Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, mbadilishe Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu hatoshi

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, mbadilishe Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu hatoshi

Yaani wewe ni bumunda kweli. Hivi preintetnship mantiki yake ni ipi hada? Kinachofanywa kwenye Logbooks hua ni kitu gani au kinasaidia nini?
Pre-intership imepangwa na MCT kuhakiki ubora wa MD aliyemaliza shahada...hapo kuna mengi wanapata na kugundua.....(yako mapendekezo ya maboresho ya elimu yetu yanatoka hapo).

Katika Pre-Internship ni kumwezesha mtahiniwa kufuzu kupewa (PROVISIONAL REGISTRATION)....ili aende akafanye INTERNSHIP(mafunzo ya utarajali).

Post-Internship ni kumtahini daktari aliyekwisha kupata cheti chake cha kumaliza INTERNSHIP(mafunzo ya utarajali katika hospitali husika) kuweza kupewa LESENI na MCT(full registration)....ili akaanze kutibu...

Sasa wewe zwazwa unataka bodi ya madaktari isiwe na vigezo vyao* vya kuboresha huduma zetu za afya kwa MACHUJIO hayo?!!!

Sakala wewe[emoji1787][emoji1787]
 
Yaani wewe ni bumunda kweli. Hivi preintetnship mantiki yake ni ipi hada? Kinachofanywa kwenye Logbooks hua ni kitu gani au kinasaidia nini?
Sikiza wewe hobobo....

Hivi unajua kuwa wako wanafunzi wanatunukiwa SHAHADA zao za udaktari na kutokwenda kufanya INTERNSHIP na kuingia mitaani kubangaiza njia nyingine za kimaisha(hatakiwi kutibu)...japo anabaki kuwa ni "DAKTARI...ILA ASIYETIBU"

Kwa sababu ya hili ndio maana MCT wakaweka utaratibu wa PRE-INTERSHIP EXAMS ili kuwafanya wale wahitimu wanaotaka KUTIBU wawe na mipango ya NIDHAMU bora ya kimasomo toka wakiwa mavyuoni...unapewa "pepa" ili uweze kupata cheti cha kwenda kufanya INTERNSHIP(mafunzo ya utarajali) kinaitwa PROVISIONAL REGISTRATION....

Huko katika mafunzo ya utarajali hupewa vitabu(log books) wanatakiwa wakishamaliza internship wavipeleke MCT...pamoja na cheti cha taaluma Kutoka hospitali waliofanyia mafunzo ili "wakishatahiniwa" wapewe FULL REGISTRATION &LESENI YAO...sasa wako ambao wanapita njia za panya(hawako serious huko mafunzoni ,wako wanaofoji kujaza hizo LOG BOOKS hata kwa kubebwa....rushwa tofauti....).

Ukiyakusanya hayo utamaizi kuwa MCT haijakosea kuweka hatua hizo na WAZIRI UMMY MWALIMU hana kosa lolote...

Umesikia "pungerrr sese" ?!!

Sawa "pungerrr sese"?!!!

Umeelewa wee "pungeeer"?!!
[emoji1787][emoji1787]
 
Nchi nyingi Duniani hakuna Dactari anayeingia moja kwa moja bila ya mtihani wa leseni ... USA wana USMLE ambapo wanafanya hadi oral , India wana FMGE na kadhalika kwa ufupi ni lazima kuwe na lesence exam na hiyo ipo maeneo mengi duniani .. haya malalamiko ya madactari taraji hayana maana vijana wasome .. ila tu kuwe na standard ya mtihani isiwe kama ile ya vyuoni
Hawataki mitihani wakati wanajiona wajuaji sana. Angalia waliopo makazini utaelewa nasema nini. Mitihani iwepo ni muhimu sana kuchuja na hii italeta nidhamu kazini. Wakiajiriwa utasikia wanaanza kudai nyongeza za mishahara bila kujali kwamba wao ni watoa huduma siyo wazalishaji.
Mitihani iwepo na tena iwe migumu na kila mwaka itungwe mipya ili kwenda na wakati, wasiache mtihani ukawa ule ule utachuja kisha itakuwa siyo haki kwa waliotangulia maana wafuatao wataanza kuyafahamu maswali na kuacha kujifunza badala yake wakaanza kusoma kufaulu mitihani.
Hili la mitihani liwe kwa kada zote nchini, hakuna mshahara unaonyesha kama mvua. Wahitimu watahiniwe ili tupate wataalamu wenye kuleta tija, badala ya wasaka tonge.
Na mitihani isiwe rahisi, maana tunaona nchi inavyochezewa, unakuta wanunua vyeti ndio viongozi wakuu, kapachikwa na aliyekuwa kiongozi mkuu ama kwa rushwa, au kujuana. Hatutaki haya yajirudie.
 
