Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
Ni kweli unavyosema nadhani washauri wake ndio wanamuongoza vibaya, yote ni propaganda za kampeni wamuone kuwa anawajali na yuko pamoja naye huku akisahau kuwa si njia sahihi ya kuhamasisha michango ya ujenzi wa waislamu sasa sijui itakuwaje kama Masheikh wataupokea huo mchango au la maana tayari umehamasihwa kwa njia isiyo sahihi.
 
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
Mkuu ulikuwa unatakiwa utafakari kwa kina na kwa mapana kabla ya kuleta hili bandiko, Hakuna logic Kabisa kwenye bandiko lako, mwaka Jana nikiwa safarini kwenda Tanga kutokea Bagamoyo, tulipofika Handeni alipanda mtu mmoja kwenye gari yetu baada ya hapo akajitambulisha Kama kiongozi wa dini ya kisilaam kutoka eneo fulani huko handeni, akesema yeye anaomba mchango wa kusaidia kukamilisha ujenzi wa msikiti na kuanza ujenzi wa madrasa, je kwenye hizo hela alizopewa siku hiyo kwenye Basi, za wakrisito hazikuwemo???

Kingine fahamu kazi ya kiongozi ni kutatua changamoto na kero za raia wake rais alikuwa specific Kabisa kuelezea kuwa kuna watumishi anafanya nao kazi lkn sehemu yao ya ibada ni ndogo, kwahiyo inahitajika zaidi ya hiyo, halfu Mbona alisema pia Rostam alichangia ujenzi wa kanisa je hilo nalo watu waache kwenda kwenye hilo jengo kisa muisalamu katoa hela, pia kutoa ni moyo, Kama ni hivyo hiyo ni sadaka, sadaka yaweza kutumika kumsaidia yeyote yule.

Halfu mambo ya kutuambia sijui msikiti unajengwa kwa hela sijui Safi au chafu, riba imejaa na kutapakaa duniani, ni misikiti mingapi imejengwa kwa hela za riba? Au riba sio Haramu?
 
We mtoa post umekosea sana na udini unakusumbua,nataka tu kukukumbusha kwamba Rais ni kiongozi wa nchi na nchi haina dini
Unakumbuka mwaka 2011 mbowe alipochangisha pesa za kukarabati msikiti kule hai mlivyomshambulia mkiongozwa na bwakata mkoa wa kilimanjaro kuwa haikuwa sahihi mbowe kuchangisha pesa na kutangaza? Tena alichangisha kwenye swala ya ijumaa, huyu kachangisha kwenye misa kanisani tena TV ya taifa na channel 10 wakiwa live lakini mnashangilia.
 
Hakuna ubaya kuchangishana kujenga nyumba za ibada,,ili wakazi wa maeneo hayo nao wapate pa kuabudia
Unakumbuka mwaka 2011 mbowe alipochangisha pesa za kukarabati msikiti kule hai mlivyomshambulia mkiongozwa na bwakata mkoa wa kilimanjaro kuwa haikuwa sahihi mbowe kuchangisha pesa na kutangaza? Tena alichangisha kwenye swala ya ijumaa, huyu kachangisha kwenye misa kanisani tena TV ya taifa na channel 10 wakiwa live lakini mnashangilia.
 
Waislamu wao wenyewe hawajashindwa kujenga msikiti huko Ikulu ya Chamwino.
Haihitajiki harambee za kanisani kujenga msikiti wa waislamu!. Yeye atoe tu eneo kisha awaachie waislamu wenyewe wafanye mchakato wa ujenzi, wskitaka kumshirikisha watamshirikisha

Mbona wakati anajenga kanisa hilo hakuomba harambee za waislamu?

Au anataka baadae, Waislamu wasimangwe kuwa hata huo msikiti wenu ndani ya Ikulu yetu ya dodoma ulijengwa kwa sadaka za Wakiristo?
Hahaha mkiachwana eneo bila kuchangiwa hamtajenga na eneo linaweza kuleta migogoro baadaye mkamsumbua sheikh Ponda kuanza kufuatilia mali za waislamu.

Jamani kuweni na shukrani kawaombea pesa huyo rais.

Hivi uliisha shuhudia ngumi msikitini wewe, kwamba moja ya viongozi wa msikiti anashutumiwa kula pesa za misaada?!

Binafsi naona ni jambo la kawaida kabisa na hajaanza yeye, hata Lowassa enzi zake kafanya sana hizi.

Juzi hapa Nakonda alikuwa anazunguka mchana na usiku kuwaomnbea pesa mjengewe msikiti na ofisi za bakwata.

Kusema asante tu hamuwezi?! Hahaha nyie kiboko.
 
Unakumbuka mwaka 2011 mbowe alipochangisha pesa za kukarabati msikiti kule hai mlivyomshambulia mkiongozwa na bwakata mkoa wa kilimanjaro kuwa haikuwa sahihi mbowe kuchangisha pesa na kutangaza? Tena alichangisha kwenye swala ya ijumaa, huyu kachangisha kwenye misa kanisani tena TV ya taifa na channel 10 wakiwa live lakini mnashangilia.
Mimi sijawahi kumshambulia mbowe,kwa ishu hiyo,,mbowe ni mmoja wa wanasiasa wazuri kabisa,,kama kuna mtu alimshambulia kwa suala hilo,itakuwa vilikua vijembe vya kisiasa tu..
 
