Uchaguzi 2020 Rais Magufuli aingilia kampeni za Tundu Lissu Kazuramimba Kigoma

Uchaguzi 2020 Rais Magufuli aingilia kampeni za Tundu Lissu Kazuramimba Kigoma

#Lissu ametangazwa shujaa huko mjini Lagos nchini Nigeria magharibi mwa Afrika

Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tundu Lissu, ametangazwa katika kongamano la kimataifa lililofanyika jijini Lagos, nchini Nigeria, kuwa ndiye mwanasiasa kiongozi katika kutetea matumizi mazuri ya raslimali za taifa lake,anaandika Jabir Idrissa.

Wanakongamano waliokusanyika kujadili amani duniani, wamesema: “Lissu ni kielelezo kizuri cha kiongozi mwenye maadili na shujaa wa haki za binadaamu… mpenda haki na mwanasiasa mkweli anayestahiki kuombewa na wapenda amani hata kufikia kuwa rais katika nchi yake.”

Kwa ujasiri wake katika kukataa dhulma na kuitumia vema fani ya sheria katika kusimamia raslimali za taifa lake, wanakongamano wamesema, “mamilioni ya vijana duniani kote wameanza kuomba kusoma fani ya sheria vyuoni baada ya mitandao ya kijamii zaidi ya 11,000 kuripoti habari zake kwa muda wa siku 11 mfululizo kuliko habari za rais yoyote duniani.”

Taarifa zilizofikia Mwanahalisi Online kutoka Nigeria, zimesema hatua hiyo imefikiwa kwenye kongamano lililomalizika jana likishirikisha vijana wasomi wa Kikristo kutoka vyuo vikuu 283 vya Afrika, Marekani, Asia na Ulaya waliokubaliana kuwa Lissu ni kielelezo kizuri cha kiongozi mwenye maadili na shujaa wa haki za binaadamu.

Profesa Bigs Ezziel kutoka Marekani ambaye katika kongamano hilo la siku tano alifundisha mada ya HAKI, ameonya kuwa nchi nyingi za Afrika bado hazijui thamani ya haki ambayo ndiyo tunu nguzo kuu ya amani na demokrasia.

Akimzungumzia Lissu, Prof. Ezziel alisema wamefuatilia kwa karibu habari za mwanasiasa huyo na kuridhika kuwa ni mtu wa pekee kwa kusema ukweli. “Kwenye Balozi zetu wamekuwa wakituletea mambo yote pale Tanzania bila ya shaka anatakiwa apewe tuzo maalum ili kuwachochea vijana wa kizazi hiki kukataa dhulma.”

Prof. Ezziel ameshauri wasomi wa sheria katika nchi za Afrika kumualika Lissu kwenye vyuo vyao ili atoe elimu itakayowezesha wasomi kuielewa fani ya sheria kwa mapana yake kuliko ilivyo sasa kukikosekana tija hasa ya wanasheria katika nchi zao.

“Ni muhimu tutambue kuwa HAKI ni nguzo muhimu kwa amani, upendo na maendeleo. Mwenyezi Mungu anajitambulisha waziwazi kuwa yu Mungu wa haki… inasikitisha wanasiasa wengi barani Afrika wapo kama mafisi kwa kutamani madaraka badala ya kutamani kumtambua Mungu kwa kufanya yale yanayojenga jamii zao.

“Badala yake wanatumia siasa za kugawa wananchi huku wakitumia nguvu za dola kuharibu amani na utulivu katika nchi zao. Tanzania inakwenda vibaya kutokana na wanasiasa kutoenenda katika kuonesha ni kielelezo cha maadili kama alivyokuwa Mwalimu Nyerere ambaye hakutaka kujilimbikizia mali wala kupenda kutumia nguvu za dola kuonea wananchi,” alisema.

Amehimiza viongozi wa kiroho barani Afrika kumuomba Mwenyezi Mungu kulisaidia taifa la Tanzania ili kulinusuru na balaa linaloweza kutokea kutokana na maongozi yanayokiuka haki za binaadamu huku wakimuombea Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baraka ili kutimiza ndoto yake ya kuona maliasili na raslimali za Tanzania zinanufaisha Watanzania.

