Zero Hours
JF-Expert Member
- Apr 1, 2011
- 12,942
- 18,669
Huyu mzee ni kiongozi mbovu, wa hovyo. Kwa alichoongea leo ni kwamba ana tatizo kubwa kuliko tunavyomdhania. Mungu tusaidie
Chato anafanya nini? Tulimchagua akae ikulu, huko anafanya nini?Kuna athari kubwa sana kwa mtu akijijengea fikira ya kupinga kila kitu,hebu fikiria kidogo makao makuu ya umoja wa mataifa yako Marekani,unataka kuniambia katibu mkuu wa umoja wa mataifa akitaka kutoa hotuba hadi aende Marekani,hawezi kuwa Tanzania na bado akahutubia mataifa yote?
Chato ni Tanzania,tupunguzeni manunguniko yasiyo tija
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe kama unaona aliyoongea ni sahihi basi akili yako ina matatizo makubwa sana!Wewe ndio unatatizo,bahati mzuri tumepata rais isiyependa blah blah,nyeupe iitwe nyeupe kadhalika nyekundu
Sasa kama mlizoea siasa kila kitu kwa jpm mtaugua presha ,hotuba ilikuwa mzuri na nimeipenda sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Hongera sana mheshimiwa Rais kwa kutengeneza viumbe kama huyu mtoa mada ambao ni adimu sana kuwapata katika ulimwengu wa sasa. Ni aina fulani ya binadamu ambayo ilishatoweka siku nyingi na kuipata kwa urahisi labda umtumie DR LeakeySALAAM ZA PONGEZI KWA MH RAIS MAGUFULI.
Na Elius Ndabila
0768239284
Leo Mh Rais amelihutubia Taifa alipokuwa akizungumza na wakuu wa vyombo vya usalama nchi. Hotuba ya Mh Rais imegusa mambo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa, kubwa likiwa ugonjwa wa Corona ambao unaiandama dunia kwa sasa. Nilipata wasaa wa kusikiliza vizuri sana hotuba ya Mh Rais.
Ninaomba nitumie wasaa huu kumpongeza Mh Rais kwa kuzungumza na Watanzania na kutoa ushauri wake kama amiri jeshi mkuu. Hotuba ya Mh Rais ni ya kutia matumaini na kuwapa ali kubwa Watanzania. Ninaimani kubwa Kama ushauri wa Mh Rais utazingatiwa ugonjwa wa corona hautakuwa tishio Bali utakuwa sawa na magonjwa mengine.
Nimpongeze Mh Rais kwa kuzumzia pia suala la kinga na tiba. Mh Rais amesema kwa kuwa bado hakuna dawa za kutibu corona ni vema WATANZANIA tukajiongeza kwa kutumia dawa za asili ikiwepo kujivukiza. Waafrika tumekuwa na tabia za kupuuza dawa za asili na kuamini dawa za magharibi. Wakati mwingine hata dini zetu zimekataza kutumia dawa za asili na kutushauri kutumia dawa za hospital. Tumedanganywa kwa kuwa watu hawajui hata hizo dawa za hospital ni dawa za kienyeji zilizoboreshwa zaidi. Ni vema tuwape furusa Wataalamu wetu wa asili kuonyesha juhudi zao ktk hili ambalo limewashinda wazungu. Hotuba ya Mh Rais inawapa nguvu madakitari wa asili kuonyesha vipaji vyao. Ugonjwa huu ni vita ya KIUCHUMI, hata dawa wakipata wazungu si rahisi kutufikia huku kwa kuwa maombi Yao ni afrika kufa ili wapate fursa ya kuja kuchukua Uchumi wetu.
Mh Rais ninampongeza pia kwa kutolea ufafanuzi suala la mask. Hivi tunategemea kama virus vya corona ni watu walitengeneza wanaweza kututengenezea maski za kuzuia? Ninaamini ile tathimini tuliyoambiwa Afrika kufikia mwezi wa nne itakuwa na wagonjwa wengi hupenda walikuwa wamepiga ni idadi ya mask zilizoingia Africa ambazo zinaweza kuwa na virus. Walitegemea kadiri tutakavyotumia maski ndivyo tutakavyoambukizwa. Mh Rais amesema kuna tetesi kuwa baadhi ya nchi hizi barakoa zimeonyesha kuwa na virus. Mh Rais amewapongeza wale wote wanaotumia mask za vitambaa vilivyotengenezwa hapa nchini. Hongera sana Mh Rais kwa kushauri viwanda vya hapa nchini vijiongeze na kuanza kutengeneza barakoa n.k
Mh Rais amesema uoga ni hatari kuliko ugonjwa wenyewe. Ameshauri tuchukue tahadhari zinazotolewa na Wataalamu lakini tusitishike. Rais ameonya pia wanaosambaza habari za uzushi kuwa watafutwe na washughulikiwe. Kwa hili ninampongeza mh Rais kwani kila mtu alikuwa anaandika anachokitaka.
