Raia wa Zanzibar wapigwe marufuku kupiga kura ya kumchagua Rais wa Tanganyika

Raia wa Zanzibar wapigwe marufuku kupiga kura ya kumchagua Rais wa Tanganyika

Bandiko hili ni kielelezo cha uhitaji mkubwa wa elimu ya uraia kwa Watanzania wenzetu!. Watu wenye ufahamu na hili watamuona mleta mada kama ni lijinga fulani, kumbe huu ndio uelewa wa baadhi ya Watanzania wenzetu, ni wajinga tuu kwa kutoelewa. Dawa ya mjinga ni kumuelimisha.
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT, ina rais mmoja, rais wa JMT ambaye anachaguliwa na Watanzania wote.
2. Tanzania ina uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania, hivyo Watanzania wote wana haki sawa ndani ya JMT, ikiwemo haki ya kupiga kura, na haki ya kugombea.
3. Tanzania ilitokana na muungano wa nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar, na kuwa nchi moja yenye sehemu mbili, Tanzania bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.
4. Tanzania bara haina utawala wake wa ndani, hivyo rais wa JMT ndie rais wa nchi anayechaguliwa na wote, lakini Zanzibar inao utawala wake wa ndani, seclusion, na rais wake, rais wa Zanzibar ambapo ni Wanzanzibari wakaazi pekee ndio wenye haki ya kuchamchagua rais wa Zanzibar.
5. Baada ya muungano wetu adhimu, Tanganyika ilikufa na kugeuka Tanzania, ila Zanzibar iliendelea kubaki sio kama nchi bali ilibaki kama sehemu ya JMT inayojitegemea.

Hivyo Wanzanzibari wote ni Watanzania na wana haki zote za kumchagua rais wa JMT ila wenye haki ya kumchagua rais wa Zanzibar ni Wazanzibari pekee!.

P
Mkuu mbona inakuwa mkali!.mleta MADA anahitaji umtajie faida ya muungano.

Maswala ya kuungana anajua historia yake.Faida yake nn.
Zanzibar Bado ni Nchi yenye Serikali mfumo mzima wa kiongozi wanao.Why Serikali ya Tanganyika ife,irihali JMT ni muungano wa Nchi mbili?.
Nchi ya Kwanza ni Zanzibar,na Nchi ya Pili ni ipi Kwa Sasa?.

Mzanzibari ana haki bara,ila wa bara hana haki Zanzibar,mbona nnajizima DATA wakubwa,mnakuwa na kigugumizi Cha Nini hasa.

Au Zanzibar kivingine no Koloni letu ama!.
Hapo ntaitwa mchochezi,ila kiukweli Mtanganyika Yuko wapi maana Mzanzibari yupo.Watanzania pia wapo.
Tupeni faida Kwanza,afu elimu ya uraia Kwa sisi wajinga itafata.
 
Duh...!. Naomba kuheshimu mchango wako, huku nikielewa Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojifahamu!. Japo ukichaa uko ndani ya akili ya mtu, ila kupitia maandishi, ukisoma tuu, unaweza kujua mwandishi ni kichaa!. Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania?
P


Nakuheshimu sana Pascal Mayalla

Jibu Hoja ya Mleta Hoja!

Naelewa Tanzania ni Muunganiko wa zilizokuwa nchi mbili (Tanganyika & Zanzibar)

1.Mleta Hoja kauliza ni Kwanini Tanganyika haturuhusiwi kumchagua Rais wetu wa Tanganyika ilihali wazanzibar wao wanampigia Kura na kumchagua Rais wao pia wanamchagua na kumpigia Kura Rais wa Jamhuri ya Muungano.

2.Kama nchi hizi mbili ziliungana na ikapatikana Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ni kwanini Zanzibar ina rais wake na Tanganyika haina Rais wake?

Sasa usije na hoja mfu na kuniambia eti, "Rais wa Jamhuri ndo huyo huyo wa Tanganyika"
 
Duh...!. Naomba kuheshimu mchango wako, huku nikielewa Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojifahamu!. Japo ukichaa uko ndani ya akili ya mtu, ila kupitia maandishi, ukisoma tuu, unaweza kujua mwandishi ni kichaa!. Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania?
P
Mzee ni muda sasa wa wewe kupumzika na kula pensheni yako taratibu.
Usituletee tafsiri zenu za kwenye maandiko.
Tuache tutafsiri uhalisia.
Tunatafsiri tunacho kiona na kukiishi.
ZANZIBARI ipo hai.
TANGANYIKA imemezwa na jina TANZANIA.
Zanzibari wanapata haki nyingi tofauti na watanzania wengine.
Kwenye mambo yenye faida kwao nao hujiita WATANZANIA na hili hutokea mara chache sana MZANZIBARI kujiita MTANZANIA.
Nyie vizee mna shida, kujiona mnaweza kudanganya watu vizazi na vizazi.
Vijana wanafikiri yale wanayoyaishi, kipindi nyie wenye mitumbo mikubwa mnafikiri yale yaliyoandikwa.
Kilichoandikwa kama kipo tofauti na uhalisia hapo kuna shida.
 