Amesema Afrika inahitaji mabadiliko makubwa kisiasa, tofauti na siasa zinazoshuhudiwa zama hizi kwa marais kunogewa na madaraka hata kujifanya Miungu watu. Waruhusu mawazo ya wengi kutawala badala ya kauli ya mtu mmoja kuongoza taifa la mamilioni ya watu. Huko ni kumkataa Mwenyezi Mungu ambaye humsikiliza na kumlisha kila mtu na kila ndege wa angani.

Prof. Ezziel, mwanasheria na mshauri wa sheria kwenye vyuo vikuu 17 vya Palestina, Djibouti, Ghana, Marekani na Jerusalem, amepongeza wanasheria wa Tanzania kwa kumchagua Lissu kuwa rais wa jumuiya ya wanasheria ya Tanganyika. Uamuzi wao wakati wa mkutano mkuu wa Tanganyika Law Society (TLS), amesema umewapata kuheshimika duniani.

Kadhalika, Lissu ametajwa na Dk. Marucus Bahod na Dk. Chris Zulu kuwa “mwanasiasa wa mfano katika karne hii” ambaye ameifundisha dunia umuhimu wa kusimamia haki na sheria na kuifanya taaluma ya sheria kung’aa kwa muda mfupi kiasi cha kusababisha macho yote ya wanazuoni duniani kuiangalia Tanzania kwa kumfuatilia Lissu.

“Ni mwanasheria anayejiamini kutetea matumizi mazuri ya raslimali na maliasili za taifa lake bila ya kujali nguvu kubwa inayotumika na serikali kumkatisha tamaa… mwanasiasa anayeweza kuiongoza Tanzania kwa uwezo wake wa kimaadili na kuitafsiri sheria kwa faida ya Watanzania wote.

“Ni mfano mzuri kwa wanasheria wengine Afrika ambao wanakuwa wazito kusimamia matumizi ya manufaa ya maliasili katika nchi zao na hivyo kuzinyima fursa za maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kutokuwa mbele katika kutetea maliasili za mataifa ya Afrika kunachangia kuua demokrasia, utawala wa haki na sheria,” alisema.

Madaktari hao walisema ni vema wanaotafuta uongozi wa kisiasa barani Afrika wawe watu wema na kamwe wasiruhusu watu wenye visasi kupewa dhamana ya uongozi kwani wakishapata madaraka, huzalisha chuki na fitna katika jamii badala ya maendeleo.

Askofu William Muller kutoka Ujerumani, aliongoza dua ya kuiombea Kenya kuendelea na amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi huu. Nazo nchi za DR Congo, Tanzania, Afrika Kusini, Msumbiji, Ghana, Nigeria, Uganda, Burundi na Gabon zimeombewa ili zirudi kwenye maendeleo makubwa ya kiuchumi.

Jabir Idrisa,
Mwanahalisi Online.
 
#Lissu ametangazwa shujaa huko mjini Lagos nchini Nigeria magharibi mwa Afrika

Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tundu Lissu, ametangazwa katika kongamano la kimataifa lililofanyika jijini Lagos, nchini Nigeria, kuwa ndiye mwanasiasa kiongozi katika kutetea matumizi mazuri ya raslimali za taifa lake,anaandika Jabir Idrissa.

Wanakongamano waliokusanyika kujadili amani duniani, wamesema: “Lissu ni kielelezo kizuri cha kiongozi mwenye maadili na shujaa wa haki za binadaamu… mpenda haki na mwanasiasa mkweli anayestahiki kuombewa na wapenda amani hata kufikia kuwa rais katika nchi yake.”

Kwa ujasiri wake katika kukataa dhulma na kuitumia vema fani ya sheria katika kusimamia raslimali za taifa lake, wanakongamano wamesema, “mamilioni ya vijana duniani kote wameanza kuomba kusoma fani ya sheria vyuoni baada ya mitandao ya kijamii zaidi ya 11,000 kuripoti habari zake kwa muda wa siku 11 mfululizo kuliko habari za rais yoyote duniani.”

Taarifa zilizofikia Mwanahalisi Online kutoka Nigeria, zimesema hatua hiyo imefikiwa kwenye kongamano lililomalizika jana likishirikisha vijana wasomi wa Kikristo kutoka vyuo vikuu 283 vya Afrika, Marekani, Asia na Ulaya waliokubaliana kuwa Lissu ni kielelezo kizuri cha kiongozi mwenye maadili na shujaa wa haki za binaadamu.

