Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naona umekariri mapepo,mapepo ...mpaka unashangaza! Mwenye post yake amesema Hakuna Mungu anayewaambia watu wawe wapumbavu. Ndio,huwezi kumuomba Mungu akuponye na korona huku ukiacha kuchukua tahadhali kulingana na miongozo ya kitaalamu. Kama kuvaa barakoa na social distancing. Kumuomba Mungu bila kuchukua hatua ni kumkejeli. Ni upumbavu!una mapepo wewe sio bure mpaka unasema hakuna Mungu
Bunge lingekuwa credible walistahili kuanza mchakato wa impeachment. JPM hafai, ameshindwa kuongoza nchi wakati wa janga.
For stupid questions, sometimes a backflip sends a message faster!Ukiwa na tabia ya kutukana wengine bila sababu unapoteza hekima ya asili,kakukosea nini?Kila mmoja aachwe atoe hoja na mawazo yake kwa Uhuru.Don't Judge people according to your own mentality, every one have the right to express themselves.
Yapo matukio ya ajabu kama haya; wasabato wa uwanja ndege JKN wakitaka kwenda ughaibuni kwa miujiza bila nauli. Wapo wachungaji wanasema wanaponya ukimwi. Wengine wanakataza waumini kumeza dawa.Nafurahi sana napomuona Rais wangu akiijua sana dini kuliko watu wote duniani (ukimtoa Askofu Rasheed) Jinsi anavyomjua sana Mungu kuliko hata Watumishi wa Mungu! Jinsi anavyomjua sana Mungu kuliko wale waliotuletea habari za Mungu! Yaani Rais wangu mpendwa anamjua sana Mungu kuliko hata Bible inayosema "Imeandikwa pia, usimjaribu Mungu wako"!
Hivi anamuona Bwana Yesu ni zuzu aliyemgomea shetani kujitupa chini kutoka juu ya mnara, au Rais wangu anafikiria nini hasa? Mbona Yesu hakujitupa pamoja na bible kusema Mungu atawaamuru malaika wake watamchukua mikononi mwao ili asijikwae?
John Pombe Joseph Magufuli alipopitishwa kuwa mgombea wa CCM alisema "..nitamtanguliza Mungu mbele, na sitowaangusha...". Hotuba Yake baada ya kuapishwa ilikuwa na maneno haya.Mhe. Rais naona ameumaliza mzizi wa fitina leo katika mazishi ya Balozi Kijazi na kusema kuwa magonjwa yalikuwepo, yapo na yataendelea kuwepo, na sisi si pekee ndiyo tunaotaabika na matatizo haya ya magonjwa ya milipuko hata nchi zingine wamekufa wengi sana. Na tatizo linapokuwa kubwa kuzidi uwezo wa binadamu tulisogeze kwa Mungu.
Rais anasema mwaka jana tulimuona Mungu akitusaidia lakini sasa naona wengine hawana imani tena wanatengeneza taharuki na kutishana mimi sifanyi lokudauni tuchape kazi Mungu yupo. Kwanini au amwamini kuwa Mungu anaweza kuishinda Korona?
Mimi mtoto wa mchungaji nahoji hivi hawa baadhi ya viongozi wa dini ambao nao pia wanaogopa Corona kiasi cha kwamba wanatushauri tuwasikilize watu wa afya na wamitandaoni hivyi hawa watumishi wa Mungu si wangeacha hiyo kazi na kuja huku mchangani ijulikane moja.
Nawauliza na ninyi wana janvi Mungu yupo au, maana babuzetu waliomba mvua zilinyesha, waliomba nzige waondoke asubui waliwakuta chali kificha mende, magonjwa ya mlipuko hayakuwagusa, hivi na yule Mungu wa babu zetu yupo wapi siku hizi na huyu wa kanisani na msikitini yupo wapi.
Mwisho wa siku mmechezea tu mpapaso , mnaambiwa muandamane mnaishia tu kutoa mapovu mitandaoni, endeleeeni na ndoto zenu ma keyboard warriorsNa Maria Sarungi ni keyboard warrior?Na Fatuma ni keyboard warrior?And other countless people talking and show their displeasure to this useless political class ni keyboard warriors?
