Rafiki yangu kanipa kesi, kisa nimemsaidia mtoto wake mwenyewe

Rafiki yangu kanipa kesi, kisa nimemsaidia mtoto wake mwenyewe

Mtoto akikukana utafanyaje? Kuna matukio mtoto katestify uongo kwa maelekezo ya wazazi mhusika anajikuta kwenye aibu. Anadanganywa na vi icecream na vipipi unashangaa mtoto anakuwa upande wa wazazi wake unaingia aibu.

Mshkaji alitakiwa awasiliane na baba mtoto ambae ni rafiki yake na amueleze kuwa kuna mzigo atampa shemeji.

Sasa ananunua zawadi, anampelekea mke wa rafiki yake huku rafiki yake hana habari ilihali anajua kabisa mkewe ana roho mbaya.

Na wanawake walivyosmart akijua bado mnamfatilia na akataka kuharibu zaidi hii miezi kadhaa mtoto anaweza pendwa kinafiki, siku mnamuita huyo rafiki yenu anawaona wote mnamtamani mkewe.
Mtoto mdogo aki testify uongo inajulikana.
Mtoto chini ya miaka kumi muulizi kitu zaidi ya mara tano ukiona mara ya tatu anatoa taarifa inayopishana na ya kwanza, basi jua cha kwanza ni uongo.
Ukimuuliza mara ya sita ashasahau yale aliyolishwa atautapika ukweli wooteee.
Hii mbinu mahakama ya mirathi Chang'ombe Temeke nimeiona.
 
1. Usiingilie yasiyokuhusu.
Hiyo NI Kanuni Namba Moja.

2. Ikiwa utaingilia, Basi kuwa mwangalifu, chukua tahadhari na Work smart.

Sikuona sababu ya Mtoto kuteseka Miaka nenda Rudi alafu kumbe NI Mtoto WA Mshikaji wako.
Ulishindwa nini kumwambia mapema kama kweli ninyi NI marafiki?

Siku zote mnapoonana mnazungumzia mambo gàni ya maana?

Alafu unampaje shemeji zawadi Kwa Mtoto asiye wake, Kosa.
Unampaje Zawadi shemeji àmbaye tayari ushajua anaroho Mbaya?

Kama wanauwezo wa kumnunulia nguo na Viatu huyo Mtoto na hawajamnunulia, ulikuwa na uhakika gani nguo utakazopeleka huyo Mwanamke angempa azivae?

Ninyi mnasema Wanawake NI wabaya lakini ubaya wa Mwanamke mara nyingi hutokana na uzembe wa Mwanaume.
Mfano huyo Mwanamke kama ungekuwa smart Sana Wala huyo ràfiki yako msingegombana.

NI aidha ungemwambia Mshikaji pekeake, au Siku uende ukamchane live wakiwa wôte wawili ili shemeji asipate Nafasi ya kuongea uongo.
Akibisha unamwambia Dogo aitwe aulizwe.

Maana huyo ràfiki yako ungeweza kumwambia mapema lakini akitoka akaenda kumuuliza Mkewe akapewa tàarifa potofu na Hali ikawa kama ya Sasa.

Siku ñyiñgine kama Huna best solutions NI Bora usiingilie Kesi za Watu.
Wengi wamekufa Kwa sababu hizohizo
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Jirani na hapa nnapoishi mimi kuna home boy fulani ambae tumetokea kuzoeana, kushauriana na hata sometimes kutembeleana. Tulitokea kujuana nae miezi 6 iliyopita baada ya yeye na familia yake kuhamia hapa. Kwa Tanzania ni mzaliwa wa Kinondoni, wakati mimi mzaliwa wa Magomeni Dar es salaam, hivyo tunaishi kama ndugu.

Kabla ya kuishi na mke alie nae sasa hivi, alikuwa ashaoa mke wake wa kwanza ambae alizaa nae mtoto mmoja wa kiume. Lakini kwa bahati mbaya mkewe alifariki miaka 3 iliyopita na kuacha mtoto huyo akiwa na umri wa miaka 4.

Baada ya mkewe kufariki, mwamba hakuchelewa, akakutana na huyu mkongo, akatangaza ndoa na kuanza maisha mapya (kumbuka hapo jamaa alikuwa na mtoto wa miaka 4), baadae na mkongo akamletea mtoto mungine wa kike, so jumla jamaa ana watoto wawili. Maisha yao huko walipokuwa haswa kwa upande wa mtoto wa kambo sijui yalikuaje, ila baada ya kuhamia jirani yetu na kufahamiana na jamaa, ndo nikaanza kuona mateso anayopitia mtoto.

