Rais Magufuli kuondoa sherehe za Uhuru ili fedha zikajenge hospitali Dodoma si jambo la sifa, ni kuonesha Serikali haina mipango hususan ya maendeleo

Rais Magufuli kuondoa sherehe za Uhuru ili fedha zikajenge hospitali Dodoma si jambo la sifa, ni kuonesha Serikali haina mipango hususan ya maendeleo

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kwa mtu mwenye akili za chini, atamsifia Rais Magufuli kwa kutangaza kwamba mwaka huu hatutakuwa na sherehe za uhuru ili kuokoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Dodoma.

Kwa mtu mwenye akili ya kufikiria, atajiuliza, hivi inakuwaje tunakuwa hatuna mipango hususan inayotia ndani kutengwa kwa fedha kwa ajii ya ujenzi wa miundo mbinu muhimu kama Hospitali Dodoma?

Naingia sana wasiwasi, kwamba inafikia mahali mambo muhimu kwa ajili ya miundo mbinu na miradi ya nchini hayapangwi kwa kufuata uratatibu maalum, bali inakuwa ni uamuzi kutokana na hisia za Rais Magufuli.

Kuamua kujenga barabara ndefu ya kiwango cha lami kwa ghafla na kumpigia simu Mkurugenzi wa TANROAD, au kuamua ghafla kwamba fedha za uhuru ndio zikajenge Hospitali, ni wonyesho dhahiri wa udhaifu mkubwa sana katika uongozi wa Magufuli katika kuwa na mipango hususa ya miradi ya maendeleo nchini. Magufuli asifikiri hiyo inamfanya kuwa raisi bora au mzalendo. Ni udhaifu katika uongozi.

Labda tungemuelewa Magufuli ikiwa angesema fedha za sherehe za Uhuru zinaenda kusaidia emergency fulani, kama mafuriko, kipindupindu kimezuka mahali, nk.

Lakini kupeleka fedha za sherehe kwenye kujenga Hospitali, kitu ambacho kinapaswa kupangwa na kutengewa fedha toka mapema, ni udhaifu mkubwa katika kupanga. Kwa namna hii kuna siku tutauza Ikulu ili tumalizie SGR.

Hatuwezi kufanikiwa kufanya mambo haya kwa kutegemea Rais Magufuli siku hiyo kawaza nini kichwani, au kasukumwa na nini kabla hajachukua simu na kutoa agizo mradi fulani mkubwa nchini utekelezwe fedha atajua kwa kuzipata kwa kuwa yeye ndio raisi. Huko ni kuendesha nchi kama duka la baniani. Hayo ni mambo ya kichifu, siyo nchi iliyo Jamhuri.
 
Tofauti kubwa kati ya Tanzania na North Korea ni kuwa North Korea hakuna nyumba za matope na nyasi, serikali imejenga nyumba (flats) kwa mahitaji ya raia wote wasio na uwezo wa kujenga au kununua. Huduma zao za kijamii ni bora zaidi.
 
Hivi hawa watoto wanaokua sasa hivi wajifunze nini juu ya Sherehe za Uhuru?

Ikiwa Uhuru hawakuuona na Sherehe zake wasizione?

Nchi inayoghairi Sherehe za kitaifa kwa Mujibu wa Katiba ni Nchi mfu.
Sherehe za Uhuru zinamaliza hela tu. Hongera Rais Magufuli kwa kuliona hilo. Hii nchi imepigwa sana enzi za Kikwete kupitia visherehe vya ajabuajabu.
 
Dodoma panahitajika kujengwa hospitali ya Taifa kubwa na si hii ya Muhimbili haina idara nyingi kama ya mifupa.
 
Sherehe za Uhuru zinamaliza hela tu. Hongera Rais Magufuli kwa kuliona hilo. Hii nchi imepigwa sana enzi za Kikwete kupitia visherehe vya ajabuajabu.
Nini sasa umeandika? Au bado uko kwenye kampeni? Hii ni sawa na kusema somo la History lifutwe mashuleni kwani tunawapotezea wanafunzi muda.

Wakati mwingine muwe mnfikiri kabla ya kuandika ulichokusudia.
 
Mwaka kesho bora awaambie mapema kabisa wakati wanapanga budget wasipoteze muda wao kuplan hela kwenye sherehe ya aina yoyote na pesa hizo zipangiwe matumizi mbadala in advance. Hatuwezi kuendelea kuoperate kiimla namna hii
 
Kwani ujenzi wa hiyo hospitali pesa zake hazikuwepo kwenye bajeti?

Na kama pasingekuwepo na sherehe za uhuru hizo pesa za kupeleka huko kwenye ujenzi wangezitoa wapi?

Ina maana bajeti ya ujenzi wa hiyo hospitali iliyotengwa mwanzo ilikuwa haitoshi halafu wakafanya siri.

Hii tabia ikomeshwe, taifa linaweza kuwa linaibiwa kwa mtindo huu halafu watu wanashangilia bila kujua.

Kwa sababu mtu anaefanya haya ameshaonesha hafuati sheria za nchi, anajiamulia anavyotaka yeye na hakuna wakumuuliza, anaweza kuchomoa pesa za serikali akafanyia mambo yake binafsi huku akijiita mzalendo.
 
Sherehe za Uhuru zinamaliza hela tu. Hongera Rais Magufuli kwa kuliona hilo. Hii nchi imepigwa sana enzi za Kikwete kupitia visherehe vya ajabuajabu.
Umeelewa uzi lakini?
Shida sio sherehe kuahirishwa shida ni mipango ya kujenga hospital ilikuwa hakuna mpk isubiri fedha za emergence zilizotengwa kwa ajiri ya sherehe za uhuru.?
 
