Rais Kagame amejenga nyumba kwa wasio na uwezo wa kujenga makazi bora, wengi wao ni wazee.

Rais Kagame amejenga nyumba kwa wasio na uwezo wa kujenga makazi bora, wengi wao ni wazee.

Binafsi sipendelei serikali kuwajengea watu nyumba. Serikali haina uwezo wa kujengea watu wote nyumba na suala zima haliko sustainable.

Napendelea serikali kuwa na sera za kuwawezesha watu kujijengea/ kununua nyumba.

Kwa mfano, hakuna sababu yoyote ya muhimu ninayoielewa ya kuzuia mfumo wa mortgage, watu wakauziwa nyumba kwa mfumo wa kulipia kidogo kidogo katika miaka kadhaa. Na wakishindwa kulipia kwa mwaka nyumba inapigwa mnada.

Shirika la Nyumba lingefanya utafiti kwa ushirikiano na benki zetu kuhusu mfumo huu, watu wengi sana wangeweza kumiliki nyumba.

Unakopa benki kununua nyumba, unalipa kidogo kidogo, with interest. Collateral ni nyumba.

Wewe unapata nyumba bila kulipa hela nyingi kwa pamoja. Benki inapata interest, shirika la nyumba linapata faida kwa kuuza nyumba. Nchi inaondokana na watu kukaa kwenye makazi hafifu.

Mtu anafanya kazi ya kawaida miaka 30, anachukua mkopo mwanzo wa kufanya kazi, akistaafu amemaliza kulipia nyumba, anarithisha familia nyumba. Huyo mfanyakazi wa kawaida tu. Hahitaji kuchukua rushwa wala dili kujenga nyumba.

Kwa kiasi kikubwa, serikali ya Tanzania imeshindwa katika yote hayo mawili. Imeshindwa kuwajengea watu nyumba, na imeshindwa kuweka sera za kuwawezesha watu kujenga au kununua nyumba. Mpakq mtu kuwa na nyumba inaonekana ni tajiri. Wakati nyumba bora ni hakinl ya kila mtu.

Mfano mzuri wa karibuni kuhusu kushindwa kwa serikali kuwa na.sera nzuri kwenye ujenzi wa nyumba ni kupanda kwa bei ya sementi.
Kuna hali za maisha hutokea mtu akashindwa kulipa mortgage, mfano kufiwa na mwenza ambae ndiye mwenye kipato kikubwa, kupata redundancy kazini, kuugua ugonjwa wa muda mrefu.

Kwa hali kama hizi social housing zinasaidia jamii. Nyumba zinazopangishwa chini ya gharama za soko la nyumba mtaani. Mradi raia akidhi vigezo vya kupata nyumba hizo.

Nyumba bora husaidia kuimarisha afya ya jamii na afya njema hukuza uchumi.
 
Hivi Rwanda ina wazee na wasiojiweza wangapi? Na Tanzania tunao wangapi na wako wapi? Tunaweza kusema Kagame amefanya jambo kubwa sana kuliko yanayofanyika hapa TZ na tumuige? Kagame si ndio alibadili katiba aendelee kutawala? Tumuige?
 
Hivi Rwanda ina wazee na wasiojiweza wangapi? Na Tanzania tunao wangapi na wako wapi? Tunaweza kusema Kagame amefanya jambo kubwa sana kuliko yanayofanyika hapa TZ na tumuige? Kagame si ndio alibadili katiba aendelee kutawala? Tumuige?
Wale jamaa unaowaambia, bahati mbaya sana, kwa masikitiko makubwa, hawana full view ya matukio wala hawafikiri katika dimensions zote 16, na mduara wa nyuzi 360. Mtazamo wao ni wa ^kisaidi mira^ ya motokaa, na lazima kuna blind spots zinawakosesha kufanya tathmini na mrejesho uliokamilika. Wanastahili, siyo kubezwa na kukosolewa na kupuuzwa, bali kuonewa huruma, kusikitikiwa na kufundishwa kama tutoto tudogo labda huenda pengine possibly kuna some hopefulness kwao huko mbeleni sana; vinginevyo, ^adios!^
 
Kuna hali za maisha hutokea mtu akashindwa kulipa mortgage, mfano kufiwa na mwenza ambae ndiye mwenye kipato kikubwa, kupata redundancy kazini, kuugua ugonjwa wa muda mrefu.

Kwa hali kama hizi social housing zinasaidia jamii. Nyumba zinazopangishwa chini ya gharama za soko la nyumba mtaani. Mradi raia akidhi vigezo vya kupata nyumba hizo.

Nyumba bora husaidia kuimarisha afya ya jamii na afya njema hukuza uchumi.
Huko umeenda mbali, basic mortgage tu sijaona ikitumiwa kwa kiasi kikubwa Tanzania.

Kitu kimoja naona hatuna credit bureaus/ history kuangalia creditworthiness in a systemic way.

Lakini, mtu akishindwa kulipa mortgage ya nyumba si collateral ipo nyumba yenyewe, hapo kuna tatizo gani?
 