Japo imezoeleka kuona mama wa kambo wengi ni makatili, lakini huyu aisee ni zaidi ya shetani. Hana chembe ya huruma, utu wala ubinadam. Anaweza kumpa mtoto adhabu ya kuweka miguu juu (ukutani) mikono chini (mfano wa sarakasi) kwa muda mrefu zaidi, bila kushusha miguu chini, na akishusha anakula kipondo ambacho anatakiwa kupigwa mwizi huko polisi.

Yote tisa, kumi ni pale anapomshindisha na njaa, alafu akigundua kuwa alikuja kwangu na wenzake (watoto wangu) akala, basi atachokutana nacho atajuta ni kwanini alimpoteza mama yake akiwa bado mdogo. Atapigwa, atapewa adhabu ya kuweka miguu juu, na kushindishwa na njaa.

Kila nlipotaka kumwambia jamaa kuhusu mateso anayopitia mwanae, moyo ulisita, nisije kuharibu ndoa ya watu au kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto mwenyewe. So niliamua kushona mdomo wangu tu kama sijui kinachoendelea.

Huyu mama mwanzoni alianza kuwa karibu na mke wangu, kutokana na ukaribu uliopo mimi na mumewe. Lakini alipogundua kwamba mke wangu huwa na tabia ya kumpa chakula mtoto anaeteswa, na sometimes kumpa hela pamoja na watoto wangu ili wanunue vitu vidogo vidogo vya kula, basi yule mama wa kambo akakata mawasiliano na mke wangu, na madam nae akampotezea kwa kufuata ule msema wa "akunyimae kunde, anakupunguzia kuja...m..ba.

Mtoto bado mdogo (miaka 7) kumweleza baba yake anashindwa, na mama huwa hampi nafasi ya kumsogelea baba yake akae nae mwenyewe. Halaf mtoto nguo, na viatu vimemuishia mpaka aibu naona mimi.

Juzi alhamisi nikaona upuuzi, wakati natoka mihangaikoni kwangu nikaingia dukani nikanunua nguo suruali 5, T'shirt 5, mashati mawili, jacket za baridi 3, viatu pea 3 na sandroz pea 1. Nikaenda mpaka kwa home boy nikamkabidhi mkewe nikamwambia kuwa zile nguo na viatu nilikuwa nimemnunulia mwanangu, lakin kwa bahati mbaya nimekuta havimtoshi, so ndomaana nikaona nimpe yeye ambae vinaonekana kumtosha, alaf mimi nitaenda na mtoto wangu town nikamnunulie vingine. Yule mama akapokea, lkn ni kwa shingo upande (kumbuka ni shemej yangu) halaf sina ugomvi nae yeye wala mumewe. So hakuwa na nguvu ya kukataa uso kwa uso.

Kumbe na yeye jana alienda town, akanunua nguo zake kadhaa, na kuja nazo nyumban kwa malengo yake binafsi. Usiku mumewe alipofika akaanza kumwambia kuwa mimi nimekuwa nikimtongoza na kumtaka kimapenzi muda mrefu bila mafanikio, na kwamba nilifikia hadi hatua ya kumnunulia yeye na mtoto (wa kambo) nguo ili anikubali, lakini bado alinikwepa na kuchukua tu nguo ili aje amuonesha (mumewe) nk.

Home boy alipotaka ushahidi yule mama akaenda kutoa zile nguo alizoenda kununua jana town, akajumlisha na zile nilizopeleka kwa ajili ya kumpa mtoto wa kambo anaeteseka. Aisee sijui jamaa alikuwa katika hali gani usiku ule na sijui alilalaje.

Asubuhi naona home boy anakuja nyumban bila salam anaanza kunibwatukia mbele ya mke wangu na watoto wangu. Namuuliza tatizo nini, anabwaga zile nguo mbele yangu na kusema eti ashajua kila kitu kuhusu mpango wangu wa kumtongoza mkewe.

Eti natongoza kishamba sana kwa kukimbilia kuhonga nguo. Yani nikashindwa kumuelewa vizuri, mpaka alipofafanua kwamba nilikuwa namtongoza mkewe, nilipoona hakubaliani na mimi ndo nikaenda town kununua vijinguo vya kumlaghai ili nimpate kiurahisi nk.

