Rafiki yangu kamfumania mkewe gesti

Rafiki yangu kamfumania mkewe gesti

Inauma sana..Ila bado maisha yako yanabak kuwa yako tu..usiyakabidhi kwa mwenzako bila kujal ni mwenza au mzazi.U wll be highly disspointed.
LIVE UR LIFE FOR U N U ALONE.
 
Mwambie amsamehe tu kwani yeye hajawahi mcheat? Huenda yeye ndiye chanzo
anamaliza kila kitu nje kwa mkewe anarudi kutimiza wajibu ndoa zinaficha mengi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli. Hapo ndiyo tatizo linaanzia. Utasikia mke wangu hakati kiuno. Uliyaonewa wapi hayo kama mwanaume angekuwa hajakutana kimwili na mwanamke kabla ya ndoa?
Wanaume hutaka mke bikira wakati yeye wanawake aliopitia unaweza jaza behewa la trein ya mwakwembe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi wanaume kwenye suala la kusalitiwa huwa wagumu sana kusamehe. Hapa ukisikia binadamu kala samaki siyo habari ila habari samaki kala binadamu. Hapa vyombo vya habari vitaandika kwenye magazeti, kutangazwa kwenye radio, tv pamoja na vyombo vya ulinzi vitaanza kumtafuta samaki wamuue. Ndivyo inavyotokea kwa mwanaume kumsaliti mwanamke na mwanamke kumsaliti mwanaume. Kuna rafiki yangu, anaweza kuulizwa na mkewe jambo la kawaida tu lakini akamjibu vibaya mpaka ukashindwa kumuelewa. Nakumbuka nilikuwa na mwanamke msaliti. Mtu akikuuliza mkeo hajambo au mkeo yupo, unatamani kumjibu siyo mke wangu.
Mwambie amsamehe tu kwani yeye hajawahi mcheat? Huenda yeye ndiye chanzo
anamaliza kila kitu nje kwa mkewe anarudi kutimiza wajibu ndoa zinaficha mengi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nilishamwambia wife ikiwa nimembamba na mchepuko iwe kwa njia ya SMS, Fb au popote pale muda huohuo ndio mwisho wa ndoa yetu, simpigi. Wife ananiogopa kama ukoma.
Huyo sasa ana mawazo ya nini huku mke kakimbia ndoa yeye mwenyewe?
Mkuu,vipi akikufumania wewe ?
 
Client miss you so much mummy[emoji8]

Sent using Jamii Forums mobile app
1580490091170.png

Is this D??🤗
 
Tatizo liko kwa mtonyaji! Nia labda ilikuwa nzuri, lakini madhara yake yanaweza kuwa makubwa. Sasa huyo mtonyaji awe fair,akimuona mme wa huyo mke nae anachepuka amtonye!

Nakumbuka mwaka fulani, niliingia Shinyanga nikitokea Musoma! Nilivofika nilienda kutafuta sehemu ya kulala, kwa bahati mbaya au nzuri chumba nilichokuwa natizamana nacho kulikuwa na jamaa mmoja nafahamu, japo yeye alikuwa anifahamu! Alikuwa Mtumishi mpya katika hospital ya mission iliyopo kijijini kwetu!

Jioni, natoka kula, nikaona anaingia na mwanamke, ambaye ni mke wa ndugu yangu, ameaga anaenda Msibani kumbe ameenda shinyanga kula raha na mchepuko!

shemeji hakuwa ameniona, so kipindi anaingia ndani, huku ameshikwa kiuno, mi Uvumilivu ukanishinda! Nikaanza kumfikiria ndugu yangu, nikaanza kumfikiria anavyojigamba juu ya utulivu wa mke wake!

Basi ikabidi tu, nimwite Mama chitimbo, akshituka, nikamuita na yule jamaa kwa Jina, Dr. Chikelembwe, wakaduwaaaa!

