Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Wakati mitandaoni kukiwa na tafsiri nyingine kuhusu hili la kanisa kuchangia ujenzi wa msikiti, mitaani ndio habari njema na wenye Imani Yao wanaona hiyo ndio nzuri imekaa kiupendo na kuondoa dhana ya chuki iliyojengeka miongoni mwa dini hizi

Lakini pia huku mitaani kuna visima vingi vilivyojengwa na waislamu na mpaka vingine vipi jirani na makanisa, watumiaji ni watu wote, vivyohivyo kwa visima vilivyojengwa na Wakristo, tnajinywea Tu

Ni zamu ya Dunia nzima kujifunza Tanzania namna Imani inavyopaswa iwe
 
Ni mpumbavu pekee ndio atahoji kwa ubaya maamuzi ya Rais kuchangisha mchango wa ujenzi wa msikiti kanisani

sio kwamba waslamu au Rais hawana hera za kujenga msikiti ila JPM alitaka kuonesha jinsi watanzania tulivyo wamoja hatuna udini wala ukabila

kwa lugha nyingine ni salaam kwa mabeberu
Umesoma Quran Sura ya 9 aya 17 soma kwanza halafu uchangie.
 
Pu
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
P
Pumzi imekata
Delete ccm Oct 28
 
MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
Unaonekana so muislam umedandia tu hoja ili kukidhi kiu yako ya kisiasa
Uislam inaruhusu kujengewa msikiti na asie muislam au hata kupewa pesa za kujengewa msikiti
Msikiti wameombewa waislam,wewe kinakuuma Nini?
 
Anawashurutisha Wakiristo kufanya ibada zisizo zao!

Wakiristo walikataa Mahakama ya kadhi kwa hoja kuwa kodi zao zisitumike kwenye ibada ya wengine, sasa leo Magufuli anakwenda kanisani kuwachangisha ili ijengwe nyumba ya kuabudia isiyo ya ibada yao!

Kama Magufuli ni Mkiristo mwenye kuwapenda waislamu na ibada yao basi awape mahakama ya kadhi kwanza!

Hapa umeweka kisu kwenye mfupa. Halafu nilishangaa sana anasema anachangisha ili waislamu wawe na msikiti mkubwa, kwani msikiti mkubwa ndio Mungu anasikiliza zaidi sala zao? Huenda alikuwa na nia nzuri, au anasaka kura kupitia nyumba za dini, lakini alifanya jambo sahihi sehemu ambayo sio sahihi. Yaani hata uvae suti nzuri vipi, lakini huwezi kwenda kukimbia nayo marathon maana sio vazi sahihi kwa ajili ya marathon. Halafu kawadhalilisha sana waisilamu kuwa hawawezi kujenga msikiti mkubwa mpaka wajengewe na waisilamu. Yeye alitakiwa aende msikitini akaitishe hiyo harambee yake, sio kuchangusha hela kwa makafiri ili kuwajengea waisilamu msikiti mkubwa, huku akiacha matatizo ya msingi ya waislamu.
 
Na waroma wengi biashara yao Ni kitimoto hii sijui imekaaje au pesa sio Haram
 
Ni mpumbavu pekee ndio atahoji kwa ubaya maamuzi ya Rais kuchangisha mchango wa ujenzi wa msikiti kanisani

sio kwamba waslamu au Rais hawana hera za kujenga msikiti ila JPM alitaka kuonesha jinsi watanzania tulivyo wamoja hatuna udini wala ukabila

kwa lugha nyingine ni salaam kwa mabeberu

Aende msikitini akachangishe hela za kujenga kanisa kama ataeleweka. Kaishiwa mbinu za kusaka kura huyo. Waisilamu wana matatizo ya msingi, sio kichangishiwa hela ya kujengewa msikiti mkubwa huko kanisani kwake. Shehe Ponda juzi katoa waraka, na ulibeba matatizo ya msingi ya waislamu, hakuna popote waisilamu walitaka michango ya kujengewa msikiti na wakristo. Kama ni kura tayari NEC ina idadi ya kupika ya watu 29m+, kwanini alete siasa za kudhalilisha dini nyingine huko kanisani kwake, huku tayari ana kura nyingi za kupika?
 
Ndugu zangu , Amani iwe juu yenu pamekuwepo na madai na majitapo mengi kutoka kwa baadhi ya political laymen tangu jana baada ya baba mwenye nyumba kutembeza bakuli kanisani kuomba fedhwa za kujenga msikiti,

Hapo nina maswali mawili matatu.

Moja, Baba mwenye nyumba alitumwa na masheikh kuwaombea michango kanisani, bila shaka mamlaka za waislamu zitatujulisha.

Pili, Je ni upendo wa baba mwenye nyumba kwa wapangaji wake kutaka kuonesha religious equilibrium katika kipindi hiki cha kutafuta political pasture?, sina hakika sana kama iko hivyo.