Nikataka kutumia ukaribu wetu kumueleza kile kinachoendelea katika familia yake mpaka mimi kufikia hatua ya kununua zile nguo za mtoto wake, lakini bingwa hakunielewa, akawa mtata mwisho nikamuacha aongee akichoka aamue mwenyewe anachotaka kufanya.

Baada ya kuona lengo lake la kunichafua mbele ya familia yangu limefeli akaondoka akidai kuanzia leo mimi na yeye ni maadui. Nisimjue, asinijue, nisiende kwake, na hatokuja kwangu, kila mtu aangalie maisha yake, nikamwambia poa.

Kwa bahati nzuri mke wangu anajua kila kinachoendelea, so ile complain ya kumtongoza mkewe haikumuingia akilini.

Namuonea huruma sana home boy, ni kama mapenzi yamemfanya asifatilie kinachoendelea katika nyumba yake. Damu yake inateswa, na sisi tunaosaidia tunaonekana wabaya. Mateso anayopitia yule mtoto hakuna mtu yoyote mwenye huruma hapa JF anaweza kuyaona akayavumilia.

Nilikuwa na mpango wa kwenda ku report swala hili katika mamlaka husika, lakini kuna rafiki yetu (mimi na yeye) amesema nisubiri kwanza jamaa hasira ziishe hata week 1 au 2, halafu aite kikao kati yangu na home boy kwa ajili ya maridhiano, halaf hapo kwenye kikao ndo nitumie chance hiyo kumueleza home boy kile kinachoendelea katika familia yake, na sababu ya mimi kumpelekea yule mtoto zile nguo na viatu.

Huyu rafiki mimi nimemuelewa, lkn sielewi ni vipi mpaka leo jamaa haoni kuwa mtoto wake anateseka hata kwa muonekano tu wa macho. Ama kweli tenda wema uende zako. Na sio kila mwenye macho huona kilichopo mbele yake. Jamaa haoni na hasikii.

Dah...
ulikosea, kabla ya kununua hizo nguo ungeongea na jamaa na kumpa full story kuhusu mateso ya mtoto wake. Badala ya kumkabidhi nguo huyo mama wa kambo.
 
Mtoto mdogo aki testify uongo inajulikana.
Mtoto chini ya miaka kumi muulizi kitu zaidi ya mara tano ukiona mara ya tatu anatoa taarifa inayopishana na ya kwanza, basi jua cha kwanza ni uongo.
Ukimuuliza mara ya sita ashasahau yale aliyolishwa atautapika ukweli wooteee.
Hii mbinu mahakama ya mirathi Chang'ombe Temeke nimeiona.
Ok mkuu
 
Mtoto mdogo aki testify uongo inajulikana.
Mtoto chini ya miaka kumi muulizi kitu zaidi ya mara tano ukiona mara ya tatu anatoa taarifa inayopishana na ya kwanza, basi jua cha kwanza ni uongo.
Ukimuuliza mara ya sita ashasahau yale aliyolishwa atautapika ukweli wooteee.
Hii mbinu mahakama ya mirathi Chang'ombe Temeke nimeiona.
Umetoa mfano mzuri mkuu. Nahisi uliemwambia amekuelewa.
 
ulikosea, kabla ya kununua hizo nguo ungeongea na jamaa na kumpa full story kuhusu mateso ya mtoto wake. Badala ya kumkabidhi nguo huyo mama wa kambo.
Sikutegemea wala kufikiria kama haya yangetokea mkuu. Najilaumu sana.
 
Umetoa mfano mzuri mkuu. Nahisi uliemwambia amekuelewa.
Nimehudhuria kesi za familia mara kadhaa mahakama ya Chang'ombe.
Dogo alikua kamezeshwa uongo dhidi ya babaake alooo!!
Dogo kaulizwa mara ya pili ya tatu kakanganya maelezo,wakamshusha pembeni apumzike sakata lilivyoendelea kafunguka yote mama aibu mahakamani.
Huwa wanashindwa ku recall yale waliyomezeshwa.
 
