Trends Readers, sio wanajimu, sio wabashiri ni watu wa kawaida tuu ambao ni wasoma mielekeo, trends na kuweza kusema kitatokea nini in future kutokan na matendo au matukio ya nyuma, matukio ya sasa na hivyo kujua matukio yajayo.

Kwa vile mimi ni mtu wa mastori mastori, kwa wapenda mastori, sasa kwa faida ya wenzetu wasio penda long stories, mnaweza kuishia hapa, na kwenda kusoma conclusion.
Kwa wale tunao endelea tuanze na Psychoanalysis ni nini na ya kazi gani au inasaidia nini?.
Psychoanalysis ni Nini, na ya Kazi Gani?
Kuna msemo usemao, information is power, yaani ukiwa na taarifa sahihi, unakuwa na nguvu, hivyo hii psychoanalysis ni somo la kujifunza kwa nini watu wana behave kwa namna fulani kwenye situations fulani. Hivyo ukijua tabia za watu, kwa nini they behave the way they behave, wewe unakuwa na power ya kuwafahamu na sometimes bila wenyewe kujifamu, hivyo kwa kuandika humu kuhusu human behaviors, hii inaweza kuwasaidia kubadilika, and changing for the better kwa kupunguza maneno na kuongeza vitendo. Waalimu wakuu wa hili somo la psychoanalysis, ni wawili, Carl Jung na Sigmund Freud.
Carl Jung na Sigmund Freud ni Nani na Walifundisha Nini kwenye Psychoanalysis?
Hawa ni mabingwa wa somo la saikojia ya watu na walijikita katika kufanya analysis za kubaini chanzo, the motive behind, tabia, maneno na matendo ya baadhi ya watu, huku Freud akijikita zaidi katika mahusiano ya kifamilia na Jung akijikita katika mahusiano ya kijamii, hivyo Freud kuheshimika kama mwanzilishi wa psychoanalysis na Jung akawa ni muasisi wa analytical psychology au Jung psychology, tena ingekuwa ni amri yangu, ningeamrisha viongozi wetu wote wapatiwe semina ya Jung Pschology inafundishwa katika kituo cha TAGLA pale IFM, kwa njia ya distance learning, kutawasaidia sana, maana kuna wengine wanadhani kuongea sana, kuhutubia sana, au kuongea kwa ukali na vitisho, ndiko kutalisaidia taifa hili kupata maendeleo!. No way, maendeleo ya kweli hayaletwa na maneno, na ukali au vitisho, bali yataletwa na matendo na mipango mkakati!, Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno
Trends Readers Humu JF ni Kina Nani na Jee Hizo Trends Zao, Zilikuja Kutokea? Humu jf tuna trends readers kibao, na kila uchao, kuna trends humu huwa zinawekwa na kweli mwisho wa siku zinakuja kutokea. Mimi ni mmoja wa hao ma trends readers wa humu jf, na kuna trends zangu nyingi tuu zimekuja kutokea, na moja ya tends zangu zangu kubwa kabisa kutokea, ni trend ya ujio wa JPM, hii niliisema hapa Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli kwenye bandiko hilo kuna vitu nilivisema, na kweli vikaja kutokea, hivyo JPM kweli ajaja kuwa ni rais wa JMT. Baada ya ushindI wa JPM, nilizungumzia trends za uwezekano wa jambo fulani na nikasema Watanzania tuombe sana Mungu ndio uzuie hili lisitokee Elections 2015 - If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him! na kweli hili lilikuja kutokea na ni kweli Mungu aliingilia kati ndio akatuletea Samia.

Wengi wetu humu baada ya uchaguzi mkuu mmoja, hutulia na kusubiria uchaguzi mkuu mwingine, lakini mimi baada tuu ya JPM kushinda ile 2015, niliwapa trends za matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2020, toka ile ile 2015. Kwa kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020? sasa kwa vile sio wengi humu ni wasoma trends, kuna wengi walishangazwa na matokeo ya uchaguzi wa 2020, lakini kwa wale wote waliosoma nyuzi kama hizi Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition? Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? Swali la Ukweli Mchungu: Je, 2020 Magufuli ana mpinzani au mshindani, au ni Magufuli tu?. Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Trends Za Rais Mwanamke Tanzania na Kutajwa Kwa Jina la Samia Suluhu Hassan.