Nikawaambia siyo sawa kabisa, shemeji mi namwambia ndugu yangu! Ooh shemeji ,hapana! Shemeji tafadhali! Nikamwambia njoo, tuzungumze, nikamhoji, akasema alivyodanganya, na blah blah nyingi! Nikamwambia hata Picha ninazo, akasema shemeji nisamehe, nipo radhi nikupe ila usniseme! Watoto wangu watateseka!


To cut the story short, nikamwambia yule jamaa, nitamlaza ndani maana, picha na ushahid ninao! Mwisho wa siku jamaa akaniomba msamaha. Akaamua na kuondoka, shemeji akalala Asubuhi akaondoka!

Hadi leo sijamwambia mme wake, wako na wanaendelea na maisha yao vizuri na mme wake! Lkn ningemtonya brother, wangelikuwa wameshatengana! Huwa naenda kuwatembelea, shemeji anafikir nitamsemea, sijui maana anakosa amani!

So wakt mwingine, utonyaji si deal! Maana we are all part of that stuff!

Sent using Jamii Forums mobile app
Dr.Chitelembwe!!...nimecheka kinoma ulivyowaita hao wachepukaji
 
Tumepakizana kwenye ki-boxer chetu tunaenda kazini,tupo barabarani tunakutana na jamaa nikashangaa wanasalimiana kwa bashasha,wakapeana kaishara fulani hv,nikazuga sijaona huo mtaa ndiyo kwanza tulikuwa na miezi miwili tu tukiwa tumehamia ndiyo nikawa najiuliza kivipi apete wenyeji mapema kiasi hiki???

Hazikupita siku nikaidaka sms ya mshikaji ikiulizia anarudi saa ngapi kutoka kazini,
Nokaichukua namba nikaweka kwenye simu yngu kuchungulia WhatsApp nikaiona profile mshikaji ni yuleyule tulikutanaga naye barabarani siku kadhaa zilizopita.

Nilimuuliza swali moja tu mwenye namba hii ni nani???
Hakujibu,niliuliza mara kadhaa yupo kimya,nikazuga yameisha,baada ya mwezi nikapanga safari ya kwenda kwao kusalimia,tukaenda wote nililala siku moja tu nokazuga nimeitwa kazini kwa dharura isiyoepukika hivyo nililazimika kurudi haraka iwezekanavyo,na nitakutumia nauli,nilipofika nyumbani nilimjulisha tu kwamba asije tena aendelee na mshikaji wake,alilia na kuomboleza nyimbo na mapambio yote lakini msimamo wangu ulikuwa ni uleule.
Leo mwaka wa tatu ndoa yangu ilivunjika rasmi baada ya kuona elements za uchepukaji ambazo hazikuwa na chembe ya shaka.

Sioi kwa sasa mpaka wanangu wakue kwanza wajitambue ili nitakapooa wawe na uwezo wa kujieleza pale watakapofanyiwa ndivyo sivyo.
Nawapenda wanangu Travis and Tresha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao wenye gesti nao ni maboya, huwezi kuruhusu Mtu kumfuata Mgeni wenu chumbani bila ridhaa ya Mgeni.
 
Mimi nilishamwambia wife ikiwa nimembamba na mchepuko iwe kwa njia ya SMS, Fb au popote pale muda huohuo ndio mwisho wa ndoa yetu, simpigi. Wife ananiogopa kama ukoma.
Huyo sasa ana mawazo ya nini huku mke kakimbia ndoa yeye mwenyewe?
Kwa mfano unakuja kujua mkeo anakusaliti wakati mna watoto wadogo chini ya miaka 10 unamuacha hivyo hivyo bila kusubiri watoto angalau wafikishe miaka 10?
Huo mtihani kiongozi wangu kama una wapenda wanao.
Unaweza kuona jinsi familia zilizo vurugika watoto wanavyo pata malezi ya ajabu.
 
Back
Top Bottom