Mwisho Rais amekemea vikali kufanya upuliziaji wa dawa kwenye miji na magari . Amesema hii haisaidii. Ameenda mbali kwa kusema hawezi kutangaza kuiweka lockdown DSM. Binafsi ninampongeza Mh Rais kwa kuwa amesaidia kuweka sawa suala la ubaguzi lililokuwa limeanza kujitokeza kwani ni wiki iliyopita tu moja ya wateule wake alionekana mbele ya camera akisema watu wa Dar Es salama muwakimbie na msiwakaribishe.
Mwisho ninampongeza mh Rais kwa kuonyesha msimamo wa kijasiri. Tutoke nje tukafanye kazi. Kukaa ndani ni hatari kuliko corona. Hivi Corona isipoisha wale wenzetu wa Kenya wataendelea kukaa ndani? Tupambane na corona tukiwa kazi ni na si kujifungia ndani. Ninaamini kwa kauli ya Mh Rais sasa vyuo na shule si MUDA mrefu masomo yataendelea.
#corona inaua chukua tahadhari
Kijijini Lali Ibaba.
Duh uchunguzi tena ??By G Malisa:
"Hakuna virusi wanaokufa kwa fumigation. Kilichofanyika Dar es Salaam kupuliza dawa yenye kemikali ni upuuzi. Wanaokufa kwenye fumigation ni mende na si virusi ikiwemo virusi vya Corona. Suala la kupuliza dawa ni upumbavu mtupu. Hakuna kirusi cha Corona kinachoweza kufa kwa Chlorine. Naomba IGP na Vyombo ulinzi mkachunguze walikuwa na lengo gani na nani alitoa hizo dawa” Rais JPM, 22/04/2020, Chato, Geita.
Nini maoni yako??
Ama kweli kukopa sherehe, kulipa matanga.Raisi wa Tanzania JPM amesema Tanzania inalipa bilioni 700 katika taasis mbalimbali duniani zilizoikopesha nchi yetu kila mwezi ikiwemo benki ya dunia inayolipwa bilioni 200 kila mwezi. Hii ina maana kwa mwaka hulipwa zaidi ya trillion 8.4 fedha ambazo ni zaidi ya mishahara yote wanayolipwa watumishi wa umma.
Kwa hili nani anabisha kuwa Tanzania siyo koloni la mabeberu? Tuna safari ndefu ndugu Watanzania.
Sent using Jamii Forums mobile app
Unachekesha...yaani nitumie madakika kadhaa kumsikiliza Magufuli?! That will never happen!!Bado unategemea summary zinazofanywa na some members wa JF? Hotuba ipo hapo, huu uvivu mtaacha lini?
Atata wakitukanwa eti WANYONGE,wanashangilia!Ukitaka kuongoza watu kama mfalime hakikisha wanakuwa masikini. Masikini ni rahisi sana kuwatawala. Sababu masikini anatabia ya kujipendekeza, na mnafiki.
Sent using Jamii Forums mobile app
Rais Magufuli yuko sahihi kwa 100%By G Malisa:
"Hakuna virusi wanaokufa kwa fumigation. Kilichofanyika Dar es Salaam kupuliza dawa yenye kemikali ni upuuzi. Wanaokufa kwenye fumigation ni mende na si virusi ikiwemo virusi vya Corona. Suala la kupuliza dawa ni upumbavu mtupu. Hakuna kirusi cha Corona kinachoweza kufa kwa Chlorine. Naomba IGP na Vyombo ulinzi mkachunguze walikuwa na lengo gani na nani alitoa hizo dawa” Rais JPM, 22/04/2020, Chato, Geita.
Nini maoni yako??
Mkuu Marekani ni kubwa, Ina majimbo 52 na kila Jimbo linautawala wake, sema ni wamarekani wa Jimbo gani wameandamana?Sijakuambia kuwa iko USA yote hata hiyo NY mbona imeendelea kwa muda mrefu sana unataka kuniambia walikuwa wameambukizwa wote?. Kwa taarifa yako tangu juzi wamarekani hawataki tena lockdown wanaandamana mitaani. Bado hatujapata mwarobani wa kumaliza tatizo hili sana sana ni hali ya hewa na immune ya MTU husika. Utaona next month maambukizi US yatapungua kwa sababu ya mabadiriko ya hali ya hewa toka baridi kwenye kwenye joto. Hapa TZ tunatoka joto kwenda baridi hivyo maambukizi yanaweza ongezeka ingawaje sisi immune yetu iko juu kidogo ukilinganisha na watu weupe hivyo inaweza saidia sana.
Hata mchungaji Msigwa alipuliziwa!kinachositisha hata PM alipulizwa
Usikalili kijana,rais ni higher authority anaweza endesha shughuri zake akiwa popote pale,rais ndio Ikulu ,Ikulu sio jengo...Chato ni kijijini kwa Magufuli.
..JK hakuwa kuzungumza toka Msoga.
..Mkapa hakuzungumza toka Lupaso.
..Mwinyi hakuzungumza toka Zanzibar au Mkuranga.
..Mwalimu Nyerere hakuwahi kuzungumza toka Butiama.
..Raisi anapaswa kuendesha shughuli zake toka IKULU, na siyo toka ktk nyumba yake binafsi. Serikali siyo KAMPUNI binafsi ya Raisi.