Bandiko hili ni kielelezo cha uhitaji mkubwa wa elimu ya uraia kwa Watanzania wenzetu!. Watu wenye ufahamu na hili watamuona mleta mada kama ni lijinga fulani, kumbe huu ndio uelewa wa baadhi ya Watanzania wenzetu, ni wajinga tuu kwa kutoelewa. Dawa ya mjinga ni kumuelimisha.
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT, ina rais mmoja, rais wa JMT ambaye anachaguliwa na Watanzania wote.
2. Tanzania ina uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania, hivyo Watanzania wote wana haki sawa ndani ya JMT, ikiwemo haki ya kupiga kura, na haki ya kugombea.
3. Tanzania ilitokana na muungano wa nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar, na kuwa nchi moja yenye sehemu mbili, Tanzania bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.
4. Tanzania bara haina utawala wake wa ndani, hivyo rais wa JMT ndie rais wa nchi anayechaguliwa na wote, lakini Zanzibar inao utawala wake wa ndani, seclusion, na rais wake, rais wa Zanzibar ambapo ni Wanzanzibari wakaazi pekee ndio wenye haki ya kuchamchagua rais wa Zanzibar.
5. Baada ya muungano wetu adhimu, Tanganyika ilikufa na kugeuka Tanzania, ila Zanzibar iliendelea kubaki sio kama nchi bali ilibaki kama sehemu ya JMT inayojitegemea.

Hivyo Wanzanzibari wote ni Watanzania na wana haki zote za kumchagua rais wa JMT ila wenye haki ya kumchagua rais wa Zanzibar ni Wazanzibari pekee!.

P
Wewe unafikiri mleta mada hayafahamu haya yote uliyoandika?
 
Mzee ni muda sasa wa wewe kupumzika na kula pensheni yako taratibu.
Usituletee tafsiri zenu za kwenye maandiko.
Tuache tutafsiri uhalisia.
Tunatafsiri tunacho kiona na kukiishi.
ZANZIBARI ipo hai.
TANGANYIKA imemezwa na jina TANZANIA.
Zanzibari wanapata haki nyingi tofauti na watanzania wengine.
Kwenye mambo yenye faida kwao nao hujiita WATANZANIA na hili hutokea mara chache sana MZANZIBARI kujiita MTANZANIA.
Nyie vizee mna shida, kujiona mnaweza kudanganya watu vizazi na vizazi.
Vijana wanafikiri yale wanayoyaishi, kipindi nyie wenye mitumbo mikubwa mnafikiri yale yaliyoandikwa.
Kilichoandikwa kama kipo tofauti na uhalisia hapo kuna shida.
Well said 👏👏👏
 
Mtu ukiwa hujui kitu fulani, ni mjinga!, mtu kuwa mjinga sio kosa, kwasababu kutokujua kitu fulani sio kosa, ukiisha julishwa, ujinga unakutoka unakuwa mwerevu.

Ili nchi kuwa taifa, sio eneo, sio rais, sio bendera, sio wimbo wa taifa, nchi kuwa taifa ni kitu kinachoitwa sovereignty, dola!, Zanzibar haina sovereignty, sio dola!. Tanzania ni nchi moja ya JMT, ndio yenye sovereignty, yenye dola, yenye vyombo vya dola, yenye sarafu, Zanzibar ni jina tuu, la nchi lakini sio nchi, na rais wa Zanzibar ni rais jina tuu wa sehemu inayoitwa Zanzibar lakini kimataifa sio rais, rais ni mmoja tuu, rais wa JMT na nchi ni moja tuu, JMT, Zanzibar sio nchi ni sehemu ya JMT!.
P
Hii ndio shida ya wanaojiita WASOMI kwenye nchi nyingi za kiafrika.
Unatuletea tafsiri za kimataifa, wakati sisi tunahitaji tafsiri za tunachokiona na kukishuhudia.
Tukikuita wewe ndio mjinga, litakuwa kosa?
 
Acha kusifia ujinga wewe! jaribu ku' google "criterias of statehood under international law" ujue nchi inatakiwa kuwa na sifa gani.
Hizo sifa mnazozieleza hata Palestina wanazo, lakini wameshindwa kutambulika kama nchi nchi, halafu unajiita Benjamin Netanyahu! hii tabia yako ya kujinasibisha na ukristo wakati elimu yako ni ya madrassa, acha mara moja!
Umeanza konyagi asubuhi hivi mkuu
 
Nawapongeza Zanzibar kwa kuwa na msimamo, huwezi kupiga kura ya kumchagua rais wa Zanzibar ikiwa wewe si mzanzibari.

Cha ajabu serikali ya Tanganyika inaingiliwa na Zanzibar, yaani raia wa nchi jirani (Zanzibar) wanapiga kura kuchagua Rais wa Tanganyika.

