MeinKempf
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 11,093
- 7,229
Punguzo la 1% (kutoka 15% hadi 14%) kwenye kodi ya mishahara (PAYE) ni dhihaka kwa wafanyakazi wa Tanzania kwani gharama za maisha ziko juu sana kufuatia mfumuko mkubwa wa bei. Ifike wakati sasa serikali iwaonee huruma wafanyakazi kwa kuwapunguzia mzigo wa kodi badala ya kufawafanyia mzaha kama huu. Wafanyabiashara wakubwa na mafisadi kibao wanasamehewa kodi lakini mfanyakazi masikini anazidi kukandamizwa tu kila kukicha. Hii haikubaliki hata kidogo.
Kwa jinsi serikali ilipokuwa inatamba kwa mbwembwe kwamba itapunguza kodi ya mishahra, sikutegemea kwamba mwisho wa siku wangekuja kupunguza kiasi kidogo kama hiki cha kodi. Ni aibu kwa kweli. Wafanayakazi mnanapaswa kutambua kwamba seriklali ya CCM haina nia njema katika kuwapunguzia ukali wa maisha, hivyo basi fanyeni uamuzi sahihi hapo mwaka 2015 ili kurejesha nidhamu kwa serikali hii isiyokuwa na mwelekeo.
Kana kwamba hili halitoshi, bado wafanyakazi hao hao watakamuliwa Tsh 2500 kama kodi ya kumiliki simu kwa kila mwezi! Wananchi mmnatakiwa kuacha uzezetaamkeni tukawafundishe adabu hawa mafisadi mwaka 2015. Saa ya ukombozi ni sasa. Bila kufanya hivyo, tutaendelea kukandamizwa hadi mwisho wa dahari.
Tafakari, chukua hatua!
-------
Mwananchi (Juni 14)
Hakika huo ni upembuzi yakinifu kuhusu Pay As You Earn (P.A.Y.E). Wataalamu wa uchumi kama kina mhadhiri msataafu mnene daktari mgimwa mtupe majibu juu ya ukokotozi wa mahesabu yenu juu ya hiyo kitu kama sio kuendeleza unyonyaji kwa mfanyakazi "wanambania hata kile kidogo alichonacho mpaka jasho lake linazidi kunyonywa a.k.a mfanyakazi " na ndo maana katika nchi kuna makundi makubwa mawili " WENYE NCHI & WANANCHI".