Profesa Bigs Ezziel kutoka Marekani ambaye katika kongamano hilo la siku tano alifundisha mada ya HAKI, ameonya kuwa nchi nyingi za Afrika bado hazijui thamani ya haki ambayo ndiyo tunu nguzo kuu ya amani na demokrasia.

Akimzungumzia Lissu, Prof. Ezziel alisema wamefuatilia kwa karibu habari za mwanasiasa huyo na kuridhika kuwa ni mtu wa pekee kwa kusema ukweli. “Kwenye Balozi zetu wamekuwa wakituletea mambo yote pale Tanzania bila ya shaka anatakiwa apewe tuzo maalum ili kuwachochea vijana wa kizazi hiki kukataa dhulma.”

Prof. Ezziel ameshauri wasomi wa sheria katika nchi za Afrika kumualika Lissu kwenye vyuo vyao ili atoe elimu itakayowezesha wasomi kuielewa fani ya sheria kwa mapana yake kuliko ilivyo sasa kukikosekana tija hasa ya wanasheria katika nchi zao.

“Ni muhimu tutambue kuwa HAKI ni nguzo muhimu kwa amani, upendo na maendeleo. Mwenyezi Mungu anajitambulisha waziwazi kuwa yu Mungu wa haki… inasikitisha wanasiasa wengi barani Afrika wapo kama mafisi kwa kutamani madaraka badala ya kutamani kumtambua Mungu kwa kufanya yale yanayojenga jamii zao.

“Badala yake wanatumia siasa za kugawa wananchi huku wakitumia nguvu za dola kuharibu amani na utulivu katika nchi zao. Tanzania inakwenda vibaya kutokana na wanasiasa kutoenenda katika kuonesha ni kielelezo cha maadili kama alivyokuwa Mwalimu Nyerere ambaye hakutaka kujilimbikizia mali wala kupenda kutumia nguvu za dola kuonea wananchi,” alisema.

Amehimiza viongozi wa kiroho barani Afrika kumuomba Mwenyezi Mungu kulisaidia taifa la Tanzania ili kulinusuru na balaa linaloweza kutokea kutokana na maongozi yanayokiuka haki za binaadamu huku wakimuombea Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baraka ili kutimiza ndoto yake ya kuona maliasili na raslimali za Tanzania zinanufaisha Watanzania.

Amesema Afrika inahitaji mabadiliko makubwa kisiasa, tofauti na siasa zinazoshuhudiwa zama hizi kwa marais kunogewa na madaraka hata kujifanya Miungu watu. Waruhusu mawazo ya wengi kutawala badala ya kauli ya mtu mmoja kuongoza taifa la mamilioni ya watu. Huko ni kumkataa Mwenyezi Mungu ambaye humsikiliza na kumlisha kila mtu na kila ndege wa angani.

Prof. Ezziel, mwanasheria na mshauri wa sheria kwenye vyuo vikuu 17 vya Palestina, Djibouti, Ghana, Marekani na Jerusalem, amepongeza wanasheria wa Tanzania kwa kumchagua Lissu kuwa rais wa jumuiya ya wanasheria ya Tanganyika. Uamuzi wao wakati wa mkutano mkuu wa Tanganyika Law Society (TLS), amesema umewapata kuheshimika duniani.

Kadhalika, Lissu ametajwa na Dk. Marucus Bahod na Dk. Chris Zulu kuwa “mwanasiasa wa mfano katika karne hii” ambaye ameifundisha dunia umuhimu wa kusimamia haki na sheria na kuifanya taaluma ya sheria kung’aa kwa muda mfupi kiasi cha kusababisha macho yote ya wanazuoni duniani kuiangalia Tanzania kwa kumfuatilia Lissu.

“Ni mwanasheria anayejiamini kutetea matumizi mazuri ya raslimali na maliasili za taifa lake bila ya kujali nguvu kubwa inayotumika na serikali kumkatisha tamaa… mwanasiasa anayeweza kuiongoza Tanzania kwa uwezo wake wa kimaadili na kuitafsiri sheria kwa faida ya Watanzania wote.