Tatu, Ni uumini na uchamungu wa kiwango cha juu cha baba mwenye nyumba?, nadhani hili ni jibu sahihi.

Nne, Ni ipi hukumu ya kisheria katika dini ya uislamu kujenga msikiti kwa fedhwa ambazo yakinani zimetokea kanisani bila wasiwasi wowote?

Hapo maulama watatusaidia

Tano, Je hili halina athari yoyote kisiasa khasa wakati huu wa uchaguzi?

Sita, Ni lini msikt wa mfalme wa Moroko utazinduliwa nao waislamu wachangie kanisa?

Wakati makonda anajenga msikiti pale dar waislamu walimuomba?
Kuna misikiti na makanisa huku watu huchangisha kwa malafiki zao ambao ni waislam na wasio waislam je huwa ni dhambi?
Lengo la Raisi ni kwamba dini zote ziwe pale chamwino ili watu wanao ishi au kufanya kazi maeneo hayo na wageni wapate sehemu yao ya kusali sasa kosa liko wapi?
Je wewe kuchangia huko kunakuuma nini mpaka uanzishe uzi hapa?
Mwisho, kuna wapiga diri na wauza madawa ya kulevya hapa nchini hujenga maisikiti na makanisa kisha kuyakabidhi kwa viongozi na ni pesa haramu, je makanisa hayona misikiti huwa ni haramu?
Nakuachia na wewe ujibu unalojua.
 
Mkuu,

Unaonekana ni mtu wa maana sana. Sina uhakika na hilo. But yeah at least unaonekana ni mtu!

Unajua mimi sijasema kwamba huu mchukiano ni two way traffic, kaa yupo anaesema hivyo aje atoe hoja zake.

Mimi ninachosema historia ya nchi yetu ni kwamba wakristo hususan wakatoliki wamekuwa wakiwachukia waislam (historically) na labda niseme hili ni tatizo la kimfumo zaidi kuliko individuals maana sote tunaishi vizuri kwa nje.

Hoja ikaja kwamba, aliyoyafanya Mheshimiwa rais magufuli ndio yanapingwa hapa na mimi nikafikia kuelezea kwamba hakutokuwa kamwe na mapenzi hayo ambayo yeye Mheshimiwa rais ametaka kuya portray kwa sababu chuki kutoka kwao (wakristo hususan wakatoliki) kwa uislam au waislam ni kubwa zaidi kuliko mapenzi yao.

Hebu imagine tu brother, katika umri wako na pengine kwa elimu yako eti Leo ndio Unamjua Sheikh Suleiman Takadir?? Sikulaumu mkuu ni mfumo ndio uliopelekea hivyo. Kwa hiyo lililofanyika ni geresha tu au danganya toto na wala si kwa mapenzi ya dhati ya wakristo juu ya uislam. Ukweli ni ule aliousema GWAJIMA juu ya miskiti, kwamba ataugeuza kuwa Sunday schools ile ni chuki ya hali ya juu na yale ni machache tu aliyoyasema ambayo kwa chuki ilimvyomjaa alishindwa kuendelea kukaa nayo moyoni.

Allah anatuambia kwamba ubaya wao (makafiri) waudhihirishao dhidi yetu (waislam) ni mdogo mno ukilinganisha na ule waufichao vifuani mwao.

Ukweli ni ule wa waziri lukuvi juu ya kauli anazozitoa kuhusu Zanzibar na mengine mengi mno mno mno mno.

Kwa hiyo ndugu yangu kimfumo, huu upendo kamwe hautokuwepo. Ile kuchangisha pesa ni geresha tu au nyinyi mnaita siasa tu.
Watoe hukumu kwa masheikhe walioko mahabusu kama wana mahaba na uislam ova,
 
..nadhani tunazunguka-zunguka bila kwenda kwenye MSINGI/KIINI cha tatizo.

..mimi nadhani Jpm ni mwanasiasa asiye na hoja na haiba ya uongozi, hivyo amekuwa akitumia makanisa na misikiti kufanya siasa.

..ili Jpm akubalike ni lazima apitie kwenye "uchochoro" wa imani za watu, akipitapita makanisani na misikitini huku akimwaga MAPESA.

..inawezekana kuna kasoro ndogo-ndogo namna ambavyo harambee iliitishwa, lakini msingi na kiini cha yote haya ni Jpm kutumia DINI na FEDHA ktk siasa.

cc tindo, Phillipo Bukililo , Kilatha, Nguruvi3
Mkuu, siku zote wanasiasa wasio na ushawishi wa kisiasa hutumia maeneo mengine kuziba pengo hata kama kufanya hivyo ni hatari. Kumbuka lengo la wanasiasa ni ku survive.