Sikiza wewe hobobo....

Hivi unajua kuwa wako wanafunzi wanatunukiwa SHAHADA zao za udaktari na kutokwenda kufanya INTERNSHIP na kuingia mitaani kubangaiza njia nyingine za kimaisha(hatakiwi kutibu)...japo anabaki kuwa ni "DAKTARI...ILA ASIYETIBU"

Kwa sababu ya hili ndio maana MCT wakaweka utaratibu wa PRE-INTERSHIP EXAMS ili kuwafanya wale wahitimu wanaotaka KUTIBU wawe na mipango ya NIDHAMU bora ya kimasomo toka wakiwa mavyuoni...unapewa "pepa" ili uweze kupata cheti cha kwenda kufanya INTERNSHIP(mafunzo ya utarajali) kinaitwa PROVISIONAL REGISTRATION....

Huko katika mafunzo ya utarajali hupewa vitabu(log books) wanatakiwa wakishamaliza internship wavipeleke MCT...pamoja na cheti cha taaluma Kutoka hospitali waliofanyia mafunzo ili "wakishatahiniwa" wapewe FULL REGISTRATION &LESENI YAO...sasa wako ambao wanapita njia za panya(hawako serious huko mafunzoni ,wako wanaofoji kujaza hizo LOG BOOKS hata kwa kubebwa....rushwa tofauti....).

Ukiyakusanya hayo utamaizi kuwa MCT haijakosea kuweka hatua hizo na WAZIRI UMMY MWALIMU hana kosa lolote...

Umesikia "pungerrr sese" ?!!

Sawa "pungerrr sese"?!!!

Umeelewa wee "pungeeer"?!!
[emoji1787][emoji1787]
Hata kama hataki ujumbe umeshafika. mitihani lazima hata kama wakipewa mitihani ya USMLE wafanye tu, wao si wamehitimu? sas wa prove kwamba wako tayari, ujanja ujanja ndio tatizo la nchi yetu hii. Kuna watu wanasoma wako makazini, mitihani wananunua na wanfaulu kuliko hata wale wanaojituma haswa. Hakuna kulegeza MCT isimame imara, hatutaji madaktari mabishoo sisi.
 
Acha vijana wafanye mitihani, hiyo mikopo yao ya HELSAB isiwe kigezo cha kulegeza, wakaze tupate vijana bora. Hatutaki kila siku wananchi tukimbilie India, tunataka ngoma ziishie hapa hapa mkuu.
 
Rais kwanza nikupe pole na heshima yako na nikupongeze sana Mama kwa uwajibikaji wako katika kulisaidia Taifa hili kwa kuliponya kutoka katika mazingira magumu miaka 8 iliyopita. Hakika tunaweza kusema ya kwamba mabadiliko ni makubwa sana katika sekta zote ispokua baadhi ya Watendaji wako ndio wanaokuharibia na kuendelea kukuchelewesha kufika kule mbali unakotazama.
Bila hiyana wala unafki kwakweli kongole Mama!👏👏

Rais tunafahamu kwamba falsafa yako kubwa katika utendaji ni kuwaacha watendaji wako wafanye kazi wenyewe kwa kujisimamia bila pressure yeyote ya mamlaka tena kwa ubinifu mkubwa. Hii ndio misingi ya kweli ya kiutawala.

KWANINI WAZIRI UMMY ABADILISHWE?

Rais, nikiwa kama Mtanzania Mzalendo,Mdau katika masuala ya Afya na kada/kiongozi mtiifu katika chama cha Mapinduzi, sipendi tuharibikiwe nitaelezea mambo kadhaa muhimu ambayo pengine Mhe Waziri hakuambii ukweli au watendaji walio chini yake hawamwambii ukweli kwa vile yeye siyo mwanataaluma katika sekta ya Afya.