Huko umeenda mbali, basic mortgage tu sijaona ikitumiwa kwa kiasi kikubwa Tanzania.

Kitu kimoja naona hatuna credit bureaus/ history kuangalia creditworthiness in a systemic way.

Lakini, mtu akishindwa kulipa mortgage ya nyumba si collateral ipo nyumba yenyewe, hapo kuna tatizo gani?
Katika miji mingi mikubwa duniani ndiko kuna familia zinazoishi katika umasikini uliokithiri. Tabaka la watu hawa ndiyo linalotumiwa na wafanya biashara na wawekezaji wakubwa kupata faida katika uwekezaji wao. Jamii hii hulipwa ujira mdogo kwa ajira ya masaa mengi.

Wazazi hulazikimia kutokuwepo nyumbani muda mrefu wakisaka hela za kodi ya nyumba, chakula na mavazi. Hata katika nchi zilizoendelea ambako kuna socia housing, jamii hii inahitaji jicho la karibu kwani kuna uwezekano mkubwa ya vizazi vyao kuishi maisha haya haya. Watoto wanatumiwa na wafanya biashara haramu kufanya biashara zao kwasababu wazazi wao hawawezi kuwapa malezi, muda mwingi wako makazini.

Kwa nchi kama zetu jamii hii, baba unamkuta ameajiriwa anauza duka mjini, mshahara kwa mwezi ni laki mbili. Mke wake anaamuma kuuza mboga mboga mtaani siku nzima. Wamepangisha chumba kimoja na wana watoto. Watoto usiku wanaombewa kulala kwa jirani. Kumbe jirani anawatumia vibaya watoto usiku, wakiume wana lawitiwa na wakike kupata uja uzito.

Mtu anaepata mshahara laki mbili kwa mwezi atapa mortgage gani au anaweza vipi kupata hela ya deposit?
 
Katika miji mingi mikubwa duniani ndiko kuna familia zinazoishi katika umasikini uliokithiri. Tabaka la watu hawa ndiyo linalotumiwa na wafanya biashara na wawekezaji wakubwa kupata faida katika uwekezaji wao. Jamii hii hulipwa ujira mdogo kwa ajira ya masaa mengi.

Wazazi hulazikimia kutokuwepo nyumbani muda mrefu wakisaka hela za kodi ya nyumba, chakula na mavazi. Hata katika nchi zilizoendelea ambako kuna socia housing, jamii hii inahitaji jicho la karibu kwani kuna uwezekano mkubwa ya vizazi vyao kuishi maisha haya haya. Watoto wanatumiwa na wafanya biashara haramu kufanya biashara zao kwasababu wazazi wao hawawezi kuwapa malezi, muda mwingi wako makazini.

Kwa nchi kama zetu jamii hii, baba unamkuta ameajiriwa anauza duka mjini, mshahara kwa mwezi ni laki mbili. Mke wake anaamuma kuuza mboga mboga mtaani siku nzima. Wamepangisha chumba kimoja na wana watoto. Watoto usiku wanaombewa kulala kwa jirani. Kumbe jirani anawatumia vibaya watoto usiku, wakiume wana lawitiwa na wakike kupata uja uzito.

Mtu anaepata mshahara laki mbili kwa mwezi atapa mortgage gani au anaweza vipi kupata hela ya deposit?
Zi lazima kuwapa mortgage watu wote, kutaka kila mtu awe na nyumba ni moja ya sanmbabu iliyopelekeq kutokeq kwa mortgqge crisis late 2000s.

Serikali haiwezi kumsaidia kika mtu, inatakiwa na mtu naye aweke effort kuj8kwamua, kusoma na kupata career, kupata mtaji wa biashara etc.

Hivyo, hakuna sababu watu wenye formal employment na careers kupata shida sana kujenga nyumba, au kujenga nyumbabsehemu mbali sana na mjininwakati kazi zao ziko mjini.

Kwa sasa hivi kujenga nyumba ama kutamchukua mfanyakazi wa kawaida muda mrefu sana ama kuko nje ya uwezo wake kabisa. Kuna watu wengi tu wanalipwa kati ya 500,000 mpaka 1,000,000 na zaidi, wana skills, training na careers, wangewezwa kuingizwa kwenye some sort of a mortgage. Mtu anayelipwa sh 1,000,000 kwa mwezi, ukimpa mkopo wa 100,000,000 aulipe kwa miaka 30 kwa ajili ya nyumba ambayo kasha close, na collateral ni nyumba, atashindwa kulipa? Huo ni kama mshahara wake wa miaka minne tu discounting all else.

Sasa hawa watu wanaolipwa 500,000 mpaka 1,000,000 kwa mwezi wapo wengi hawana nyumba na hawawezi ku afford kulipa 100,000,000 kwa mpigo. Matokeo yake, ili kujenga, wanajiingiza katika mambo ya rushwa na njia za panya makazini.

Hao ndio wangekuwa target market. Ukimsaidia huyo mmoja umesaidia wengi, Kiafrika hiyo nyumba ninnadra yeye kukaa peke yake.
 
