Rais Magufuli aagiza Madaktari waliohama Hospitali ya Rufaa mkoani Tabora kwenda Hospitali binafsi kwa kisingizio cha maslahi wafuatiliwe

Rais Magufuli aagiza Madaktari waliohama Hospitali ya Rufaa mkoani Tabora kwenda Hospitali binafsi kwa kisingizio cha maslahi wafuatiliwe

Kwahiyo ukikosea ww kama serikali nisikwambie, na hili ndilo linalofanywa na viongoz ngazi ya juu, wanaona mtu anakoenda si salama wanakausha? Hii nchi yetu sote kila mmoja anatakiwa kujivunia nchi yetu, ukiiharibu nam naona ntakuwa mjinga sana lazima nikukemeee
Serikali. Kwanini serikali.
Badala ya kujiulizia wapi tunakwama mnataka ndo mharibu kabisaaaa, haya umefungia hiyo hospital kwahiyo wale waliokuwa wameajiriwa kufanya kaz kwenye hiyo hospital utawaajiri ww? Mambo mengine yakukurupuka sanaaaaa
Tatizo lako wewe uelewi hata kwanini serikali inafanya aina fulani za investment.

Serikali inajukumu la kugharamia ‘merit goods’ maana yake nini serikali isiposomesha, kujenga shule, kutoa huduma za afya na uwekezaji mwingine wenye faida za jamii watakaofaidika ni wachache wenye hela.

Sasa serikali imekusomesha kwa faida ya jamii maana yeye ndio mtoaji huduma pia kwa watanzania maskini tulio wengi.

Mtu anatakiwa akaitumikie jamii ambayo inamuhitaji kama sababu za kusomeshwa kwake na kupewa experience. Anafika huko anaona hakufai sijui amepewa offer yenye maslahi mapana zaidi yule aliyekutengeneza unamuona fala.

Na unadhani Drs are entitled to that wakati kupata replacement yake ni shida.

Magufuli yupo right hapa huyo daktari ateme hela ya serikali tena anaondoka bila ya kujali kama kuna mtu wa-ku replace nafasi; halafu mnataka achekewe.
 
This man is mad
Amekuwa mwenda wazimu kwa kutaka tu kanuni zifuatwe? Nimeeleza kanuni husika katika Uzi Na. 25. Mimi mwenyewe nilisomeshwa na serikali mpaka shahada ya kwanza na kwa masomo ya juu zaidi nilisomeshwa na Umoja wa Mataifa. Mfadhiri wangu huyo alisisitiza nitie sahihi mkataba kwamba baada ya kuhitimu nirudi nchini kwangu na kufanya kazi nitakapopangiwa na serikali kwa kipindi kisichopungua miaka mitano. Vivyo hivyo na wenzangu waliofadhiriwa na mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali. Sasa yote hayo tuyaseme kuwa ni wenda wazimu?
 
Anatafuta Dr. aliyekimbia hospital kufuata masilah na mazingira bora ya kazi,anayetoa maagizo yeye pia alikimbia ualimu na kwenda kuwa mkemia kwa kufuata masilah Mazur, licha ya kusomeshwa na serikali buree bila hata kurejesha sh. huku hata nauli na MIKATE wakipewa buree.Mtoa maagizo hajaridhika hapo akaacha ukemia akaingia kwenye siasa kula kwa mrija Sasa, amesahau alipotoka. HAPO NANI NI MZALENDO?
Ukitenda dhambi kabla hujawa mchungaji, ukiwa mchungaji hutaacha kuikemea hiyo dhambi eti kwa kuwa na wewe uliwahi kuitenda???

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
View attachment 1689777
Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la magonjwa ya dharura Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, akiwa katika eneo hilo ameagiza Madaktari waliohama Hospitali hiyo ya Serikali na kuhamia Hospitali binafsi kwa kigezo cha maslahi wafuatiliwe.