KUSHINDWA KUSIMAMIA NA KUTATUA KERO NA MALALAMIKO YA MADAKTARI TARAJALI(INTERNS) KUTOTENDEWA HAKI NA BARAZA LA MADAKTARI TANGANYIKA(MCT).

Rais wangu, ikumbukwe kua Madaktari tarajali waliwahi kukuandikia Barua ya wazi kwamba hawatendewi haki na Baraza la Madaktari Tanganyika(MCT) wakilalamikia mambo kadha wakadha ambayo nitayabainisha hapa.Lakini baada ya Barua hiyo Mhe Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alimtuma Naibu waziri wake Dr Godwin Moleli ambaye alikutana na Watarajali hao na kisha kueleza kero na changamoto zao. Baadaye Mhe Waziri Ummy Mwalimu alitoa taarifa kuunda tume ya kiuchunguzi kushughulikia changamoto hizo, lakini cha ajabu mpaka sasa hakuna mrejesho na walalamikiwa wanaendelea na kile kile kinacholalamikiwa.

Rais, katika mambo yanayolalamikiwa na watarajali hawa ni kama ifuatavyo;

(i)Kunzishwa kwa mitihani ya Pre-intetnships ambayo haieleweki msingi wake ingawa baraza lilidai kuwapima watarajali hao kutokana na kutilia shaka vyuo vikuu waliotoka. Lakini swali la kujiuliza ni kwamba, TCU kikiwa kama chombo cha kupima ubora wa vyuo vikuu kina kazi gani? Huyu Mwanafunzi aliyesoma miaka yote 5 chuoni kisha akafuzu mafunzo yote ya nadharia na vitendo hospitalini miaka yote anapimwa kitu gani hasa? Unampimaje kwa maswali 150 ya nadharia ya kuchagua masaa peke yake masaa 3 ambapo kwa vitendo hujui ataenda kufanya kitu gani?
Mhe Rais, Kazi ya baraza ni kupima ubora wa mwanafunzi kabla ya kuanza mafunzo au mpaka amalize mafunzo ya hospitalini kwanza?
Ni taifa gani wana mfuno huu wa Pre and post Internship ikiwa hata mwongozo wa WHO hausemi hivyo?
Kwanini tusihisi kwamba hii ni janja janja ya kujikusanyia pesa wanazolipa watarajali hawa kabla ya kujisajili kufanya mitihani hiyo bila sababu za msingi?
Kusu hili Mhe Waziri hajui kabisa chochote Mhe Rais.

(ii)Watarajali kupewa mitihani ambayo haikutathminiwa wala kufanyiwa utafiti matokeo yake hali hii ilipelekea zaidi ya nusu kufanya vibaya kwenye mitihani hii.
Kulikua na kigezo cha mtarajali kwenda kufanya mafunzo mpaka afaulu mtihani huo kwanza, lakini mhe Waziri alipoona kuna malalamiko makubwa na hali ni mbaya sana mahospitalini hakuna madaktari wa kutosha ampapo kimsingi hawa watarajali ndio nguvu kazi kubwa kwenye mahospitali yote nchini, akaondoa zuio hilo la kwenda mafunzoni hadi mtarajali afaulu mtihani huo, ikawa sasa wafaulu wasifaulu wataenda mafunzoni tu na mtihani lazima ufanyike. Mtu unajiuliza, ni ipi sababu ya kuwapima kabla ya ilikua ikiwa wote wanaofeli na wanaofaulu wanaenda mafunzoni? Mantiki ya kipimo hapa ni ipi? Kwanini tusichukulie kua mitihani hiyo ninkitega uchumi tu cha baraza?

Kwenye hili Mhe Waziri Ummy alisema aneunda tume ya kuchunguza Malalamiko ya Watarajali hao na kutoa majibu ndani ya muda mfupi, lakini Mhe Rais Mpaka naandika hivi sasa ni zaidi ya Mwezi mmoja tume hiyo haijatoa mrejesho wala taarifa yeyote na Mhe Waziri yupo kimya.
Mhe Rais, Mpaka sasa Baraza hili ambalo linalalamikiwa na limeundiwa tume kuchunguzwa linaandaa mitihani mingine ya Preinternship, Watarajali hawa wanajiuliza, kuna usalama na uhalali kiasi gani kwenye mitihani hiyo?
Ni sahihi Baraza kuendelea na uandaaji wa mitihani wakati wanachunguzwa?