“Ni mfano mzuri kwa wanasheria wengine Afrika ambao wanakuwa wazito kusimamia matumizi ya manufaa ya maliasili katika nchi zao na hivyo kuzinyima fursa za maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kutokuwa mbele katika kutetea maliasili za mataifa ya Afrika kunachangia kuua demokrasia, utawala wa haki na sheria,” alisema.

Madaktari hao walisema ni vema wanaotafuta uongozi wa kisiasa barani Afrika wawe watu wema na kamwe wasiruhusu watu wenye visasi kupewa dhamana ya uongozi kwani wakishapata madaraka, huzalisha chuki na fitna katika jamii badala ya maendeleo.

Askofu William Muller kutoka Ujerumani, aliongoza dua ya kuiombea Kenya kuendelea na amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi huu. Nazo nchi za DR Congo, Tanzania, Afrika Kusini, Msumbiji, Ghana, Nigeria, Uganda, Burundi na Gabon zimeombewa ili zirudi kwenye maendeleo makubwa ya kiuchumi.

Jabir Idrisa,
Mwanahalisi Online.
Kama ni kweli basi hilo ni kongamano Uchwara sana. Ukigoogle majina ya wasemaji wake wakuu wote hawajulikani;
1600633822905.png


1600633904609.png


1600633989698.png
 
Chonde, chonde Mh. Tundu Lisu usije ukaingia kwenye MTEGO ukafanya mkutano kwenye eneo ambako Mgombea wa URAIS yuko kwa MUJIBU WA RATIBA YA NEC.

WANATAFUTA SABABU.
 
wewe wakati mwengine muwe mnatumia ubongo kufikiri badala ya makalio. CCM ni chama tawala kinamiliki vyombo vyote vya ulinzi. Jeshi letu lina wajuzi waliobobea katika fani mbali mbali za mapigano tuna snipers wakutosha ambao wanahitaji risasi moja tu kumdondosha panya yeyote alie umbali wa zaidi ya mita 1000. Huyo uliemtaja anasema kapigwa wapo waliompiga bt kusema CCM ndio waliompiga ni kulivunjia heshima jeshi letu.
CCM kinamiliki vyombo vyote vya ulinzi!?
Hivyo, aliyempiga risasi Mh. Lissu yuko vizuri kuliko vyombo vya ulinzi vya ccm kwa kutopatikana!?
Hivyo,ccm imeshindwa kuwalinda raia wa Tanzania!?
 
Kumbuka Magufuli bado ndio rais wa nchi hii, yaani aache kutekeleza mipango ya maendeleo kwa sababu kuna mmoja anayedhani anaweza kuwa rais wa nchi anaongea matusi yake! Hell no!! lazima maisha yaendelee.
Ni aibu kwa JF kuwa na watu wenye kufikiri Kama hivi.Hata mtoto wa form 2 aliyefaulu Civics anakuzidi ufahamu!
 
Katika uchaguzi huu kuna kanuni zilizokubaliwa na vyama vyote. Msimamizi wake ni Tume ya uchaguzi. Moja ya Kanuni hizi ni ile inayomkataza kutoa ahadi yoyote ya kutoa msaada wa kimaendeleo, ajira, fedha n.k. katika kipindi hiki. Amevunja kanuni na angeadhibiwa ila bahati yake tume ni yake, kaiteua yeye na inamsikiliza yeye.
CCM zamani kabla ya upinzani kuimarika ilikuwa ikijificha kwenye kivuli Cha demokrasia.Sasa hivi imeshajulikana kwamba ni dubwana la aina gani.Haiwezi ondoka madarakani kupitia sanduku la kura!
 
Ukiitwa kutoa ushahidi utathibitisha ?
Ni hatari Mimi sipend CCM kwa kigezo kimoja tu kwa Nini wampige Lissu risasi kwa Nini walitaka kumpoteza mwenzao ili Hali mungu akatuleta wote dunian?
 
Wakati Tundu Lissu akiwa uwanjani huko Kazuramimba Kigoma amepita Rais Magufuli akasimama barabarani na kufanya mkutano karibu kabisa na alipo Tundu Lissu ambapo ameahidi kutoa milioni 10 siku chache zijazo.

