Q-Net na Forever Living zimenipotezea marafiki zangu wa karibu

Q-Net na Forever Living zimenipotezea marafiki zangu wa karibu

Niliitwa na jamaa yangu mmoja....akawa ananiambia kuna siku ataniita nije nione ujasiriamali aufanyao. Nikawa najaribu kudadisi nijue anajihusisha na nini katika biashara yake mpya? Jamaa akawa hataki kusema, akidai nitajua tu siku nikienda.

Kichwani nikaanza kujiuliza inawezekanaje kama mtu amefungua biashara na hataki watu waijue? Hapo tayari nikachezwa chale.siku ikawadia akanipigia simu jioni akanielekeza, nikafika ofisini.

Kwa nje inaonekana ni nyumba tu ya kuishi watu, kumbe ndani ni ofisi. Nikapokelewa na zile goodmorning etc...kuona mabango tayari nikawa nimewatambua. Qnet.

Kwenye semina nikasikiliza stori za mamilioni...then nikauliza swali kuwa toka nimeingia humo kwao sijaona Certificate of incorporation ya kampuni yao, sijaona TIN ya kampuni, sijaona leseni ya biashara n.k ktk mazingira hayo nawezaje kuwekeza kwenye entity ambayo haitambuliki?

Wakaanza kujikanyaga, mara walionyeshwa kwenye taarifa ya habari, mara waziri alikuja kuzindua ofisi yao, mara sijui gazeti liliwaripoti,...tayari nikahitimisha kuwa these people are after my hard earned money. Nilipoondoka sikurudi kwa semina ya pili.
 
Qnet nawasifu sana kwa mbinu za kushawishi na kuwatoa watu ufahiamu (brainwashing) hasa wanachama wao. Ukiwa na tamaa lazima upigwe, lakini ukitulia na akili zako timamu na ukijiuliza maswali ya msingi utajifunza jinsi watu wengi walivyokata tamaa za maisha, wanavyopenda kutafuta fedha na maisha bora kwa njia za mkato.

Kuna jamaa yangu mmoja namheshimu sana, siku moja aliniomba tuonane akisema kwamba 'ana jambo zuri angependa kunishirikisha', akisisitiza kwamba 'kizuri kula na mwenzio'. Tukakutana jioni moja mahali fulani tulivu akiwa na wenzake ofisini kwao waliponitambulisha Qnet, wakinipa ushawishi kwamba baada ya muda mfupi sitahitaji kufanya kazi tena, maana fedha zitakuwa zikitiririka kama maji. Ndani ya dakika tatno moyoni nilishafanya maamuzi kwamba sitajiunga nao kwenye biashara hii, lakini nikajiambia acha niwasilikize na niwaulize maswali maana sikuwa cha kupoteza, na huenda nikajifunza kitu. Yule jamaa yangu alionekana sio msemaji sana, inaonekana kazi yake ilikuwa kunishawishi nifike pale halafu kuna 'mkuu' fulani aliyepangiwa kuongea na mimi akiwa na uhakika kwamba nitaingia. Kwa nyakati tofauti niliwauliza swali moja tu ambalo hadi leo hakuna hata mmoja wao aliyenipa jibu si huyu 'mkuu' wala yule jamaa yangu. Niliwauliza kila mmoja wao anioneshe kwa mifano hai wamepata mafanikio gani kupitia Qnet, wakashindwa nami nikawaambia kwamba itakuwa vigumu kwangu kuingiza fedha mahali ambapo wewe mwenyewe unanishawishi sioni jinsi unavyofanikiwa. Nikamwambia jamaa yangu kwamba siku mambo yake yatakapokuwa mazuri anijulishe nami nitajiunga. Hadi leo mimi na yule jamaa yangu mawasiliano yamekatika.



oyaaaaaaaaa si wslikupeleka kuleeee mikocheni b kwenye ki chochoro Chao???? ?
 
ngoja tuendelee kupigwa labda tutashituka huko mbeleni
 
Ahahaha am global walikuta na vitu vyangu kichwan halafu nilitoka kutapeliwa kilo SITASAHAU ILE SIKU
 