Huyu vipi!? Ndio wale wale wanaosema wanataka maendeleo ya watu siyo vitu! Hivi ni kipi kitendo cha maendeleo - watu kutumia Tshs. 834,742,000/= kwa ajili ya sherehe za uhuru za siku moja au kutumia hizo pesa kujenga miundombinu ya maendeleo kama hiyo hospitalini? Jamani mbona mmevurugikiwa sana hasa baada ya kupigwa kwenye GE ya juzi kiasi hata hamjui nini ni maendeleo na nini ni STAREHE!?
 
Umeelewa uzi lakini?
Shida sio sherehe kuahirishwa shida ni mipango ya kujenga hospital ilikuwa hakuna mpk isubiri fedha za emergence zilizotengwa kwa ajiri ya sherehe za uhuru.?
Yaani walitenga fedha za kutosha za sherehe za uhuru wakaacha kutenga fedha za kutosha za ujenzi wa hospitali Dodoma hadi Rais aje kuamuru fedha za uhuru zikajenge hospitali; ajabu sana hii!

Halafu kama ni uhitaji wa mahospitali na huduma nyingine za kijamii mahitaji ni mengi; ni bora sasa kama kinachokausha hazina ya taifa ni sherehe za uhuru imefika wakati sasa sherehe hizo zifutwe kabisa ili kupata fedha za kujenga na kuboresha huduma zote za jamii.
 
Kwani ujenzi wa hiyo hospitali pesa zake hazikuwepo kwenye bajeti?

Na kama pasingekuwepo na sherehe za uhuru hizo pesa za kupeleka huko kwenye ujenzi wangezitoa wapi?

Ina maana bajeti ya ujenzi wa hiyo hospitali iliyotengwa mwanzo ilikuwa haitoshi halafu wakafanya siri.
Basi siku hizi Serikali hii ikifanya kitu cha maana namna gani lazima mtauliza - kilikuwa kwenye bajeti au kimepitishwa na Bunge na maswali mengine ya hovyo hovyo kama hayo! Kama una chanzo cha ziada na ukikitumia kwa maendeleo, kuna ubaya gani!?

Hivi ni lazima kiende Bungeni na kupangiwa bajeti, by the way budget nini, kama siyo dira tu ya kukuonyeshA wapi pa kupata pesa na namna ya kuzitumia hizo pesa!?

Kama umezipata kutoka kwenye makanikia au Barrick au Buzwagi, matumizi yoyote, as long as ni kwa maendeleo, BASI NI HALALI!
 
Sio kila mwenye madaraka anafaa kuwa kiongozi!
 
Sio kila mwenye madaraka anafaa kuwa kiongozi!
Kiongozi yoyote lazima awe na MADARAKA NA MAMLAKA! Hivyo viwili vinatoka kwa MUNGU na hunavyo, basi huwezi kuwa kiongozi. Mfano mzuri ni Lissu hakuwa na vyote viwili, yaani hakupewa na Mungu bali alikuwa anataka kuvilazimisha kupitia rhetorics na noise huko majukwaani na "nyomi" bandia alizoona zikamuaminisha kuwa anaweza kuwa kiongozi - subutu au thubutu!
 
Kiongozi yoyote lazima awe na MADARAKA NA MAMLAKA! Hivyo viwili vinatoka kwa MUNGU na hunavyo, basi huwezi kuwa kiongozi. Mfano mzuri ni Lissu hakuwa na vyote viwili, yaani hakupewa na Mungu bali alikuwa anataka kuvilazimisha kupitia rhetorics na noise huko majukwaani na "nyomi" bandia alizoona zikamuaminisha kuwa anaweza kuwa kiongozi - subutu au thubutu!
Soma uelewe usisome kujibu!
 
Mleta maada na wenzako wa kupinga kila kitu. Saa nyingine mpunguze ujuaji. Umeanza kwa kuita akili ndogo wale watakao unga mkono uamuzi huu. Wahenga walipatia kusema "werevu mwingi mbele kiza".

Kuna kitu kinaitwa intuition. Kiongozi mzuri pamoja na kufuata taratibu zilizopo anapaswa pia kuwa na utashi wake binafsi umwongoze kuchukua hatua za hapa na pale hata ikiwa hakuagizwa kufanya hivyo.

Uamuzi wa kujenga hospitali hiyo ulikuwa utashi binafsi. Kuna wale Bharti Airtel nao waliunga mkono kwa kuchangia huo ujenzi. Sasa rais kuamua pia kufuta hizo sherehe ili kupata pesa za kununulia vifaa tiba hizo ni akili zake binafsi ambazo kupinga lazima uwe na kawendawazimu flani kichwani.

Miradi inayopangwa iko mingi sana kiasi kwamba kudai kuwa hii miradi miwili mitatu ya utashi binafsi inaakisi mwelekeo wa jamii nzima kuwa mambo yetu hayako planned ni zaidi ya ujuha! Labda kama mnaigiza.

Natambua namna vichwa vyenu viko brainwashed na mfumo wa maisha wa kiliberali ambao mamlaka pekee makubwa kiongozi wa nchi anapaswa kuwa nayo ni kutangaza vita au kuitangazia vikwazo nchi flani. Hapo ndio roho zenu husuuzika nyie watumwa.
 
Back
Top Bottom