Jambo hilo lingekuwa na mantiki endapo nasisi Watanganyika tungeruhusiwa kushiriki kuwachagulia Rais watu wa Zanzibar. Kwakuwa hatuwaingilii kwenye uchaguzi wao, na wao wazuiliwe maramoja kutuchagulia Rais.
Kumbuka hao wapo sababu ya ccm.

so bila kutoa ccm na Kiongozi mkuu ni wahuko huamini kama unapaka rangi upepo?
 
we bwege hiyo Tanganyika umeijulia wapi, nani aliipa hilo jina. Fanyeni kazi acheni mambo ya kipuuzi nchi yetu ni Tanzania, mpaka unakufa hutakaa uipate hiyo nchi yako ya kufikirika
Kwenye bandiko langu umeona nikiitaja Tanganyika kama nchi?
Nahitaji TANZANIA yenye umoja wa kweli,
Kabla sijasahau BWEGE bibi yako!
 
katika huu Muungano ilitakiwa Tanganyika iwe na katiba na utawala wake hali kadhalika nayo Zanzibar.

Rais awe ni mmoja tu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ila Tanganyika na Zanzibar zinaweza kuwa na viongozi wao wakuu lkn si ma Rais.
Hakuna hata haja ya Tanganyika na Zanzibar kuwa na viongozi wake wakuu, vitu viwili vikiungana kinazaliwa kitu kimoja kikubwa nacho ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rais mmoja wa Tanzania na makamu ambao watapatikana kwa utaratibu ulipo sasa.

Kwani Zanzibar ingefanywa kama mkoa kama ilivyo DSM, isingetawalika?
 
Nakuheshimu sana Pascal Mayalla

Jibu Hoja ya Mleta Hoja!

Naelewa Tanzania ni Muunganiko wa zilizokuwa nchi mbili (Tanganyika & Zanzibar)

1.Mleta Hoja kauliza ni Kwanini Tanganyika haturuhusiwi kumchagua Rais wetu wa Tanganyika ilihali wazanzibar wao wanampigia Kura na kumchagua Rais wao pia wanamchagua na kumpigia Kura Rais wa Jamhuri ya Muungano.

2.Kama nchi hizi mbili ziliungana na ikapatikana Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ni kwanini Zanzibar ina rais wake na Tanganyika haina Rais wake?

Sasa usije na hoja mfu na kuniambia eti, "Rais wa Jamhuri ndo huyo huyo wa Tanganyika"
Kwa kuongezea tu, Zanzibar ina Rais wake, Jeshi lake, mkuu wa majeshi yake na Amiri Jeshi Mkuu wake.
 
Kuwa na kila kitu chake hakuifanyi kuwa nchi, kitu pekee kinachoifanya nchi kuwa nchi ni kitu kinachoitwa sovereignty!, Zanzibar haina sovereignty, hivyo sio nchi!.
Hata uwe na kila kitu, kama hauna sovereignty, you are nothing!.
P
Kivipi wakati ina mpaka Jeshi lake na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi yake?
 
Naomba kuheshimu maoni yako, ujinga ni kutokujua, hivyo mtu yoyote anayedhani Zanzibar ni nchi, ni mjinga kwa kutokujua kuwa Zanzibar sio nchi kwasababu haina sovereignty na haina dola!. Wale majeshi yake ya KMKM, JKU na vikosi vya SMZ, sio majeshi!, wale ni migambo tuu!. Zanzibar haina polisi, haina jeshi, haina sarafu, haina sovereignty!. Sio nchi!.
P
Kwa kawaida migambo TANZANIA wanamiliki virungu.
Pia migambo TANZANIA wana jezi zao.
Hao migambo wa Zanzibar wapo hivyo?
Kuna mfanano wowote kuanzia mavazi hadi siraha kati ya mgambo wa huku bara na hao wazanzibari?
 
Naomba kuheshimu maoni yako, ujinga ni kutokujua, hivyo mtu yoyote anayedhani Zanzibar ni nchi, ni mjinga kwa kutokujua kuwa Zanzibar sio nchi kwasababu haina sovereignty na haina dola!. Wale majeshi yake ya KMKM, JKU na vikosi vya SMZ, sio majeshi!, wale ni migambo tuu!. Zanzibar haina polisi, haina jeshi, haina sarafu, haina sovereignty!. Sio nchi!.
P
Hili siyo Jeshi?

Labda uniambie unawasilisha ujumbe wako kwa "code", vinginevyo utaonekana kituko kusema Zanzibar haina Jeshi wakati iko wazi kabisa kuwa Zanzibar ina Jeshi lake na mkuu wake wa majeshi na Amiri Jeshi Mkuu.
 

Attachments

  • Mkuu_wa_JKU_awapandisha_vyeo_wapiganaji_wa_Jeshi_la_Kujenga_Uchumi_katika_ngazi_mbalimbali(144p).mp4
    22.4 MB
  • RAIS_MWINYI_AWAPANDISHA_VYEO_MAAFISA_WA_NGAZI_YA_JUU_WA_JKU_KANAL_DAIMA_AWAVALISHA_KWA_NIABA_Y...mp4
    2.7 MB
Back
Top Bottom