Kuna nyakati wanasiasa hutengeneza matatizo ili waje na solution kama hoja za umahiri wao.

Kinachosababisha haya yote ni reaction inayotoka kwa Waislam.

Kwa muda kumekuwa na some reservations kwamba kuna tatizo katika awamu hii kama utarejea Waraka wa Sheikh Ponda.Majuzi kamati kuu ya CCM imempitisha Gwajima.

Leo mitandaoni kuna clips za Gwajima si moja au mbili ni nyingi zikionyesha chuki ya wazi dhidi ya Uislam

Kamati ilichukua uamuzi wa kisiasa bila kuitazama jamii. Hili ni kosa kubwa !

CCM wanashindwa kuwaangalia Waislam machoni, huwezi kumkubali Gwajima bila kukubali ushawishi wake hasa chuki dhidi ya Waislam

Katika jitihada za kujikosha na 'uchafu' wa Gwajima ambao CCM imeukumbatia ikidhani Waislam hawaoni ndio sasa tunaona haya ya michango n.k.

Kamati kuu ilidhani hili ni la Kawe, kadri muda unavyosonga wanabaini kuwa hoja ya Gwajima imegusa jamii yote ya Waislam, na inathibitisha hoja ya Ponda na hivyo waliokuwa na wasi wasi na Ponda sasa hawana shaka tena!

Gwajima kasema na CCM imemuunga mkono na imemthibitisha
Gwajima naye kasaidia sana kuthibitisha kile Ponda alichokisema.
 
Wale ambao wanaona hakuna tatizo kwa raisi kuendesha mchango kanisani wa kujenga msikiti kwa kigezo cha undugu

Je Waislamu walipotaka Iwepo mahakama ya kadhi nchini mlisemaje?
Si mlisema waazishe wenyewe kwa hela zao wenyewe, na kwamba pesa ya Mkristo(kodi) isiendeshee ibada za waislamu!

Sasa vipi Rais anatumia madhabahu kuchangisha hela za kuendeshea ibada za Waislamu na nyie mnaona sawa?
Kumbe hoja siyo hela za Wakiristo kutumika kwenye ibada ya waislamu bali mnachagua ibada ipi ya kuwachangia na ibada ipi ya kuwakatalia?
Hakuna mapenzi hayo bhana.

Hizo wanazofanya sijui kina Makonda sijui nani sijui Lowassa ni kwa maslahi yao ya kisiasa tu na sio eti kwamba wanataka waislam wapate pa kuabudia.
 
Anawashurutisha Wakiristo kufanya ibada zisizo zao!

Wakiristo walikataa Mahakama ya kadhi kwa hoja kuwa kodi zao zisitumike kwenye ibada ya wengine, sasa leo Magufuli anakwenda kanisani kuwachangisha ili ijengwe nyumba ya kuabudia isiyo ya ibada yao!

Kama Magufuli ni Mkiristo mwenye kuwapenda waislamu na ibada yao basi awape mahakama ya kadhi kwanza!
Hata mimi ningekuwepo pale kanisani wala nisingethubutu kuchanga. Maana ni kuabudu miungu wengine.
 
Mkuu, siku zote wanasiasa wasio na ushawishi wa kisiasa hutumia maeneo mengine kuziba pengo hata kama kufanya hivyo ni hatari. Kumbuka lengo la wanasiasa ni ku survive.

Kuna nyakati wanasiasa hutengeneza matatizo ili waje na solution kama hoja za umahiri wao.

Kinachosababisha haya yote ni reaction inayotoka kwa Waislam.

Kwa muda kumekuwa na some reservations kwamba kuna tatizo katika awamu hii kama utarejea Waraka wa Sheikh Ponda.Majuzi kamati kuu ya CCM imempitisha Gwajima.

Leo mitandaoni kuna clips za Gwajima si moja au mbili ni nyingi zikionyesha chuki ya wazi dhidi ya Uislam

Kamati ilichukua uamuzi wa kisiasa bila kuitazama jamii. Hili ni kosa kubwa !

CCM wanashindwa kuwaangalia Waislam machoni, huwezi kumkubali Gwajima bila kukubali ushawishi wake hasa chuki dhidi ya Waislam

Katika jitihada za kujikosha na 'uchafu' wa Gwajima ambao CCM imeukumbatia ikidhani Waislam hawaoni ndio sasa tunaona haya ya michango n.k.

Kamati kuu ilidhani hili ni la Kawe, kadri muda unavyosonga wanabaini kuwa hoja ya Gwajima imegusa jamii yote ya Waislam, na inathibitisha hoja ya Ponda na hivyo waliokuwa na wasi wasi na Ponda sasa hawana shaka tena!