Rais Magufuli amenukuliwa akisema
“Madaktari wanapata mkopo 100% wakiwa Chuoni, halafu tunawapa ajira Serikalini wanakimbia kisa maslahi, si ungekimbia wakati unasoma? Hela yetu umekula halafu unakimbia kwenda Hospitali binafsi kwa kisingizio cha maslahi, ni kukosa uzalendo”

“Mtafuteni huyo Daktari aliyekimbia Hospitali ya Serikali na hiyo Hospitali binafsi aliyokimbilia, ikiwezekana tunamfungia Daktari, tunaifungia na Hospitali aliyoenda, wakati wa kusomesha hawatuchangii, tukishawasomesha wanakwenda kuwaiba, sio sawa”
Hata hivyo kabakiza miaka minne tu achomoke.
 
Tatizo lako wewe uelewi hata kwanini serikali inafanya aina fulani za investment.

Serikali inajukumu la kugharamia ‘merit goods’ maana yake nini serikali isiposomesha, kujenga shule, kutoa huduma za afya na uwekezaji mwingine wenye faida za jamii watakaofaidika ni wachache wenye hela.

Sasa serikali imekusomesha kwa faida ya jamii maana yeye ndio mtoaji huduma pia kwa watanzania maskini tulio wengi.

Mtu anatakiwa akaitumikie jamii ambayo inamuhitaji kama sababu za kusomeshwa kwake na kupewa experience. Anafika huko anaona hakufai sijui amepewa offer yenye maslahi mapana zaidi yule aliyekutengeneza unamuona fala.

Na unadhani Drs are entitled to that wakati kupata replacement yake ni shida.

Magufuli yupo right hapa huyo daktari ateme hela ya serikali tena anaondoka bila ya kujali kama kuna mtu wa-ku replace nafasi; halafu mnataka achekewe.
Bwan na magufuli wako.
 
Inawezekana alipata Grant sio Mkopo... Grant kuna amsharti yake
Basi angesema kama huyo daktari alipata grant! Asikimbilie kusema tu tumekuwa mkopo 100%. Kwani ukinipa mkopo lazima nifanye kazi serikalini? Huyu mzee aache unyanyasaji wa kijinga wa Kisukuma! Maana unaponipa mkopo ni sawa na nimejisomesha mwenyewe maana hiyo ni pesa nitakayoilipa, ni sawa tu na serikali inapokopa hela Ulaya halafu inatutangazia kwamba tunajenga kwa fedha zetu?
 
Hospital binafsi pia anatibu watanzania wale wale.Kwani hospital binafsi anatibu warundi? Bado anatumika kwa wale wale waliomsomesha.
 
Anatafuta Dr. aliyekimbia hospital kufuata masilah na mazingira bora ya kazi,anayetoa maagizo yeye pia alikimbia ualimu na kwenda kuwa mkemia kwa kufuata masilah Mazur, licha ya kusomeshwa na serikali buree bila hata kurejesha sh. huku hata nauli na MIKATE wakipewa buree.Mtoa maagizo hajaridhika hapo akaacha ukemia akaingia kwenye siasa kula kwa mrija Sasa, amesahau alipotoka. HAPO NANI NI MZALENDO?
Huyu kabakiza miaka minne tu, achomoke tuvute subila tu
 
Siyo tunakoelekea bali tangu awali ndivyo ilivyokuwa. Unasomeshwa na serikali; ukihitimu unafanya kazi serikalini au kwenye shirika la umma kufuatana na utakavyopangiwa, kwa miaka mitano kipindi ambacho kinachukuliwa kinatosha kufidia gharama za kukusomesha. Ukitaka kwenda kwinginepo kabla ya utumishi wa miaka mitano ulikopangiwa, ruksa lakini ulipe gharama za kukusomesha. Mtu 'objective' hawezi kukosoa hilo. Agizo la JPM katika bandiko hili linafuata kanuni hii.
Wewe nawe,, unaweza kutuwekea hiyo kanuni hapa? Kwa nini mnapendaga kutetea ujinga? Hilo la kufanya kazi serikalini au kwenye shirika la umma ilikuwa enzi za zamani wakati wasomi wakiwa wachache! Halafu kumbuka wakati huo watu walikuwa wanasoma bure!
 
Na mm naunga mkono arudi ale vumbi la chaki [emoji1787][emoji1787][emoji1787], sihami Tanzania raha tupu
 
Back
Top Bottom