Si ndiyo vizuri na Kariakoo yetu sasa ina sura ya kimataifa badala ya zamani ya kizaramo. Na wazungu wanakaribishwa Kariakoo kuchoma mahindi na kuuza mitumba.Inapumbaza na kukufanya usiwakatalie lolote watakalokwambia.
Kumbuka walimpa Kikwete U professa wa Heshima, matokeo yake leo hii Kariakoo kuna wachina wanarusha Mpesa Tigopesa na Kuchoma mahindi.
Tafakari
Hu
Huyo mchina alieko na mzee wa mbepa za tasker baridi ndio nani?
Mrabaha ni 4% sio 3%.Mikataba yote alisaini JK ni yakupitia upya na kufanya marekebisho na mingine bora kuivunjilia mbali km haina tija kwa taifa letu.China inataka ubia na mataifa ya Afrika kwa ajili ya makampuni yake ya ujenzi nk na pia kuongeza ushawishi wao Afrika.Angeenda Vietnam tuna mengi ya kujifunza kutoka kwao kuliko wachina wanaongoza kwa biashara ya pembe za ndovu na kuifanya tz dampo mpk la yeboyebo
Mbona mapema mno kuanza kutembeza bakuli?Kwa mujibu wa duru muhim ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje, Mheshimiwa Rais anatarajiwa kufanya ziara rasmi nchini China baadae mwezi huu.
Katika ziara hiyo Pamoja na matukio mengine Mhe Raisi atashiriki mazungumzo na kusaini makubaliano mbalimbali juu ushirikiano wa China na Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Kadhalika Mheshimiwa atatunukiwa Shahada ya juu ya heshma toka chuo kikuu kimojawapo mashuhuri Jijini Beijing.
Hoja kwamba eti "mikataba yote alisaini JK" ni ya uongo mkubwa. JK hakusaini mikataba yote yote ile. Isipokuwa ni kweli mikataba mingi ilisainiwa chini ya uongozi wake. Kuweni makini na taarifa zenu. Humu ndani ya JF siyo wote mambumbumbu...
Sema tena!Usinilazimishe nikudharau kama Mh.Jussa Ladhu alivyomdharau Mpanju.Ziara pekee ninazoweza kuzihesabu kama ziara zenye tija kwangu ni zile zilizofanywa na Mwl.Nyerere(R.I.P)za kwenda Uingereza "kufuatilia Uhuru wa Tanganyika".
Zaidi ya hapo sioni cha Maana toka kwa hao unaowaabudu.Kama ni suala la uwekezaji,hakuna uwekezaji wowote uliowahi kufanywa na mgeni ukaleta tija kwa Taifa letu.Uwekezaji unaokomba Rasilimali zetu huku Taifa likiambulia Mlabaha wa 3% kwangu mimi sioni kama ni jambo la kujivunia kiasi cha kupongeza ziara za ng'ambo.
Iko wapi mikataba 17 iliyisainiwa Ikulu baina ya Uchina na Tanzania? Imeleta tija gani kwa Taifa letu? Wachina hao unaowashabikia ndiyo walioligeuza Taifa letu kuwa " dampo"la kutupia kila aina ya bidhaa feki toka uchina kwa kisingizio cha kukuza biashara kati yetu.Leo hii hadi baadhi ya member wa jf wapo hatarini kutoweka jukwaani kwa sababu ya kutumia "vifaa feki" vya kichina.
Sijaona mchango wa maana ulioletwa na Uchina,zaidi sana Wachina ndiyo wanaonufaika na kandarasi za miradi mbalimbali ya Maendeleo ambayo inafadhiliwa na Mataifa mengine,Wachina wanatajirika zaidi toka kwetu kuliko sisi tunavyopokea toka kwao.
hahahahaha mkuu kwani ile 11 ulijua kuna nini hadi ustuke? maana hadi leo hatujapata madhara,kwa hiyo tuamini itakuwa ya manufaa kama iliyotangulia tu.Ninaposikia habari ya kusaini mikataba moyo unafanya ''paaah''
Hivi mbona Marekani na Ulaya haikufungua vikwazo vya Zimbabwe baada ya Mugabe kufungamana na China? Mbona China hakumwaga hayo mapesa kuokoa uchumi wa Zimbabwe? Sio kosa lenu.... Lishe duni imewatafuna akili zenu kiasi cha kushindwa kufikiri.
Nakuunga mkono. Nadhani ana washauri wazuri. Hizi nchi za Ulaya zinakwenda kufilisika na kufa wakati mashariki inaibuka juu. ni karne ya mashariki hii ijayo na vizuri kuweka misingi imara. Ingawaje JK pia aliendeleza uhusiano na China ila alikuwa na mioyo miwili. Anapenda kujiona zaidi kuwa ni mzungu. Hata utaona namna alivyomlaki Obama na rais wa China. Obama alimpa heshima kubwa wakati Wamarekani hawana msaada wowote wa maendeleo. Kazi yao kubwa ni majungu tu na mambo ya kuuwana, sijui terrorism na kupambana na mbu!Kama ni kweli. Basi JPM ana akili sana
Asijione kwamba anamkomoa mzungu kwa yeye kwenda china, hawa wachina si watu kabisa. Namkubali mzungu mara 200% kuliko mchina kwa .002%.Marekani na Yuropa wakisikia hivi, lazima warejeshe hela walizosusa kuzitoa.
Hawatakubali kuona mchina anapata influence kubwa namna hii ukanda huu.
Na ukitaka kupata influence kwa masikini, we mwaga mihela, utapendwajeee
Sasa unakubali nini na unakataa nini?? Ok ila inafahamika na ilitangazwa kua jamaa alisaini mikataba 17 at per na rais wa China alivyokuja hapa Tz , tunajua kwa nini ilimbidi asaini hiyo mikataba yote bila kubisha wala kushauriana na wanasheria wa wizara husika.
Nakuunga mkono. Nadhani ana washauri wazuri. Hizi nchi za Ulaya zinakwenda kufilisika na kufa wakati mashariki inaibuka juu. ni karne ya mashariki hii ijayo na vizuri kuweka misingi imara. Ingawaje JK pia aliendeleza uhusiano na China ila alikuwa na mioyo miwili. Anapenda kujiona zaidi kuwa ni mzungu. Hata utaona namna alivyomlaki Obama na rais wa China. Obama alimpa heshima kubwa wakati Wamarekani hawana msaada wowote wa maendeleo. Kazi yao kubwa ni majungu tu na mambo ya kuuwana, sijui terrorism na kupambana na mbu!
Akitoka huko aende Vietnam, nchi inayokuja juu sana na yenye mengi ya kuiga. Kisha aende Uturuki. Huko iatuwa ndege wawili kwa jiwe moja. Ziara yake Uturuki utawapoza moyo wazungu kuwa hailekei Mashariki tuu, lakini pia Uturuki inapenda sana kujipanua ufukwe wa Mashariki ya Afrika. Labda Iran pia itakuwa vizuri kuzatiti uhusiano. Wanaweza kutusaidia kujenga mabwawa ya kuzalisha umeme dams, na pia kujenga mtambo wa kusafishia mafuta huko Tanga. Wapange ziara hii wakiwa na akili za mwaka 2050 wakati idadi ya watu wa Tanzania itafikia milioni 100.
Sawa kabisa.Tunataka mikataba ya uwazi na ipelekwe Bungeni