(iii)Kwanini ni taaluma ya Udaktari kuna mitihani miwili ya Pre and Post internships tofauti na taaluma ziingine ambazo watarajali huenda kufanya mafunzo ya vitendo kwanza chini ya Wasimamizi ambao ni wanataaluma waandamizi kisha baadaye mitihani ya kumaliza hufuata na kupatiwa leseni zao?
Kama hoja ilikua ni kutilia shaka uwezo wa vyuo vikuu kuandaa wataalam, kada zingine wamesomea vyuo gani? Kwanini baraza la madaktari Tanganyika wanafanya kitu ambacho yumkini hata wao hawajui maana yake?

(iv)Kuhusu watarataji waliofeli mitihani yao ambao kwa rekodi ya mtihani uliopita nibzaidi ya nusu ya waliofanya watahiniwa, wao kuendelea kukaa mtaani huku hawana leseni hadi mwaka mzima wakisubiri hadi wengine wamalize ndio waje wafanye mitihani pamoja, tunajiuliza huu ni utaratibu wa wapi kwa vijana hawa ambao tayari wana mikopo ya HESLEB ina mkataba baada ya muda flani kutakiwa kurejesha pesa walizokopa? kama wataendele kukaa mtaani maana yake hawana leseni hawawezi kufanya yeyote ile, siyo hasara kwa serikali iliyowakopesha?

USHAURI KWAKO MHE RAIS
Ikiwa vijana hawa waliandika barua ya wazi kwako Mhe Rais, Mhe Waziri akawahadaa kwa nia ya kuwapooza kwa kuunda tume ambayo mpaka sasa haijatoa mrejesho wala ripoti yeyote huku walalamikiwa wakiendelea na yale ambayo yalilalamikiwa.Kabla vijana hawa hawajakuangukia kwa njia ambayo pengine leo watahitaji tena kukutana nawe ana kwa ana, Mhe Rais wangu chukua hatua ya kumbadilisha Mhe Waziri kwenda wizara nyingine au uamuzi wowote utakaoona unafaa kwa mamlaka yako.
Hii inatafsiriwa ya kwamba amepuuza malalamiko ya wataalam hawa ambao taifa hili linawahitaji kwa kiasi kikubwa maana wamesomeshwa kwa gharama kubwa sana.
Mbona Wizara ya katiba na sheria walichukua hatua haraka baada ya Shule ya sheria(School of law) kulalamikiwa kutotenda haki kwa watahiniwa wa kada hiyo? Wizara ya Afya kuna nini?

Yangu ni hayo Mhe Rais.
Kazi endelee kwa jina la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wewe unayalalamika ni mjinga sana. Zamani Medical Drs walisoma kwa mwaka then final exam ya mwaka but baadaye wakasoma kwa semester kitu ambacho kinapelekea kuwa na medical doctors wabovu (baadhi). MCT wapo sahihi na ndiyo maana nchi zilizoendelea kuwa medical doctor siyo suala la kujaribu. Fanyeni hiyo mitihani muache ujinga. Nayajua mengi sana sema sima muda ila MCT wapo sahihi na mitihani lazima mfanye, kutibu siyo kujaribu!
 
Binafsi jana nilileta uzi humu kulisemea hili humu MCT kwa kiburi chao wakaandika taarifa kwa umma wakijua itawasaidia. Hili baraza bure tu lipanguliwe
Wewe ni idiot, MD lazima wapimwe. Eti unakuta doctor ana google ugonjwa kama raia. Nyie MD wa semester mnasumbua ndiyo masna vifo vingi
 
S

Shit, USA wana Pre and post USMLE?
Mantiki ya pre internship ni kupima utayari wako wa kutoa huduma chini ya usimamizi na una pata "provisional licence" na mantiki ya post intern ni kupima utayari wako kwenda kuachiwa mgonjwa mwenyewe bila usimamizi na unakuwa registered rasmi you are on your own ... Ukifeli hapo maana yake wewe bado ...
 
