Uchaguzi 2020 Rais Magufuli azungumzia wapinzani wanaohamia CCM na kupewa kipaumbele cha uongozi na kugombea

Uchaguzi 2020 Rais Magufuli azungumzia wapinzani wanaohamia CCM na kupewa kipaumbele cha uongozi na kugombea

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731


Rais Magufuli akijibu swali la Sojo, MNEC kutoka Songwe aliyesema kwamba ametumwa na wanasongwe kuwasemea kuwa wanasononeka pale ambapo wapinzani wanapohamia CCM na kupewa kipaumbele cha uongozi na kuwaacha wanachama ambao walikipigania chama kufa na kupona 2010-2015, wanavunjika moyo wanapoona wageni wanapita bila mbadala.Sojo ameyataja majimbo ya Momba na Tunduma.

Pia soma > Rais Magufuli: Cecil Mwambe moyo wake uko CCM, Chama kilifanya makosa makubwa kumfanyia figisu 2015


Rais Magufuli amesema hilo lilipaswa kuzungumziwa kwenye kamati ya vikao vya CCM Wilaya au Mkoa kwamba wanaokuja kule huwahitaji. Lakini chama hiki ni cha watu, kina misingi yake, kinameza watu wote. Suala hilo lizungumziwe kwenye kamati za wilaya na mikoa na mlitafutie ufumbuzi.

Rais ameongeza kuwa CCM ina watu wengi ambao walikuwa vyama vingine kama Makongoro Nyerere na Mzee Wassira ambao walikuwa NCCR Mageuzi lakini sasa hivi ni CCM damu damu. Amewataka wanaccm kuwa na mioyo ya kuvumiliana ya kumtanguliza Mungu.

Amesema labda wana wasiwasi huyu aliyekuja huenda akawashinda na ndiyo maana amekuwa aliwashinda kila mara, otherwise mngekuwa mnamshinda, sasa kwa sababu anawatandika na mlikuwa mmejiandaa na akipigiwa kura za maoni atachaguliwa na wananchi.

Rais Magufuli ameendelea kusema kuwa Tatizo moja la siasa zetu tunajiwekea vizingiti kwamba akija huyu atashinda lakini mkiachiwa ninyi hamshindi. Nafikiri meseji umenipata.

Lakini Chama hiki kinapokea watu wote ilimradi wanazingatia masharti ya chama. Sasa mkiingia kwenye grupu zenu za kuanza kubishana mbona amerudishwa huyu! Amerudishwa kwa misingi kwamba mlimzuia njia akapitia dirishani, amerudi sasa apitie mlangoni mnataka tena mumzuie!! Muwe na uvumilivu. Ningependa huyo aliyeingia aendelee kushinda ili siku moja aingie kuwa mjumbe wa NEC.


Kwani mwanamke au mme wako akikosea, siku nyingine akaja kukuomba msamaha kwani utakataa? Siyo ajabu akaja na mapenzi mazuri mazuri kuliko ya zamani amejifunza huko mbinu nyingi na mbadala, Sasa unakataa uhondo huo?. Rais amemaliza kwa kusema CCM oyeee
 
Ndani ya chama kuna watu wenye ubinafsi na fitna. Jamaa waliamua kuleta mazoea ya kutengeneza zengwe na fitna!

Mwenyekiti ametoa jibu ambalo ni fundisho kwa wengi wenye njama za kutengeneza mizengwe kwa wagombea katika ngazi za nafasi mbalimbali.
 
View attachment 1502731
Nashauri Pole Pole azungumze Ni kwa Sheria gani, vinginevyo awajibike
Kwani ni sheria gani ya chama imeruhusu wagombea uraisi wasimpinge Dr. Magufuli? Kwa nini hamkuwapa fomu za uraisi mwaka huu? Huenda CCM mna taratibu nyingi (nje ya katiba na sheria za chama) ambazo hazijaandikwa lakini zinatumika . Fuatilia
 
Inamaana hiyo ni hatua ya awali, kitakachofuata ni kuhakikisha mpinzani hapiti.

Ingekua sio hivyo wangewaacha hao wagombea wapambane na wenzao kwa uwezo wao.
 
Kama ni kweli basi hii ni taarifa njema kwa Wapinzani wao. Mara nyingi Ccm imekuwa ikipoteza Majimbo mengi hasa yale ya Mjini kutokana na aina hii ya migawanyiko baina yao.
 
Safi sana. Hili litawafanya wana ccm wanajigamba kuwa kuna demokrasia huko, kuwa chama ni cha mwenyekiti na anauwezo wa kufanya analolitaka yeye na siyo wanayo yataka wao (Wanachama)

Waache tu waendelee kungangania huko, rais/Mwenyekiti mwenyewe hawataki kabisa, na ndiyo maana wengi waliohamiaccm toka upinzani waliewa nafazi serikalini.
 
Back
Top Bottom