Rais Magufuli ataja sababu kusitisha ujenzi bandari ya Bagamoyo kwa Mkopo wa Dola Bilioni 10

Rais Magufuli ataja sababu kusitisha ujenzi bandari ya Bagamoyo kwa Mkopo wa Dola Bilioni 10

Mfano wako ni irrelevant kabisa

Hvi unafahamu mradi wa trillion 20+ ? Faida zake ni kama kiwanja cha hoteli?

Faida za mradi wa bagamoyo ni mtambuka sio za moja kwa moja kma kodi n.k. kumbuka sheria zetu za uwekezaji zinataka serikali ipewe 16% shares, kampuni itunze pesa zake walau 25% kama sikosei benki za ndani, haya local content inataka ajira za wabongo kwa zile nafasi ambazo kuna Mtanzania ana skills hizo n.k hizo ni direct tu

Sasa multiplier effect ni kwamba SGR itaongeza volume ya mizigo, ATCL itakuwa na route nyingi zaidi, makampuni ya bima na logistics/maritime kama yote yatahamia TZ so yatalipa kodi hayo na kutoa ajira lukuki. DSE itaongezeka listed companies hivyo kuchochea Capital markets, benki zitaongeza deposits hivyo ukwasi kutanuka.

Jamani Multiplier effect itakuza mradi wa bagamoyo kwa nchi nzima tusikariri kodi na ajira tu!! Fikirieni jinsi mradi utakaribisha miradi mingine mizito zaidi
Mkuu Zitto Junior! Asante Kwa pointi hii!!

Unadhani ni kivipi mradi wa bagamoyo, ndio uwe suluhisho la kuubeba uchumi wetu mbali na Gas yetu pale Mtwara

Mimi nadhani, Wakati wa Miradi ya kinyonyaji kama huu tunaotaka kuuingia, Tufike mahali kama nchi tukatae

Mikataba Kwa mfano ya Madini, Nayo huwenda ilisainiwa Kwa lengo kama Hilo ambalo umebainisha, na ndio Maana mrahaba tukawa tunapata 2% Kwa mauzo yote, na Mkataba ukisoma ni miaka 💯

Ukimuuliza aliyesaini, naye atakwambia alitarajia kuona viwanja vya ndege vyetu vikiwa bize, Bandari zetu kuwa bize, Kwa hiyo kama ni mapato makubwa watayapata huko

Wazungu wanazijua Sana Hesabu, sio wa kwendea hivihivi, hawana Mkataba wa kukunufaisha wewe na Wala hawajawahi kupanga hivyo, Ila hulazimika Ikiwa watakuta viongozi wenye uwezo kichwani

Mradi wa bagamoyo Kwa masharti yake, usipojadiliwa ili kuondoa Baadhi ya masharti ya kinyonyaji, hauna Tija, ni Bora tudili na bomba letu kutoka Hoima, Hilo ndilo litazifanya Bandari zetu kuwa bize
 
Semantics tu za kutokukukubali facts; ni mapendekezo ya kuweka mkataba! Magufuli hakufuta mkataba bali alikaa kuingia mkataba huo kwa mapendekezo hayo.
Atakataaje kuingia mkataba usiokuwepo; huoni kwamba unajichanganya?

Ili pawepo na mkataba ni lazima pawe na mapendekezo na majadiliano kati ya pande mbili. Haya ni mapendekezo ya mchina ndiyo aliyoyakataa Magufuli na sio mkataba.
Hakuna cha 'semantics hapa, labda uwe hujui maana halisi ya neno hilo.
 
Hapa ni swala la Tanzania na hao wawekezaji; Tanzania ndiyo iliyokataa mapendekezo ya wawezekezaji kuwa hayakulingana na interest za Tanzania, je kuna upande gani mwingine ambao Tanzania ilitakiwa kusikiliza tena kabla ya kutoa uamuzi?
Unauliza swali la kitoto.
Huoni kuna pande mbili hapo? China na Tanzania?

Kama Tanzania imekataa mapendekezo aliyotoa mchina, yenyewe haiwezi kutoa mapendekezo ya upande wake kulinda 'interests' zake?
 
Ndio tatizo la mods wa JF kuunganisha threads zenye premise tofauti kisa topic ni moja.

Hiyo point imekuja kutokana na kwamba kulikuwa na mada usiku wa kuamkia leo inayotoa hints za elements za mkataba wenyewe ambazo TPA inazikataa kwa mujibu wa mkurugenzi wao aliotelewa hapo. Na aliongea points za msingi sana.

Ungesikiliza kwanza hiyo clip uone the logic behind my point. Isitoshe hayo mengine yote uliyo orodhesha yanaweza fanyika separately bila ya ubia wa serikali hao wachina wakipitia TIC be it multipliers zingine ulidhoorodhesha hapo not sure if you can back them back up conclusively.

Umejiuliza kwanini wanataka kufanya huo uwekezaji wa biashara zingine nyuma ya kivuli cha mradi wa bandari?
Mkuu unaweza kushare upya hiyo clip
 
Mkuu Zitto Junior! Asante Kwa pointi hii!!