Rais kwanza nikupe pole na heshima yako na nikupongeze sana Mama kwa uwajibikaji wako katika kulisaidia Taifa hili kwa kuliponya kutoka katika mazingira magumu miaka 8 iliyopita. Hakika tunaweza kusema ya kwamba mabadiliko ni makubwa sana katika sekta zote ispokua baadhi ya Watendaji wako ndio wanaokuharibia na kuendelea kukuchelewesha kufika kule mbali unakotazama.
Bila hiyana wala unafki kwakweli kongole Mama!👏👏

Rais tunafahamu kwamba falsafa yako kubwa katika utendaji ni kuwaacha watendaji wako wafanye kazi wenyewe kwa kujisimamia bila pressure yeyote ya mamlaka tena kwa ubinifu mkubwa. Hii ndio misingi ya kweli ya kiutawala.

KWANINI WAZIRI UMMY ABADILISHWE?

Rais, nikiwa kama Mtanzania Mzalendo,Mdau katika masuala ya Afya na kada/kiongozi mtiifu katika chama cha Mapinduzi, sipendi tuharibikiwe nitaelezea mambo kadhaa muhimu ambayo pengine Mhe Waziri hakuambii ukweli au watendaji walio chini yake hawamwambii ukweli kwa vile yeye siyo mwanataaluma katika sekta ya Afya.

KUSHINDWA KUSIMAMIA NA KUTATUA KERO NA MALALAMIKO YA MADAKTARI TARAJALI(INTERNS) KUTOTENDEWA HAKI NA BARAZA LA MADAKTARI TANGANYIKA(MCT).

Rais wangu, ikumbukwe kua Madaktari tarajali waliwahi kukuandikia Barua ya wazi kwamba hawatendewi haki na Baraza la Madaktari Tanganyika(MCT) wakilalamikia mambo kadha wakadha ambayo nitayabainisha hapa.Lakini baada ya Barua hiyo Mhe Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alimtuma Naibu waziri wake Dr Godwin Moleli ambaye alikutana na Watarajali hao na kisha kueleza kero na changamoto zao. Baadaye Mhe Waziri Ummy Mwalimu alitoa taarifa kuunda tume ya kiuchunguzi kushughulikia changamoto hizo, lakini cha ajabu mpaka sasa hakuna mrejesho na walalamikiwa wanaendelea na kile kile kinacholalamikiwa.

Rais, katika mambo yanayolalamikiwa na watarajali hawa ni kama ifuatavyo;

(i)Kunzishwa kwa mitihani ya Pre-intetnships ambayo haieleweki msingi wake ingawa baraza lilidai kuwapima watarajali hao kutokana na kutilia shaka vyuo vikuu waliotoka. Lakini swali la kujiuliza ni kwamba, TCU kikiwa kama chombo cha kupima ubora wa vyuo vikuu kina kazi gani? Huyu Mwanafunzi aliyesoma miaka yote 5 chuoni kisha akafuzu mafunzo yote ya nadharia na vitendo hospitalini miaka yote anapimwa kitu gani hasa? Unampimaje kwa maswali 150 ya nadharia ya kuchagua masaa peke yake masaa 3 ambapo kwa vitendo hujui ataenda kufanya kitu gani?
Mhe Rais, Kazi ya baraza ni kupima ubora wa mwanafunzi kabla ya kuanza mafunzo au mpaka amalize mafunzo ya hospitalini kwanza?
Ni taifa gani wana mfuno huu wa Pre and post Internship ikiwa hata mwongozo wa WHO hausemi hivyo?
Kwanini tusihisi kwamba hii ni janja janja ya kujikusanyia pesa wanazolipa watarajali hawa kabla ya kujisajili kufanya mitihani hiyo bila sababu za msingi?
Kusu hili Mhe Waziri hajui kabisa chochote Mhe Rais.