Angalia tarehe ya bandiko hili la Trend ya Tanzania kupata rais mwanamke ikawekwa lini na aliyetajwa kufiti urais ni nani Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?

Trends za Samia Suluhu Hassan.
Kabla sijazizungumza Trends za Samia Suluhu Hassan, naomba kutoa crédits kwa mwana JF huyu Political Jurist , kwa bandiko lake hili ndilo lime ni inspire kupandisha bandiko hili.
RAIS SAMIA HAJAJIKWEZA, AMEWASHUKURU WATANZANIA

Na Mwandishi Wetu.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wakati akiwasili nchini Rais wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa shukrani za dhati sana kwa thamani kubwa aliyopewa na watanzania.

Pamoja na uchovu mkubwa baada ya Safari ndefu, Rais Samia amekubali kuongea na maelfu ya Watanzania waliojitokeza kumpokea katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mwl JK Nyerere.

"ASANTE" Hii ndiyo kauli kubwa iliyotawala katika mazungumzo yake yote. Rais ametambua maombi na dua mbalimbali za watanzania, hii ni faraja kuu.

Pamoja na Rais kufanya vizuri sana katika hotuba zake huko UN, bado hakupenda kujikweza bali aliamini ni kwa maombi na dua na sala za Watanzania wote.

Tuendelee kumuombea Mama, tuliombee Taifa

#TwendePamojaView attachment 1952825
Samia Suluhu Hassan, hivyo ndivyo alivyo, unyenyekevu ni asili yake, ni nature yake, ni jadi yake na nadhani hivyo ndivyo walivyo lelewa, kufunzwa na kukuzwa kwa mwanamke wa Kiislam. Tufike mahali tukubali hata ustaarabu wa modern civilisation ulianzia Arabuni Misri enzi za ma Farao, hivyo hata kuna msemo wa Kiswahili "kuwa mstaarabu kama mwarabu" Neno ustaarabu limetokana na neno Ustaadhi kushika dini na Uarabu, na ni kweli washika dini wengi ni Wastaarabu sana, hata mimi nikiwa TBC niliwahi kuwa attached kule TVZ tena nikiwa nimeisha oa ndoa ya Kikristo Kikatoliki, almanusura nibadili dini kugeuka Muislamu ili nioe Zanzibar, kisa ni ustaarabu tuu sa binti mmoja wa Kizanzibari.

Mimi nimemfahamu Samia tangu akiwa nobody kule Zanzibar, Samia was humble, akawa Waziri wa Muungano, wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano, nilifanya nae mahojiano, she was humble. Akiwa Makamo Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, nikafanya naye tena mahojiano mengine, she was humble. Akiwa Makamo wa Rais, alikuwa mgeni rasmi Nane Nane Simiyu, she was humble.

Akiwa VP, siku nilimuona ZBC akihojiwa, nilishindwa kujizuia nikapandisha bandiko hili humu JF.

Na hadi sasa Samia Suluhu Hassan ni somebody, ni Rais wa JMT, Rais Samia Suluhu Hassan, na bado yuko humble vile vile hivyo hii humbleness yake ni kawaida yake!. Huyu sio mtu wa kujikweza, kujitutumua na kujimwambafai!, she is very down to earth.

Kwa msio mfahamu vizuri Samia, msije kusema namsifia kwa sababu sasa ni Rais wa JMT, karibuni mitaa hii na wale wenye uwezo to read in between the lines, utabaini Trends za urais wa Samia kuwa rais wa JMT zilitolewa way back bila hata kujua kitakuja kutokea nini .
Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth! na kwa vile nyingi ya sifa hizi ni za lugh ya Kiingereza, kwa Kiswahi hizi ni baadhi na sii zote
Mama Mwema,
Mama wa neema ya Mungu,
Mama mwenye usafi wa moyo,
Mama Mpole, Mama mpendelevu, Mama Mstahimilivu
Mama mstaajabivu,
Mama wa shauri jema,
Mama mwenye utaratibu,
Mama mwenye heshima,
Mama mwenye sifa stahiki
Mama mwenye huruma, (sio mama huruma)
Mama mwenye amini,
Mama mpenda haki,
Mama mwenye hekima,
Mama wa sababu ya furaha yetu,
Mama wa neema,
Mama wa heshima,
Mama wa kimbilio ya wanyonge
Mama mfariji wa taifa
Chifu Hangaya ni Malkia wa amani Tanzania.
Conclusion
Trends za Samia, zinaonyesha tunaelekea kwenye Tanzania njema yenye rais humble, mpole, mnyenyekevu, mstahimilivu, na hata kule UN, tumemshuhudia katika hotuba yake, amehutubia UN akiwa humble vile vile. Once humble, always humble!.
Mungu ambariki sana, Mama Samia aendelee na hii humbleness yake asibadilike.