Nimehudhuria kesi za familia mara kadhaa mahakama ya Chang'ombe.
Dogo alikua kamezeshwa uongo dhidi ya babaake alooo!!
Dogo kaulizwa mara ya pili ya tatu kakanganya maelezo,wakamshusha pembeni apumzike sakata lilivyoendelea kafunguka yote mama aibu mahakamani.
Huwa wanashindwa ku recall yale waliyomezeshwa.
Ni kweli mkuu 🤣🤣🤣
 
Waswahili walikuwa na msemo kwamba "tenda Wema uende zako"
Kakosea wapi jirani hapo? Mbona mara nyingi amekua anatenda WEMA na anaenda zake, au mi ndio sijaelewa? Mtoto amekua anapewa chakula, pesa za kununua vitu vidogo vidogo na baadae kaamua kumnunulia nguo; hajawahi kutangaza popote (according to the story ) isipokua baada ya kukutwa na hi!
 
Learn to mind yout own business
We mtoto wa mjini lakini inakuwaje kufatilia mambo ya watu,utakuja kufungwa siku kwa uzembe wako,dunia ya kibepari hii,bora ungeripoti kwenye mamlaka husika sio kumnunulia mtoto nguo,big mistake
Kwahiyo ile slogan ya "mtoto wa mwenzio muone kama mtoto wako" kwa watoto wa mjini waachane nayo?
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Jirani na hapa nnapoishi mimi kuna home boy fulani ambae tumetokea kuzoeana, kushauriana na hata sometimes kutembeleana. Tulitokea kujuana nae miezi 6 iliyopita baada ya yeye na familia yake kuhamia hapa. Kwa Tanzania ni mzaliwa wa Kinondoni, wakati mimi mzaliwa wa Magomeni Dar es salaam, hivyo tunaishi kama ndugu.

Kabla ya kuishi na mke alie nae sasa hivi, alikuwa ashaoa mke wake wa kwanza ambae alizaa nae mtoto mmoja wa kiume. Lakini kwa bahati mbaya mkewe alifariki miaka 3 iliyopita na kuacha mtoto huyo akiwa na umri wa miaka 4.

Baada ya mkewe kufariki, mwamba hakuchelewa, akakutana na huyu mkongo, akatangaza ndoa na kuanza maisha mapya (kumbuka hapo jamaa alikuwa na mtoto wa miaka 4), baadae na mkongo akamletea mtoto mungine wa kike, so jumla jamaa ana watoto wawili. Maisha yao huko walipokuwa haswa kwa upande wa mtoto wa kambo sijui yalikuaje, ila baada ya kuhamia jirani yetu na kufahamiana na jamaa, ndo nikaanza kuona mateso anayopitia mtoto.

Japo imezoeleka kuona mama wa kambo wengi ni makatili, lakini huyu aisee ni zaidi ya shetani. Hana chembe ya huruma, utu wala ubinadam. Anaweza kumpa mtoto adhabu ya kuweka miguu juu (ukutani) mikono chini (mfano wa sarakasi) kwa muda mrefu zaidi, bila kushusha miguu chini, na akishusha anakula kipondo ambacho anatakiwa kupigwa mwizi huko polisi.

Yote tisa, kumi ni pale anapomshindisha na njaa, alafu akigundua kuwa alikuja kwangu na wenzake (watoto wangu) akala, basi atachokutana nacho atajuta ni kwanini alimpoteza mama yake akiwa bado mdogo. Atapigwa, atapewa adhabu ya kuweka miguu juu, na kushindishwa na njaa.

Kila nlipotaka kumwambia jamaa kuhusu mateso anayopitia mwanae, moyo ulisita, nisije kuharibu ndoa ya watu au kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto mwenyewe. So niliamua kushona mdomo wangu tu kama sijui kinachoendelea.

Huyu mama mwanzoni alianza kuwa karibu na mke wangu, kutokana na ukaribu uliopo mimi na mumewe. Lakini alipogundua kwamba mke wangu huwa na tabia ya kumpa chakula mtoto anaeteswa, na sometimes kumpa hela pamoja na watoto wangu ili wanunue vitu vidogo vidogo vya kula, basi yule mama wa kambo akakata mawasiliano na mke wangu, na madam nae akampotezea kwa kufuata ule msema wa "akunyimae kunde, anakupunguzia kuja...m..ba.

Mtoto bado mdogo (miaka 7) kumweleza baba yake anashindwa, na mama huwa hampi nafasi ya kumsogelea baba yake akae nae mwenyewe. Halaf mtoto nguo, na viatu vimemuishia mpaka aibu naona mimi.