Unadhani ni kivipi mradi wa bagamoyo, ndio uwe suluhisho la kuubeba uchumi wetu mbali na Gas yetu pale Mtwara

Mimi nadhani, Wakati wa Miradi ya kinyonyaji kama huu tunaotaka kuuingia, Tufike mahali kama nchi tukatae

Mikataba Kwa mfano ya Madini, Nayo huwenda ilisainiwa Kwa lengo kama Hilo ambalo umebainisha, na ndio Maana mrahaba tukawa tunapata 2% Kwa mauzo yote, na Mkataba ukisoma ni miaka 💯

Ukimuuliza aliyesaini, naye atakwambia alitarajia kuona viwanja vya ndege vyetu vikiwa bize, Bandari zetu kuwa bize, Kwa hiyo kama ni mapato makubwa watayapata huko

Wazungu wanazijua Sana Hesabu, sio wa kwendea hivihivi, hawana Mkataba wa kukunufaisha wewe na Wala hawajawahi kupanga hivyo, Ila hulazimika Ikiwa watakuta viongozi walioiona Asubuhi kichwani

Mradi wa bagamoyo Kwa masharti yake, usipojadiliwa ili kuondoa Baadhi ya masharti ya kinyonyaji, hauna Tija, ni Bora tudili na bomba letu kutoka Hoima, Hilo ndilo litazifanya Bandari zetu kuwa bize
Nimeelewa concern yako lakini tukubaliane kabisa hata serikali ina justify Stendi ya Magufuli, ATCL, kutopandisha mishahara kwa hoja ya hiyo hiyo ya "uchumi ni mtambuka". Kwamba faida ya ATCL sio kuingiza mabilion kupitia mauzo ya ndege ila utalii, ku ease logistics, n.k. kwahiyo tukubaliane kabisa kwamba hiyo justification ipo kwa miradi yote ya kiserikali sasa kivp kwa bagamoyo ndio iwe mutual exclusive?

Mimi nadhani kuliko kuvutana sana kati ya serikali, wananchi,spika, AZAKI n.k huo mkataba (at least draft) upelekwe kwa kamati ya bunge ya uwekezaji walau waishauri serikali na pia kuruhusu maoni ya stake holders ikiwemo sisi wananchi.

Mwisho wa siku mradi ufanyike kwa Win Win situation.... Hata ile vurumai ya ACACIA tulikua tuna demand trillion 400 lakini tukasettle for less kwa kuanzisha subsidiary bila kuvunja kabisa mkataba.

So kikubwa mradi uungwe mkono (pending amendment chache kwenye makubaliano) kuliko mawazo ya kufutilia mbali hiko kitu ndio nachopinga. Maana kuna watu hawataki hata mazungumzo wanataka ufutwe outright sasa kwa staili hiyo tutafika kweli?
 
Mimi nadhani kuliko kuvutana sana kati ya serikali, wananchi,spika, AZAKI n.k huo mkataba (at least draft) upelekwe kwa kamati ya bunge ya uwekezaji walau waishauri serikali na pia kuruhusu maoni ya stake holders ikiwemo sisi wananchi.

Mwisho wa siku mradi ufanyike kwa Win Win situation.... Hata ile vurumai ya ACACIA tulikua tuna demand trillion 400 lakini tukasettle for less kwa kuanzisha subsidiary bila kuvunja kabisa mkataba.
Ubarikiwe Sana mkuu!!
 
Unauliza swali la kitoto.
Huoni kuna pande mbili hapo? China na Tanzania?

Kama Tanzania imekataa mapendekezo aliyotoa mchina, yenyewe haiwezi kutoa mapendekezo ya upande wake kulinda 'interests' zake?
Haya sawa mzee; wewe umejibu kikubwa kwa kujua kuna kuna pande mbili yaani Tanzania na China lakini Tanzania imekataa mapendekezo ya China halafu unauliza kwa nini ilikataa mapendekezo ya upande mmoja tu- sijui ulitaka ikate na mapendekezo ya upande upi tena. Counter offer unataka ndiyo ambayo Kakoko anasema wanaendelea na majadiliano. Serikali ilikuwa haijaingia nao mkataba wowote, ila kwa upande wao wawekekezaji hao walitaka mkataba ambao serikali itawapa concessions hizo ambazo serikali ilikataa.
 
Counter offer unataka ndiyo ambayo Kakoko anasema wanaendelea na majadiliano. Serikali ilikuwa haijaingia nao mkataba wowote, ila kwa upande wao wawekekezaji hao walitaka mkataba ambao serikali itawapa concessions hizo ambazo serikali ilikataa.
'Full circle', unarudi pale pale nilipoanzia, sasa sijui unabishia kitu gani?
 
Mkuu unaweza kushare upya hiyo clip




Clip iliyowekwa jana ilikuwa ☝️ ndio premise ya mchango wangu. Mkurugenzi katoa maelezo mazuri ya areas of negotiation ambazo awazikubali.

