Raia wa Zanzibar wapigwe marufuku kupiga kura ya kumchagua Rais wa Tanganyika

Waliwahi waomba waingie kwenye Muungano?

Kwa kuwa nyie ndio wenye shida lazima mfuate matakwa Yao.
 
katika huu Muungano ilitakiwa Tanganyika iwe na katiba na utawala wake hali kadhalika nayo Zanzibar.

Rais awe ni mmoja tu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ila Tanganyika na Zanzibar zinaweza kuwa na viongozi wao wakuu lkn si ma Rais.
Muhimu ni kuweko kwa usawa kwa kadiri wananchi watakavyoamua na si kama ulivyo sasa kwa huu Muungano ambao ni matokeo ya maamuzi ya watu wawili.
 
Wa
Watafurahi sana tu. Maana muda wa kwenda msikitini wakati mwengine wapo vituo vya kupigia kura
 
Vikosi vya Zanzibar siyo Jeshi ni migambo tu😃

Unamaanisha nini mkuu? Zanzibar haina Jeshi? Kwani hujui kuwa hata Mgambo nao ni "wanajeshi"?

Unajua anayewafunza mgambo?

Unajua kuwa na ng'ambo nao wanapinga saluti?

Kama ulikuwa hujui, Vikosi vya SMZ ni Jeshi la Zanzibar.
 
Umeelezea mengi,nikajua utajibu swali la mleta mada
Mwishoni ukarudi pale pale kwenye swali la mleta mada
 
Sijui Zanzibar..sijui Tanganyika.....sijui Tanzania...sijui blah blah

Who cares about those pieces of shitty holes?

All are managed like shit by CCM...who cares?

Aint nothing left,fvck em all.

Just tafuta hela achana na huu ufala wa kulilia upumbavu managed by CCM and bure politicians
 
Paskali kapuyanga Sana[emoji2]
 
Ni mtu MPUMBAVU,ZEZETA,TAHIRA,ZWAZWA &
MJINGA ambaye anasema Zanzibar siyo nchi,huwezi kusema Zanzibar siyo nchi kisa inakosa kitu inaitwa "SOVEREIGNTY".
Duh...!. Naomba kuheshimu mchango wako, huku nikielewa Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojifahamu!. Japo ukichaa uko ndani ya akili ya mtu, ila kupitia maandishi, ukisoma tuu, unaweza kujua mwandishi ni kichaa!. Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania?
P
 
MUUNGANO FEKI
UVUNJWE TUANZE KUUNGANA UPYA.

samahani hicho ni kichwa cha habari.
Labda naota au, au daah....
 

Paskali unazeeka vibaya,
Unatwambiaje znz Haina sovereignity wkt kimataifa inatambulika Kama nchi inayojitegemea
 
CCM ni ya Wazenji kwa zama hizi hivyo ni faida kwenye chaguzi za Sisiemu hiyo hoja yako sahau kabisa. Kinachoangaliwa ni ushindi tu hata kula wakipiga warabu wa Qatar ilihali ni wana CCM basi hapana shida.
 
Hata ardhi ni Kwa wazanzibar tuu
 
Umeongea vizuri sn, ni mjinga pekee anaweza kusema Zanzibar siyo nchi na wakati ina kila kitu chake, kwanza muungano uvunjwe haraka
Acha kusifia ujinga wewe! jaribu ku' google "criterias of statehood under international law" ujue nchi inatakiwa kuwa na sifa gani.
Hizo sifa mnazozieleza hata Palestina wanazo, lakini wameshindwa kutambulika kama nchi nchi, halafu unajiita Benjamin Netanyahu! hii tabia yako ya kujinasibisha na ukristo wakati elimu yako ni ya madrassa, acha mara moja!
 
Hivi wewe jamaa hizo fani zako za uandishi na uanasheria umezipata wapi mbona nakuona unabwabwaja tu kama mtu aliyetoka kuota ndoto za kutisha! Eti alaumiwe Nyerere! Wakati unajua huyo Nyerere ameshakufa lakini sio kama ameondoka na akili zetu zote.
Huu Muungano haueleweki hata mfumo wake mara utasikia serikali ya Tanganyika ipo ndani ya serikali ya Muungano sasa unajiuliza ikiwa ndiyo hivyo ina maana Rais wa JMT akiwa Mzanzibar automatically anakuwa pia ndiye Rais wa Tanganyika sasa tujiulize Mzanzibar anakuwaje Rais wa Tanganyika wakati yeye si Mtanganyika! Kwa sababu yeye Utanzania wake unatokana na Uzanzibar wake na hiyo haimfanyi kuwa Mtanganyika moja kwa moja na ndiyo maana hata wao Wazanzibar hawaruhusu mtu asiye Mzanzibar kushiriki mambo yao,sasa hilo kama watu wazima tunashindwa kukaa na kurekebisha hizo kasoro zilizopo kwenye muundo wa Muungano wetu hadi tuseme aah tumlaumu Nyerere tu,kwani Nyerere ni zindiko tuseme tukiligusa tu tutapata matatizo na hata ingekuwa hivyo huo ungekuwa ni ushirikina, Je tupo tayari kuabudu mazindiko na mizimu ya Nyerere?
Watanganyika tuendelee kupaza sauti kurekebisha muundo wa Muungano kwani muundo uliyopo ni wa ovyo kwa sababu hata huyo Rais unayemuita wa Muungano hana mamlaka yoyote upande wa Zanzibar hawezi kumwajibisha hata mtendaji wa mtaa labda akamchongee kwa Rais wa Zanzibar na Rais wa Zanzibar akikataa kumwajibisha huyo mtendaji huyo Rais wako unayemuita wa Muungano hana la kufanya.
Sasa anakuwaje Rais wa Muungano ambaye hana mamlaka upande mmoja wa Muungano.
 
Hakuna serikali ya Tanganyika wala Raisi wa Tanganyika, Ashukuriwe au alaumiwe Nyerere. Wazanzibari wana haki ya kumchagua Raisi wa Tanzania, kwa sababu nao ni sehemu ya Tanzania.
Nyerere sio Mungu kwamba alichokileta yeye hata kama hakitufai tuendelee kuking'ang'ania ,muungano kwa ufupi haufai na ipo sku utavunjika sio kwa serikali hii
 
Acha kupotosha watu wewe yule Mwinyi wa Zanzibar ni mbunge au rais ? Kama Zanzibar ni sehem ya Tz kuna nchi ina marais 2? Huu ni upuuz na huu ni muungano wa hovyo haijawahi kutokea
 
Kaka elimu ya uraia kwa kiwango kikubwa huwa inapatikana shuleni katika level tofauti, napata mashaka kidogo na hawa wadau kama ni Watanzania wenzetu, kwa kuwasaidia nimewaambia watafute 'criterias of statehood under internatioanal law' itawasaidia!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…