Juzi alhamisi nikaona upuuzi, wakati natoka mihangaikoni kwangu nikaingia dukani nikanunua nguo suruali 5, T'shirt 5, mashati mawili, jacket za baridi 3, viatu pea 3 na sandroz pea 1. Nikaenda mpaka kwa home boy nikamkabidhi mkewe nikamwambia kuwa zile nguo na viatu nilikuwa nimemnunulia mwanangu, lakin kwa bahati mbaya nimekuta havimtoshi, so ndomaana nikaona nimpe yeye ambae vinaonekana kumtosha, alaf mimi nitaenda na mtoto wangu town nikamnunulie vingine. Yule mama akapokea, lkn ni kwa shingo upande (kumbuka ni shemej yangu) halaf sina ugomvi nae yeye wala mumewe. So hakuwa na nguvu ya kukataa uso kwa uso.

Kumbe na yeye jana alienda town, akanunua nguo zake kadhaa, na kuja nazo nyumban kwa malengo yake binafsi. Usiku mumewe alipofika akaanza kumwambia kuwa mimi nimekuwa nikimtongoza na kumtaka kimapenzi muda mrefu bila mafanikio, na kwamba nilifikia hadi hatua ya kumnunulia yeye na mtoto (wa kambo) nguo ili anikubali, lakini bado alinikwepa na kuchukua tu nguo ili aje amuonesha (mumewe) nk.

Home boy alipotaka ushahidi yule mama akaenda kutoa zile nguo alizoenda kununua jana town, akajumlisha na zile nilizopeleka kwa ajili ya kumpa mtoto wa kambo anaeteseka. Aisee sijui jamaa alikuwa katika hali gani usiku ule na sijui alilalaje.

Asubuhi naona home boy anakuja nyumban bila salam anaanza kunibwatukia mbele ya mke wangu na watoto wangu. Namuuliza tatizo nini, anabwaga zile nguo mbele yangu na kusema eti ashajua kila kitu kuhusu mpango wangu wa kumtongoza mkewe.

Eti natongoza kishamba sana kwa kukimbilia kuhonga nguo. Yani nikashindwa kumuelewa vizuri, mpaka alipofafanua kwamba nilikuwa namtongoza mkewe, nilipoona hakubaliani na mimi ndo nikaenda town kununua vijinguo vya kumlaghai ili nimpate kiurahisi nk.

Nikataka kutumia ukaribu wetu kumueleza kile kinachoendelea katika familia yake mpaka mimi kufikia hatua ya kununua zile nguo za mtoto wake, lakini bingwa hakunielewa, akawa mtata mwisho nikamuacha aongee akichoka aamue mwenyewe anachotaka kufanya.

Baada ya kuona lengo lake la kunichafua mbele ya familia yangu limefeli akaondoka akidai kuanzia leo mimi na yeye ni maadui. Nisimjue, asinijue, nisiende kwake, na hatokuja kwangu, kila mtu aangalie maisha yake, nikamwambia poa.

Kwa bahati nzuri mke wangu anajua kila kinachoendelea, so ile complain ya kumtongoza mkewe haikumuingia akilini.

Namuonea huruma sana home boy, ni kama mapenzi yamemfanya asifatilie kinachoendelea katika nyumba yake. Damu yake inateswa, na sisi tunaosaidia tunaonekana wabaya. Mateso anayopitia yule mtoto hakuna mtu yoyote mwenye huruma hapa JF anaweza kuyaona akayavumilia.

Nilikuwa na mpango wa kwenda ku report swala hili katika mamlaka husika, lakini kuna rafiki yetu (mimi na yeye) amesema nisubiri kwanza jamaa hasira ziishe hata week 1 au 2, halafu aite kikao kati yangu na home boy kwa ajili ya maridhiano, halaf hapo kwenye kikao ndo nitumie chance hiyo kumueleza home boy kile kinachoendelea katika familia yake, na sababu ya mimi kumpelekea yule mtoto zile nguo na viatu.

Huyu rafiki mimi nimemuelewa, lkn sielewi ni vipi mpaka leo jamaa haoni kuwa mtoto wake anateseka hata kwa muonekano tu wa macho. Ama kweli tenda wema uende zako. Na sio kila mwenye macho huona kilichopo mbele yake. Jamaa haoni na hasikii.

Dah...
Makosa ni yako mwenyewe, katika khali ya kawaida haiingii akilini kumnunulia mtoto wa mwenzako nguo bila sababu ya msingi.
Ulichotakiwa kufanya ni kukusanya ushahidi na kumuonesha baba mtoto changamoto alizokuwa anapitia mtoto na siyo kumnunulia nguo utafikiri baba yake aneshindwa kufanya hivyo.
 
