Rais gani atakuja kumaliza tatizo sugu la mgao wa Umeme?

Rais gani atakuja kumaliza tatizo sugu la mgao wa Umeme?

ubarinolutu

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2012
Posts
2,424
Reaction score
4,954
Tatizo la Mgao wa Umeme limekuwepo kwa muda mrefu sana, Toka enzi za Nyerere, na Sasa tatizo hilo linaendelea kuwepo , sisi watu wazima tumeona mgao Kwa Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na sasa mgao upo kwa Samia.

Hili ni Tatizo kubwa sana, japokuwa Wamebadilishwa mawaziri na watendaji wakuu wa TANESCO Mara kwa mara bado tatizo limeendelea kuwepo na wananchi wanazidi kulalamika.

Kipindi cha Magufuli ulitumika ujanja ujanja Ili kupunguza Makali ya mgao , japo mabwawa yalikauka na mgao ulikuwepo, kwa maana kilichofanyika Serikali ilitoa maelekezo kwa watumiaji wachache ambao wana matumizi wakubwa ya umeme kuzima mitambo hali iliyopelekea watumiaji wengi/wapiga kura kuonja kidogo makali ya mgao, ila athari zilikuwapo sana kiuchumi mana uzalishaji ulipungua.

Kwa mwaka huu tumekuwa na mgao wa umeme Toka January kwasababu mbalimbali hasa hitilafu za mitambo na mabwawa kukauka maji.

Sasa Swali langu he ni nani atakuja kutumalizia tatizo hili Sugu/Cronic la mgao wa Umeme, huku ndani ya tatizo Hilo tukiwa na tatizo jingine la kukatika katika kwa umeme ambalo halisababishwi na mabwawa kupungua maji.
 
Tuliambiwa bwawa la Nyerere likikamilika mgao utakuwa historia
Wajuvi mtuambie
 
Tatizo la Mgao wa Umeme limekuwepo Kwa muda mrefu sana, Toka enzi za Nyerere, na Sasa tatizo Hilo linaendelea kuwepo
Tatizo la watanzania ni wajinga wewe ,Magu alionyesha nia na njia ya kutatua hilo suala na umeme ulikuwa haukatiki sana kaondoka watu wamelishwa vitu kwama alikuwa anafanya non sense na wameamini na kumuona alikuwa si kitu .Watanzania tunatawalika kijinga sana
 
Hili ni Tatizo kubwa sana, japokuwa Wamebadilishwa mawaziri na watendaji wakuu wa TANESCO Mara Kwa mara Bado tatizo limeendelea kuwepo na wananchi wanazidi kulalamika...
Bila kuwa na long term plan ya kuhifadhi mazingira Nyanda za juu Kusini na Kaskazini tutabaki kuimarisha uchumi wa wahuni wachache wanaouza majenereta
 
Jiwe ndo alikua anataka haya mambo yaishe ila ndo basi tena Mungu akampenda zaidi ...ila jamaa alikua na nia nzuri sana na taifa hili.

Alitaka hilo tatizo lipungue kwa kujenga bwawa la maji ambapo unaambiwa tatizo ni mabadiliko ya tabia nchi?! Au angeleta mvua zake?
 
Usimamizi mbovu na ufinyu wa kutumia taaluma ya namna ya kuzuia umeme usikatike.

Serikali haina usimamizi mzuri wa kuhakikisha umeme unakuwa imara na upo kwa wakati wote, miundombinu ya umeme mdogo(MV) ni chakavu pia vituo vya kupozea umeme ni vichache tena vya zamani vingi vyake haviendani na ukuaji wa nchi(wateja).

.Mifumo ya utendaji kazi ipo kisiasa Tu yaani wataalum wa Tanesco wameelemea kwenye paper works zaidi tena kwa kutumia watu wa Chini kiujuzi(Foremen's, Technicians) wakati kazi wanafanya kwa mazoea kwakuwa ufahamu wao upo kwa kikomo fulani kwa masuala ya technical( wanapaswa kutumia Engineers).

.Serikali inapaswa kuisimamia Tanesco kwa vitendo namna ya kuhakikisha mifumo ya usambazaji umeme inakuwa imara na wateja wanapata huduma iliyo nzuri (no power outages) tofauti na hapo umeme utakuwa kikwazo cha maendeleo ya Taifa na Kero kwa wananchi.
 
Tatizo la watanzania ni wajinga wewe ,Magu alionyesha nia na njia ya kutatua hilo suala na umeme ulikuwa haukatiki sana kaondoka watu wamelishwa vitu kwama alikuwa anafanya non sense na wameamini na kumuona alikuwa si kitu .Watanzania tunatawalika kijinga sana

Lile dubwasha lilikuwa ni takataka.
 
Tatizo ni sheria zilizopo zinazoipa serikali monopoly kwenye hii biashara ya umeme, waruhusu sekta binafsi kufanya hii biashara in full, kwa wasiolewa Tanzania sekta binafsi hairuhusiwi kuuza na kusambaza umeme moja kwa moja kwa wateja, unaweza kuzalisha na kuiuzia TANESCO na wanakupangia bei ila huwezi kuuza kwa wananchi au wazalishaji, hakuna mtu mwenye pesa anaweza kufanya biashara kichaa kama hiyo, ni sheria na sera zetu ndio zinaleta matatizo yote haya, imagine biashara ya simu ingekuwa TTCL peke yake ndio anaruhusiwa kuuza huduma za simu
 
Back
Top Bottom