Kumbuka wanapata momentum and people resonate towards them ndio maana wana nguvu
Endelea kusema keyboard warriors...tatizo ni denial ya kila kitu...siku utakuta ni kweli what we are saying to you
Nafurahi sana napomuona Rais wangu akiijua sana dini kuliko watu wote duniani (ukimtoa Askofu Rasheed) Jinsi anavyomjua sana Mungu kuliko hata Watumishi wa Mungu! Jinsi anavyomjua sana Mungu kuliko wale waliotuletea habari za Mungu! Yaani Rais wangu mpendwa anamjua sana Mungu kuliko hata Bible inayosema "Imeandikwa pia, usimjaribu Mungu wako"!
Hivi anamuona Bwana Yesu ni zuzu aliyemgomea shetani kujitupa chini kutoka juu ya mnara, au Rais wangu anafikiria nini hasa? Mbona Yesu hakujitupa pamoja na bible kusema Mungu atawaamuru malaika wake
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa......Kumwamini Mungu ni jambo moja ila haiondoi umuhimu wa kupractice common & sensible preventive measures.
Hata Kitabu kitakatifu kimesema wazi kwamba “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”
Mpambane sasa sio uanaharakati wa keyboard tu sasa mnakamatwa mnarudi nyuma??si mnapendaga kujipa moyo mkiona huko wenzenu wa nchi nyingine wanakinukisha kweli , hao wakishikwa wanaachaga kuandamana? Just a bunch of cowards mtatishia mapunguani tuMpapaso ndio nini mzee?
Waoga ni nyie,mnaogopa nini watu wakiandamana?
Wewe mtu anaandamana barabarani anafika mwembeyanga anasimama anarudi kwao,wewe unapaniki nini kama sio uoga?
Unaenda washika kabla hata hawajaandamana?
Yanini wenye dola waoga namna hii?
Unataka kusema njia hajafanya kwenye hili?Usisahau Mungu ufanya njia pasipo na njia
Wasabato Masalia wanaitwa, wapumbavu sana, sasa si wangeenda ulaya wakiwa kanisani kwao, walienda airport kufanya nn?Kama ana itikadi Kali hivyo kama wasabato walokwenda airport Mungu awapeleke (sijui ulaya?) Haspitali zinajengwa za nini?
Katulizwa....mtatulizwa wakija wapumbavu wengine watatulizwa nyie leteni maneno wenye nguvu wanafanya vitendo tu.........yaani hata ukipiga chafya tu utatulizwa endeleeni na ukamanda wenu wa keyboard na majina yenu bandia ndo kitu pekee mnachoweza,,,, taarabu mingi....mlidhani nchi mnapewa kwa kuimba taarabu tu mitandaoni ...........mwanaume vitendo sio taarabu nyuma ya keyboard na ma kemera.....yani unalia unashindwa kujikomboa kisa unakamatwa sasa ulidhani ukombozi ni kama kuletewa keki ya besdei magetoni..........textbook warriors.....Yall are cowards of poor people with no silaha wanao andamana ku-express their displesure with your stupid rullings
Yaani mnaogopa mwananchi asie na silaha yeyote anaetembea barabarani
Tutaandamana tu,sio kwa tarehe unazotaka wewe....ni kwa tarehe zetu wenyewe tunazojipangia
Mwamakula kawa-beep mmeanza kupaniki mamaeee....
Hivi watu wanaokaa vijijini unawachukuliaje, unawaonaje, lakini!? Kwa taarifa yako ni watu kama wewe. Wana utashi kama wewe.Mimi naweza kuchukua sawa vipi kuhusu wanaokaa vijijini
sasa wewe unaona yupo sawa kuandika hivyo nawewe utakua na mapepo tu sio bure. Ilitakiwa aandike Mungu huwa hawaambii watu wawe wapumbavu. Hiyo kauli ya hakuna Mungu ambaye maana yake anaaminisha kuna Mungu zaidi ya mmoja. Mapepo yakiwa kaziniNaona umekariri mapepo,mapepo ...mpaka unashangaza! Mwenye post yake amesema Hakuna Mungu anayewaambia watu wawe wapumbavu. Ndio,huwezi kumuomba Mungu akuponye na korona huku ukiacha kuchukua tahadhali kulingana na miongozo ya kitaalamu. Kama kuvaa barakoa na social distancing. Kumuomba Mungu bila kuchukua hatua ni kumkejeli. Ni upumbavu!