Kakosea wapi jirani hapo? Mbona mara nyingi amekua anatenda WEMA na anaenda zake, au mi ndio sijaelewa? Mtoto amekua anapewa chakula, pesa za kununua vitu vidogo vidogo na baadae kaamua kumnunulia nguo; hajawahi kutangaza popote (according to the story ) isipokua baada ya kukutwa na hi!
Asante mkuu kwa ufafanuzi, nina imani uliem quote kakuelewa vizuri sana 🙏
 
Kakosea wapi jirani hapo? Mbona mara nyingi amekua anatenda WEMA na anaenda zake, au mi ndio sijaelewa? Mtoto amekua anapewa chakula, pesa za kununua vitu vidogo vidogo na baadae kaamua kumnunulia nguo; hajawahi kutangaza popote (according to the story ) isipokua baada ya kukutwa na hi!
Jirani alikuwa anatenda Wema lakini akaishia kulipwa ubaya

Ndiyo maana nimesema "tenda Wema nenda zako"
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Jirani na hapa nnapoishi mimi kuna home boy fulani ambae tumetokea kuzoeana, kushauriana na hata sometimes kutembeleana. Tulitokea kujuana nae miezi 6 iliyopita baada ya yeye na familia yake kuhamia hapa. Kwa Tanzania ni mzaliwa wa Kinondoni, wakati mimi mzaliwa wa Magomeni Dar es salaam, hivyo tunaishi kama ndugu.

Kabla ya kuishi na mke alie nae sasa hivi, alikuwa ashaoa mke wake wa kwanza ambae alizaa nae mtoto mmoja wa kiume. Lakini kwa bahati mbaya mkewe alifariki miaka 3 iliyopita na kuacha mtoto huyo akiwa na umri wa miaka 4.

Baada ya mkewe kufariki, mwamba hakuchelewa, akakutana na huyu mkongo, akatangaza ndoa na kuanza maisha mapya (kumbuka hapo jamaa alikuwa na mtoto wa miaka 4), baadae na mkongo akamletea mtoto mungine wa kike, so jumla jamaa ana watoto wawili. Maisha yao huko walipokuwa haswa kwa upande wa mtoto wa kambo sijui yalikuaje, ila baada ya kuhamia jirani yetu na kufahamiana na jamaa, ndo nikaanza kuona mateso anayopitia mtoto.

Japo imezoeleka kuona mama wa kambo wengi ni makatili, lakini huyu aisee ni zaidi ya shetani. Hana chembe ya huruma, utu wala ubinadam. Anaweza kumpa mtoto adhabu ya kuweka miguu juu (ukutani) mikono chini (mfano wa sarakasi) kwa muda mrefu zaidi, bila kushusha miguu chini, na akishusha anakula kipondo ambacho anatakiwa kupigwa mwizi huko polisi.

Yote tisa, kumi ni pale anapomshindisha na njaa, alafu akigundua kuwa alikuja kwangu na wenzake (watoto wangu) akala, basi atachokutana nacho atajuta ni kwanini alimpoteza mama yake akiwa bado mdogo. Atapigwa, atapewa adhabu ya kuweka miguu juu, na kushindishwa na njaa.

Kila nlipotaka kumwambia jamaa kuhusu mateso anayopitia mwanae, moyo ulisita, nisije kuharibu ndoa ya watu au kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto mwenyewe. So niliamua kushona mdomo wangu tu kama sijui kinachoendelea.

Huyu mama mwanzoni alianza kuwa karibu na mke wangu, kutokana na ukaribu uliopo mimi na mumewe. Lakini alipogundua kwamba mke wangu huwa na tabia ya kumpa chakula mtoto anaeteswa, na sometimes kumpa hela pamoja na watoto wangu ili wanunue vitu vidogo vidogo vya kula, basi yule mama wa kambo akakata mawasiliano na mke wangu, na madam nae akampotezea kwa kufuata ule msema wa "akunyimae kunde, anakupunguzia kuja...m..ba.

Mtoto bado mdogo (miaka 7) kumweleza baba yake anashindwa, na mama huwa hampi nafasi ya kumsogelea baba yake akae nae mwenyewe. Halaf mtoto nguo, na viatu vimemuishia mpaka aibu naona mimi.