Kwa mujibu wa ratiba ya tume, Magufuli leo hapaswi kuwepo Kigoma kwa ajili ya kampeni.

Maswali yangu:
Rais Magufuli alidhamiria kubaki Kigoma ili kufanya haya?

Kwanini anashindwa kuheshimu demokrasia?

Je, ingekuwa ni Tundu Lissu kamfanyia hivyo nini kingetokea?

Nini dhamira yake?
Tundu Lissu leo Kazuramimba-Uwanjani kwa mujibu wa tume
View attachment 1575244

Magufuli Leo Kazuramimba-Makao makuu ya wilaya pembezoni mwa barabara. Mkutano alioandaliwa na CCM
View attachment 1575246
hapo ni kuongeza ulinzi kwa tundu lissu, maana huyo anatembea na watu wasio julikana kwenye misafara take.
 
Kumbuka Magufuli bado ndio rais wa nchi hii, yaani aache kutekeleza mipango ya maendeleo kwa sababu kuna mmoja anayedhani anaweza kuwa rais wa nchi anaongea matusi yake! Hell no!! lazima maisha yaendelee.
Shikeni adabu zenu zenu mbona mnataka kuleta Shari? NEC ilipopanga ratiba unadhani haikujua yeye ni rais bado?
Mlitaka itokee misuguano hapo ili yale mabunduki mnayobeba utadhani mnasindikiza gari la hela LA BOT muyatumie?
Mna hamu sana na damu nyie! Shauri yenu. Wapo wababe kama Gaddafi waliishia kuangua kilio mtaroni utadhani wale mbuzi pale Vingunguti
 
Uzuri wa maisha ya binadamu ni kwamba kila kitu kina mwisho, so ukifanya ubaya ukaina ni wema mbele ya jamii, kuna ujira wake pia kwa baadaye.
Mungu alie mtuma amjua vizuri kuliko binadam yoyote maana ilisha kua na tiyari imekua asema bwana
 
Ratiba ilikwisha kuwa updated na tume kutokana na Magufuli kuwa na ugeni wa kiserikali uliomzuia kuendelea na kampeini; wagombea wote walitaarifiwa updates hizo. Kwa vile ratiba ya Lissu ina mapengo mengi, yaani haina specifity; wao wanasema atakuwa mkoa upi lakini hawaelezi atafanyia mkutano sehemu ipi, inakuwa ni vigumu kwa tume kutrace whereabouts zake.

Ratiba inakuwa updated mara kwa mara kutokana na hali halisi; kwa mfano mgombea akiumwa au akipata accident barabarani, ratiba yake itakuwa updated na tume, na wagombea wote watataarifiwa kuhusu mabadiliko hayo.
Mbona haujaleta ambayo ni updated umeleta old version ?

Magufuli ni mchokozi na hana busara na heshima kama kiongozi wa umma.

Kifupi ana tabia za kitoto
 
Mungu alie mtuma amjua vizuri kuliko binadam yoyote maana ilisha kua na tiyari imekua asema bwana
Wewe inaonekana ni mkristo mzuri ila sasa, nasema ila haujui lolote kuhusu maandiko, Mungu kamtuma nani sasa?
 
CCM kinamiliki vyombo vyote vya ulinzi!?
Hivyo, aliyempiga risasi Mh. Lissu yuko vizuri kuliko vyombo vya ulinzi vya ccm kwa kutopatikana!?
Hivyo,ccm imeshindwa kuwalinda raia wa Tanzania!?
Mara ngapi ameitwa yeye na dereva wake waje watoe ushirikiano Kwanini hakutoa ushirikiano?
 
Mlimshindwa nyie mnatakiwa mkiri ni kwamba mtu anaepanga mtu afe ni Mungu na siyo mwadamu wa kawaida tu hata ukipanga Mungu akisema no ni big no mkuu halaf risasi Lina umbali wa kuua,na kujeruhi na pia itategemea na siraha uliyotumia na kingne obstacle iliyokutana nayo Hadi kumfikia mlengwa wako
Wewe unadhani ni risasi za aina gani zilizotumika kumpiga huyo mshikaji wenu na zilitokea umbali gani?
 
Back
Top Bottom