Rais Magufuli awatumbua Kitila Mkumbo, Ole Sendeka na Katambi, awateua Jumanne Fhika, Dr. Aloyce Nzuki, Allan Kijazi, Josephat Paulo, Kemikimba

Apo nimekupata sawa sawa Shukrani sana 🤝
 
Mbona hajawakataza, alichofanya ni kutoa angalizo kwamba ukitaka ubunge lazima uachie nafasi uliyonayo. lakini pia kwa utitiri wa watia nia ilikuwa ni busara kwa hawa wateuliwa kubaki na nafasi zao kwa sababu wao siyo bora kuliko watia nia wengine.

Tegemea ulichokishika mkononi, usitegemee utakachotafuta. Unaweza kufanya vizuri kwenye nafasi uliyopewa na ikaonekana na baadaye ukawa promoted to the next level.
 
umeshaambiwa vigezo ni kujua kusoma na kuandika zaidi sana kuwa ccm

Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
 
Katambi hana base yoyoye Shinyanga mjini na hajulikani maana 2015 alibebwa tu na nguvu ya Chadema.
Pale mjini GAKI, Fresho na Kwilasa ndio wanaamua mbunge awe nani

Na utamu zaidi GAK(Gaspar Kileo) nae anagombea mwaka huu hataki kunwaga hela zake tu anaona bora ajimwagie mwenyewe.

Chupi zinabana🤣🤣
 
Huu ni uonevu nadhani kuanzia ngazi fulani,mbona kuna baadhi ya mawaziri kabisa tena ngazi za juu wao hatengii uwaziri wao sasa kama ni hivyo
watu wanachanganya.. Uwaziri siyo sehemu ya utumishi wa Umma. Uwaziri ni Cheo cha kisiasa, ndo maana mtu asipokuwa mbunge Rais akitaka amchague kuwa waziri lazima amchague kwanza kuwa mbunge.. lakini Ukurugenzi, ukuu wa wilaya, ukuu wa mkoa n.k ni utumishi wa Umma moja kwa moja Mhusika kama siyo likizo anapaswa awepo kazini kila siku za kazi, Rais akijisikia anaweza kupangua wizara na kuzipunguza kutoka 40 zikabaki hata 20.. lakini wilaya ikizhaundwa au mkoa Rais hawezi kuamka na kusema leo Amefuta mikoa 10, hivyo waziri yeyote ni Mwanasiasa automatically, hivyo kugombea ubunge ni sehemu ya sifa ya kwanza..

JamiiForums mobile app
 
Na ndio upungufu ninao uona. Hajaacha kuteua wana siasa. Kateua makada kibao wa CCM kuwa DED, DAS na RC. Acha maisha yaendelee
 
Wewe fikiria Hadi Jana walioomba kupitia CCM Ni elfu nane Kati Yao elfu 6 ni watumishi wa umma hivi unataka ofisi za serikali afanye kazi Nani? Magufuli Yuko sahihi ku replace angeruhusu ungekuta wafanyakazi wa umma laki mbili wanataka ubunge ofisi wameacha tupu hazina wa kuhudumia wako foleni ya kuchukua fomu za uteuzi
 
Kwa uongo uko vizuri,watu elfu themanini unawajua wewe lkn?
 
Wao ktk teuzi siwaoni kabisa au wapo Kenya siku hizi
Be dynamic.. wakibana huku unatokea kwingine.

Ona sasa Msukuma mwenzako anasema Gaspar Kileo na Fred Shoo ndio wanaamua Mbunge wa Shinyanga Mjini awe nani hahahaha...
 
Kijazi wa TANAPA ameteuliwa kua Naibu katibu Mkuu Wizara ya Mali asili huku akiendelea pia na u-boss wake pale TANAPA.

Hao ndio wenye nchi sasa,wanyonge walie na umaskini wao tu.
Prof. Mkenda Ina maana naye kaenda kugombea ubunge au katumbuliwa?
 
Ahaa sawa
 
Hizi Ni dharau kwa mwenyekiti wao, kwamba pamoja na angalizo alilolitoa bado wanamuona si lolote si chochote.

Ngoja tuone Kama Mwenyekiti wao atawalamba miguu kwa kuruhusu uteuzi wao, maana alishawapiga ban wasithubutu
Kujua hii game inahitaji uwaze nje ya box,kama unawaza ndani ya box comment ni kama ulivyoileta
 
Mimi naona mwenyekiti na yeye wangemzuia kugombea mimi naisi asingefika hapo alipo hii ni kuzuia demokrasia.
Angekuwa mwl huko kwao sengerema hadi muda huu.. anasubiri mafao yake nssf na kadi yake ya benki kwa wakopeshaji wa mtaani.
 
Kumbe wana mdharau Mwenyekiti kiwango hiki, yaani ingekuwa mimi ni Mh. Mwenyekiti JPM, wote walioacha kazi serikalini kuanzia Katibu Mkuu, PS, RC, RAS, DC, DAS, DED, CEO, MD, DPS, wotee wenye vyeo vikubwa na wakaachia ni tamaa kubwa, majina yakija kwangu nakata yote, itakuwa funzo kubwa kwa wengine. Yaani naamini Mh. Rais alilisema sana hili, wenye tamaa kama Mwananzila atawakata wote. Tusubiri tuone, hii ni dharau kubwa ya wazi wanafanya kwa Mwenyekiti
 
Yeye alipokua mwalimu mbona hakuridhika na cheo chake akaenda kugombea ubunge?Ni tamaa au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…