Tripo9
JF-Expert Member
- Sep 9, 2009
- 4,357
- 3,550
Hizi quotes zingewekwa kwa ki English maana ndio lugha inayoeleweka vizuriMuongo sana huyu mzee halafu msahaulifu.View attachment 1609479View attachment 1609480
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hizi quotes zingewekwa kwa ki English maana ndio lugha inayoeleweka vizuriMuongo sana huyu mzee halafu msahaulifu.View attachment 1609479View attachment 1609480
Vipi nyomi hapo Arusha!! Mnaona aibu eeh!!?..bora angeendelea kukaa garage akikarabatiwa.
..kwanini anasema UONGO wa waziwazi namna hii?
Vipi nyomi hapo Arusha!! Mnaona aibu eeh!!?
Mwambie Lema.atafite kazi nyingine ubunge asahau!Kama Mrisho Gambo atanyimwa kura na watu wa Arusha anapaswa kumlaumu Magufuli.
Kama kuna mtu anadhani Magufuli amemfanyia kampeni Gambo ukweli ni kwamba amemuharibia na wananchi wataamini hawa wote wawili ni waongo na matapeli watupu.
Lema anakwenda kuwamaliza na clip za nyuma halafu atawawekea hii ya leo, kura zitakapopigwa mtakumbuka maandishi yangu.
Huyu mzee sijui ana matatizo gani huwa sielewi kabisa.
Bado siku 5 tu! Tuone nani mkweli..aibu kwa niaba ya CCM.
..Bwana mkubwa kusema UONGO wa kitoto mbele ya nyomi kubwa namna hiyo ni aibu.
Kwa upuuzi ulioandika unatikiwa ufungwe jiwe kichwani alafu uzamishwe baharini.Kwa hulka yake, hakupaswa kuwa rais. Na kwa bahati mbaya hakuwahi kuwa na ndoto ya urais hadi pale Jakaya alipolikoroga na hivyo huyu akasukumizwa. Kwa hivyo aliingia kwa nafasi hiyo bila kuwa hata na chembe ya vision. Ndio maana tumeshuhudia vituko lakini vituko ambavyo vinamtesa na kumyanyasa mwananchi wa kawaida. Njiani amelewa pombe ya madaraka kufikia kuona pesa za serikali ni zake na waTz ni vijakazi wake anaweza akawafanyia cho chote na wasimfanye kitu, asubuhi anaweza kutoa kauli hii, jioni akasema hajaisema. Hii yote ni kuamini waTz, yaani vijakazi wake, ni wajinga na mwenye akili na busara ni yeye peke yake. Ulevi wa madaraka. Jakaya na vizazi wako mlaaniwe milele!
Rais Magufuli amesema kuna watu wanadai anamchukia Mrisho Gambo na kwamba alimfukuza kazi ya mkuu wa mkoa wa Arusha lakini hiyo siyo kweli.
Gambo alinifata akaniomba agombee ubunge ili aiokoe Arusha ambayo inaonekana kukwama, amesema Dr Magufuli.
Ningekuwa namchukia ningempitisha kugombea ubunge? ameuliza.
Nileteeni Mrisho Gambo kwa ajili ya maendeleo ya Arusha amesisitiza Dkt. Magufuli.
Maendeleo hayana vyama!
Bado siku 5 tu! Tuone nani mkweli
Mzee atakuwa ni mchawi Tu sio bureMzee kameza maneno yake.
Sasa Rais amesema hakumfukuza na yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuajiri na kutengua. Sasa wewe unabisha nini sasa?..unahitaji siku 5 kujua kama Magufuli alimfukuza kazi Mrisho Gambo?
Mliiona barua ya kufukuzwa kazi ya Gambo?..unahitaji siku 5 kujua kama Magufuli alimfukuza kazi Mrisho Gambo?
Hawa vijana wa Chadema ni watu wa ajabu sana!Sasa Rais amesema hakumfukuza na yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuajiri na kutengua. Sasa wewe unabisha nini sasa?
Mliiona barua ya kufukuzwa kazi ya Gambo?
Kujitokeza kwenye tv ni kwa mujibu wa sheria?..wewe una barua inayothibitisha kwamba hakufukuzwa?
