Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Sijaona ubaya wowote na ukisoma waliochanga hizo fedha ni pamoja na Rostam Aziz huyu ni mwislamu au amebatizwa? Mbele ya Mungu Waislamu na Wakristo wote ni kitu kimoja. Acheni udini wote ni Watanzania
 
Jaribu kupiga picha msikiti unajengwa na mchango wa mgalatia kwa fedha alizopata faida kwenye biashara ya kitimoto...
Dah!...nyie raia mna propaganda sana, kwani pesa zote zinazopita mikononi mwetu kuna anayejua zinatoka wapi?

Pesa ni kama kiungo cha mabadilishano ya bidhaa au huduma, hivyo haihusiani na dini au imani.
 
Kingine sina Hakika kama Mungu wa waislamu ndo Mungu wa Wakristo.

Hapa mtu unaweza ukajikuta unachuma dhambi bila kujua.

Sisi wakristo tunajua Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu. Siwezi kuchangia ujenzi wa msikiti au ujenzi wa shaulin temple ili Mungu mwingine aka abudiwe. Kwa imani yangu iyo ni dhambi.

Dini zote kasoro wahindi ,Buddhism na wa misri wa kale zinaamini Mungu ni yule aliyeumba hii Dunia, hayo mambo mengine sijui ya kanisa,msikiti ni mbwembwe tu.
 
Wenye dini yao wala hawana tatizo na hilo suala la michango. Nchi yetu sote hii na wala sio mara ya kwanza kuchangiana ujenzi wa makanisa na misikiti. Tatizo kila jambo linachanganywa na siasa.

Ni juzi tu Joketi Mwogelo Mkuu wa Wilaya Kisarawe amechagua ujenzi wa Msikiti na Waislamu wenyewe wamechagua kuwa mlezi wa kamati ya ujenzi.

..nadhani tunazunguka-zunguka bila kwenda kwenye MSINGI/KIINI cha tatizo.

..mimi nadhani Jpm ni mwanasiasa asiye na hoja na haiba ya uongozi, hivyo amekuwa akitumia makanisa na misikiti kufanya siasa.

..ili Jpm akubalike ni lazima apitie kwenye "uchochoro" wa imani za watu, akipitapita makanisani na misikitini huku akimwaga MAPESA.

..inawezekana kuna kasoro ndogo-ndogo namna ambavyo harambee iliitishwa, lakini msingi na kiini cha yote haya ni Jpm kutumia DINI na FEDHA ktk siasa.

cc tindo, Phillipo Bukililo , Kilatha, Nguruvi3
 
Acheni umbea na uzwazwa mimi ni.mkristo na nimeshachangishwa ujenzi mbal mbal za misikiti.kma ww huna cha kuchangia kaa kimya .hiyo mnayoswalia mnajua ilijengwa na nani? Na vyanzo vya mapato ya kuijenga mnaifahami au ni unafiki
Ww sio mkristo, kuna wakristo jina wasiofuata misingi ya ukristo. Msingi mkuu wa ukristo ni kutangaza injili ya kristo kote duniani ili mataifa wamjue Yesu. Sasa hayo misikiti inatangaza habari za kristo
 
Acheni umbea na uzwazwa mimi ni.mkristo na nimeshachangishwa ujenzi mbal mbal za misikiti.kma ww huna cha kuchangia kaa kimya .hiyo mnayoswalia mnajua ilijengwa na nani? Na vyanzo vya mapato ya kuijenga mnaifahami au ni unafiki
Hakuna anayekataa au kukataza watu kuchangishana lakini kuna utaratibu wake. Huwezi kuchangisha sadaka ndani ya Kanisa wakati wa ibada ya kikristo kwenda kujengea nyumba ya ibada ya wasio wakristo.

Sadaka ina utaratibu wake. Sadaka inapotolewa, ni lazima anayetoa awe na kusudi lake kwa Mungu. Ndiyo maana hata harambee za kijamii zinazofanywa na wakristo, hazifanyiki ndani ya Kanisa ambako ni madhabahu ya bwana.

Ndani ya Kanisa, kwa imani ya kikristo, ni nyumba ya Mungu. Ile tebanakuli inaashiria uwepo wa Kristo Mzima katika umbo la mkate na divai. Ndani ya Kanisa kunastahili kufanyika mambo ya ibada tu. Mathalani ingetokea waislam walikuwa msikitini, wamepatwa na ajali ya moto au jengo limewaangukia, kufanya mchango katikati ya ibada ni halali, kwa sababu ni tendo la huruma, na hiyo tumeagizwa na Kristo mwenyewe.

Michango isiyo ya kiibada ina utaratibu wake. Wakristo au waislam au mwingine yeyote, anapokuwa mahali pengine popote anaruhusiwa, na wala siyo tatizo kuchangia chochote. Kwaajili ya arusi watu wanachangishana. Lakini huwezi kusikia kwenye ibada Kanisani , watu wakachamgishwa kununua bia za sgerehe ya arusi.

Unapofanya jambo lolote, zingatia mahali, wakati na tukio.

Kuchangisha kwaajili ya ujenzi wa msikiti si jambo baya, lakini mchango huo hauwezi kufanyika kwenye ibada ya wakristo ambao hawaamini uwepo wa mtume, halafu mchango huo uende kwaajili ya wasioamini umungu wa Kristo. Kutoamini kuwa Kristo ni Masiha, Mwana wa Mungu, Mungu Kamili, Nafsi ya tatu ya Mungu, kiimani ni kumkufuru Roho Mtakatifu.

