Rais Magufuli amemtaka Katibu Mkuu Kiongozi kuwapunguzia mishahara watumishi wote TMAA kwa kufanya kazi ya hovyo

Rais Magufuli amemtaka Katibu Mkuu Kiongozi kuwapunguzia mishahara watumishi wote TMAA kwa kufanya kazi ya hovyo

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
RAIS John Magufuli amemtaka Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, kuwapunguzia mishahara watumishi wote waliokuwa wakifanya kazi Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) ambao umefutwa na kuhamishiwa Wizara ya Madini, kwa sababu kazi waliyoifanya wakiwa TMAA ilikuwa ya hovyo

Amesema watumishi hao wa TMAA ambao hawataridhika na uamuzi huo wa kupunguziwa mishahara, waache kazi wakafanye kazi zingine.

Alitoa maagizo hayo jana Ikulu Chamwino jijini Dodoma baada ya kumuapisha Naibu Waziri wa Madini, Profesa Shukrani Manya.

Magufuli alisema aliamua kulizungumza jambo hilo hadharani ili asijetafutwa ‘mchawi’ wa TMAA, kwa kuwa watumishi hao walipokuwa TMAA walikuwa na mishahara mizuri, lakini baada ya kuhamishiwa wizarani wamekuja na mishahara yao.

“Hiyo mishahara Katibu Mkuu Kiongozi ipunguzwe. Wale walitakiwa kupunguzwa kazi, kwa sababu kazi waliyokuwa wakiifanya TMAA ilikuwa ya hovyo. Ila hatutaki kuhukumu kwa ujumla, kwa hiyo wamerudi huku. Haiwezekani upelekwe Tume ya Madini wakati umetoka kule na mshahara wa shilingi milioni 10, ukamzidi hata mkurugenzi wako, ukamzidi hata mwenyekiti mtendaji, wakati bosi wako anapokea mshahara wa shilingi milioni tano, wewe una shilingi milioni 10.

“Hatuwezi tukafanya hivyo. Anayetakiwa kuzidiwa mshahara ni mimi, mimi napata mshahara wa shilingi milioni tisa lakini mtu wa Mamlaka ya Mapato (TRA) ana mshahara wa shilingi milioni 15. Nasema mtu yeyote anayefanya kazi vizuri apate mshahara mzuri, lakini wanaofanya vibaya, nataka wakose kabisa au wapate kidogo sana ili iwe fundisho kwao kufanya kazi kwa bidii” alisema Rais Magufuli.
 
Ila kuna watu wanakula nchi na maisha duniani, mm kachwamba na laki 5 zangu nasema nina salary kubwa, mwenzako anapiga 15m.
15m hela ndogo Kama unazalisha zaidi ya hiyo,
We laki 5 unazalisha Nini?
 
TRA wanamshahara mikubwa balaa.

Waliongezewa mwaka jana.

Meneja tu wa mkoa karibu 12M

Principal officers ni karibu 7M.

Seniors ni 5M

Juniors wanaanza na zaidi ya 2M

Mwenye diploma ana mshahara wa zaidi ya 1M.

Wizarani ama kwenye wizara seniors tena mwenye masters degree hamfikii mwenye diploma wa TRA.

Maisha haya hayako sawa kabisa.
 
Walipwe kwa rate za TGS

Kama kweli serikali inathamini usawa kwa watumishi wake

TGS B - Certificate
TGS C - Diploma
TGS D - Degree (arts & businnes courses)
TGS E - Degree (science courses)
 
TRA wanamshahara mikubwa balaa.

Waliongezewa mwaka jana.

Meneja tu wa mkoa karibu 12M

Principal officers ni karibu 7M.

Seniors ni 5M

Juniors wanaanza na zaidi ya 2M

Mwenye diploma ana mshahara wa zaidi ya 1M.

Wizarani ama kwenye wizara seniors tena mwenye masters degree hamfikii mwenye diploma wa TRA.

Maisha haya hayako sawa kabisa.

Na bado ni wala rushwa walioshindikana
 
Back
Top Bottom