..Raisi si alijitokeza kwenye TV na kutoa lawama kwa Mrisho Gambo, mpaka akamtuhumu kwa mambo ya udini?
Exquisite..1. Elimu iongezeke, hususan elimu ya uraia kwa watu wengi zaidi. Mtaji wa CCM ni ujinga wa Watanzania wengi.
2.Watu waache utamaduni wa "hewala, hewala". Hata ukiwa na elimu, ukiwa mwoga hutaweza kuuondoa mfumo dhalimu.
3.Wanaotaka mabadiliko wamaanishe hilo kwa kweli. Wao wenyewe waanze kuishi kwa utamaduni wa kidemokrasia na kupenda mawazo mbadala. Siyo mtu analalamikia udhalimu wa CCM isivyo na demokrasia, wakati nyumbani yeye baba akishasema jambo halina mjadala. Au chama cha upinzani anakiendesha kama familia yake binafsi.
4. Vyama vya upinzani viache kuwa vyama vya msimu wa uchaguzi.Nimeshangaa sana upinzani umekubali kunyamazishwa na Magufuli miaka yote hii.Hususan katazo la kufanya mikutano ya hadhara ambalo liko kinyume na katiba. Kama wapinzani wameshindwa kupinga hili, nawaona bado sana hawajajizatiti kuiondoa CCM.
5. Tuandae watoto na vijana wanaokua sasa kukua katika utamaduni wa kuukata ujinga bila tahayari.Kwa sasa naona kama na wao tayari wanaondolewa kutoka kwenye "kizazi cha kuhoji" na kupelekwa kwenye "kizazi cha hewala hewala".
6. Vyama vya upinzani vijizatiti zaidi kimataifa kuchukua uzoefu sehemu nyingine na kutengeneza urafiki na network kubwa za kimataifa zitakazosaidia kuleta maendeleo chanya bila kuleta hofu ya siasa zetu kutawaliwa na watu wa nje. Kuna mitandao inayojulikana na kuheshimika kama vile Amnesty International, The Committee To Protect Journalists, Human Rights Watch etc inafanya kazi kubwa na nzuri kumulika serikali dhalimu, lakini sioni kama wapinzani wetu wanazitumia hizi taasisi vizuri.
7. Vyama vya upinzani bado sana havijatumia mitandao ya kijamii kujitangaza. Presence ya chama kama CHADEMA Youtube, Twitter, au hata JF ni ndogo sana kulinganisha na ukubwa wa chama. Mitandao inasaidia sana kupasha habari watu wengi kwa wakati mfupi sana. Upinzani bado unacheza kwenye hili.
8.Vyama vya upinzani vinatakiwa kuonesha mifano ya shughuli za kiuchumi. Sio kupiga siasa za midomo tu.Yako wapi mashamba ya vyama vya upinzani? Yako wapi maduka yao? Iko wapi miradi ya kusaidia ajira kwa vijana? Wapinzani wakianzisha vitu hivi, humo humo kwenye miradi kuna nafasi ya kuongeza wanachama na kutanua wigo wa kueneza sera kwa wananchi, tena kwa kuonesha mifano, si maneno tu.Waswahili wanasema "Maneno matupu hayavunji mfupa". Waingereza wanasema "Action speaks louder than words".
9. Wapinzani wanatakiwa kuwashawishi watumishi wa umma, hususan vyombo vya dola, kwamba wao hawana ugomvi nao, wanataka kuitoa serikali ya CCM tu. Vyombo vya dola vinatakiwa kufanya kazi pamoja na wapinzani, si kudhibiti wapinzani. Vikidhibiti wapinzani ushahidi uchukuliwe na washitakiwe.
10.Vuyama vya upinzani vijizatiti zaidi kupanga mkakati wa kisheria kuhakikisha haviibiwi kura. Hii ni pamoja na mabadiliko ya katiba, kuongeza teknolojia, kuongeza waangalizi wanaoheshimika kutoka nje, na kuongeza kujitambua miongoni mwa wananchi.
Kuna mengi sana, ila kwa leo niishie hapa.
Vichaa husahau.Muongo sana huyu mzee halafu msahaulifu.View attachment 1609479View attachment 1609480