Rais anavyotembea na walinzi waliobeba mitutu anaonesha nini wananchi?

Rais anavyotembea na walinzi waliobeba mitutu anaonesha nini wananchi?

Raisi ni raisi tu lazima alindwe hadi amalize muda wake kikatiba. Ingawa simkubali Mh.Samia toka anakuwa makamu wa raisi lakini hili la ulinzi mkubwa namuunga mkono tena aongezewe ulinzi mkubwa zaidi.
Mungu amjalie maisha marefu alee wajukuu zake.
Unamiss the point mkuu. Kwa nini marais wengine wakija ziara humu nchini hawaji na majamaa yamebeba himars hadharani? Kuna protocol za kidiplomasia, yani unakuwa na ulinzi, tena wa kutosha tu, lakini silaha hazionekani hadharani. Umenipata mkuu?
 
Chief mimi huwa namkosoa mama kwenye mambo mengi tu lakini kwenye swala la usalama wa Rais bado hata huo uliouona hautoshi.Rais ni lazima alindwe mkuu.
tupo na maadui wengi wa nje na ndani.
Umemjibu vyema,maana tusijekufikia kuchukia hata tembea ya mama wa watu tukadai atembelee mguu mmoja
 
Unamiss the point mkuu. Kwa nini marais wengine wakija ziara humu nchini hawaji na majamaa yamebeba himars hadharani? Kuna protocol za kidiplomasia, yani unakuwa na ulinzi, tena wa kutosha tu, lakini silaha hazionekani hadharani. Umenipata mkuu?
Mikwala ni Deterrence ya gharama nafuu mkuu
 
Hata ujilinde na mamilioni ya Askari,siku wakiamua kukutoa wanatumika hao hao wa ndani na walinzi.
Uwe kama Nyerere tu. Ukiwa kawaida kwa wananchi hao. Unatenda yaliyo sawa kwa nchi. Keki ya Taifa inagawiwa sawa mpaka kwa wakulima masikini huko chini,hakika unaweza ukatembea bila hata mlinzi mmoja.
Lakini sio kama sasa mafisadi wachache wameikamata nchi. Wanaitafuna nchi kuanzia madini,mpaka gesi. Kuanzia Mali asali mpaka wanyama. Kuanzia ardhi mpaka tozo. Kuanzia madawa ya kulevya mpaka pesa yote wameficha. Hapo unategemea nini wakati wananchi wengi wananung'unika?.
Mkuu rejea ile video ya issis wa Msumbiji walisema wanataka kumla kichwa Rais wa TZ.
maadui wapo wa nje na ndani uwezi kuwa Rais kwa nchi zetu hizi za matopeni alafu ukaacha kujilinda,hata uwe unagawa mamilioni kwa wanachi bado kuna maadui watakuwepo tu.
 
Rais ni icon ya nchi. Usalama wake ndio usalama wa nchi. Intelijensia inaliangalia hili kwa ukaribu sana, na kupanga safu ya ulinzi kwa Rais kwa kadiri wanavyoona inafaa kwa siku husika. Kwa hiyo, kumbe ulinzi wa Rais sio jambo lisilobadilika (kama tulivyozoea). Kumbuka tunakwenda na mabadiliko ya tekinolojia, ulinzi wa miaka ya 2000 hauwezi kutumika leo. We respond due to technological changes!
Kizungu miiiingi, umeelewa pointi yangu mkuu? Kuna wananchi kama kulivyo na rais pia. Lakini tukianza kuingiza siasa kwenye suala la usalama, mwishowe watu watakuja lipuana au kupotezana(rejea watu wasiojulikana).
 
Maadui wetu ni ujinga, umasikini na maradhi. Nini kilimtoa mtangulizi wake, licha ya ulinzi kama kundi la ng'ombe?
Niambie wewe ni nchi zipi Duniani zilizoendelea Rais akakosa ulinzi madhubuti?

ntajie nchi isiyo na wajinga,maradhi na umasikini alafu Rais alindwi?
 
Mbona huwa sioni wanajeshi walioshika Mitutu kwenye ziara za Macron au marais wa mbele?
Ahsante. Kuna watu wabishi humu hawajaelewa mada.... je inamaanisha hao marais hawana ulinzi wa kutosha?
 
Anaogopa wananchi watampiga.Maana nchi ameiharibu sana toka arithi utawala wake kwa mzalendo magufuli
Kabisaaaaa!!! Wewe ndio umeread between the lines ukanisoma... na sio kwamba asiwe na ulinzi wa kutosha, bali anaweza kuwa na majamaa yamebeba mpaka mabomu ya nuclear, ila hazionekani hadharani.....rais anatakiwa ku appear approachable kwa wananchi. Ila ile ni move ya kisiasa, ili hata kama kuna mwenye duku duku lake...aogope asiseme chochote. Tungoje tuone wakati anafanya kampeni, kama hizo himars zitaonekana hadharani.
 
Mpaka hapo uzi kamili....

Nimeona mama yuko ziara, halafu majamaa yamepiga combat, na mitutu juu, halafu ziara yenyewe ni kaenda kuona wananchi wake.

Hii ina effect gani kisaikolojia kwa wananchi? Na inamaanisha nini? Maanake sio kwamba usalama wameshindwa kuweka usalama pasipo 'ku send message'....sijui kama naeleweka lakini.
Usalama wenye akili walishawekwa kando.

Sasa ni matumizi ya nguvu kisha akili baadaye
 
Back
Top Bottom