Mtu mcha Mungu, mpole, mnyenyekevu wa type ya Mama Samia, akitibuliwa na akatibuka... JPM atakuwa ni mtakatifu!.

Kama alivyo sema mwenyewe kuhusu uwezo wa macho yake yale.... yanaona hayo!, na akasema wazi yeye sio mtu wa kufoka foka na akatoa onyo tusimzengue "mkinizengua, tuta zenguana"
Wito
Kama ilivyokuwa kwa JPM, alikuwa ni chaguo la Mungu kwa Tanzania, na baadae Mungu akabadili mawazo na kuamua kumuita kwake, na badala yake sasa Mungu ametuletea Samia, hivyo kwa sasa Samia ndio chaguo la sasa la Mungu kwa Tanzania, hivyo natoa wito kwa sisi wana Jf, la Watanzania kwa ujumla lets give her time, tumpe muda wa kutosha kuisuka nchi. Lets not take upole wake, unyenyekevu wake na humbleness yake for granted tukaanza kumzengua...

She will be....
Naomba nisimalizie

Nakutakia Jumapili Njema.

Paskali
 
Wanabodi,
Moja ya topic ngumu sana humu JF, ni topic za kitu kinachoitwa Trends Readings za psychoanalysis trends, kinacho tokana na ku psychanalyse Trends kisaikolojia kwa kutumia tabia za mtu za nyuma...
Amka kunywa supu, ondoa hangover then andika vizuri, muda huo nitakua nimetoka ibadani. Kwasasa naona ni Kvant ndio imeandika sio Wewe
 
Unyeyekevu wake unatokana na malezi yake bora aliyo yapata.

ni mtu mcha Mungu mwenye hofu ya Mungu, anaye amini kuwa cheo au madaraka vyote hivyo haviwezekani isipokuwa kwa Mkono wa Mungu.

Hivyo kiongozi anayejua hayo kamwe hawezi kuinua mabega juu. Rais Mama Samia ni mfano mzuri sana kwa viongozi wengine wa juu, wa chini na hata wananchi wa kawaida, kama Amiri Jeshi Mkuu anakuwa mnyenyekevu kwa kila mtu kiasi hiki! sembuse mimi na wewe!

kwa wenye akili tayari wamejiongeza lkn kwa wenye akili nusu kikombe wanaweza kujenga dharau na udhaifu kumbe sivyo.

Kiongozi yeyote anayejua maaana ya uongozi lazima awe mnyenyekevu.
 
Mkuu Pascal Mayalla! wewe nyoosha tu maelezo ya kwamba Rais Samia Suluhu Hassan, anaurejesha rasmi utawala wa JK! Na kwa sasa tunakaribia kabisa kurudi enzi zileeee za miaka ya 2005 mpaka 2015.

Na ni vyema ungewashauri MATAGA kuchukua hatua sahihi mapema kabla ya kuondolewa wote kwenye utafunaji wa keki ya Taifa. Mifano ni mingi, muda ni mchache!

Kweli kutesa kwa zamu! No JPM, no MATAGA!
 
Pasco nakumbuka trend reading zako zilisema Askofu Gwajima atachanjwa, mpaka sasa zimebuma 🤣
 
Wanabodi,
Moja ya topic ngumu sana humu JF, ni topic za kitu kinachoitwa Trends Readings za psychoanalysis trends, kinacho tokana na ku psychanalyse Trends kisaikolojia kwa kutumia tabia za mtu za nyuma, tabia za sasa kuweza ku détermine tabia kitakachokuja kutokea baadae in near future kwa short term, médium term na long term.