Past concerns on the same areas.

Unaweza kupitia na hiyo mada nyingine uangalie na michango ya wengine.

In terms of financial appraisal ya mradi concerns za mkurugenzi mtu mwingine yoyote makini will come to the same conclusion with logic alone bila ya hata kuona huo mkataba.

Ukisikiliza anachosema huyo Kakoko ni confirmation of their fears kwa watu ambao walishatafakari kwa makini hiyo $10 billion inaenda wapi na mkurugenzi gave an honest opinion in financial terms.

Uwekezaji mwingine wachina wanatakiwa kwenda TIC kwa sababu TPA hawana shida nao. Ndio maana nikakuuliza why wanataka na viwanda vyao viwe sehemu ya uwekezaji wa bandari?

Ni mkataba mmbovu.
 
You actually think that’s a good idea?

Mtu aje kujenga hotel kwenye kiwanja chako bila kukulipa ata senti moja,

Biashara ikianza wewe usipate chochote.

Anarudisha faida ya ujenzi ndani ya miaka 5 lakini hataki umdai chochote mpaka baada ya miaka 20.

Asilipe kidi yoyote kwa serikali ndani ya muda huo.

Sehemu ya kiwanja chako ulichomkatia baada ya kujenga kama kuna spare space huna say. Akitaka na yeye anaweza muuzia mtu mwingine afanye uwekezaji wowote kwa masharti kama uliyompa yeye?

Yote hayo kwa sababu kaajiri ndugu zako kwenye kazi za uhudumu (kutandika vitanda, usafi, kutunza maua, na nyingine zisizo na skills).

You actually think that is a good investment? Kama bado lazima utakuwa na matatizo.

Hao ni wa kwenda TIC tu serikali isipoteze muda na hao watu, useless kweli kweli.
Umenisoma vema lakini au umekurupuka.... Sasa mbona ni kama unaongea kile kile ninachokikemea mimi?! Hebu nisome upya kisha ucomment vema kama mtu anesoma na kuelewa alichosoma.
 
Mradi unaanza tena.Je Jiwe alitudanganya?
Jiwe alidanganya sababu mradi hakuubuni yeye ndio maana kaenda kujenga uwanja wa Ndege huko kwao.... kwenye Biashara meza ya mazungumzo ndio inaamua Kila kitu unategemea mtu aingize mahela yake Kisha aje kibwege kama mchina alikuja na terms zake ilitakiwa nasisi twende na zetu kisha tunakubaliana Sasa sisi tunategemea tuletewe dhahabu kwenye sahani ni ujinga kwakweli
 

RAIS John Magufuli amesema sababu kubwa ya kusitishwa kwa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ni masharti magumu yaliyomo katika mkataba wa utekelezaji wa kazi hiyo.

Jiwe la msingi la ujenzi wa bandari hiyo liliwekwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete mwaka 2015 na ulitarajiwa kugharimu dola za Marekani bilioni 10. Bandari hiyo endapo ingejengwa ingekuwa kubwa zaidi Afrika Mashariki ikiwa na ukubwa wa ekari 3,000 na viwanda 190 vingejengwa.

Akizungumza jana kwenye mkutano wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliowashirikisha wafanyabishara kutoka wilaya 139 nchini, Rais Magufuli aliweka wazi sababu za kusitishwa kwa ujenzi wa bandari hiyo. Rais Magufuli alisema “kwenye mkataba wa ujenzi wa bandari hiyo kulikuwa na vipengele vya ovyo”. Rais Magufuli alisema mojawapo ya masharti ni kutojengwa wala kuendelezwa kwa bandari yoyote kuanzia eneo la Tanga hadi Mtwara.

"Yaani kwenye eneo lote kuanzia Tanga hadi Mtwara kusijengwe bandari yoyote. Bandari ya Kilwa tusiiendeleze, Bandari ya Mtwara ambayo itawezesha mikoa ya kusini kupokea mafuta badala yake Dar es Salaam kisha yarudi huko, hatutakiwi kuiendeleza, Barabara kutoka Mtwara hadi Bamba Bay ambayo itatuwezesha kusafirisha mizigo hadi Msumbiji tusiijenge," alisema Rais Magufuli

Pia alisema wawekezaji hao wangeweza kumiliki ardhi kwa hati ya miaka 99 pamoja na kutoruhusiwa kuuliza nani anamiliki eneo hilo. Rais Magufuli alisema sharti lingine ni gharama zitakazotumiwa na mwekezaji huyo katika ujenzi wa bandari hiyo kutakiwa kurejeshwa.

Soma pia:
Bandari ya Bagamoyo: Je, sababu alizotoa Rais Magufuli ni za kweli?. Je, haya mazungumzo ni ya nini tena kama wameachana na mradi huo? - JamiiForums
Bila shaka sasa hivyo vipengele vya ovyo watakuwa wameshaviondoa vyote
 
Back
Top Bottom