Mchango huo ulistahili kufanyika kijamii na siyo kiibada.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mpumbavu pekee ndio atahoji kwa ubaya maamuzi ya Rais kuchangisha mchango wa ujenzi wa msikiti kanisani

sio kwamba waslamu au Rais hawana hera za kujenga msikiti ila JPM alitaka kuonesha jinsi watanzania tulivyo wamoja hatuna udini wala ukabila

kwa lugha nyingine ni salaam kwa mabeberu
 
Hakuna anayekataa au kukataza watu kuchangishana lakini kuna utaratibu wake. Huwezi kuchangisha sadaka ndani ya Kanisa wakati wa ibada ya kikristo kwenda kujengea nyumba ya ibada ya wasio wakristo.

Sadaka ina utaratibu wake. Sadaka inapotolewa, ni lazima anayetoa awe na kusudi lake kwa Mungu. Ndiyo maana hata harambee za kijamii zinazofanywa na wakristo, hazifanyiki ndani ya Kanisa ambako ni madhabahu ya bwana.

Ndani ya Kanisa, kwa imani ya kikristo, ni nyumba ya Mungu. Ile tebanakuli inaashiria uwepo wa Kristo Mzima katika umbo la mkate na divai. Ndani ya Kanisa kunastahili kufanyika mambo ya ibada tu. Mathalani ingetokea waislam walikuwa msikitini, wamepatwa na ajali ya moto au jengo limewaangukia, kufanya mchango katikati ya ibada ni halali, kwa sababu ni tendo la huruma, na hiyo tumeagizwa na Kristo mwenyewe.

Michango isiyo ya kiibada ina utaratibu wake. Wakristo au waislam au mwingine yeyote, anapokuwa mahali pengine popote anaruhusiwa, na wala siyo tatizo kuchangia chochote. Kwaajili ya arusi watu wanachangishana. Lakini huwezi kusikia kwenye ibada Kanisani , watu wakachamgishwa kununua bia za sgerehe ya arusi.

Unapofanya jambo lolote, zingatia mahali, wakati na tukio.

Kuchangisha kwaajili ya ujenzi wa msikiti si jambo baya, lakini mchango huo hauwezi kufanyika kwenye ibada ya wakristo ambao hawaamini uwepo wa mtume, halafu mchango huo uende kwaajili ya wasioamini umungu wa Kristo. Kutoamini kuwa Kristo ni Masiha, Mwana wa Mungu, Mungu Kamili, Nafsi ya tatu ya Mungu, kiimani ni kumkufuru Roho Mtakatifu.

Mchango huo ulistahili kufanyika kijamii na siyo kiibada.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umemaliza Mkuu.
 
Naomba kuuliza kwani zile fedha zilizochangwa hazistahili kujengewa msaikiti?

Uwez kumwimarisha mtu ambae unahisi amepotea

Uwez kusema nguruwe ni haramu wakati ndio kwanza unauza vyakula vya kunenepesha Hao ngurue

Waslam wanataka wakristo waende kule coz wanaamini wamepotea na wakristo wanataka Waslam waje coz wanaona wamepotea
 
Mbona wakati kanisa lile linajengwa hakwenda msikitini kuomba waisamu nao wachangie ujenzi wa hilo kanisa?
Hoja si kuomba msaada ..nadhan hoja inafaa kuwa unaenda kusali ikiwa na nia ya kusali ama unaedna kusali ukijiuliza pesa za kujenga zimetoka wapi!!?

Hili suala ukileta kiuhalisia yani kirohoni kabisa halina shida hata punje..maana kitakachohojiwa je kwa kuwa waktristo ndio wamechanga ujenzi..hii haina maana ya kwamba wao watakuja kusalia hapo ...

Wakti mwingine vyema ukafikiri kwa mtazamo was tatu kuliko kujificha kwenye kichaka cha Quran inasemaje ama biblia inasemaje..pale unaoeleka nafsi yako...so kama msikiti utajengwa kwa kufuata masharti ya kiislamu katika ujenzi..haiondoi maana ya kwamba haufai kuswaliwa.
 
Anawashurutisha Wakiristo kufanya ibada zisizo zao!

Wakiristo walikataa Mahakama ya kadhi kwa hoja kuwa kodi zao zisitumike kwenye ibada ya wengine, sasa leo Magufuli anakwenda kanisani kuwachangisha ili ijengwe nyumba ya kuabudia isiyo ya ibada yao!

Kama Magufuli ni Mkiristo mwenye kuwapenda waislamu na ibada yao basi awape mahakama ya kadhi kwanza!
Hahaha Magufuli akiwapa hiyo mahakama ya kadhi nayo mtakataa kwasababu ni mkristo.

Nyie dawa yenu msipewe hata walimu wa madrasa.

Tunawajengea msikiti, hamtaki.

Sasa mkipewa mahakama ya kadhi mtaomba na majengo yenu, mtaomba na polisi wenu, mtaomba na magereza yenu.

Tumeamua tutawajengea misikiti kila kata.
 
Ni mpumbavu pekee ndio atahoji kwa ubaya maamuzi ya Rais kuchangisha mchango wa ujenzi wa msikiti kanisani

sio kwamba waslamu au Rais hawana hera za kujenga msikiti ila JPM alitaka kuonesha jinsi watanzania tulivyo wamoja hatuna udini wala ukabila

kwa lugha nyingine ni salaam kwa mabeberu

Mwambie atupe na Mahakama ya Kadhi
 
Ni mpumbavu pekee ndio atahoji kwa ubaya maamuzi ya Rais kuchangisha mchango wa ujenzi wa msikiti kanisani

sio kwamba waslamu au Rais hawana hera za kujenga msikiti ila JPM alitaka kuonesha jinsi watanzania tulivyo wamoja hatuna udini wala ukabila

kwa lugha nyingine ni salaam kwa mabeberu
Hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi anahitaji kura za watu wa imani zote.
 
Back
Top Bottom