Zi lazima kuwapa mortgage watu wote, kutaka kila mtu awe na nyumba ni moja ya sanmbabu iliyopelekeq kutokeq kwa mortgqge crisis late 2000s.

Serikali haiwezi kumsaidia kika mtu, inatakiwa na mtu naye aweke effort kuj8kwamua, kusoma na kupata career, kupata mtaji wa biashara etc.

Hivyo, hakuna sababu watu wenye formal employment na careers kupata shida sana kujenga nyumba, au kujenga nyumbabsehemu mbali sana na mjininwakati kazi zao ziko mjini.

Kwa sasa hivi kujenga nyumba ama kutamchukua mfanyakazi wa kawaida muda mrefu sana ama kuko nje ya uwezo wake kabisa. Kuna watu wengi tu wanalipwa kati ya 500,000 mpaka 1,000,000 na zaidi, wana skills na careers, wangewezwa kuingizwa kwenye some sort of a mortgage. Mtu anayelipwa sh 1,000,000 kwa mwezi, ukimpa mkopo wa 100,000,000 aulipe kwa miaka 30 kwa ajili ya nyumba ambayo kasha close, na colletqral ni nyumba, atashindwa kulipa? Huo ninkama mshahara wake wa miaka minne tu discounting all else.

Sasa hawa watu wanaolipwa 500,000 mpaka 1,000,000 kwa mwezi wapo wengi hawana nyumba na hawawezi ku afford kulipa 100,000,000 kwa mpigo.

Hao ndio wangekuwa target market. Ukimsaidia huyo mmoja umesaidia wengi, Kiafrika hiyo nyumba ninnadra yeye kukaa peke yake.
Ninaona umeangalia uchumi wa watu wenye kipato cha kati, lakini watu wenye kipato cha chini ni wengi sana na hawa ndiyo wanasaidia uwepo wa watu wenye kipato cha kati.

Kuna dereva aliyajiriwa kupeleka watoto wa boss shuleni,
Mkata majani, housekeeper, house girl. Hawa mishahara yao haizidi laki tatu.

Socialisation pia, kama kukiwa na nyumba za Wilaya, self contained ya vyumba viwili unaipata kwa laki moja na nusu. Itasaidia kuondoa ushamba. Mimi nanaeishi Buza Kwa Mpagale nimezoea choo cha shimo. Leo ninalazwa Mloganzila si ndiyo nitatumia karatasi ya fullscape kujisafishia kumbe inaziba choo.
 
Akili kubwa ni Prezidenti Bulldozer anayewaandaa vijana mapema ili hatimaye waweze kununua viwanja vyao wenyewe

Anawaandaa vijana kwa kuwasomesha chini ya miti na shule zisizokuwa na vyoo? Unawaandaa vijana kwa kuwaminyia uhuru wa kujieleza na kuwa waoga wa kukosoa? Taifa linaloloendelea huletwa na umoja na sio mgawanyiko wa wananchi wake!! Jiwe apende asipende nchi imeganyika kati ya watu wa Chato na wasio wa Chato!!! Wale wa Chato ndio wanaofaidika na utawala wake wakati hao wengine ni watazamaji tu!!!
 
Ninaona umeangalia uchumi wa watu wenye kipato cha kati, lakini watu wenye kipato cha chini ni wengi sana na hawa ndiyo wanasaidia uwepo wa watu wenye kipato cha kati.

Kuna dereva aliyajiriwa kupeleka watoto wa boss shuleni,
Mkata majani, housekeeper, house girl. Hawa mishahara yao haizidi laki tatu.

Socialisation pia, kama kukiwa na nyumba za Wilaya, self contained ya vyumba viwili unaipata kwa laki moja na nusu. Itasaidia kuondoa ushamba. Mimi nanaeishi Buza Kwa Mpagale nimezoea choo cha shimo. Leo ninalazwa Mloganzila si ndiyo nitatumia karatasi ya fullscape kujisafishia kumbe inaziba choo.
Ukianza kusaidia watu wenye uchumi wa kati, eventually utaongeza watu wenye uwezo wa kusaidia wengine na methodically utanyanyua hata wa uchumi wa chini.

Ukitaka kuanza kwa kusaidia watu wote kwa mpigo, hutapata hata nafasi ya kuanza. Watu hao ni wengi sana.
 
View attachment 1684151
View attachment 1684152
View attachment 1684153
Kila aliyekabidhiwa funguo za nyumba alipewa na chakula cha kuanzia maisha. Kijiji kina huduma zote za jamii, kuanzia shule, hospitali, kituo cha Polisi, soko, umeme, maji na barabara.
Hata akijenga hakuna jipya. Asipo weza kuachia ngazi nakufanya nchi iwe na utaratibu wakubadilisha madaraka Rwanda haitopona. Rwanda ina hitaji kiongozi atawaponya vidonda vya madhila ya ukabila na kuwaunganisha kuwa wamoja hayo majengo na maendeleo hayatoweza kuwaponya changanya serikali hutus and tutis. Tungeni katiba itaruhusu makabila yote kukaa kwenye kiti.
 
Back
Top Bottom