Juzi alhamisi nikaona upuuzi, wakati natoka mihangaikoni kwangu nikaingia dukani nikanunua nguo suruali 5, T'shirt 5, mashati mawili, jacket za baridi 3, viatu pea 3 na sandroz pea 1. Nikaenda mpaka kwa home boy nikamkabidhi mkewe nikamwambia kuwa zile nguo na viatu nilikuwa nimemnunulia mwanangu, lakin kwa bahati mbaya nimekuta havimtoshi, so ndomaana nikaona nimpe yeye ambae vinaonekana kumtosha, alaf mimi nitaenda na mtoto wangu town nikamnunulie vingine. Yule mama akapokea, lkn ni kwa shingo upande (kumbuka ni shemej yangu) halaf sina ugomvi nae yeye wala mumewe. So hakuwa na nguvu ya kukataa uso kwa uso.

Kumbe na yeye jana alienda town, akanunua nguo zake kadhaa, na kuja nazo nyumban kwa malengo yake binafsi. Usiku mumewe alipofika akaanza kumwambia kuwa mimi nimekuwa nikimtongoza na kumtaka kimapenzi muda mrefu bila mafanikio, na kwamba nilifikia hadi hatua ya kumnunulia yeye na mtoto (wa kambo) nguo ili anikubali, lakini bado alinikwepa na kuchukua tu nguo ili aje amuonesha (mumewe) nk.

Home boy alipotaka ushahidi yule mama akaenda kutoa zile nguo alizoenda kununua jana town, akajumlisha na zile nilizopeleka kwa ajili ya kumpa mtoto wa kambo anaeteseka. Aisee sijui jamaa alikuwa katika hali gani usiku ule na sijui alilalaje.

Asubuhi naona home boy anakuja nyumban bila salam anaanza kunibwatukia mbele ya mke wangu na watoto wangu. Namuuliza tatizo nini, anabwaga zile nguo mbele yangu na kusema eti ashajua kila kitu kuhusu mpango wangu wa kumtongoza mkewe.

Eti natongoza kishamba sana kwa kukimbilia kuhonga nguo. Yani nikashindwa kumuelewa vizuri, mpaka alipofafanua kwamba nilikuwa namtongoza mkewe, nilipoona hakubaliani na mimi ndo nikaenda town kununua vijinguo vya kumlaghai ili nimpate kiurahisi nk.

Nikataka kutumia ukaribu wetu kumueleza kile kinachoendelea katika familia yake mpaka mimi kufikia hatua ya kununua zile nguo za mtoto wake, lakini bingwa hakunielewa, akawa mtata mwisho nikamuacha aongee akichoka aamue mwenyewe anachotaka kufanya.

Baada ya kuona lengo lake la kunichafua mbele ya familia yangu limefeli akaondoka akidai kuanzia leo mimi na yeye ni maadui. Nisimjue, asinijue, nisiende kwake, na hatokuja kwangu, kila mtu aangalie maisha yake, nikamwambia poa.

Kwa bahati nzuri mke wangu anajua kila kinachoendelea, so ile complain ya kumtongoza mkewe haikumuingia akilini.

Namuonea huruma sana home boy, ni kama mapenzi yamemfanya asifatilie kinachoendelea katika nyumba yake. Damu yake inateswa, na sisi tunaosaidia tunaonekana wabaya. Mateso anayopitia yule mtoto hakuna mtu yoyote mwenye huruma hapa JF anaweza kuyaona akayavumilia.

Nilikuwa na mpango wa kwenda ku report swala hili katika mamlaka husika, lakini kuna rafiki yetu (mimi na yeye) amesema nisubiri kwanza jamaa hasira ziishe hata week 1 au 2, halafu aite kikao kati yangu na home boy kwa ajili ya maridhiano, halaf hapo kwenye kikao ndo nitumie chance hiyo kumueleza home boy kile kinachoendelea katika familia yake, na sababu ya mimi kumpelekea yule mtoto zile nguo na viatu.

Huyu rafiki mimi nimemuelewa, lkn sielewi ni vipi mpaka leo jamaa haoni kuwa mtoto wake anateseka hata kwa muonekano tu wa macho. Ama kweli tenda wema uende zako. Na sio kila mwenye macho huona kilichopo mbele yake. Jamaa haoni na hasikii.

Dah...
Huyo shemeji mkongo ana kalio la maana?
 
Back
Top Bottom