Gwajima kasema na CCM imemuunga mkono na imemthibitisha
Gwajima naye kasaidia sana kuthibitisha kile Ponda alichokisema.
Na huu ndio ukweli, enzi na enzi.

Toka kipindi cha Mwalim Nyerere na mpaka sasa.

Kwa taifa makini na chama makini kinachohitaji ustawi wa jamii yake, amani na upendo kwa wanachi wake basi Gwajima hakupaswa hata kuruhusiwa kuchukua form ndani ya chama hicho.

Ila kwa vile lengo la CCM ni kumuondoa tu madarakani Halima Mdee basi kwa gharama yoyote ile hata kuhatarisha mshikamano wa wananchi wapo tayari kufanya hivyo.
 
Na huu ndio ukweli, enzi na enzi.

Toka kipindi cha Mwalim Nyerere na mpaka sasa.

Kwa taifa makini na chama makini kinachohitaji ustawi wa jamii yake, amani na upendo kwa wanachi wake basi Gwajima hakupaswa hata kuruhusiwa kuchukua form ndani ya chama hicho.

Ila kwa vile lengo la CCM ni kumuondoa tu madarakani Halima Mdee basi kwa gharama yoyote ile hata kuhatarisha mshikamano wa wananchi wapo tayari kufanya hivyo.
Wakati wa Mwalimu hata waliofuata dini ilikuwa ni 'taboo'' kuizungumzia katika mazingira ya kisiasa.
Sasa hivi tunaambiwa watu wasichanganye dini na siasa, lakini wanasiasa ni haki kuchanganya na dini.

Kiti kimoja cha ubunge wa Kawe hakina sababu zozote zile za kuweka amani ya nchi katika mstari.
Hili ni kosa kubwa sana na sijui huko ndani ya CCM hakuna mwenye jicho la kuona na uthubutu wa kukemea

Kinachotokea sasa hivi, Wagombea wote wa CCM bila kujali imani zao, kila wanaposimama mbele ya jamii wanasoma nyuso za wananchi hasa Waislam zikiwa na swali moja '' Haya ya Gwajima mumeyakubali''?

CCM hawana jibu, hawawezi kumkubali Gwajima na kukataa ujumbe wake.
Kauli zimetoka kwenye kinywa cha Gwajima! Zipo mitandaoni zinasomeka, ni chuki tu iliyothibitishwa na CCM

Kibaya zaidi CCM imefungua ''floodgate'' Utakmakamata vipi Sheikh Ponda kwa uchochezi halafu umzawadie Gwajima kwa Ubunge na jamii ikuelewe!!!

Kwa maneno mengine Sheikh Ponda amepata 'natural immunity'' Atasema chochote
Ukimkamata Sheikh Ponda utaulizwa, vipi Ponda enede Ukonga , Gwajima aende Dodoma?
Kuna tatizo kubwa sana sijui kwanini CCM hawalioni!

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Ndugu zangu , Amani iwe juu yenu pamekuwepo na madai na majitapo mengi kutoka kwa baadhi ya political laymen tangu jana baada ya baba mwenye nyumba kutembeza bakuli kanisani kuomba fedhwa za kujenga msikiti,

Hapo nina maswali mawili matatu.

Moja, Baba mwenye nyumba alitumwa na masheikh kuwaombea michango kanisani, bila shaka mamlaka za waislamu zitatujulisha.

Pili, Je ni upendo wa baba mwenye nyumba kwa wapangaji wake kutaka kuonesha religious equilibrium katika kipindi hiki cha kutafuta political pasture?, sina hakika sana kama iko hivyo.

Tatu, Ni uumini na uchamungu wa kiwango cha juu cha baba mwenye nyumba?, nadhani hili ni jibu sahihi.

Nne, Ni ipi hukumu ya kisheria katika dini ya uislamu kujenga msikiti kwa fedhwa ambazo yakinani zimetokea kanisani bila wasiwasi wowote?

Hapo maulama watatusaidia

Tano, Je hili halina athari yoyote kisiasa khasa wakati huu wa uchaguzi?

Sita, Ni lini msikt wa mfalme wa Moroko utazinduliwa nao waislamu wachangie kanisa?
Wakati wa ufunguzi wa kanisa huko miaka ya nyuma kijijini Butiama Hayati Baba wa taifa Mwalimu Nyerere alitangaza rasmi kuwa angependelea kuona pale kijijini Butiama panajengwa Msikiti mkubwa. Kwa maombi yake kwa kiongozi wa Libya hayati Ghaddafy fedha za kujenga msikiti huo ulipatikana na msikiti huo ulijengwa kwa usimamizi wa ofisi ya Rais huyo mstafuu. Leo kwa mheshimiwa Rais Magufuli kuchangisha fedha ya kujenga msikiti pale sio kosa.
Mwache kupotosha vitu.
 
Back
Top Bottom