Kuna kidem changu cha chuo kwasasa yupo likizo ila yupo bze sana namaswala ya pesa yn kama yupo ofis flan ivi zamichongo yapesa sasa leo ndo nimepata jibu mana juz kati alinitext "Habari Majan Samahani kesho kama hutojali naomba Uje ofcn Kwetu saa nane kuna program muhimu kwa wageni nakuomba nimekununulia ticket" ila kila nikimuuliza ofis zao zinahusika na nini hajawai kuniambia
Hawa jmaa wanatapeliwa alafu na wao wanafundishwa kutapeli wengine. Process zao ni moja. Watakuambia njoo oficn kuna semina unafika unakuta wamejipanga kuanza kukutapeli wewe.
 
Kuna dem amenitafuta sana wiki ya pili hii simjui ila anapiga simu anasema tuonane kuna ishu ya maana tukajadili lakini hasemi ni nini.sasa namvutia upepo tu amesema weekend hii tukutane makumbusho.ila nazani ni hizi mambo
Kma ni makumbusho usiende[emoji23][emoji23]ndo ofisi zao zilipo.kuna mxkaji alitumiwa msg na dem flani anasoma ardhi akaambiwa kuna kazi inahusu mambo ya health.anahitaji vijana wanne.mxkaji wangu akanitonya mm na wana wengne watatu,tumetoka IFM na mvua kubwa kishenzi adi makumbusho,kufika makumbusho tumelowa mana alituelekeza twende kwenye crdb ss sisi tukaenda millenium tower branch ya crdb kumbe alimaanisha ATM ya crdb iliokuwepo makumbusho stand pale.tulivyokutana nae tushalowa vibaya sana af ndo katupandisha ofisini kwao pale juu akaanza kutuambia huo upuuzi.
 
HAO BHANA NAWAOGOPA HAO TOKA WAMSABABISHIE MAANANGU MMOJA CHUO ALE ADA HADI LEO WAMESHIKILIA CHETI CHAKE SHENZI HAWA AFU MMOJA WA HAWA MADADA NI CLASS MATE WETU CHUO FLANI HVI..... BACK IN DAYS
20181007_011921.png
 
Unanikumbusha GNLD mwaka 2011 kipindi nipo A level kuna best yangu alitumia pesa yote ya kupiga mapindi tuition kwa mudi physics kisa kujiunga na GNLD

Alikua anajisifia mafanikio ya maisha bora na mkwanja mrefu wakati kiuhalisia tulikua tunasota kwa kushindia mihogo na maji kandoro ya miamia kwa mgosi mwisho alikuja kukiri alitapeliwa tuliporudi shule baada ya likizo kuisha na kudai kazi ilikua ngumu sana mana ni kujenga network ya watu

Alijitahidi kunishawishi kinoma ili namimi nijiunge but sikuwa interest ukizingatia shule ya PCB A level ilivyo kuwa ngumu sikutaka kuchanganya madesa
 
Kma ni makumbusho usiende[emoji23][emoji23]ndo ofisi zao zilipo.kuna mxkaji alitumiwa msg na dem flani anasoma ardhi akaambiwa kuna kazi inahusu mambo ya health.anahitaji vijana wanne.mxkaji wangu akanitonya mm na wana wengne watatu,tumetoka IFM na mvua kubwa kishenzi adi makumbusho,kufika makumbusho tumelowa mana alituelekeza twende kwenye crdb ss sisi tukaenda millenium tower branch ya crdb kumbe alimaanisha ATM ya crdb iliokuwepo makumbusho stand pale.tulivyokutana nae tushalowa vibaya sana af ndo katupandisha ofisini kwao pale juu akaanza kutuambia huo upuuzi.
Sipati Picha, hahahaha
 
pole kaka nimempoteza rafiki kipenzi kwa sababu ya Qnet

Hata anipigie simu sipokei kwa sasa na bahat mbaya ukienda Qnet hta kama ni usiku utaambiwa Goodmorning

watu wana mashati yaliyochakaa na viatu vilivyoisha soli cha ajabu wanakuelezea return ya mamilioni!!!
Wanajiita upcoming billionaires hahahaha dah
 
Back
Top Bottom