Putin na Kim Jong Un wakibishana nani kuwa wa kwanza kuingia kwenye gari

Desturi za kiarabu/kiislamu hizo, na wao wameanza kuyaiga mdogo mdogo kwa waarabu/waislamu. Ni heshima kubwa kufanya hivyo
 
Hawa ni watawala wadhalimu, ni kitu Cha kawaida kabisa kwa Watu wadhalimu kutokumwakini mtu yoyote yule. Wanahofia kwamba huenda anaweza kufanyiwa udhalimu kama ambavyo yeye mwenyewe amekuwa akiwafanyia Watu wengine.
Kama putin na Kim ni madhaalim, je makafiri wa kizayuni, mmarekani na washirika wake wameuwa watoto/civilians utasemaje? Rais wetu wa afrika marhum Ghaddafi ameuawa chini ya utawala wa obama na washirika wake, halafu unakuja kusema putin na kim ni madhaalim! Sometimes ushabiki wekeni pembeni, ongea uhalisia wenyewe.
 
Hawa ni watawala wadhalimu, ni kitu Cha kawaida kabisa kwa Watu wadhalimu kutokumwakini mtu yoyote yule. Wanahofia kwamba huenda anaweza kufanyiwa udhalimu kama ambavyo yeye mwenyewe amekuwa akiwafanyia Watu wengine.
Kama walivyo Wamarekani mpaka wanatembea na gari zao popote waendapo duniani.
 
"In the world of spies, the greatest battle is not fought with guns, but with secrets."
 
If this was the case, huoni kwamba walinzi binafsi wa Kim Jong Un walipata shida sana? Kukubali kiongozi wenu aendeshwe na dereva Mrussia ninaamini walikuja na convoy yao ya gari na dereva kutoka Kremlin. Pia wakati gari inaondoka ulinzi wa ndani ya gari unakuwa ni wa warusi? Wakorea walikubali vipi hilo?? Ingekuwa Mimi ni Kim ningepiga chini idara yangu ya usalama.
 
Ni complex situation sababu Kim Jong un mwenyewe alikubali kuingia Sasa kwenye situation kama hiyo walinzi wake wangefanyaje kukaba raisi wao Kwa nguvu asiingie gari ya Putin au ? Wangemkaba kumlazimisha asipande gari ya Putin warusi wangecharuka kuwa kwenye hiyo gari wameweka Nini? Kungetokea varangati sio la kitoto pale na Putin angegeuza ndege kurudi Urusi na uhusiano na Korea ungekufa

Ule ulikuwa mitihani mzito Kwa Raisi Kim Jong Un na walinzi wake

Kim Jong Un kama Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya Korea akafanya maamuzi yake kuingia kumaliza kesi chap chapi bila kufanya kikao na walinzi muda ulikuwa mfupi na maamuzi yanatakiwa yatolewe haraka

Ila ziara ikiisha ndipo watakas na kukesha ku access hiyo situation na kujadili Kwa undani nani awajibike na kama kulikuwa na technical error wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…