Trends Reading ni Nini, na Zina Kazi Gani, na Zina Faida Gani?.
Kwa kifupi, trends ni mielekeo, hivyo trends readings ni kusoma mielekeo, faida ya kusoma mielekeo, au direction, na kuangalia kule mliko toka, hapo mlipo mlipo, ili kujua kule mnakokwenda. Ni kama somo la Historia, ni kujifunza mambo ya zamani, kule tulikotoka, kulinganisha ya sasa hapa tulipo, hivyo kuweza kujua kule tuendako. History is the study of the past in relation to the present, to determine the future. Hivyo faida kubwa kabisa ya trends reading is the determination of the future. The future haijiji tuu kama kudra ya Mwenyezi Mungu, inakuwa determined na matendo yako ya nyuma, matendo yako ya sasa, hivyo kuipanga kesho yako iweje.

Trends Reading Sio Utabiri, Sio Ubashishiri, Ni Usomaji wa Mienendo na Mielekeo, Matokeo ya Trends ni Uhakika Zaidi Kuliko Utabiri na Ubashiri.
Kuna watu wanachanganya ubashiri, utabiri na trends readings. Japo yote matatu, yanaweza kusema kitatokea nini in future, mtabiri yeye anatumia mizimu kuuliza na kuona kitatokea nini, hawa wanaitwa scorchers, kuna wasoma nyota wanaoweza kukuambia yajayo kwa kusoma nyota yako, hawa wanaitwa astrongers, kama Sheikh Yahaya Hussen. Kuna wabashiri, hawa ni watu wa kubahatisha tuu kama bahati nasibu, Simba na Yanga zikicheza, kuna matokeo matatu tuu, au kushinda, kushindwa na sare. Wabashiri wanabahatisha lolote likitokea, wanakula bingo kwenye betting. Trends Readers, sio wanajimu, sio wabashiri ni watu wa kawaida tuu ambao ni wasoma mielekeo, trends na kuweza kusema kitatokea nini in future kutokan na matendo au matukio ya nyuma, matukio ya sasa na hivyo kujua matukio yajayo.

Trends Readers Humu JF ni Kina Nani na Jee Hizo Trends Zao, Zilikuja Kutokea?
Mimi ni mtu wa mastori mastori, kwa wapenda mastori, sasa kwa faida ya wenzetu wasio penda long stories, mnaweza kuishia hapa, na kwenda kusoma conclusion

Conclusion
Trends za Samia, zinaonyesha tunaelekea kwenye Tanzania njema yenye rais humber, mpole, nyenyekevu, mstahimilivu, na hata kule UN, tumemshuhudia katika hotuba yake, amehutubia UN akiwa humble vile vile. Once humble, always humble.
Mungu ambariki sana, Mama Samia aendelee na hii humbleness yake asibadilike.

Mtu mcha Mungu, mpole, mnyenyekevu wa type ya Mama Samia, akitibuliwa na akatibuka... JPM atakuwa ni mtakatifu!.

Kama alivyo sema mwenyewe kuhusu uwezo wa macho yake yale, yanaona hayo!, na akasema wazi yeye sio mtu wa kufoka foka na akatoa onyo tusimzengue "mkinizengua, tuta zenguana"
Natoa wito kwa sisi wana Jf, la Watanzania kwa ujumla lets give her time, tumpe muda wa kutosha kuisuka nchi. Lets not take upole wake, unyenyekevu wake na humbleness yake for granted tukaanza kumzengua...

She will be....
Naomba nisimalizie

Nakutakia Jumapili Njema.

Paskali
Probably PASKALI MAYALA at his best.
Ni Afrika tu tuna Marais wacha Mungu, Marais wa wanyonge na wanyenyekevu japo hawapendi haki, Marais wetu huingia madarakani kwa njia rahisi na wskiingia husema watafuata nyayo za aliyemuachia kijiti, hii imamaana vitendo vyake havitabadilika; Ninaamini waingekuwa wanaingia kirahisi tusingekuwa hapa tulipo na kila mmoja asingetabirika mwelekeo wake.
 
Katiba mpya is the only solution' periodd!
Mkuu LoyalTzCitizen , huyu Mama, atatupatia katiba mpya, ila wakati wa kipindi chake cha pili cha 2025- 2030.
Hivyo nyie wote mnaotaka katiba mpya, kama mnaitaka kwa dhati, then 2025 twende na Mama.
P
 
Back
Top Bottom