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!

Kwahiyo kila atakae kwenda Ikulu atajenga kanisa lake why government inajichanganya hivi?.
Rais unachanganya watanzania . Kuruhusu Roman Catholic liwe na kanisa ikulu vipi waislam vipi mathehebu mengine? Ina maana kila Rais awe anajenga ikulu makanisa na misikiti? Hili umeharibu mzee wangu.
 
Azam Dewji achangia Milion 10. Kufanikisha ujenzi wa "Nyumba Yangu" katika Harambee aliyoianzisha Mh Rais Jumapili Agosti 23 huko Chamwino.
 
Mkuu ulikuwa unatakiwa utafakari kwa kina na kwa mapana kabla ya kuleta hili bandiko, Hakuna logic Kabisa kwenye bandiko lako, mwaka Jana nikiwa safarini kwenda Tanga kutokea Bagamoyo, tulipofika Handeni alipanda mtu mmoja kwenye gari yetu baada ya hapo akajitambulisha Kama kiongozi wa dini ya kisilaam kutoka eneo fulani huko handeni, akesema yeye anaomba mchango wa kusaidia kukamilisha ujenzi wa msikiti na kuanza ujenzi wa madrasa, je kwenye hizo hela alizopewa siku hiyo kwenye Basi, za wakrisito hazikuwemo??? Kingine fahamu kazi ya kiongozi ni kutatua changamoto na kero za raia wake rais alikuwa specific Kabisa kuelezea kuwa kuna watumishi anafanya nao kazi lkn sehemu yao ya ibada ni ndogo, kwahiyo inahitajika zaidi ya hiyo, halfu Mbona alisema pia Rostam alichangia ujenzi wa kanisa je hilo nalo watu waache kwenda kwenye hilo jengo kisa muisalamu katoa hela, pia kutoa ni moyo, Kama ni hivyo hiyo ni sadaka, sadaka yaweza kutumika kumsaidia yeyote yule. Halfu mambo ya kutuambia sijui msikiti unajengwa kwa hela sijui Safi au chafu, riba imejaa na kutapakaa duniani, ni misikiti mingapi imejengwa kwa hela za riba? Au riba sio Haramu?
Tatizo unaongea katika perspective isiyo ya kiislam.

Uislam una taratibu zake za kuendesha mambo.

Na halafu mimi nikivaa suti yangu na nkipanda kwenye basi nkianza kuchangisha huku najiita John unakuwa na uthibitisho gani kwamba mimi siwapigi tu hiyo pesa abiria?? I am not saying huyo mtu hakuwa muislam laaaa, I am just trying kujenga hoja.

Katika uislam kuna aina mbali mbali za sadaka na kila moja inayo aina ya watu wanaoistahili.

Kuna hadithi nyingi sana za Mtume zinazozungumzia watu muflis, yaani mtu aliefilisika. Ni nani huyo?? Kwa mujibu wa uislam ni yule ambae itakuja siku ya kiama na yale yote aliyoyatenda dunia kuwa ni sawasawa na vumbi tu hayastahili malipo yoyote toka kwa Allah.

Kiufupi diamond hawezi kwenda janga msikiti kwa hela yake haramu halafu eti ategemee malipo na pepo. Labda pepo ya udongo.

Huyo rostam kuchangia kanisa anafanya huku akijua kwa Mungu hapati chochote atapata tu maslahi yake ya kidunia aliyokusudia kuyapata kupitia mchango huo.

Muda mchache mambo ni mengi mkuu
 
Kwahiyo kila atakae kwenda Ikulu atajenga kanisa lake why government inajichanganya hivi?.
Rais unachanganya watanzania . Kuruhusu Roman Catholic liwe na kanisa ikulu vipi waislam vipi mathehebu mengine? Ina maana kila Rais awe anajenga ikulu makanisa na misikiti? Hili umeharibu mzee wangu.

Amejenga kasehemu ka kumsalia bikira Maria ndani ya eneo la kanisa hilo la Ikulu huko Dodoma, Sijui kama Walutheri na Walokole watapenda hiyo move ya Magufuli, ngoja tuone kama nao atawapa eneo lao kujenga makanisa yao!
 
Mbona mi nishawahi kufatwa kuombwa nichangie mikeka ya kuswalia wakati mi mkristu.
Jamaa alikua anatembea na barua kuomba mchango huo toka msikiti husika.
 
Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!
Mkuu hapa haupo sahihi.
Zaidi ya mara tano wanapita hapa nyumbani kwangu na kuomba mchango wetu watu wa kamati za kukusanya michango ya ujenzi wa msikiti.
Hawaulizi dini wala jina, hapa kwangu sisi sote ni wakristo. Na sidhani kama ukitoa mchango ukaandika jina la kikristo kwenye daftari lao watakurudishia mchango wako.

Tunawaona wanakaa barabarani wanakusanya michango na hawasemi wakristo wasichangie.

Usije ukasema hawa ni walaghai hawapeleki michango msikitini sitakuamini sababu wanakuja na vibali vya kukusanya michango na tunawajua kwa sura na majna ni kweli hao ni watu wa kutoka msikiti flani.
 
Back
Top Bottom