(ii)Watarajali kupewa mitihani ambayo haikutathminiwa wala kufanyiwa utafiti matokeo yake hali hii ilipelekea zaidi ya nusu kufanya vibaya kwenye mitihani hii.
Kulikua na kigezo cha mtarajali kwenda kufanya mafunzo mpaka afaulu mtihani huo kwanza, lakini mhe Waziri alipoona kuna malalamiko makubwa na hali ni mbaya sana mahospitalini hakuna madaktari wa kutosha ampapo kimsingi hawa watarajali ndio nguvu kazi kubwa kwenye mahospitali yote nchini, akaondoa zuio hilo la kwenda mafunzoni hadi mtarajali afaulu mtihani huo, ikawa sasa wafaulu wasifaulu wataenda mafunzoni tu na mtihani lazima ufanyike. Mtu unajiuliza, ni ipi sababu ya kuwapima kabla ya ilikua ikiwa wote wanaofeli na wanaofaulu wanaenda mafunzoni? Mantiki ya kipimo hapa ni ipi? Kwanini tusichukulie kua mitihani hiyo ninkitega uchumi tu cha baraza?

Kwenye hili Mhe Waziri Ummy alisema aneunda tume ya kuchunguza Malalamiko ya Watarajali hao na kutoa majibu ndani ya muda mfupi, lakini Mhe Rais Mpaka naandika hivi sasa ni zaidi ya Mwezi mmoja tume hiyo haijatoa mrejesho wala taarifa yeyote na Mhe Waziri yupo kimya.
Mhe Rais, Mpaka sasa Baraza hili ambalo linalalamikiwa na limeundiwa tume kuchunguzwa linaandaa mitihani mingine ya Preinternship, Watarajali hawa wanajiuliza, kuna usalama na uhalali kiasi gani kwenye mitihani hiyo?
Ni sahihi Baraza kuendelea na uandaaji wa mitihani wakati wanachunguzwa?

(iii)Kwanini ni taaluma ya Udaktari kuna mitihani miwili ya Pre and Post internships tofauti na taaluma ziingine ambazo watarajali huenda kufanya mafunzo ya vitendo kwanza chini ya Wasimamizi ambao ni wanataaluma waandamizi kisha baadaye mitihani ya kumaliza hufuata na kupatiwa leseni zao?
Kama hoja ilikua ni kutilia shaka uwezo wa vyuo vikuu kuandaa wataalam, kada zingine wamesomea vyuo gani? Kwanini baraza la madaktari Tanganyika wanafanya kitu ambacho yumkini hata wao hawajui maana yake?

(iv)Kuhusu watarataji waliofeli mitihani yao ambao kwa rekodi ya mtihani uliopita nibzaidi ya nusu ya waliofanya watahiniwa, wao kuendelea kukaa mtaani huku hawana leseni hadi mwaka mzima wakisubiri hadi wengine wamalize ndio waje wafanye mitihani pamoja, tunajiuliza huu ni utaratibu wa wapi kwa vijana hawa ambao tayari wana mikopo ya HESLEB ina mkataba baada ya muda flani kutakiwa kurejesha pesa walizokopa? kama wataendele kukaa mtaani maana yake hawana leseni hawawezi kufanya yeyote ile, siyo hasara kwa serikali iliyowakopesha?

USHAURI KWAKO MHE RAIS
Ikiwa vijana hawa waliandika barua ya wazi kwako Mhe Rais, Mhe Waziri akawahadaa kwa nia ya kuwapooza kwa kuunda tume ambayo mpaka sasa haijatoa mrejesho wala ripoti yeyote huku walalamikiwa wakiendelea na yale ambayo yalilalamikiwa.Kabla vijana hawa hawajakuangukia kwa njia ambayo pengine leo watahitaji tena kukutana nawe ana kwa ana, Mhe Rais wangu chukua hatua ya kumbadilisha Mhe Waziri kwenda wizara nyingine au uamuzi wowote utakaoona unafaa kwa mamlaka yako.
Hii inatafsiriwa ya kwamba amepuuza malalamiko ya wataalam hawa ambao taifa hili linawahitaji kwa kiasi kikubwa maana wamesomeshwa kwa gharama kubwa sana.
Mbona Wizara ya katiba na sheria walichukua hatua haraka baada ya Shule ya sheria(School of law) kulalamikiwa kutotenda haki kwa watahiniwa wa kada hiyo? Wizara ya Afya kuna nini?

Yangu ni hayo Mhe Rais.
Kazi endelee kwa jina la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Yaani Issue ya interns ndio iondoe mtu

Naona mmevimba vichwa hata kabla hamjapewa vibali
 
Atoke
Cupace20230923075117117.jpg
 
Back
Top Bottom